Zitto alia na Mzumbe kuzuia mjadala wa madini

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Zitto alia na Mzumbe kuzuia mjadala wa madini

na Nasra Abdalah, Morogoro

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amelaani kitendo cha uongozi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe kuzuia kufanyika mjadala wa kitaifa juu ya sekta ya madini na kusema jambo hilo ni aibu kwa taifa.

Mjadala huo uliodhamiwa na Kampuni ya Capital Promoters ulitarajiwa kufanyika jana, chuoni Mzumbe baada ya kufanyika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine cha Mwanza.

Kwa mujibu wa tamko lake la kwa vyombo vya habari ‘kulaani utawala wa chuo hicho kuzuia mjadala wa madini kufanyika chuoni’, mbunge huyo alisema jambo hilo limemshtua kwani anaamini kuwa mjadala huo ungechochea majadiliano kwa jamii ya wanazuoni kwa lengo la kuibadili sekta hiyo ili kuinufaisha jamii.

“Nimeshtushwa na uamuzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe wa kuzuia mdahalo huu katika eneo la chuo, kwani mjadala huu unachochea majadiliano kwa jamii ya wanazuoni ili kuibadili sekta ya madini iweze kufaidisha maisha ya Watanzania,” alisema katika tamko lake.

Zitto katika alisema jambo linalofanya maamuzi hayo ya chuo kuwa ya ajabu na aibu kwa taifa linatokana na ripoti ya hivi karibuni ya Action Aid iliyoitwa ‘Breaking the Curse’, iliyothibitisha namna ambavyo nchi za Kiafrika zisivyofaidi sekta ya madini, Tanzania ikiwa ni miongoni.

Alisema baada ya Shirika hilo kutoa ripoti hiyo na mapendekezo yake kwa mabunge na serikali, kampuni za madini zimepinga na sasa zimejitokeza na kufanya majadiliano ya wazi juu ya sekta hiyo jambo ambalo awali halikufanyika.

“Hivyo mjadala umekuwa wa pande zote, ndiyo maana wanazuoni kama wadau walipaswa kutilia maanani mijadala hii, hivyo Chuo Kikuu kuzuia mjadala wa sekta nyeti na yenye malalamiko makubwa kama hii ni jambo la ajabu na aibu kwa Taifa,” alisema.

Akimnukuu hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, katika hotuba yake Chuo Kikuu cha Dar es Salaam aliyoiita ‘Jukumu la Vyuo Vikuu’, mwaka 1966 alisema chuo chenye wanafunzi na wahadhiri wake wasioshiriki mijadala hakina faida kwa jamii.

Zitto aliwapa pole wanafunzi hao waliojiandaa kushiriki mdahalo huo na kusema kitendo kilichofanywa na utawala wa chuo hicho unatakiwa kulaaniwa na kwamba kitendo hicho kinadhihirisha taarifa iliyotolewa hivi karibuni kuwa zaidi ya wahadhiri wake 15 wamepata shahada zao za uzamivu katika vyuo visivyotambuliwa.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni Capital Promoters International (CPI) ambayo imedhamini mdahalo huo, Gabriel Nderumaki, alieleza kusikitishwa kwa mkutano huo kuzuiwa kwani kampuni yake ilikuwa imetumia kiasi cha sh milioni 20 kwa ajili ya maandalizi.

Alisema taarifa za kuzuiliwa kwa mkutano walizipata juzi jioni wakati wakiwa hatua za mwisho za maandalizi, muda ambao umekuwa mgumu kwao kuwaarifu wawezeshaji ili kuairisha mdahalo huo.
 
kuna mambo mengi hapa!


Capital Promoters International (CPI) - ndio kampuni gani hii! Je mahusiano yake na sekta ya madini ni yapi? Kwanini inaandaa mijadala mavyuoni?

Je ni riporti tu ya Breaking the Curse tu iliyofanya Mzumbe ikatae huo mjadala? Ama kunataratibu nyingine ambazo hazikufuatwa!
 
Asipoteze lengo.......atujibu ya Dowans mbona anarukia mengine haya hajamaliza?

....
 
DOGO MNYOKA UPO??? naona kaupepo ka mabadiliko kanapiga mpaka puani.... husikiki kabisa ndugu yetu??
 
Kuna haja ya kupeleka majadiliano kama haya vyuo vyote nchini ili information ziweze kusambaa vizuri nchi nzima na kuwajenga wanazuoni kuchambua issues na kutafuta suluhu
 
Naye Mkurugenzi wa Kampuni Capital Promoters International (CPI) ambayo imedhamini mdahalo huo, Gabriel Nderumaki, alieleza kusikitishwa kwa mkutano huo kuzuiwa kwani kampuni yake ilikuwa imetumia kiasi cha sh milioni 20 kwa ajili ya maandalizi.
Pesa hizi ni kwa ajili ya maslahi ya taifa au kuna jambo? Zitto you are too smart brother, please quit these cheap games.
 
Kama kweli Zitto kabwe ni mzalendo wa kweli na mtaifa kama anavyodai anapigania maslahi ya Taifa aje na atueleze ni maslahi gani alikuwa anapigania DOWANS. Inawezekana wasomi wanamkimbiza kiani baada ya kugundua hana lolote jipya naye ni walewale tu. Msema kweli ni kama Slaa ageukigeuki haogopi media wala wananchi wake.

Tangia Zitto amelikoroga anajifanya kakakuona. Nanyi wana Chadema wenzangu lazima mjue kuwa chama si kwa ajii ya kubeba uozo na si mtu mmoja ila ni wananchi na misingi inayoeleweka. sisi washika pembe tumechoka siasa za kulindana kwa ajili ya kupata millioni saba. Tunataka ukweli na haki.

Mnyika mwache Zitto atueleze kwanza ya Dowans sio kuleta topic za kiujanja ujanja ili tusahau aliyoyafanya, Hatukubali kurudia makosa ya serikali ya CCm ambayo ilitumia kufunika kombe la babu na kulea majipu.Sasa yameanza kupasuka na maradhi yanatapakaa kwa kasi.
 
Kama kweli Zitto kabwe ni mzalendo wa kweli na mtaifa kama anavyodai anapigania maslahi ya Taifa aje na atueleze ni maslahi gani alikuwa anapigania DOWANS. Inawezekana wasomi wanamkimbiza kiani baada ya kugundua hana lolote jipya naye ni walewale tu. Msema kweli ni kama Slaa ageukigeuki haogopi media wala wananchi wake.

Tangia Zitto amelikoroga anajifanya kakakuona. Nanyi wana Chadema wenzangu lazima mjue kuwa chama si kwa ajii ya kubeba uozo na si mtu mmoja ila ni wananchi na misingi inayoeleweka. sisi washika pembe tumechoka siasa za kulindana kwa ajili ya kupata millioni saba. Tunataka ukweli na haki.

Mnyika mwache Zitto atueleze kwanza ya Dowans sio kuleta topic za kiujanja ujanja ili tusahau aliyoyafanya, Hatukubali kurudia makosa ya serikali ya CCm ambayo ilitumia kufunika kombe la babu na kulea majipu.Sasa yameanza kupasuka na maradhi yanatapakaa kwa kasi.
\

Sidhani KAMA wanachuo wa mzumbe wana akili mgando kama VC wao....Pamoja na hivyo wangetakiwa wa stand up ili kuonesha kuwa wao hawawezi kuburuzwa!!!

nadhani VC mzumbe anataka kuwapelekea wanamzumbe waandamane kuunga mkono....KIKWETE TENA CAMPAGNE!!!!
 
Kama kweli Zitto kabwe ni mzalendo wa kweli na mtaifa kama anavyodai anapigania maslahi ya Taifa aje na atueleze ni maslahi gani alikuwa anapigania DOWANS. Inawezekana wasomi wanamkimbiza kiani baada ya kugundua hana lolote jipya naye ni walewale tu. Msema kweli ni kama Slaa ageukigeuki haogopi media wala wananchi wake.

Tangia Zitto amelikoroga anajifanya kakakuona. Nanyi wana Chadema wenzangu lazima mjue kuwa chama si kwa ajii ya kubeba uozo na si mtu mmoja ila ni wananchi na misingi inayoeleweka. sisi washika pembe tumechoka siasa za kulindana kwa ajili ya kupata millioni saba. Tunataka ukweli na haki.

Mnyika mwache Zitto atueleze kwanza ya Dowans sio kuleta topic za kiujanja ujanja ili tusahau aliyoyafanya, Hatukubali kurudia makosa ya serikali ya CCm ambayo ilitumia kufunika kombe la babu na kulea majipu.Sasa yameanza kupasuka na maradhi yanatapakaa kwa kasi.

Hebu muacheni Zitto wangu, imetosha sasa. Siasa na uongozi ni zaidi ya Dowans. Mbona hamuulizi kuhusu Karamagi na Buzwagi? Ameshaweka msimamo wake wazi, na sasa ni wakati wa yeye kufanya mambo mengine. Kwa hiyo wewe unaona mzumbe kuzuia kujadili huu mjadala wa madini ni poa tu kwa sababu ya mtizamo wa Zitto kuhusu Dowans. Poor you!

Asha
 
Kama kweli Zitto kabwe ni mzalendo wa kweli na mtaifa kama anavyodai anapigania maslahi ya Taifa aje na atueleze ni maslahi gani alikuwa anapigania DOWANS. Inawezekana wasomi wanamkimbiza kiani baada ya kugundua hana lolote jipya naye ni walewale tu. Msema kweli ni kama Slaa ageukigeuki haogopi media wala wananchi wake.

Tangia Zitto amelikoroga anajifanya kakakuona. Nanyi wana Chadema wenzangu lazima mjue kuwa chama si kwa ajii ya kubeba uozo na si mtu mmoja ila ni wananchi na misingi inayoeleweka. sisi washika pembe tumechoka siasa za kulindana kwa ajili ya kupata millioni saba. Tunataka ukweli na haki.

Mnyika mwache Zitto atueleze kwanza ya Dowans sio kuleta topic za kiujanja ujanja ili tusahau aliyoyafanya, Hatukubali kurudia makosa ya serikali ya CCm ambayo ilitumia kufunika kombe la babu na kulea majipu.Sasa yameanza kupasuka na maradhi yanatapakaa kwa kasi.


Kakosa posho toka kwa waandaaji ...
 
Asha thanks a lot nimependa comment yako kwa kweli.

Jamani Zitto si malaika kujikwaa imo na huenda si kwa kuchukua pesa wala kwani hatuna ushahidi wa hizo milioni sabini.

Tusonge mbele jamani kwani wote tunajuwa namna ambavyo mwananchi hanufaiki kwa lolote na madini zaidi ya kuachiwa mashimo tu which is very bad. Sielewi sababu ya Mzumbe kuzuia mdahalo lakini kiutaratibu inaonekana awali walikubali then wakageuka na hapo ndipo panapozua maswali mengi kuliko majibu. Anyway we should not give up ila kazi tunayo kubwa zaidi kuliko tunavyofikiri.
 
upinzani wa sasa hivi ulikuwa ni mwepesi kuliko wa kipindi cha nyuma, wakati mrema alipokuwa kwenye peak na ccm ilikuwa united, sasa ccm inaanza kuwa na makundi na upinzanin nao unakosa msimamona hata ule mdogo uliokuwepo sasan unalegalega,
huo mjadala wa madini kwenye vyuo vikuu hauna maana yoyote, ulipofanyika pale chuo kikuu nini zilikuwa outcomes zake, miminadhani zitto asimameme mbele ya watu na kutueleza misimamo yake na sio kuanzisha mijadala isiyokuwa na maana yoyote
hao wakuu wa vyuo vikuu wana haki ya kumkataa zitto pamoja na hiyo kampuni yake(capital) kwani washamuona ni m2 asiye na misimamo na yupo kwa maslahi ya mafisadi,
 
Jamani kwa anae fahamu vizuri chuo cha mzumbe asishangae haya. Mzumbe ni maalumu kufundisha/kupika viongozi wa CCM wale ambao hawakuwa na sifa hata za kuwa admitted. Sasa wakiruhusu mijadala kama hiyo wanawakosea wakubwa, angalia chuo hicho kilivyo pata usajili kuwa university, ni uhuni tu chuo hakina ofisi za walimu halafu unasema university?? lakini kwa sababu kiliandaliwa mahsusi kwa ajili ya kutoa shahada kwa wakubwa ili mkate wao serikalini uendelee kupakwa siagi ndo hayo sasa.

Sidhani kama chuo kikuu unaweza kupita kwenye barabara zake ukakuta mtu amevunja chungu na takataka zingine kwenye makutano ati anatambika halafu utegemee mabadiliko (japo kuwa siamini ushirikina) lakini mambo haya mzumbe yapo ingawa kuna mwalimu mmoja alitoa shutuma hizo na baadaye akafukuzwa kazi mwaka jana.

Kuhusu mjadala wa madini, mi nadhani zitto lengo lake ni zuri ila najua uongozi wa chuo uliogopa kwa sababu maazimio ambayo yangepitishwa ingeonekana uongozi umebariki, na kufanya hivyo ni kukiuka matakwa ya serikali fisadi.
 

...jamani muwe fair basi angalau kidogo. kuna mengi mazuri Mh. Zitto Kabwe aliyoyaibua katika kusaidia maslahi ya taifa hili. Maoni yake, hata kama hayakutupendeza wengi ni uthibitisho tosha wa ukomavu wake kisiasa. kwamba kiongozi mzuri ni yule ambaye atasimamia maoni yake hata kama hayatafurahisha wengi, kwa kuamini kwamba historia ndiyo itayokuja kumuhukumu iliyokuwa nia yake.

Mh. JK katika jambo alilolishupalia sana wakati anaingia madarakani, ni kusimamia maslahi ya taifa kuhusiana na mikataba ya madini. Tunakumbuka Mh. Zitto alivyoliibua lile la Bw. Karamagi kule London. Leo serikali ya Mh. Kikwete inasua sua kupeleka Bungeni mapendekezo ya tume ya Jaji Bomani? pamoja na u advocate kwa utawala wa sheria, Mh.Rais tafadhali ingilia kati suala hili tena... NCHI INALIWA! ulishawahi nawe kuwa kwenye Wizara hiyo, ukweli unaujua,..nia ushaisema, kusuasua kwa faida ya nani? huogopi historia itapokuja kukuhukumu?

Nchi inavyotafunwa

2009-04-05 12:41:01
Na Abdallah Bawazir

Tanzania inaendelea kupoteza mamilioni ya fedha kutokana na serikali kusuasua kupeleka bungeni muswada wa sheria itakayoongoza sekta hiyo nchini.

soma; Nchi inavyotafunwa
 
Tanzania inataka utawala mbadala kuliko huu uliopo kwa sasa, Utawala wa CCM umemletea Mtanzania machungu mengi na kujenga matabaka makubwa ya kijamii. Sio tu yale matabaka ya kiuchumi bali kihali, cheo, na elimu ni matabaka ambayo yanamwacha mtanzania asijue la kufanya.
Haya yote hayakushuka kama jua au mvua bali yalianza taratibu, yalianza kwa wananchi kuamini viongozi wao, walikuwa hawahoji kitu, wakijaribu walishukiwa kama mwewe na kifaranga, ilikuwa zidumu fikra sahihi. Kiongozi alionekana Mungu Mtu na rushwa ilibarikiwa ikawa kama ni chai, takrima, ni kitu cha kawaida.

Maamuzi mengi yaliyotolewa na tuliowaamini, na kukatazwa tusihoji, tusiulize ndio yaliyotufikisha hapa.
Ni jambo la kawaida kwa serikali ya CCM kumhamisha mtu au kumpa mtu ubalozi pale anapoharibu, iba au kula rushwa na kusababisha kelele kwa wavuja jasho.

Leo hii ndani ya serikali kana wingu kubwa la mazingira ya rushwa mengi yakiwa bayana na mengine bado ni ukungu mkuu, wanaojua ukweli ni washiriki wayo hivyo ni vigumu kutupa ukweli kila kukicha tunapiga kelele wasulubishwe wasulubishwe.

Imejengeka tabia ya kiongozi anapoharibu kubwebwa, kufichiwa siri, kufichwa ili akitoka atoke mpya na mtakatifu, hii hali kamwe haiwezi kutufikisha mbali.

Leo hii kijana wetu, mpendwa mtetezi wa mali yetu ZITTO KABWE, naye amepatwa na ukungu kama ule tu wa wale tunaowaita mafisadi, wezi, waroho, wahujumu wazembe, na mamluki wa nchi yao, sasa kwanini inakuwa ngumu wengi kuimeza hii chungu kweli tutaweza kuingoza hii nchi kwa ukweli uliodhabiti na utawala wa sheria usiomwogopa mtu, nasema ile sheria ambayo mkulima na mbunge watakuwa sawa mbele ya sheria Chenge na maiti ya bajaji watakuwa sawa, au nasi tunataka tuwe wafalme halafu tuadhibu watwana.

Kwa utawala wa Tanzania ninayoitaka, kwa uchungu na machungu ya watu wangu waliyoyapata ni lazima kila ukungu uwekwe wazi bila woga wala kificho.
Zitto atoke aeleze nini alikitetea, hata wale Songas walisema hawawezi kununua hiyo mitambo haifai kibiashara ila kijana wetu alisema tumsahau mmiliki wake tuangalie mitambo tu ipi hiyo????

Chadema itajengwa kwa demokrasia ya kweli na wanasiasa wa kizazi kipya, siasa ya kukubali kuwajibika kwa maneno yako na matendo yako na misimamo yako.Rushwa ni adui wa haki.

Mafisadi wataendelea kutupiga kwani ni kawaida ya tanzania habari kusahaulika na maovu vilevile ndio maana wala rushwa wengi hurudi na kuchukua madaraka halafu tunahamaki.spin spin spin.

Mkapa aliondoka wizara ya sayansi na kashfa ya millioni mia sita siku miezi michache kabla ya uchaguzi, kombe la babu lilifunikwa mzimu ukaingia ikulu kwa ule wimbo wa mr. clean, leo hii tunahamaki, tunahamaki nini wakati sisi ni wazuri wa kuabudu maneno matamu.
 
Duu, huyu Muh. dogo Zitto hadi namuonea huruma, Tumsameheni kwa bure walau tukikumbuka mazuri aliyo kwisha tutendea kama yale ma buzwagi ambayo kimsingi ndo yAliamsha hali ya upinzani nchini,

Kwa niaba yake Zitto (japo hajanituma) jamani naombeni tumsamehe tu aliteleza, Na namtia moyo aje tu jamvini tuendeleze libeneke, kutenda kosa si kosa bali kosa ni kurudia kosa! Naamini hayo MADOWANS walimuuzia tu mbuzi kwenye gunia!

KARIBU MPIGANAJI ZITTO, NAAMINI WOTE WATAKUSAMEHE KAMA MUUMBA WETU ANAVYO TUAGIZA TUSAMEHEANE.
 
kinachoshangaza ni kwamba sheria ya vyuo vikuu inakataza shughuli za kisiasa vyuoni lakini wakati huohuo utashangaa kuna mkutano wa ccm kwenye chuo fulani kwaajikli ya kuzindua tawi kwenye chuo hicho sijui hizo nazo sio shughuli za kisiasa na utaona kabisa watu wamevaa matshirt ya chama hicho, sasa linapotokea suala la mijadala yenye maslahi kwa taifa ndo inazuiwa
 
Duu, huyu Muh. dogo Zitto hadi namuonea huruma, Tumsameheni kwa bure walau tukikumbuka mazuri aliyo kwisha tutendea kama yale ma buzwagi ambayo kimsingi ndo yAliamsha hali ya upinzani nchini,

Kwa niaba yake Zitto (japo hajanituma) jamani naombeni tumsamehe tu aliteleza, Na namtia moyo aje tu jamvini tuendeleze libeneke, kutenda kosa si kosa bali kosa ni kurudia kosa! Naamini hayo MADOWANS walimuuzia tu mbuzi kwenye gunia!

KARIBU MPIGANAJI ZITTO, NAAMINI WOTE WATAKUSAMEHE KAMA MUUMBA WETU ANAVYO TUAGIZA TUSAMEHEANE.

Mkuu Rwabugiri heshima mbele.
Nafurahi kwa kukiri kwamba Zitto hajakutuma kuwaomba watanzania wamsamehe kwa kuchukua msimamo wa kijinga wa kuunga mkono Tanesco kununua mitambo chakavu.
Kumsamehe Zitto ni vigumu sana kwasababu dogo alionywa sana asijichanganye katika suala la Dowans lakini akashupaza shingo sasa mnaokuja na hoja dhaifu za kumtetea dogo mnanishangaza kupita kiasi.
Kama ningekuwa mwanamzumbe na uongozi wa Mzumbe ukaruhusu mjadala nisingepoteza muda wangu kwenda kumsikiliza Zitto kwasababu kwangu mimi namchukulia Zitto kama kuwadi wa mafisadi.Hana jipya zaidi ya kutaka kutuzuga,wapo wanaosema Zitto kateleza lakini wako tayari kuwasulubu wanasiasa wengine tena kwa makosa madogo madogo tena yasiyokuwa na athari kubwa kwa taifa.

Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom