Gharama za Kitanda Muhimbili, kama Hosteli!

Vyamavingi

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2014
Posts
5,986
Reaction score
5,804
Gazeti la Mwananchi leo limeripoti kuwa gharama za kitanda kwa mgonjwa atakayelazwa zimepanda na atalazimika kulipia kitanda kwa bei ya elfu tano kila siku.

Hii ni nje ya gharama ya mlo mmoja ambayo ni shilingi elfu mbili. Hii ina maana kuwa iwapo mgonjwa atapata huduma ya kulala na malazi, itampasa kulipa si chini ya shilingi elfu tisa kila siku. Hapo ni nje ya gharama za matibabu-vipimo, ushauri, na dawa.

Najiuliza, kupanda huko kwa gharama za matibabu MNH kutaongeza ubora wa huduma kwa wagonjwa? Je, vitanda vitaongezeka na tatizo la wagonjwa kulala wawili kwenye kitanda kimoja au kulala chini litaisha?

MY TAKE
Hili ni pigo kubwa kwa sekta ya afya nchini ambayo iko kwenye hali ngumu.

Kwa maana hiyo tutegemee yafuatayo:
1. Idadi ya vifo kuongezeka badala ya kupungua maana mgonjwa kutoka Nkasi hadi afikishwe Dar lazima ndugu wabanane kwa michango ya nauli kuja Dar.

2. Wagonjwa wanaotelekezwa na ndugu Muhimbili kuongezeka, kwani mgonjwa akifikishwa Muhimbili tu, ndugu waliomleta wanaweza kumwacha ili kuepuka gharama kubwa za matibabu.

3. Kuongezeka kwa imani juu ya miti shamba na matibabu mbadala kama tunavyosikia ongezeko kubwa la matangazo ya matibabu mbadala kwenye vyombo vya habari-Tvs na redio [Dk. Ndodi na wengineo]

4. Ongezeko la waganga wa jadi na matibabu mbadala kufuatia ongezeko la wagonjwa wanaokwepa gharama za Hospitali.

5. Ongezeko la Watanzania wagonjwa kutokana na wagonjwa wengi kutopona baada ya kukosa matibabu sahihi.

6. Umri wa kuishi kwa Watanzania kupungua kwa sababu hizohizo nilizoainisha.

==================================================

Chanzo:Mwananchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…