Artificial intelligence(AI) is about enabling a machine (computer, robot, smartphone,etc) reason like a human being. Mfano: ukitengeneza app inayoweza kujibu maswali kama rwanda imepakana na nchi ngap? Au wilaya ya kisarawe inapakana na wilaya gani, mara nyingi utatumia AI. Kinachofanyika ktk mifano hiyo miwili ni kwa program 'kuangalia' ramani ya Africa (ambayo ni picha), kutambua nchi na kuzihesabu na kutoa jibu.
Kusema kweli hii sayansi bado ipo katika kiwango cha chini-bado inafanyiwa utafiti. Labda wengine tutakuwa tumewahi kuona ktk science fairs za shule huko ulaya, unakuta mwanafunzi anatengeneza robot ya mtu (machine), anaiamrisha itembee na kusimama. Lakini akiiamrisha itembee, inatembea na ikikutana na ukuta au kizuizi inakigonga-yaani haisimami wakati binadamu atasimama maana anajua hawezi kupenya ukutani. Huu ndio uchanga wa AI kwa sasa.
Binafsi, naamini linaweza likawa kosa la kawaida ktk design na programming ya hiyo app. Siamin kama kuna ubaguzi wa rangi katika hili. Maana ili hiyo app iweze kutaja kama ni jengo refu au mti mrefu lazima 'iangalie' features za picha. Gorilla ni mweusi, sisi ni weusi so kwenye picha kutakuwa na vitu vingi tunavyofanana. Kumbuka, kutengeneza apps unatumia maneno (sets of instructions)-changamoto ni kufanya maneno 'yaone' features za picha na kuweza kutofautisa mfano nyati na ng'ombe. Kwa wanaojua programming, hiki sio kitu rahisi. Tena tukumbuke wengi wanaotengeneza apps kama za kwenye android(ya google) sio programmers wazoefu, wengi ni watoto wa shule na colleges/versities.