Msaada kuhusu huu Utapeli

SaaMbovu

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2013
Posts
6,028
Reaction score
5,355
Habari wana JF.

Kulingana na ugumu wa maisha kumezuka kila aina ya mbinu ili mtu aweze kuingiza pesa kwa njia halali au haramu. Back to topic kuna mdogo wangu alikuwa anahama chumba baada ya mkataba kwisha maeneo ya Kinondoni B. Baada ya hapo akawa kapata chumba maeneo ya Kinondoni Studio baada ya kumtumia dalali ambae wanaofisi yao ya udalali pale Mkwajuni.

Kwa mujibu wa maelezo ya mdogo wangu ni kuwa alionyeshwa chumba na akaridhika tarehe 22/12/2014 na kutokana alivyoambiwa kuwa chumba wameonyeshwa wengi ikabidi akalipia siku inayofuata kwa makubaliano ya 50, 000/= kwa mwezi na alilipa miezi 6 pamoja na ya dalali jumla 350, 000/=.

Wakati wa malipo walikubaliana kuhamia pale tarehe 1/1/2015 kwakua mpangaji aliyekuwepo ndio alikuwa anaondoka siku hiyo na mdogo wangu alikubaliana na hilo kwakua alipokuwa anakaa mkataba ulikuwa unaisha tarehe 8/1/2015. Malipo yalifanyika kwa kuandikishana kwenye karatasi kama kawaida.

Baada ya hapo mwenye nyumba ambae anaitwa Andrea Michael Mkude na ndio mhusika mkuu alipokea fedha hizo na kutoa ahadi hiyo na huku wakiwa wamekubaliana. Ilivyo fika siku hiyo mdogo wangu akampigia simu baba mwenye nyumba na kumwambia leo nakuja tarehe imefika. Yule mzee alicho jibu ni kwamba mpangaji bado hajatoka mpaka tarehe 6 kwakuwa amepata shemu nyingine kwahiyo mpaka tarehe 6 ndio ahame. Ilivyofika hiyo tarehe mzee akipigiwa simu hapokei na akitumiwa sms hajibu.

Baada ya kwenda kwake mdogo wangu alimkuta mwanae na alivyoelezwa akasema hii nyumba hapangi mtu wala hakuna hilo na huyu baba yangu ni tapeli na hatujui yuko wapi na sisi tukimpigia simu hapokei ana zaidi ya wiki hajafika nyumbani na hata hicho chumba alichokuonyesha ndio chake.

Baada ya hapo tuliendelea kumfuatilia bila mafanikioa mpaka ilivyofika tarehe 8 akanza kutuma sms za kuomba msamaha ambazo zilikuwa 4 na hakuendelea tena kutuma sms wala kupokea simu. Baada ya kurudi kwa mwanae akasema kuwa hiyo ni tabia ya baba na kuna wengine anawapangisha nyumba nzima wewe unabahati chumba kimoja lakini mzee huwa anarudisha pesa baada ya mwezi. Kwahiyo huwa anakopa kwa kulazimisha.

Tulijaribu kwenda kituo kidogo cha polisi Kinondoni wakasema hizo kesi ni mpaka uende Polisi Osterbay baada ya kwenda pale Polisi wakasema hilo uanatakiwa uende kwa mjumbe wa mtaa. Baada ya kwenda mjumbe hakuwepo na baadhi ya majirani wanasema mjumbe ndio wako njia moja kwani kila mtu anajua tabia za huyo mzee.

Msaada tufanye nini?
 
Pole sana mkuu I can feel mana kuna siku chupuchupu kutapeliwa laki 6 na hao madalali,nilipelekwa kuangalia nyumba bt nikaonyeshwa mwenye nyumba feki sasa wakati wa malipo anadai tukalipie mlimani city haaa apo taa nyekundu ikaanza ku blink ndo kwenda kufanya uchunguzi kama hata hajulikaniii dah nlimshuku Mungu sana,ni wengi sana wametapeliwa pole
 
We hujaelewa tu, Wezi hapo polisi sio huyo mzee, hapo mzee ni dalali wa wezi tu. Kwani polisi hakuna kesi ya wizi wa kuaminiwa?? kwanini wasikufungulie jalada !!? Sasa wewe nenda kampasue huyo mzee yaishe ili yeye ndio aanze kukutafuta hiyo laki tano akajitibie, hakikisha unampasua kiasi kwamba matibabu yanafika laki tano
 

Hilo na wazo sahihi kabisa.
 
Kama atazilipa hizo pesa sio mbaya
 
Ndugu kwanza kabisa pole kwa masahibu hayo!2010 Nlishawahifanyiwa uhuni huu na mama mmoja pale namanga yeye anachumba cha wanawe kikubwa anakipangisha elfu 50 ukikiona tu lazma upate kichaa umlipe anakuambia mtu anatoka mwisho wa mwezi ukimpa pesa unasubiri muda ufike muda ukifika tu unakuta pesa yako cash anakurudishia kumbe kunamtu kapangishwa same room kwa either sixty au seventy anakata hela yako ilobakia anakula! Ndo mchezo wake! Cha kufanya siku ukipata nyumba next time lipia kwa account ya bank!
 
So far sasa kwa wizi wabongo ni kama wa Nigeria tu
 
Hali si hali nyakati hizi. Mwenye nyumba na madalali wote wamekuwa matapeli. Labda siku nyingine ukipata nyumba/chumba jaribu kulipia kupitia bank. pesa kurudishwa mara nyingi sana inakuwaga kwa miki miki sana.
 

Ushauri wa design hii segerea kutajazana sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…