Zitto Kabwe awabeza UKAWA na kuwaita "Wasaka Tonge"

Kwahiyo anafanyia yake Facebook?
Haya tufanye anatetea maslahi ya wananchi, na wasakatonge wanagawana vyeo, si ndio angewaacha wasinzie ili yeye apate crédit mwenyewe kwa juhudi zake ili mwisho wa siku actions zake ziwe louder kuliko maneno ya Facebook au ya wasaka tonge? Au anataka wamsaidie baada ya kugundua kelele zake pekee kama za matrilion ya Uswis hazina mashiko.
Namuhurumia sana dogo.

Zitto anasumbuliwa na ugonjwa wa 'egocentrism' (mimi, mimi, mimi mimi ndio mwanzo ndio mwisho!!). Sifa zote za mapambano dhidi ya ufisadi ni zangu na sio zetu! Mfumo wa utawala wa sasa na ambao umehifadhiwa katika katiba inayopendekezwa ndio MUUNDOMBINU MKUU wa UFISADI ambao ndio unaosababisha haya yote ambayo Zitto anadai kupigania (kama kweli anafanya hivyo kwa dhati na si kwa chati. Lakini tu-assume anayapigania kwa dhati). UKAWA walichokifanya kuanzia kususia mchakato chakachuzi wa katiba mpya hadi leo kuamua kuunganisha nguvu dhidi ya CCM lengo ni kuvunjilia mbali ama kufumua huu MUUNDOMBINU FASIDI na kujeanga MUUNDOMBINU mpya unaojali ustawi wa jamii kwa jumla. Kubeza juhudi za UKAWA ni ama kuonesha welewa mdogo ama kudhihirisha kuwa hata hicho anachodai anakipigania ni kwa chati tu. UKAWA wanafanya jitihada za kung'oa mizizi, yeye anajidai kupukutisha majani alimradi watu wote wamsifie yeye tu! Akawanadanganye akina Mtela na Juliana (wasomi wa UDSM wanaosumbuliwa na njaa za mjini)- maana nikisema akawadanganye wakulima na wavuvi Kigoma nitakuwa nawaonea. Nao pia wameishatambua haki zao na utapeli wa 'egotist' kama yeye.
UKAWA
TUMAINI LETU!
 
Kwa kweli Mtatiro kajibu kwa busara sana. Huhitaju ku blast mtu...


Alipomwambia ''Julius Mtatiro niache nifanye yangu'' nae akamjibu ''Unajua mjadala huu wa sasa umekuja kwa sababu #undelea uliacha #hayo #unayoyaita #yako, ukaja kutoa mawazo yako kuhusu #UKAWA''

Mpaka hapo nimemkubali Mtatiro kwa majibu aliyotoa kama hayajamuingia kutakua na tatizo na amemkumbusha kua "kuteleza si kuanguka'' ​
 
Copied Kutoka kwenye ukurasa wake wa INSTAGRAM;


"Taifa limevimba. Wakulima Mahindi yanawaozea na Mpunga bei imeporomoka sababu ya mchele kutoka nje na usiolipiwa Kodi. Wahisani wamezuia misaada ( sababu ya kashfa ya #TegetaEscrow ) Kiasi Serikali haiwezi hata kujiendesha. Unapoona wanasiasa wanagawana vyeo katika nyakati kama hizi ujue Taifa halina Viongozi bali wasaka utawala. Wasaka utawala badala ya uongozi ni #WasakaTonge tu"

attachment.php


My Take;
Jamaa ameamua kuwa mpinzani ndani ya upinzani..Kina kinana na nape hawaoni?!!!

Mara zote Zitto Kabwe ni mbinafsi. Ni mwanasiasa kijana anayependa kufanya kazi kwa ubinafsi bila kujali ushirikiano. Ni kweli kuwa Taifa lipo kwenye matatizo makubwa kwa sasa, lakini umoja huu wa vyama vya upinzani ni muhimu katika kupambana na CCM na vibaraka wake. Zitto ni mwanasiasa aliyefilisika kwasasa, siasa zake za ubinafsi zimefikia kikimo.
 
Mnyonge zitto anajiskia...anaona katengwa kwenye harakati ambazo yy pia aliziibua...mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
 
Huyu dogo ni wa kupuuzwa tu,viongozi wa UKAWA wampuuze kwani anataka kick tu kisiasa baada ya media kumpuuza
 
Zito amekuwa kama kinyonga. Naona anguko lake limekaribia. Wanasiasa kama zito hawafai katika hii nchi.
 
Yani ukweli siku hizi ni dhihaka? Ameongea ukweli UKAWA ni genge la wasaka madaraka!
Kilicho nichekesha zaidi Lema kuwa waziri wa mambo ya ndani!

Hiyo ni safu yenu ACT na CCM, UKAWA tuna lengo moja kuu kuing'oa CCM madarakani. Ndio maana CCM na washirika wao wanalia kitendo cha UKAWA kufanikiwa.
 
Kwa Tamaa za viongozi wa Tanzania huo Muungano wa Ukawa ni njozi za alinacha, naona bora ya Zitto, hii nchi bana, mi nishanyoosha Mikono it's better kufanya yako tu
 
Mmeguswa wasaka tonge, mmeshindwa kujadiri katiba sababu ya uchu madaraka. Katiba inamambo mengi mmetoka kisa mgawano wa madaraka, wasaka tonge nyie! Mmeshindwa kuongea hoja zenu bungeni, huku kwa wananchi mtaongea jipya gani.
 
Kufuatia Mh zitto kuwakebehi wanaukawa kuwa ni wasaka tonge, Julius mtatiro amemjia juu na kumuambia kuwa ameteleza. Hivi ndivyo ilivyokuwa.
Huyu ndio Mtatiro
MTATIRO

ZITTO AMETELEZA!

Hii habari ya Zitto kuwaita viongozi wa UKAWA kuwa ni "‪#‎wasakatonge‬" ni ya Ukweli ? is it the real Zitto Kabwe au imetumika ile akaunti feki ambayo wajanja huitumia kujidai wanatoa mikopo ya kitapeli kwa jina lake?

Kama ni yeye kweli na ni akaunti yake "it means, there is something wrong somewhere" (Kuna tatizo mahali). Nimjuavyo Zitto mara nyingi masuala ambayo anaona hayafahamu vizuri walau hukaa kimya.

Mtizamo wangu ni kuwa walau kwa sasa ‪#‎UKAWA‬ ina maana kubwa kwa watanzania na yeyote(hasa mpinzani) ambaye ataidharau anaweza kudharaulika mara mia moja. Ushirikiano wa UKAWA unaitikisa CCM na lazima utapunguza kasi ya ushindi wa CCM katika maeneo yote ya nchi, na hicho ndicho wananchi wanataka. Natabiri kuwa, chama chochote cha siasa kisicho CCM kitakachojitokeza hadharani kupambana na nguvu hi i‪#‎kitaaibishwa‬ vibaya.

‪#‎KUSHINDANA‬ ‪#‎NA‬ #UKAWA ‪#‎NI‬ #KUSHINDANA #NA ‪#‎MIOYO‬ ‪#‎YA‬‪#‎WATANZANIA‬ ‪#‎WALIOICHOKA‬ ‪#‎CCM‬.

Standup brother ‪#‎Zitto‬ ‪#‎Kabwe‬, kuteleza si kuanguka.
ZITTO

Julius Mtatiro niache nifanye yangu. Nina kazi ya kufanya kusimamia Mali za Watanzania. Wengine nao wana kazi yao ya kugawana vyeo. Kwangu Mimi kwa sasa muhimu ni kuokoa Fedha za Wafanyakazi kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kuokoa Wakulima ambao Mahindi yao hayana soko, kuokoa NBC na kuhakikisha wezi wa escrow wanakamatwa.

Tugawane majukumu tu - wengine wagawane vyeo wengine waiwajibishe Serikali


MTATIRO

Zitto Kabwe hakika hakuna shaka juu ya mchango wako kwa mabadiliko katika nchi yetu, kusimamia rasilimali za umma zitumike kuwanufaisha wananchi na kupambana dhidi ya wizi na ubadhirifu...from#Buzwagi to madudu kibao tu uliyoyasimamia.

Unajua mjadala huu wa sasa umekuja kwa sababu #undelea uliacha #hayo #unayoyaita #yako, ukaja kutoa mawazo yako kuhusu #UKAWA. Na sie wengine pia tunatoa mawazo yetu juu ya UKAWA lakini kwa kutofautiana na wewe kidogo tu, najua ni mitizamo na mwisho wa siku kila mtu anaendelea kusimamia anachokiamini.

Kwa hakika ambacho haupaswi kusahau ni kuwa hayo unayoyapigania leo, uwajibikaji, kuhakikisha wananchi wanauza mahindi katika soko la uhakika na bila vikwazo, ufisadi n.k. ni masuala ambayo yamepiganiwa na watu wengi tangu zamani mno na wapo watakaopigana baada yako na wapo wanaopigana hivi sasa kama wewe. Kujaribu kuonesha umma kuwa kuna viongozi wanagawna vyeo mahali siyo jambo sahihi hata kidogo.

Natambua wewe ni mpinzani imara, lakini siku za usoni hautakwepa dhana ya upinzani kufanya kazi pamoja, na ndiyo hii ambayo imeanza sasa. Badala ya kutumia nguvu kubwa kujaribu kuonesha kuwa kinachofanywa na UKAWA ni kugawana vyeo ni bora utumie muda huo kupambana na yale uyaitayo "yako" na kuyaacha haya mengine wenye nayo wayafanyie kazi.

Jambo la pili ni kuwa, ukianza kuwashambulia viongozi wa vyama vya upinzani kwa ujumla namna hiyo na kuwaita #WASAKA#TONGE na #WAGAWANA #VYEO huku wao wakiwa wamekukalia kimya nadhani wanaweza pia kukujibu, na kwa sasa wao ni wengi na wewe ni mmoja, kwa vyovyote vile nyote mtasikika lakini wao watasikika zaidi.

Kwa maoni yangu, huu ni muda wa kukaa kimya na kutizama na kutoongeza malumbano dhidi yako na vyama vya upinzani kwa ujumla. Maana ukiniambia #Maalim#Seif ni msaka tonge sikuelewi, ukiniambia #Lipumba ni msaka tonge sikuelewi, maana nimefanya nao kazi kwa karibu sana.

Hadi leo Maalim Seif ndo anajenga nyumba yake, Lipumba hana hata duka. Pamoja na mapungufu ya kibinadamu ya kila mmoja wetu lakini they dont deserve to be called #WASAKA #TONGE .....I strongly advice you either to keep quite on UKAWA...or JOIN THE TEAM......Sisi wakristo tunafundishwa kuwa "HAKUNA VUGUVUGU, KUNA MOTO NA BARIDI" .

Siamini kama kweli Zitto amehama Reli kiasi hiki, kuna wakati niliamini labda anaonewa ila kwa sasa nimebadili kila kitu kuhusu yeye.
 
Last edited by a moderator:
Huyu ndio Mtatiro


MTATIRO



Siamini kama kweli Zitto amehama Reli kiasi hiki, kuna wakati niliamini labda anaonewa ila kwa sasa nimebadili kila kitu kuhusu yeye.

Sasa mnaweza kuona kabisa kuwa busara,hekima na hata uongozi bora havipatikani kwa elimu ya darasani peke yake. Kwa jinsi chadema walivyomlea huyu kijana Zitto na kuweka matumaini makubwa kwake hakutegemewa kwa aliyoyafanya. Chadema wataishi kukumbuka tahadhari nyingi alizokuwa akitoa mama Zitto kumhusu mwanae. Kwa intelijensia ya chama ilivyokuwa ikiona mbali ndivyo walivyokuwa wakimuonya huyu kijana wakitegemea abadilike.Kwa kijana alietoka familia hizi masikini na ka elimu ka chuo na kwa madaraka aliyokuwa nayo kwa umri mdogo vile ikawa rahisi kutumika kwa hela kukisaliti chama na matokeo ni haya. Angekuwa na busara angejinyamazia kimya kwani hata hayo anayodai anawafanyia wananchi bado anayafanya kwa tiketi ya ukawa. Siku hukumu ya kesi yake na chadema ikiisha mahakamani ndio mwisho wake. Atasimama kwa chama kipi aweze kuupata tena ubunge? Enzi hizo akitishia atagombea Geita na bado wana Kigoma wakaendelea kumpa kura hakujua alikuwa anatembelea nyota ya chadema.Hana uwezo wa kusimama kama mgombea binafsi na kushinda.Kwa mara nyingine tena alishawaaga wapiga kura wake kuwa atagombea uraisi na ikishindikana ataenda kufundisha.
 
Back
Top Bottom