UK1..... Ghafla Michael Andrew (M.A) anapushiwa na gari aina ya Rava4 ambayo ndanimo palikuwa na msichana mmoja na dada yake waliojulikana kwa majina ya Marry na Agness. Michael aliangukia kwenye mtaro na kupoteza fahamu. Chanzo cha kugongwa kwake hakikufahamika ni nin kilichosababisha agongwe, kwan kabla ya yeye kugongwa, alionekana ni mtu mwenye mawazo na mwenye kuogopa watu wanaomuangalia sana. Alikimbia kwa kasi kubwa kutoka eneo moja kwenda nyingine kabla ya kuingia kwenye uso wa gari. Ndipo Agness aliposimamisha gari na kutoka ndan yeye pamoja na mdogo wake Marry. Walielekea kule alikoangukia michael na kumkuta ana hali mbaya. Walijawa na huruma wakaamua kumchukua na kumpeleka hospital kwa ajili ya matibabu. Hakuweza kutokea hata ndugu yake aliyediriki kumuulizia. Ili wabidi wao ndio wawe ndugu zake hapo hospital. Agness alimuamuru marry abaki na mgonjwa akimuuguza kwa muda ule. Daktari alimpima ili atambue ni eneo lipi aliloumia. Alipomaliza kumpima aligundua... INAENDELEA UK2