Zijue baadhi ya koo za Kizaramo, asili na maana yake

Bwana Banzi

JF-Expert Member
Oct 14, 2014
382
174
ZIJUE BAADHI YA KOO ZA KIZARAMO, ASILI NA MAANA YAKE.

Wazaramo/ wazaramu ni kabila linalopatikana mkowa wa Pwani, Daresalama na maeneo ya mkowa wa morogoro ( morogoro vijijini, hasa mvua na dutumi). Wazaramu wana koo nyingi sana zisizopungua arobaini (40). Baadhi ya koo hizo (koo zilizonyingi) hufanana na koo zinazopatikana katika kabila la waluguru, wakwere na pia wakutu. Kwa leo tuangalie hizi koo kwa upande wa waluguru na wazaramo. Waluguru hupatikana zaidi mkowa wa Morogoro, na Mkowa wa pwani, na bagamoyo. Zifuatazo ni baadhi ya koo za kizaramo zilizotokana au kufanana moja kwa moja na Waluguru:

1.Ukoo wa Kolelo: huu ni ukoo ambao asili yake ni kule kolelo kwenye mizimu ya asili ya uluguru. Ukoo huu hupatikana katika kabila zote mbili za wazaramu na waluguru, mwanaume anaitwa kolelo n a mwanamke mlakolelo

2. Ukoo wa Wabunga: huu ni ukoo pia unaopatikana katika kabila la wazaramu japo uluguruni pia upo,

3.Ukoo wa Semindu (Wahindu): huu ukoo wa semindu ni ukoo wenye asili ya kutoka mlima mindu, masimulizi ya kale yanasema kwamba hii koo ilihama kutoka mlima mindu uliopo morogoro kwa sababu ya kukimbia majanga ya asili. Huu ukoo wazaramo huita ukoo wa semindu na uluguruni unaitwa wahindu, mwanaume huitwa hindu( mindu) na mwanamke mlahindu au wahindi kwa upande wa uluguruni. Kwa wazaramo mwanamke huitwa mindu na mwanaume semindu

4. Ukoo Wabena: huu ukoo wa wabena asili yake pia ni uluguruni, ina maana kubena ni kuvunja. Hawajamaa walikuwa wanabena ngodi(kuni), wabena migoha( wavunja mikuki). Mwanaume huitwa m’bena na mwanamke kibena au mlam’bena.

5.Wachuma na Wakalagale: ukoo wa wachuma na ukoo wa mkalagale ni koo zinazofanana( mkalagale, chuma kimejigalagaza). Mwanamke huitwa chuma au mlachuma na mwanaume huitwa Luanda( uluguruni). Mwanaume huitwa Chuma na mwanamke Mlachuma ( uzaramoni)

6. Mzeru: huu ukoo asili yake ni uluguruni, ni kwamba huu ukoo unasifika kuwa na watu weupe ( zeru au nzeru kwa maana –upe), kwa upande wa uluguru mwanaume huitwa mogela, na mwanamke ni mzeru/mlamzeru, pia kwa wazaramo mwanamke huitwa mzeru/mlamzeru.

7.Mponda: huu ukoo wa mponda pia unapatikana uluguruni na uzaramuni, ndio hao kina makala (makaa), au mponde

8. Mgombe: huu pia ni ukoo unaopatikana uzaramuni, kina kagombe ndio ukoo wao huu pia uluguruni upo

9. Ukoo wa kihemba/kilewa( Wahemba): huu ni ukoo ambao asili yake pia ni uluguruni, kwa waluguru huita WAKINOGE, kwa upande wa waluguru mwanaume anaitwa kobelo, berege,mwinyigoha, na mwanamke huitwa kinoge au kibua au kihemba... Uzaramoni, mwanaume huitwa kihemba na mwanamke huitwa mlakihemba ( kumbuka uhemba ni mtama kwa kiluguru/kizaramo)

10. Ukoo wa Kisuru: ni ukoo unaopatikana uzaramoni, lakini pia uluguruni hasa maeneo ya mgeta sehemu ya mongwe au nyuma yam lima wa kidiwa huu ukoo hupatikana huko pia.

11.Muhafigwa (Wahafiga): kwa wazaramo huita wahafigwa na waluguru huita wahafiga, kwa upande wa waluguru mwanamke anaitwa kiluwa na mwanaume anitwa mange au mveda

12.Mlali (mulali); huu ukoo kwa wazaramo mwanume huitwa mlali na mwanamke mlamlali, kwa upande wa waluguru mwanaume huitwa mlali au BWAKILA,mindoli, minyeko na mwanamke mlali au mlamlali

13. Mtonga, huu ni ukoo unaopatikana uzaramoni pia, mwanaume ni mtongana mwanamke mlamtonga. Pia asili yake ni uluguruni , kwa upande wa waluguru mwanaume huitwa MSUMI na mwanamke huitwa mtonga.

14. MWELUGURU; huu ukoo wa mweluguru hupatikana uzaramoni, maana yake ni kwamba mimi ni mluguru haswa, hujipambanua kwamba asili yangu ni mluguru. Kwa leo tuishie hapa koo zipo nyingi sana, kama msakuzi, setembe, sekamba, kizigo,setumbi, mponela, mkwayu,msemwa, mhondo, wa pazi, WAKILIMA(husema kwamba sisi ni wa mlimani kwelikweli, humaanisha wakutu/ waluguru), Mavula { kivula, Mwamvua, kibago, hayo majina kwa upande wa uluguruni na uzaramoni hutumika kuwakilisha ukoo wa mavula}.
 
Naona pia wanaingiliana sana na Wagogo, Wakaguru.ukiijua vzr lugha mojawapo hapo hakuna kati ya hoa wataweza kukuteta.
 
Kumbe ndiyo maana watu wa Morogoro pwani Dar wanaongea harakaharaka kama wamemeza motor kumbe chimbuko lao ni moja
 
ZIJUE BAADHI YA KOO ZA KIZARAMO, ASILI NA MAANA YAKE.

Wazaramo/ wazaramu ni kabila linalopatikana mkowa wa Pwani, Daresalama na maeneo ya mkowa wa morogoro ( morogoro vijijini, hasa mvua na dutumi). Wazaramu wana koo nyingi sana zisizopungua arobaini (40). Baadhi ya koo hizo (koo zilizonyingi) hufanana na koo zinazopatikana katika kabila la waluguru, wakwere na pia wakutu. Kwa leo tuangalie hizi koo kwa upande wa waluguru na wazaramo. Waluguru hupatikana zaidi mkowa wa Morogoro, na Mkowa wa pwani, na bagamoyo. Zifuatazo ni baadhi ya koo za kizaramo zilizotokana au kufanana moja kwa moja na Waluguru:

1.Ukoo wa Kolelo: huu ni ukoo ambao asili yake ni kule kolelo kwenye mizimu ya asili ya uluguru. Ukoo huu hupatikana katika kabila zote mbili za wazaramu na waluguru, mwanaume anaitwa kolelo n a mwanamke mlakolelo

2. Ukoo wa Wabunga: huu ni ukoo pia unaopatikana katika kabila la wazaramu japo uluguruni pia upo,

3.Ukoo wa Semindu (Wahindu): huu ukoo wa semindu ni ukoo wenye asili ya kutoka mlima mindu, masimulizi ya kale yanasema kwamba hii koo ilihama kutoka mlima mindu uliopo morogoro kwa sababu ya kukimbia majanga ya asili. Huu ukoo wazaramo huita ukoo wa semindu na uluguruni unaitwa wahindu, mwanaume huitwa hindu( mindu) na mwanamke mlahindu au wahindi kwa upande wa uluguruni. Kwa wazaramo mwanamke huitwa mindu na mwanaume semindu

4. Ukoo Wabena: huu ukoo wa wabena asili yake pia ni uluguruni, ina maana kubena ni kuvunja. Hawajamaa walikuwa wanabena ngodi(kuni), wabena migoha( wavunja mikuki). Mwanaume huitwa m’bena na mwanamke kibena au mlam’bena.

5.Wachuma na Wakalagale: ukoo wa wachuma na ukoo wa mkalagale ni koo zinazofanana( mkalagale, chuma kimejigalagaza). Mwanamke huitwa chuma au mlachuma na mwanaume huitwa Luanda( uluguruni). Mwanaume huitwa Chuma na mwanamke Mlachuma ( uzaramoni)

6. Mzeru: huu ukoo asili yake ni uluguruni, ni kwamba huu ukoo unasifika kuwa na watu weupe ( zeru au nzeru kwa maana –upe), kwa upande wa uluguru mwanaume huitwa mogela, na mwanamke ni mzeru/mlamzeru, pia kwa wazaramo mwanamke huitwa mzeru/mlamzeru.

7.Mponda: huu ukoo wa mponda pia unapatikana uluguruni na uzaramuni, ndio hao kina makala (makaa), au mponde

8. Mgombe: huu pia ni ukoo unaopatikana uzaramuni, kina kagombe ndio ukoo wao huu pia uluguruni upo

9. Ukoo wa kihemba/kilewa( Wahemba): huu ni ukoo ambao asili yake pia ni uluguruni, kwa waluguru huita WAKINOGE, kwa upande wa waluguru mwanaume anaitwa kobelo, berege,mwinyigoha, na mwanamke huitwa kinoge au kibua au kihemba... Uzaramoni, mwanaume huitwa kihemba na mwanamke huitwa mlakihemba ( kumbuka uhemba ni mtama kwa kiluguru/kizaramo)

10. Ukoo wa Kisuru: ni ukoo unaopatikana uzaramoni, lakini pia uluguruni hasa maeneo ya mgeta sehemu ya mongwe au nyuma yam lima wa kidiwa huu ukoo hupatikana huko pia.

11.Muhafigwa (Wahafiga): kwa wazaramo huita wahafigwa na waluguru huita wahafiga, kwa upande wa waluguru mwanamke anaitwa kiluwa na mwanaume anitwa mange au mveda

12.Mlali (mulali); huu ukoo kwa wazaramo mwanume huitwa mlali na mwanamke mlamlali, kwa upande wa waluguru mwanaume huitwa mlali au BWAKILA,mindoli, minyeko na mwanamke mlali au mlamlali

13. Mtonga, huu ni ukoo unaopatikana uzaramoni pia, mwanaume ni mtongana mwanamke mlamtonga. Pia asili yake ni uluguruni , kwa upande wa waluguru mwanaume huitwa MSUMI na mwanamke huitwa mtonga.

14. MWELUGURU; huu ukoo wa mweluguru hupatikana uzaramoni, maana yake ni kwamba mimi ni mluguru haswa, hujipambanua kwamba asili yangu ni mluguru. Kwa leo tuishie hapa koo zipo nyingi sana, kama msakuzi, setembe, sekamba, kizigo,setumbi, mponela, mkwayu,msemwa, mhondo, wa pazi, WAKILIMA(husema kwamba sisi ni wa mlimani kwelikweli, humaanisha wakutu/ waluguru), Mavula { kivula, Mwamvua, kibago, hayo majina kwa upande wa uluguruni na uzaramoni hutumika kuwakilisha ukoo wa mavula}.
Inasemekana kuwa kuna uhusiano mkubwa sana kati ya Wazaramo na Wamanyema kiasili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inasemekana kuwa kuna uhusiano mkubwa sana kati ya Wazaramo na Wamanyema kiasili.

Sent using Jamii Forums mobile app


Inawezekana kwa sababu kwa kawaida watu wengi wa bara( wabara, ni neno la kiluguru/zaramo/kwere maana yake wa kuja, au asiye na asili na makabila ya pwani), walipokuja mikoa ya moro, pwani na dar ( jimbo la mashariki) waliweza kulowea na kuoa au kuolewa na kushindwa kurudi makwao ( mikoa ya tabora, mwanza, kigoma n.k) kwa hiyo wakafahamiana na watu wa pwani na wakahesabiwa kuwa miongoni mwa makabila haya ya pwani, kwa mfano leo hii kuna majina ya kina mganga uluguruni, ambayo kiasili ni kina maganga wa tabora. Kwahiyo kuna wa manyema, wanyamwezi, warundi,wakongo na makabila mengine mengi yaliyokuja pwani kama manamba au watumwa au wafanyabiashara, wakaishi kuoa na kuolewa na watu wa pwani na kizazi chao kikasahau asili ya kwao na kujitambulisha kama wazaramu au wakwere au waluguru. Yaani wamekuwa wazaramu kwa kuzaliwa au kutokujua asili ya kwao, ila chimbuko halisi la wazaramo ni uluguruni,na uziguani.Kwahiyo hao wa manyema walikuja na kuwakuta wenyeji ambao ni wazaramu,waluguru,wakwere,wandengereko, wakami, wakutu na wakakaribishwa na kuwa miongoni mwao, pia vizazi vyao vilijitanabaisha kama wazaramo. Kwahiyo wakawa wazaramu wa kuzaliwa….! Kimsingi hata mngoni ambaye atahamia ngerengere au tununguo au mlandizi, vizazi vyake baadaye vinaweza kujitambulisha kama kutoka kabila la wakwere/waluguru. Kwahiyo uhusiano ulipo ni kwamba, wa manyema walihamia maeneo ya pwani na kutekwa na utamaduni wa wenyeji, na kuwa wazaramu ila wazaramu si wa manyema na wala wa manyea si wazaramu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom