Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
VIGOGO wapatao 60 wataanza kukaguliwa mali zao ili kuweza kuhakiki mali hizo walivyozipata ikiwa ni mchakato ulioundwa na serikali kukagua viongozi wote wa watumishi wa Umma wa nchini |
Mchakato huo utaanza Februari 20 mwaka huu na kumalizika mapema Machi, ambapo Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma wataendesha zoezi hilo kwa vigogo hao Hiyo imekuja baada ya kurejeshwa kwa fomu za utalaji kwa viongozi wote wa watumishi wa Umma wa Serikali kukamilika Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana ,Kamishna wa Tume ya Maadili, Jaji Mstaafu Salome Kaganda alisema kuwa, uhakiki huo ni nguzo bora ya kuijenga jamii ya Watanzania, hasa viongozi wa umma katika kuishi kwa kufuata misingi ya uadilifu, iliyowekwa na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Amewataja baadhi ya viongozi watakaoanza kukaguliwa ni akiwemo Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta , Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Hawa Suluhu Mbunge John Mnyika na wengine wengi wakiwemo na wakuu wa mikoa, wilaya, MaMeya wa majiji, madiwani, wabunge na wakurugenzi wa taasisi mbalimbali za Serikali nchini. Kaganda aliwaambia wanahabari kuwa, si kwamba viongozi watakaonzwa kuhakikiwa wana kashfa wala tuhuma zozote si kweli bali ni sheria kwa viongozi kama hao kuhakikiwa mali zao na kuwaondoa hofu viogozi hao na kuwaomba ushirikiano katika zoezi hilo Amesema kuwa lengo lingine la kukagua viongozi hao ni kuboresha utumishi wa umma kwa kuwa sasa uadilifu umeonekana kushuka ikiwa na serikali kufanya utafiti wa kisheria zaidi kutaka kutenganisha biashara na uongozi Sisi tunachokiomba kutoka kwao ni kutoa ushirikiano wa kutosha kwa maofisa wetu wakati wa zoezi zima la uhakiki wa mali zao, alisema Kaganda |