Engineer natafuta kazi

Una expiriensi yoyote mkuu?
Ume graduate jana tu, umasema umesota?
 
Badili namna ya kufikiri
Kwa mfano
Ondoa aibu vaa sura halisi ya msoteaji..ondoka mjini,elekea kwenye machaka ya ujenzi hasa wa barabarani.
Namna ya kuondoka,inabidi upande malori(madereva wa malori wengi walikuwa makandarasi,pia wana msaada mkubwa kwa mtafutaji)Kuwa huru kueleza kwamba unaenda kutafuta aidha utaonyesha na documents zako mbalimbali.
Ukifika chaka jitambulishe kwa serikali ya kijiji ,hii ni muhimu sana.
huko ndio kuna wazalendo wa kweli,Kwa elimu yako hutakosa angalau u Foreman;
Mara nyingine Camp likikuiva unaweza ibuka na maruprup mengine.
 
kama uko dar na unaweza fundisha.kuna academy nying na tuition centre nying hazina walimu wa physics na mathematics.nenda banana, ukonga kuna academy nying zina uhaba wa walim wa sayans.kuna new vision, brothers fount of academy na nyingine nying.nakuhakikishia kama uko compentent kwenye physics utapata kazi.na mishahara yao kwa walimu wa hayo masomo ni zaid ya lak 5 kwa mwez.usikae nyumban bro.kama uko dar anzia hapo banana ukonga magerezan mpaka gongolamboto.best wishes.....
 
Ok,hatukushauri kiutani tupo siliasi pia, Unasema umemaliza mwaka huu chuo chenu hapo,kuna watu wana B.Eng ya Civil, B.Sc Civil pia hawana kazi,ila kazi ziponyingi sana ujenzi unaendelea kila kukicha,sasa basi acha uhongo kwanza kusema unezunguka sana mtaani hiyo sio kweli,umemaluza juzi tu,afu unasema umesota? Cheti huna labda Matokeo ya awali,sasa basi kuwa muwazi kwanza umemaliza lini? maana uzi wako nimeona una uhongo mwingi.
 
Kijana kuamakini na nia zako, hii si sehemu za masihara tafadhali, hapa nisehemu ya watu walio makini na kujiheshimu. Kama unaona kazi hamna manaake shule ndogo au huna uzoefu basi ksjifunze upate uzoefu au rudi shule.
 
Asante sana wakuu ni kweli nimeamini hii ni sehemu ya watu makini.mawzo yenu ntayafanyia kazi wakuu kuanzia kesho.nipo dar wakuu pia nimemaliza mwaka huu july 2014,unajua msoto unakuja kuwa napata mlo mmoja ktk masaa 24 afu maisha haya sijawahi kuyaishi. Ntawapa report tarehe 27 mana ntaenda ktk machaka jamani. By one heart let me express my gratitude to you jamii forum members.I appreciate is the place of intellectual and great thinkers!!!
 
pole sana mkuu

MBONA UNA POTENTIAL KUBWA SANA
SHULE ZIPO KIBAO walimu wa physics na hesabu hamna embu omba kufundisha kwanza huku ukisikiliza michongo ya kazi
upo sehemu gani hapa tanzania??

Mkuu umenidaka mdomo hoja yako inajitosheleza nadhani kashapata mwanga. Kuna shule za private mwalimu analipwa mpaka 2m kwa mwezi. jishikize na usione aibu unaweza kwenda kwa wachina huko na ukaambulia 750K
 
Acha uoga kijana,umemaliza July unalia njaa December hii, mm nlimaliza 2007 nikakaa miezi Sita bila kazi.wenzangu wanapata nikajiuliza mm napungukiwa nini?, nikagundua soko lasasa degree kilamtu anayo tunataka sifa zaziada unazo?. Mm nlienda kujifunza software za design kabla sijamaliza kozi simu zikaanza kunitafuta.mpaka Leo nipo Kampuni kubwa tu namimi Nina firm yangu naweza kukufundisha CAD kama uko tayari maana Kampuni yangu inafundisha wiki2 tu cv yako inashiba. Watu wanatafuta mtu anaejua kutumia nyenzo za kihandisi huu niulimwengu Wa computer mkuu. Tembelea www.tancad.com
 
Hivi watu huwa twasoma tu bila kujua what next after school.
Atleast sasa unapata ukweli wa maisha maana huko zamani najua lazima ulidanganyana na watu kuwa ukimaliza tu unapata kazi.
Kupata kazi ni kazi
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…