Mh kweli kuna wenzangu humu. Kama umepita njia hiyo na unatoka Mlimani, then....Nakumbuka njia ya kupitia chuo cha maji unatokea kwenye tangi kubwa la maji kando ya ukuta wa Idara ya maji.
Namkumbuka sana huyo mama! Kibo bar ndiyo ilikuwa bar mashuhuri eneo hilo enzi hizo! Ukitaka muziki unakwenda White House kuna Maquis, Tour and Hunters kuna Mzee makassy na Orchestra Makassy! Maisha bado mazuri na Nyerere wetu anatupa hela ya kukaa nje ya chuo ili wanaotoka mbali wapate nafasi chuoni!