tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 22,093
- 18,705
Ukisikiliza kilio cha wazanzibar kuhusu unyanyasaji wanaoupata ndani ya muungano huu usioeleweka, ni kama vile Tanganyika imeikalia Zanzibar kimabavu. Ni ukweli usiopingika kwamba wazanzibar wanapata taabu sana na huu muungano. Tangu Nyerere alipomrubuni Karume na kufanikiwa kuikalia Zanzibar kimabavu, kimekuwa ni kilio kisichoisha cha wazanzibar kwa jinsi nchi yao ilivyogeuzwa kuwa koloni la Tanganyika. Ushahidi upo wazi wala huhitaji kufanya utafiti kujua ni kiasi gani wazanzibar wamegeuzwa watwana wa watanganyika. Kila kona ya Zanzibar kilio ni hiki hiki.
Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?
MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.
Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.
Pia soma: Wazanzibar: Muungano unatuumiza, unatupausha!
Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?
MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.
Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.
Pia soma: Wazanzibar: Muungano unatuumiza, unatupausha!