ijokhazubsy
New Member
- Sep 14, 2014
- 1
- 0
Mkuu! Nakupa uzoefu wangu kwasababu nimepitia hali kama yako! Tofauti na wewe (labda) ni jinsi unavyoushughulisha mwili kufanyakazi! Mimi kwangu sikosi kazi ya kufanya! Nimebahatika kuwa na eneo kubwa kidogo kiasi kwamba kuna shughuli nyingi (manual) kufanya na kutokwa jasho. Na mimi yalinivamia yakiambatana na kupiga chafya kwa saana! Sijatumia hata dawa yoyote zaidi ya kufanyakazi na kutokwa jasho na kuoga maji ya moto! Mpaka sasa yalikopotelea sijui ni wapi maana nimekaa nayo zaidi ya miezi sita hivi!Jamanii, mwenzenu nina naelekea kumaliza mwaka sasa nasumbuliwa na Mafua MAZITO hadi yanaziba pua!
Hospital naambiwa ni Allergy nijaribu kugundua kinachonikataa yaani nimeshindwa kujua kabsaa, usiku nalala nimekenua napumua kwa mdomo maana pua zinaziba, na yanatoka makamasi MAZITO.
Nimetumiwa dawa inaitwa Prednisolone kwa muda mrefu ndio inanifanya nikae sawa lakini niliacha kumeza 2dys only Hali inajirudia, kwa sasa hii dawa naiogopa maana makatari wanasema inashusha Sana body immunity.
Dawa zingine za Nasal spray, desloratadine, loratadine, nimetumia lakini hazijanisaidia.
Ili niongee vzr na watu mchana inanilazimu kumeza Prednisolone japo Nimeambiwa sio nzuri kiafya.
Naomba mwenye ujuzi au anayeweza kunisadia niondokane na Hali hii please help.
Hilo la mazoezi nakuunga mkono 💯boresha kinga yako ya mwili fanya kubadili mlo wako usiwe mlo uleule ambao hauzingatii mlo kamili..
matunda,mboga za majani na vitu vyengine vyenye lishe,kunywa maji yakutosho walau anza kufanya mazoezi mepesi hata ya mbio au kuruka kamba just to disturb your body sio mazoezi magumu simple tu,walau kwa wiki mara tatu inatosha pia hakikisha unatafuna tangawizi ama unakunywa chai ya tangawizi kila siku,tangawizi iwe ni ile fresh na humo kwenye chai usiweke kidogo tia uisikie kabisa... ukifanya haya nafikiri utaona mabadiriko ndani ya muda.