Best Business Idea

shekhe89

Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
49
Reaction score
2
Hello.
Mimi ni kijana nina miaka 25, nipo Zanzibar. Nina elimu ya Diploma ya juu (advanced diploma) katika fani ya Finance.
Kuna idea ambayo nahisi ina tija sana kwa maeneo ya dar es salaam na kila kukicha idea ninazofikiria wanatokea watu na pesa zao na kuzifanyia kazi.
Tatizo linalonikwamisha mm kutofanyia kazi hzo idaes ni.mtaji.
Idea yenyewe ni kuanzisha maduka ya ice cream katika maeneo ya mkusanyiko wa watu kama vile mikahawani, sehemu zenye maofisi, zehemu za kufurahishia watoto, mapumziko nk.
ninapozungumzia ice cream naomba nieleweke ni zile zenye mfano anazotengeneza azam.
asanteni.
kwa maelezo zaidi nitafute kwa
call/sms/whtap +255 772 993 820
 
We kijana mwaga ideas hapa usaidiwe jinsi ya kufikia malengo yako usije kudhani idea zako ni mpya sana. Sema hapa utashangaa watu kibao wana hizo idea na wanaweza kukusaidia kuiboresha. Kumbuka kama ipo ipo tu
 
Hata kama una idea huwezi kuwa umekamilika kwa unachowaza kwa asilimia 100 ungeweka hapa pia ungepata ushauri au idea uliyonayo kuna mwengin anaifanyia kazi angekusaidia kuiboresha n hayo tu
 
We kijana mwaga ideas hapa usaidiwe jinsi ya kufikia malengo yako usije kudhani idea zako ni mpya sana. Sema hapa utashangaa watu kibao wana hizo idea na wanaweza kukusaidia kuiboresha. Kumbuka kama ipo ipo tu

nadhani ipo sawa sasa, au bado mheshimiwa?
 
nadhani ipo sawa sasa, au bado mheshimiwa?
Mimi ushauri wangu kwako ni mmoja tu. Start small. Usiwaze kutembea kabla hujatambaa. Ukiona idea uliyonayo haitekelezeki kwa kuwa huna mtaji wa kutosha basi ujue wazo hilo sio sahihi kwako kwa muda huo.
 
Rekebisha heading yako.
Hiyo ni Idea ya kawaida sana tu,na biashara kama hiyo inafanyika sehem hizo.

Sasa sijaona jipya saana hapo

Pia naomba Uitendee haki Advance Diploma yako in Finance.
Najua utakuwa umesomea Chuo cha Fedha Chwaka,Zanzibar ambacho ni chuo Bora sana.

Nahisi unasumbuliwa na vitu viwili:-
a)Msongo wa Maisha
b)Kuhamisha maandishi ya kwenye kitabu kupeleka kwenye uhalisia

Ushauri ni kwamba,wewe ni msomi,mie sio msomi wa Biashara ila ni mfanya biashara.
Unajua hakuna Buisness Idea yoyote ambayo ni mpya katika dunia hii.Kila unalifikiria basi lilianza kabla hujazaliwa.
Watu wanashindana kwa namna ya kutumia fursa kwenye biashara husika na ubunifu.

Zanzibar kama unakumbuka kabla ya pale Bomba Ice cream kwa mchina na yule Jirani yake hawajaanza kufanya hii biashara,watu walikuwa wamelala sana na hakuna aliestukia.Ila sio kwamba kulikuwa hakuna Ice cream Zanzibar.Ila pale Kuna mmoja ni mjanja zaidi,maana yeye anatengenezea pale pale dukani kwake ni ni msafi sana,na watu wanaona na Mashine kazifunga pale.Anakula Tenda za harusi kama wazim vile.
Watoto wa shule za Mwanakwerekwe,Shah School,Nyuki Military School,wote anabeba.

So,issue ni ubunifu,na sio pesa nyingi sana kama unafikiria wewe.Unaweza kuanza hata na laki nne tu.
Ukawa unanunua rejareja kisha unauza,ukipata pesa unanunua Mashine ya Kutengenezea Mwenyewe.Nahisi inakaribia 6m ila ndongo ya port mbili
 

asante mkuu
 
Navyojua mm kama umesoma finance na ulikua mwanafunzi hai. Utagundua kwamba Capital si kitu cha kuumiza kichwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…