Ni lini Tanganyika itaacha kuikalia Zanzibar kimabavu?

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
22,093
18,705
Ukisikiliza kilio cha wazanzibar kuhusu unyanyasaji wanaoupata ndani ya muungano huu usioeleweka, ni kama vile Tanganyika imeikalia Zanzibar kimabavu. Ni ukweli usiopingika kwamba wazanzibar wanapata taabu sana na huu muungano. Tangu Nyerere alipomrubuni Karume na kufanikiwa kuikalia Zanzibar kimabavu, kimekuwa ni kilio kisichoisha cha wazanzibar kwa jinsi nchi yao ilivyogeuzwa kuwa koloni la Tanganyika. Ushahidi upo wazi wala huhitaji kufanya utafiti kujua ni kiasi gani wazanzibar wamegeuzwa watwana wa watanganyika. Kila kona ya Zanzibar kilio ni hiki hiki.

Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?

MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.

Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.

Pia soma: Wazanzibar: Muungano unatuumiza, unatupausha!


 
Ukisikiliza kilio cha wazanzibar kuhusu unyanyasaji wanaoupata ndani ya muungano huu usioeleweka, ni kama vile Tanganyika imeikalia Zanzibar kimabavu. Ni ukweli usiopingika kwamba wazanzibar wanapata taabu sana na huu muungano. Tangu Nyerere alipomrubuni Karume na kufanikiwa kuikalia Zanzibar kimabavu, kimekuwa ni kilio kisichoisha cha wazanzibar kwa jinsi nchi yao ilivyogeuzwa kuwa koloni la Tanganyika. Ushahidi upo wazi wala huhitaji kufanya utafiti kujua ni kiasi gani wazanzibar wamegeuzwa watwana wa watanganyika. Kila kona ya Zanzibar kilio ni hiki hiki.

View attachment 2982736
Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?

View attachment 2982739
MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.

Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.
Chochea kuni ili maharage yaive haraka.
 
Tatizo ni viongozi wa zanzibar wanajua muungano ukivunjika hawatakuwa madarakani.
Muungano ukifa na neno Mapinduzi Daima lazima litafutika.
Naamini muda si mrefu huu muungano kama sio utakufa basi muundo wake utabadilishwa
 
Tatizo ni viongozi wa zanzibar wanajua muungano ukivunjika hawatakuwa madarakani.
Muungano ukifa na neno Mapinduzi Daima lazima litafutika.
Naamini muda si mrefu huu muungano kama sio utakufa basi muundo wake utabadilishwa
Tiba ni kuifanya hii nchi ya Tanzania iwe moja.Jina Zanzibar lifutike kiaina kama jina Tanganyika lilivyofutika kiaina.Au kuwe na Serikali tatu ambayo itatambua Zanzibar kama Jamhuri na vile vile Tanganyika kama Jamhuri ili kila watu wafaidi matunda ya kwao.
 
Aya yako inayoeleza maoni yako ndo imeharibu andiko lako mkuu, Samia being mzazibari and muislam haimaanishi anaweza kufanya unayoyataka wewe. Ungeleta hoja zenye mashiko mezani sio kuonyesha ukiritimba wako
Samia kuwa muislamu maana yake ni kwamba kwa kuwa waislamu hawapendi dhulma hatakubali kuiona Tanganyika ikiidhulumu Zanzibar kwa kuikalia kimabavu. Hii ndiyoilikuwa hojja yangu. You missed my point somewhat.
 
Wakubali zanzibar iwe wilaya ya kibiti au kila mtu afe na chake,kuliko huu upuuzi unaoendelea sasa ivi
Kweli kabisa mkuu. Halafu wananchi hawapendi kabisa huu ujinga ila viongozi wao ndio wanawaauza kwa sababu za uchu wa madaraka na kutunisha matumbo yao binafsi.
 
Kila kitu kina mazuri na mabaya yake.
Hata hivyo, mazuri (faida)lazima yawe makubwa kuliko mabaya (hasara).
Hatutakiwi kuangalia upande mmoja tu.
Raia wa Zanzibar wana faida za kiuchumi na kijamii kubwa katika Muungano.
Kelele za kisiasa, vyeo na mamlaka havizidi uzito wa faida za kiuchumi na kijamii kwa raia wote.
 
Ukisikiliza kilio cha wazanzibar kuhusu unyanyasaji wanaoupata ndani ya muungano huu usioeleweka, ni kama vile Tanganyika imeikalia Zanzibar kimabavu. Ni ukweli usiopingika kwamba wazanzibar wanapata taabu sana na huu muungano. Tangu Nyerere alipomrubuni Karume na kufanikiwa kuikalia Zanzibar kimabavu, kimekuwa ni kilio kisichoisha cha wazanzibar kwa jinsi nchi yao ilivyogeuzwa kuwa koloni la Tanganyika. Ushahidi upo wazi wala huhitaji kufanya utafiti kujua ni kiasi gani wazanzibar wamegeuzwa watwana wa watanganyika. Kila kona ya Zanzibar kilio ni hiki hiki.

View attachment 2982736
Ni bahati mbaya kwamba kilo hiki kimekuwa cha muda mrefu lakini viongozi wa wazanzibar wamegeuka kuwa Chifu Mangungo wa Msovero kwa kukubali kuiuza nchi yao kwa watawala wa Tanganyika kwa sababu ya uroho wa fedha. Yuda alimuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha lakini viongozi wa wazanzibar wameiuza nchi yao kwa mkoloni Tanganyika kwa vipande 3 tu vya fedha. Hivi ni lini Tanganyika itakoma kuikalia Zanzibar kimabavu?

View attachment 2982739
MAONI YANGU
Mama Samia wewe ni mzanzibar na muislamu safi. Waislamu hawapendi dhulma. Tafadhali fanya jambo kuinasua nchi yako kutoka kwenye makucha ya Tanganyika. Au nawe umenogewa na vipande 30 vya fedha na kuwaacha wazanzibar wenzako wakiangamia? Jitihada zako za kuikwamua Zanzibar kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi (Tanganyika) ndizo zikazotoa mwanga wa Zanzibar kujikomboa kiutawala, kiuchumi na kimaendeleo.

Mungu ibariki Zanzbar, Mungu ikomboe Zanzibar.

Pia soma: Wazanzibar: Muungano unatuumiza, unatupausha!
Kwa jinsi awamu hii ilivyokula hela za tanzagiza hao wasiachwe mpaka mwisho
 
Back
Top Bottom