Ni lini Tanganyika itaacha kuikalia Zanzibar kimabavu?

Nawaomba wazanzibar wenye nia ya kupigania uhuru wa Zanzibar kupeleka mashtaka Umoja wa Mataifa kama ikishindikana litumwe jeshi la ukombozi kutoka UN kuja kuikomboa Zanzibar kutoka kwenye makucha ya Tanganyika.
Mkuu hivi upo? Hili liulizie kwa Wazanzibari utapata jibu.
 
Uzi unasema hivi Ni lini Tanganyika itaacha kuikalia Zanzibar kimabavu?
Okay naomba unisaidie majibu ya haya maswali mkuu.....
1. Rais wa Tanzania ni Mzanzibari tena hakuchanguliwa na Watanzania bali alikuwa Makamu wa Rais, je naye anachangia kuikalia Zanzibar?
2. Vyeo vingi sana kwa sasa ndani ya Tanganyika wanapewa Wazanzibari, pita kwenye halmashauri uone walivyojaa wapemba, je pale ofisi ya Mjini Magharibi kuna wasukuma wangapi? Au na Wazanzibar walipo Tanganyika wanawanyonya Wazanzibar?
3. Mtaani huku tuna wanajeshi wazanzibari wa kutosha je huko Zanzibar kuna wanajeshi kutoka Rukwa?!
4. Ni nani ambaye ameidhinisha bandari ya Dar es Salaam ambayo ipo Tangannyika kwenda kwa waarabu!? Kama sio Mzanzibari?!
5. Kipi ni rahisi katika ya hivi? Mpemba kutoka Kiembe Samaki kuja kununua ardhi Ibadakuli Shinyanga na kujenga bila matatizo au Mkinga kutoka Kihesa Iringa kwenda kununua ardhi Pemba?!!
NB: Mara kadhaa mmekuwa mkisema kuwa Zanzibar ni sehemu salama kwa Watanganyika ila sio kweli! Ukifika tu wakikuona ni mtu kutoka bara unanyimwa fursa nyingi sana zingine ni fursa ambazo hata nyie wazanzibari mnazipata huku Tanganyika.
 
Samia ndo no 1 citizen na ndugu yake yupo kule zanzibar kwa nn wasivunje wenyewe sisi tunahusika nn hapo
Nyinyi namhusika kwenye unyonyaji wa rasilimali za Zanzibar ndio maana hamtaki kuvunja ili muendelee kufisidi rasilimali za watu wa Pemba na Unguja. Mungu anawaona.
 
Samia ndo no 1 citizen na ndugu yake yupo kule zanzibar kwa nn wasivunje wenyewe sisi tunahusika nn hapo

kuwa raisi hakukuteshelezi kuwa na mamlaka ya hayo, TISS munayo nyinyi, JWTZ munalo nyinyi, zaidi 90% ya viongozi wa CCM, CHADEMA, Serikali yote kuanzia Bunge, Mahakama, mawaziri munavyo nyinyi. Kwanini yeye wakati nyinyi ndio wenye nguvu?
 
Wazanzibar ndio hawo wanalalamika hapo?
Ndiyo mkuu. Msemo wa huku kwetu tunasema 'shikeshike na mwenyewe nyuma' yaani agiza/ sema na huku mwenyewe unafanya kivyako. Tunasema na huku tunatekeleza. Ndo maana nikakuulza ' upo?'
 
Nyinyi namhusika kwenye unyonyaji wa rasilimali za Zanzibar ndio maana hamtaki kuvunja ili muendelee kufisidi rasilimali za watu wa Pemba na Unguja. Mungu anawaona.
Zitaje hizo rasilimali.

mbona Mimi naona kama Zanzibar ndiyo mnanufaika sana na huu muungano wa kiduwanzi??
 
Mkuu
Ndiyo mkuu. Msemo wa huku kwetu tunasema 'shikeshike na mwenyewe nyuma' yaani agiza/ sema na huku mwenyewe unafanya kivyako. Tunasema na huku tunatekeleza. Ndo maana nikakuulza ' upo?'
Mkuu hatutaki kufanya jambo hili kinafiki. Tunataka kweli wazanzibar wafunguliwe kutoka minyororo ya watanganyika wawe huru
Zitaje hizo rasilimali.

mbona Mimi naona kama Zanzibar ndiyo mnanufaika sana na huu muungano wa kiduwanzi??
Sikiliza hiyo video ya kwanza imefafanua kila kitu mkuu.
 
Mkuu

Mkuu hatutaki kufanya jambo hili kinafiki. Tunataka kweli wazanzibar wafunguliwe kutoka minyororo ya watanganyika wawe huru

Sikiliza hiyo video ya kwanza imefafanua kila kitu mkuu.
Na sisi Watanganyika tunataka Tanganyika yetu, tumechoka. Muungane ufe TU, Kila mtu abaki na chake. Sioni faida yoyote ya Muungano
 
Na sisi Watanganyika tunataka Tanganyika yetu, tumechoka. Muungane ufe TU, Kila mtu abaki na chake. Sioni faida yoyote ya Muungano
Hiyo itakuwa sawa mkuu. Basi tuungane pamoja tupaaze sauti zetu Zanzibar ikombolewe kutoka ukoloni wa Tanganyika. Na tujitoe kweli kweli; kupigania uhuru sio jambo jepesi.
 
Ukisikiliza kilio cha wazanzibar kuhusu unyanyasaji wanaoupata ndani ya muungano huu usioeleweka, ni kama vile Tanganyika imeikalia Zanzibar kimabavu. Ni ukweli usiopingika kwamba wazanzibar wanapata taabu sana na huu muungano. Tangu Nyerere alipomrubuni Karume na kufanikiwa kuikalia Zanzibar kimabavu, kimekuwa ni kilio kisichoisha cha wazanzibar kwa jinsi nchi yao ilivyogeuzwa kuwa koloni la Tanganyika. Ushahidi upo wazi wala huhitaji kufanya utafiti kujua ni kiasi gani wazanzibar wamegeuzwa watwana wa watanganyika. Kila kona ya Zanzibar kilio ni hiki hiki.

Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?

MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.

Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.

Pia soma: Wazanzibar: Muungano unatuumiza, unatupausha!

Badala ya kushukuru jinsi watanganyika wanavyowafanya mjiite wazanzibar, kazi kulalamika tu. Kwa taarifa yenu, nje ya muungano hakutakuwa na kitu kinachoitwa Zanzibar (in mwl. Nyerere tone). Ni muungano tu ndiyo unaowafanya mjihisi mko pamoja. Lakini ndani kwa ndani Zanzibar wana uadui au bifu kati ya hizo pande mbili kuliko wengi wanavyojua. Wakongwe tunajua, muda mfupi baada ya muungano kufa, majuma machache yatapita na Zanzibar pia itakufa. Huo ndiyo ukweli ambao wengi hawaujui.
 
Ukisikiliza kilio cha wazanzibar kuhusu unyanyasaji wanaoupata ndani ya muungano huu usioeleweka, ni kama vile Tanganyika imeikalia Zanzibar kimabavu. Ni ukweli usiopingika kwamba wazanzibar wanapata taabu sana na huu muungano. Tangu Nyerere alipomrubuni Karume na kufanikiwa kuikalia Zanzibar kimabavu, kimekuwa ni kilio kisichoisha cha wazanzibar kwa jinsi nchi yao ilivyogeuzwa kuwa koloni la Tanganyika. Ushahidi upo wazi wala huhitaji kufanya utafiti kujua ni kiasi gani wazanzibar wamegeuzwa watwana wa watanganyika. Kila kona ya Zanzibar kilio ni hiki hiki.

Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?

MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.

Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.

Pia soma: Wazanzibar: Muungano unatuumiza, unatupausha!
Mbona waukumbatia!sisi wa bara hatuutaki kabisa tuuvunje tu unatupa hasara kubwa.
 
Samia kuwa muislamu maana yake ni kwamba kwa kuwa waislamu hawapendi dhulma hatakubali kuiona Tanganyika ikiidhulumu Zanzibar kwa kuikalia kimabavu. Hii ndiyoilikuwa hojja yangu. You missed my point somewhat.
Hii ya kwamba waislam hawapendi dhuluma umeipata wapi? Ninavyojua waarabu karibu wote ni waislam. Watumwa toka Africa waliopelekwa uarabuni wakiwa wamefungwa minyororo hawakuhasiwa? Wasichana waafrika wanaolaghaiwa kwenda kufanya kazi za ndani huko wanafanywaje? (Samahani nimeenda nje ya mada)
 
Samia kuwa muislamu maana yake ni kwamba kwa kuwa waislamu hawapendi dhulma hatakubali kuiona Tanganyika ikiidhulumu Zanzibar kwa kuikalia kimabavu. Hii ndiyoilikuwa hojja yangu. You missed my point somewhat.
Hii ya kwamba waislam hawapendi dhuluma umeipata wapi? Ninavyojua waarabu karibu wote ni waislam. Watumwa toka Africa waliopelekwa uarabuni wakiwa wamefungwa minyororo hawakuhasiwa? Wasichana waafrika wanaolaghaiwa kwenda kufanya kazi za ndani huko wanafanywaje? (Samahani nimeenda nje ya mada)
 
Nyinyi namhusika kwenye unyonyaji wa rasilimali za Zanzibar ndio maana hamtaki kuvunja ili muendelee kufisidi rasilimali za watu wa Pemba na Unguja. Mungu anawaona.
Zanzibar kuna nini? Hapo kungekua hata na mafuta tu muungano ingeshakufa kitambo, hao watu ni wachoyo vibaya sana
 
kuwa raisi hakukuteshelezi kuwa na mamlaka ya hayo, TISS munayo nyinyi, JWTZ munalo nyinyi, zaidi 90% ya viongozi wa CCM, CHADEMA, Serikali yote kuanzia Bunge, Mahakama, mawaziri munavyo nyinyi. Kwanini yeye wakati nyinyi ndio wenye nguvu?
hao tiss na jwtz vinaongozwa na nani?nani amiri jeshi mkuu?au unatafuta mtu wa kumtupia lawama tu mkuu
 
Back
Top Bottom