Kwa wanandoa

Nyawayi

Member
Joined
Jan 30, 2020
Posts
16
Reaction score
11
Kwa wale ambao wameoa au kuolewa na wanauelewa wa sheria za ndoa nilitaka kujua sheria hii imekaaje pale mimi ninapo oa na baada ya kuoa mzazi wangu akanipa nyumba ya kwenda kuanzia maisha ,gari ya kutembelea etc je hizi mali pia zitahesabika ni mali ya wanandoa au ni mali yangu binafsi sababu nimepewa zawadi na mzazi wangu au pia kwa mwanamke wakati wa send off akapewa zawadi na wazazi wake je pia ni mali ya wanandoa wote au ni yake binafsi.karibu kwa wenye uelewa wa hili.
 
HONGERA SANA MKUU KWA KUJIANDAA KUOA HAYO MENGINE UTAKUTANA NAYO UKISHAZAMA NDOANI
 
Mali yenu wote (mke na mume)

Unapoingia ndoani mali zako zote zinakuwa zenu na zake pia hivyo hivyo

Kizazi kipya kimetawaliwa na ubinafsi uliokithiri ndio sababu ya matatizo yasiyoisha kila kukicha baina ya wanandoa
 
Mkuu, nenda kwenye ofisi ya Wakili, lipa consultation fee, muulize maswali yako yote atakujibu, mtawaua njaa mawakili kwa style hii.
 
Mnafanya wqtu waogope kuoa sasa.. yaani nimepigika miaka 10. Nimeoa zangu mke hana kitu tofauti na vitenge alivyo pewa kwenye sendoff (harusi za uswahilini ) halafu siku tumeachana tugawe mali sawa.

Kama anataka tugawe sawa basi inabidi wote tuanze from scratch. Tushinde njaa pamoja, tulalie mkeka, tubebe zege pamoja.
Binafsi namuonea huruma sana Jeff wa Amazon
 
Oooh sawa sawa kwa wanaume najuaga hatuna shida but kwa dada zetu 😂😂 sijui wanakwama wapi akiwa na kitu atatukan mali zangu lakini sisi hatunaga hizo
 
Sheria iko wazi sana Mali ambazo hamkuchuma pamoja si Mali za wanandoa ni Mali za aliyechuma Mali za wanandoa ni zile ambazo walichuma kipindi mko pamoja mahakama inaweza kutoa uamuzi wa kugawana Mali ambayo hamkuchuma pamoja kama tu Kuna sababu za msingi sana kufanya ivyo endapo ni nyumba ambayo Mme aliijenga kabla ya ndoa mahakama inaweza kusema kumfidia mke kwa kufanyia marekebisho mbalimbali ambayo yalifanya ile nyumba kuwa nzuri kipindi chote walichoishi pamoja
Sent using Jamii Forums mobile app
 
So mkuu unamaanisha zawadi mnazopewa siku ya harusi or send off kwa dada zetu haziusiani kuwa ni mali za wanandoa bali ni mali ya mtu mmoja mmoja !!?
 
"Nitakuwa nawe kwa shida na raha,changu chako,chako changu... nitakuwa nawe kwa uzima na maradhi mpaka kifo kitakapotutenganisha"

Formula za kwenye ndoa ni za ajabu sana,ndyo maana baadhi ya watu huandka majina ya ndugu zao kwenye mali walizopata wakiwa pekee yao!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…