Ajira za Udom

hekimanyingi

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2013
Posts
679
Reaction score
573
Chuo kikuu cha dodoma (UDOM) kilitangaza kazi september 2012 na |November mwaka huohuo waliotuma maombi wakaitwa kwenye usahili wa kuandika (Written interview). Mwezi march mwaka 2013 watu waliofanya vizuri kwenye usahili wa awali waliitwa kwenye usahili wa mahojiano.

Jambo la kushangaza na la kustaajabisha ni kwamba mpaka leo kimya hakuna cha kuajiriwa waliyofanya interview bali wanapigiwa simu vijana waliosoma pale na kuitwa kuanza kazi kwa kigezo cha kufaulu bila kufanyiwa usahili. Hatujui zilifia wapi hizo nafasi na wamesahau kuwa waliofanya usahili walitumia gharama pia.

Na hatari ninayoiona mbele ni kitendo cha mheshimiwa rais Kikwete kuruhusu vyuo vikuu kuajiri wenyewe bila kuweka sheria kali au utaratibu mzuri wa kuajiri watu kulikoni hivi sasa wanaajiri watu kiholela kisa tu mkuu wa chuo (college) au idara kafurahishwa nao.

Kwa style kama hii tutafika kweli?
 
Tutafika tuu hii ndo Tanzania..ni zaidi ya uijuavyo.

Mlacha yuko pale Udom kindugu
unatarajia atakuchukua ww sio ndugu yake?

Maji ufata mkondo mkuu
 
Tutafika tuu hii ndo Tanzania..ni zaidi ya uijuavyo.

Mlacha yuko pale Udom kindugu
unatarajia atakuchukua ww sio ndugu yake?

Maji ufata mkondo mkuu

mimi pia nilifanya huo usaili. kilichonishangaza katika nafasi niliyoomba walitangaza nafasi 6 na katika written interview tulikuwa wengi km 78 ila kwenye oral tukafanya wanne. sasa ninachoshangaa iweje tufanye 4 wakati nafasi zilitangazwa sita?
 
Toka udom iache kupokea ruzuku toka serikalini, mambo si shwari..
 
mimi pia nilifanya huo usaili. kilichonishangaza katika nafasi niliyoomba walitangaza nafasi 6 na katika written interview tulikuwa wengi km 78 ila kwenye oral tukafanya wanne. sasa ninachoshangaa iweje tufanye 4 wakati nafasi zilitangazwa sita?


pale kuna watu wachache wameodhi madaraka. Tena hali uwa mbaya zaidi kipindi ichi ambapo UDOM haipati ruzuku kutoka serikalini.

Uendeshaji wa mambo pale ni m bovu,ubabe uliokithiri,udini uliovuka mipaka, pamoja na kujuana kwingi..

Udom kupata ajira pale labda uw' una ndugu utawa mkuu pale asee
vinginevyo utasubiri sana.

Mwaka jana kashfa ya udini ilikua inawatafuna sana hasa viongozi wa juu wa utawala wa udom.

Ni jambo ambalo linakua kwa kasi sana kiasi cha kuvuka mipaka ya kawaida sana.

Inabidi serikari iingilie katiz ndugu zangu.Udom hali si shwari pale.
 
Tutafika tuu hii ndo Tanzania..ni zaidi ya uijuavyo.

Mlacha yuko pale Udom kindugu
unatarajia atakuchukua ww sio ndugu yake?

Maji ufata mkondo mkuu
Wewe ndoto yako si kwenda jeshini ama usalama wa Taifa vipi
 
Jaman hii Tanzania cjui tunaelekea wapi??
wengine tushajiondoa kwenye hiyo Tanzania, ndio maana hatupati shida hizi, lakini je we umetambua unakoelekea?..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…