Asali ya nyuki wakubwa

Hiyo gharama kwa kiasi gani cha ujazo wa asali

Tuyaache kama yalivyo
 
Mim hay mambo ya asal hebu nifafanulie kuna tofaut gan kat ya asali ya nyuki wakubwa nyuk wadog na ukisema asali mbichi kun asali ambayo sio mbichi nitoe gizan tafadhal cc asanteelimu2016
 
ccukhuty NYUKI WADOGO

1. Ni nyepesi zaidi kwani ina kiwango cha maji kuanzia asilimia 24 na zaidi.
2. Ina ladha ya UCHACHU kidogo ingawa ni tamu sana.
3. Mara nyingi ina rangi ya KAHAWIA ILIYOKOLEA inayoenda kwenye WEUSI
4. Ina harufu kali kidogo( hii ni ngumu kuileze)

NYUKI WAKUBWA

1. Ni nzito kuliko ya nyuki wadogo kwani ina kiwango cha maji cha wastani wa kuanzia asilimia 17 hadi 20.
2. Ni tamu moja kwa moja bila kua na ladha ya uchachu kama ya nyuki wadogo
3. Ina rangi nyingi kuanzia NYEUPE, NYANO, KAHAWIA ILIYOPOA, KAHAWIA ILIYOKOZA n.k
Hizo ni tofauti za muhimu kuzijua kwani zitakuwezesha kupata asali unayoitaka na kuepuka kuibiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mim hay mambo ya asal hebu nifafanulie kuna tofaut gan kat ya asali ya nyuki wakubwa nyuk wadog na ukisema asali mbichi kun asali ambayo sio mbichi nitoe gizan tafadhal cc asanteelimu2016
Watu huchemsha asali ili asali ijae na kupata asali nyingi kutoka uzito wa awali. Na asali inayochemshwa inaondoa ubora wa asali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahan mkuu, hv utajuaje asali ambayo haijachakachuliwa?

sent from my iPhone 8
1 chukua glass yenye maji dondosha asali asali ikienda chini ni pure ikichabgabyika na maji ni fake

2 dondosha tone la asali kwenye karatasi nyeupe ukiona asali imetoka upande wa pili au karatasi likilowana jua asali ni fake

3 chukua njiti ya kiberiti chovya kwenye asali kisha washa upande wa baruti ukiona baruti haiwaki jua asali imechanganywa na maji au ni fake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante kwa elimu mkuu, ya nyuki wadogo unayo pia ? gharama yake ?

sent from my iPhone 8
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…