Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 1,042
- 1,308
Mimi ingawa sisemi
Utasema ninaringa, njiani nikikupita
Mawazo yakinitinga, huenda nikabubuta
Majambo nikiyapanga,nikenda kwa kujivuta
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
Utazani nina njaa, ninavyoinywa kahawa
Hunipoza na ajaa, kichwa kikielemewa
Usije ukashangaa, nikiwapo nimelewa
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
Mara nahisi abiri, kumbe nipo nchi kavu
Upendo nikihitari, wanitupa kuti kavu
Hayo mambo ya dinari, yanitoa ushupavu
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
Hivyo nanyi mubaini, naugulia kwa ndani
Si kwamba naona shoni, ndo mazito duniani
Ninawahi kilabuni, kupoza yalo kitwani
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
✍️ Abuuabdillah
Utasema ninaringa, njiani nikikupita
Mawazo yakinitinga, huenda nikabubuta
Majambo nikiyapanga,nikenda kwa kujivuta
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
Utazani nina njaa, ninavyoinywa kahawa
Hunipoza na ajaa, kichwa kikielemewa
Usije ukashangaa, nikiwapo nimelewa
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
Mara nahisi abiri, kumbe nipo nchi kavu
Upendo nikihitari, wanitupa kuti kavu
Hayo mambo ya dinari, yanitoa ushupavu
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
Hivyo nanyi mubaini, naugulia kwa ndani
Si kwamba naona shoni, ndo mazito duniani
Ninawahi kilabuni, kupoza yalo kitwani
Mimi ingawa sisemi , ila ninayo mazito
✍️ Abuuabdillah