duh,pole sana mkuu,lakini mbona kama picha ni ya siku nyingi.nimeuliza tu,usinifikirie vibaya.
Ndugu wanajamvi habari zenu,
Mwana JamiiForums mwenzetu amevamiwa na watu wasioulikana nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo. Watu hao walifanikiwa kuvunja mlango wa nyumba yake na kumkuta akiwa na simu mikononi. Kwa maelezo yake, alikuwa katika Jukwaa la Siasa akijaribu kusoma baadhi ya taarifa ndani ya JF.
Ghafla alishitushwa na sauti ya kubomolewa kwa mlango kisha tochi ikimulika macho yake na kuambiwa atulie papohapo. Akapigwa Mapanga kichwani, mdomoni, mikononi, na tumboni; walisikika wakisema aoneshe mahali pesa zipo. Waliweza kuchukua Pikipiki, TV 2, Deki 1, Baiskeli 1 na Pesa taslimu 270,000/=.
Humu anatumia ID ya MOTOCHINI.
Tumuombee mwenzetu akiwa kalazwa mpaka sasa!
du only in Tz vibaka wanakimbia maji