Maana ya neno "Tanganyika"

dega

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2012
Posts
3,171
Reaction score
3,087
Maranyingi majina ya watu na vitu huwa vina akisi uhalisia hivyo tukijua maana ya neno Tanganyika, watanganyika hawatotumbua kwani tutajua asili yao.

Jina la Tanganyika ni mkusanyiko wa maneno mawili

1. TANGA- Ni kuhangaika, kusumbuka, na kutotulia bila ya lengo maalum.

2. NYIKA- Ni mapori msitu mikubwa ambayo Kwa sehemu kubwa huwa inatawaliwa na nyasi.

Hivyo asili ya watanganyika ni watu wakuhangaika na kuhemea misituni bila ya kuwa na malengo na ukiangalia makabila mengi ya watanganyika wapo hivyo kuhama hama na kusumbuka na kutanga na nyika, kuhemea chakula, kutafuta maji malisho au hata bila sababu za msingi.

Hivyo Kwa asili hii watanganyika (wengi wao) ni watu wababaishaji, wavurugaji hawana uaminifu wasioweza kujisimamia.

Wakitawaliwa Kwa mujibu wa Sheria watapiga kelele kwamba wana Rais DHAIFU hivyo wanataka Rais mkali.

Akija mkali DIKTETA MVUNJA katiba hatufai hasimami Sheria.

Akija Rais anayejali, anawapa haki na stahiki zao watapiga kelele Wazanzibar wanauza nchi.

Nyinyi asili yenu ni KUTANGA NA NYIKA, waachieni watawala wawatawale ili mjikomboe sasa nongwa za nini?

Mtaendelea kuwepo katika UFUKARA mpaka lini wakati rasilimali zenu hamna uwezo wakuzisimamia? Uwekezaji WA DP WORLD ndio mwanzo wa kutotanga tena kwani mnafaidishwa Kwa rasilimali mlizo nazo ambazo hamuwezi kuzisimamia.

Wazungu si mmewaleta katika sekta ya madini jiulizeni mmepata faida gani zaidi ya mahandaki na umasikini?

DP WORLD NDIO SULUHISHO KWA UOZO WA BANDARINI.

Acheni kutanga.
 
Bwege wewe achana na sisi.
 
Tatizo lenu wavaa kobazi mnadhani kuwa karibu na waarabu ni kuwa karibu na mungu
 
1. TANGA- Ni kuhangaika, kusumbuka, na kutotulia bila ya lengo maalum.
TANGA ni vile vitambaa vya kukingia upepo kwenye vyombo kama jahazi merikebu

TANGATANGA ndio kuhangaika na kusumbuka.
 
Vyovyote iwavyo, vipngele vya mkataba vyenye lengo la kuingiza nchi utumwani virekebishwe
 
Unajipa shida ya bure, Tanganyika ni jina la ziwa, ziwa Tanganyika iliitwa Tanganyika na wamanyema na watu wa kando wa ziwa hilo, baadae Wajerumani wakachukua jina hilo na kuipa jina hilo koloni lao, kwahiyo maana ya Tanganyika haiko wazi, ila kijulikanacho ni ziwa Tanganyika ndio kitu cha kwanza kuitwa hivyo
 
Mkuu Wajerumani waliiita nchi German East Africa.

Jina la Tanganyika liliwekwa na Waingereza.

Walitaka kuiita nchi hii Eburnea, New Maryland au Windsorland, lakini wakataka kupata jina la kiafrika.

 
TANGA ni vile vitambaa vya kukingia upepo kwenye vyombo kama jahazi merikebu
Maana nyingine ya Tanga ni aina fulani ya nyasi. Zilikuwa zinapatikana kwa wingi huko mkoa wa Tanga. Ndiyo asili ya mkoa huo.
 
Daah, hatari, ila..

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
TANGA ni vile vitambaa vya kukingia upepo kwenye vyombo kama jahazi merikebu

TANGATANGA ndio kuhangaika na kusumbuka.
Kutanga ni kuhangaika
 
Tutaanza kumtoa huyo mama enu na kisha tutafuata kuwatoa hao waarabu wake .

Wamekaa huko wameingizana mikenge wanadhani ni rahisi namna hiyo
 
TANGA ni vile vitambaa vya kukingia upepo kwenye vyombo kama jahazi merikebu

TANGATANGA ndio kuhangaika na kusumbuka.
Kwa nyongeza tu neno Tanganyika ni makosa ya ki matamshi ya neno "TAWANYIKA". Wakati wa mkoloni mjerumani watumwa au wafanyakazi kwenye mashamba yao iwe katani, kahawa etc watanganyika hawakuruhusiwa kukutana na hasa kukusanyika pamoja kwani waligofia njama za uasi ndipo wale nyapara wa kijerumani kila walipoona kusanyiko waliwatawanya kwa fimbo, kutishia kwa binduki na kwa kutamka neno TANGANYIKA wakimaanisha tawanyika.
Hiyo maana aloileta huyo mvaa kobasi ni kutaka kuhalisha upuuzi wake na mwisho huko zanzibar zipo bandari nyingi tu wauze au wawagawie hao wavaa kabazi wenzao lakini tanganyika wasahau
 
Mumeshikwa pabaya WATANGA NA NYIKA M60 mwaendesha puta na M 1.8 mkiambiwa hamna akili muwe mnaelewa shenzi kabixa
 
Unachengwa wewe
 
Wazanzibar mnapata tabu sana mkimuona Mtanganyika anaamka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…