ndandawamalenja
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 548
- 658
Hivi majuzi nilienda kwenye kituo kimoja cha tiba mbadala, pale Mbezi beach. Kinaitwa Fadhaget Sanitarium. Dr. akanipa kidude kidude flani hivi nishike kimeunganishwa na computer, akaclick kinini sijui kikaanza kufanya kama kinascan viungo muhimu vya mwili. Ubongo, moyo, figo, mapafu, etc. Huku kinadisplay activities na information kwenye screen ya laptop. Baada ya dakika 2 hivi kikamaliza na kutoa report. Dr akaanza kunielezea sasa, lakini alichofanya ni kunichanganya tu kwa sababu nikawaza kwamba kile kimachine ni geresha tu. Kwamba kama kupima afya ya mtu ni rahisi hivo, inakuwaje tunapopima mahospitali makubwa kabisa inachukua muda sana, mpaka wakutoe damu kibao na mambo mengine halafu kahospitali kadogo tu kanatechnolojia ya kupima mwili wote kwa sekunde sitini? Hivi hii sio program ya kutuibia ambayo inatoa majibu yaleyale but randomly kutokana na watu mnavyokuja? Naomba wataalam mnifumbue macho!!