Kukopa ni jambo la hiari si lazima hata hao mabilionea wa duniani unaowaona wanamikopo...kila mtu anakopa kulingana na uhitaji wake siku hizi watu wengi hawategemei mishaharaWakopaji wanapaswa kuwa makini sana na wakopeshai wote kwani naona ni kama vile kondoo mbele ya fisi mwenye njaa. Wakopaji wajitahidi kupunguza mihemuko ya matatizo waliyo nayo katika ukata wanaopitia kwa kuyatanguliza mbele kama tai wakisahau baada ya kukopa kuna ukurasa mpya unafunguliwa unaitwa "kulipa" aka marejesho. Changamoto za aina mbalimbali katika maisha hazitawahi kukoma mpaka mwisho wa uhai wako. Uvumilivu ni jambo la msingi kuepuka kukurupuka kukimbilia kukopa pasipo ulazima. Kopa pale unapofikiri kwa kweli unahitaji kukopa kwani ikumbukwe wakopeshaji wote ni wafanyabiashara wenye mtazamo wa kutengeneza faida na kufanya maisha yao na taasisi wanazozitumikia kuendelea kuwepo kwa mgongo wako. Jiulize maswali yafuatayo kabla hujaenda kukopa popote;
1: Ni kweli unahitaji mkopo na huna namna nyingine
2: Unajua vizuri masharti ya huo mkopo, riba ya mkopo kiuhalisia, gharama nyingine za mkopo kama vile gharama za uandaaji wa mkopo, bima ya mkopo nk
3: Aina ya dhamana inayohitajika katika huo mkopo na utaratibu wa uwasilishaji hiyo dhamana
4: Kiasi gani unahitaji cha mkopo na ni kweli unakihitaji chote kwa ajili ya mzunguko/uwekezaji wako au ni sehemu utanunulia simu ya gharama, kiatu kizuri, mkufu wa dhahabu nk sio kwamba ni vibaya ila tafakari kwa kina.
5: Unaweza kulipa huo mkopo unaoomba pasipo usumbufu au kupata ugonjwa nk
6: je ukishindwa au kuchelewesha rejesho nini kitatokea kwako na familia yako
7: Unaishije baada ya kukopa na katika kipindi chote cha marejesho ya mkopo, kumbuka mkopo kuna kitu unaleta katika maisha yako na familia yako.
hapana acha ulaghai mbona ni wewe ndiyo mtoa povu kwanini iwe ni wewevtuBank abc ni wasumbufu sana kipind nafanya kazi nlikopa kwa hawa jamaa baadae nkataka kuterminate mkataba nlisumbuka sana mara nije Dar mnirudishe Moshi mara mnipe document zisizo sahihi kiukwel bank yenu sio rafiki kwa wafanyakazi
Sent using Jamii Forums mobile app
Jibu hoja bhana acha kujibu utadhani sio biashara inayokulisha wetu wengi sana wamesumbuliwa unaambiwa mkopo masaa 24 lakini unakamilisha kila kitu ndani ya masaa 3 ila mkopo unatoka baada ya week 3 sasa hapo unamsaidia au ndio nini, unapoambiwa makosa jibu kwa hoja safi na yafanyie kazi malalamiko ya wateja ila sio kujibu kama ulivyojibu hapohapana acha ulaghai mbona ni wewe ndiyo mtoa povu kwanini iwe ni wewevtu
mi sipo ABC ila namkopo hapo na sina mda mrefu tokea nikope na nilipata mkopo ndani ya masaa 48 nimshuhuda pia kuna mwenzangu pia kakopa juzi tu naye pia kapata mkopo ndani ya masaa 48...Jibu hoja bhana acha kujibu utadhani sio biashara inayokulisha wetu wengi sana wamesumbuliwa unaambiwa mkopo masaa 24 lakini unakamilisha kila kitu ndani ya masaa 3 ila mkopo unatoka baada ya week 3 sasa hapo unamsaidia au ndio nini, unapoambiwa makosa jibu kwa hoja safi na yafanyie kazi malalamiko ya wateja ila sio kujibu kama ulivyojibu hapo
mkuu hatuna processing fee,na hiyo 1.4% ni kiasi cha riba cha makato ya mwezi ambayo utakuwa unakatwa kila mwezi baada ya calculation kulingana na kipindi ulichochagua kukamilisha malipoProcessing fee Ni kias gani, na hiyo riba 1.4% kwa mwezi inakua vipi
Sent using Jamii Forums mobile app