Zaidi ya watu 20 wafa ajalini Rufiji

poleni wafiwa.na hizi ajali zinagharimu sana maisha ya watanzania wengi sana
uzembe wa askari wa usalama barabarani na kutokuwa na elimu kwa madereva kwa kujikinga na kutoa ishara kuwa mbele kuna ajari
 
ni kweli imetokea na watu 21 wamefariki, mkuu wa mkoa wa pwani amethibitisha
chanzo: radio one breaking news
 
Kalagabaho na kibibititi, binafsi ningefurahi sana kama sote humu tukabadilishana nawazo na kujengana kimtazamo na kushindana kwa hoja badala ya kutukanana ambako kiuhalisia hakutujengi na kutuweka pamoja, nashauri tupendane

Acheni hizo washikaji hayo mambo ya ukabila na uzone yanaanzia wapi sasa? Hapa tuna msiba mzito umetupata nyie mnaleta mzaha hapa!!!! Poleni jamani wote mliopatwa na msiba huu mkubwa Mungu mwenyewe awape faraja ya kweli. Madereva tuwe makini hasa kuweka alama tunapokuwa tumepata brerakdown barabarani na tuangalie pia spidi hasa kwa magari ya abiria. Hakuna duka la roho Kariakoo.
 
Pole kwa wote waliofiwa na Mwenyezi Mungu awepe wepesi wa kupona majeruhi wa ajali.
Udereva wakujihami na kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ni muhimu.
 
Mungu awaweke mahali pema peponi,majeruhi wapone haraka ila kama kuna mashoga,mungu afanye atakavyoamua.
 
Ajali zinaua watu maskini ktk nchi nyingi za kimaskini 20 people dah very sad news. Pumzikeni kwa amani sisi bado tupo safarini.
 
attachment.php

Watu 21 wamefariki dunia katika ajali mbaya imetokea Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani ikihusisha magari 3 na wengine 11 kujeruhiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Ulrich Matei, alisema ajali hiyo imetokea katika Barabara Kuu ya Dar es Salaam-Lindi, eneo la Ikwiriri, wilayani humo.
Awali ajali hiyo ilihusisha magari mawili, Toyota Hiace (T 948 CUX), iliyokuwa ikitokea Ikwiriri kuelekea Rufiji ambalo lilikwenda kukwaruzana na Lori(T 132 AFJ) kwa nyumba, ambalo lilikuwa limeharibika na kusimama barbarani.

Alisema baada ya kulikwaruza roli hilo, mlango wa Hiace uling'oka na kubaki kwenye roli ambapo gari hiyo lilipoteza mwelekeo na kwenda kugongana uso kwa uso na gari nyingine aina ya Canter(T 774 CJW) na kupinduka.
"Katika ajali hii, watu 14 walifariki dunia papo hapo, wakati polisi na baadhi ya wananchi wakiendelea kuwaokoa majeruhi ili wakimbizwe hospitali, likatokea basi la kampuni ya Mining (President)( T 242 BXA), kuwakanyaga watu waliokuwa wakitoa msaada na kuwaua ndio maana idadi ya waliokufa imefikia 21.

"Basi hili lilikuwa linatoka Lindi kuelekea Dar es Salaam...polisi walifanya jitihada za kulisimamisha lakini dereva wake alikataa kusimama na kwenda kukanyaga watu lakini tayari tumemkamata, majeruhi mmoja amehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam," alisema Kamanda Matei.
Kamanda Matei alisema, basi hilo linashikiliwa polisi ambapo uchunguzi ukikamilika, dereva wake atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka.

Aliwataja waliokufa ni Sixtus Ally Mtanga(32) na Nassoro Mohamed Kajani(20) wakazi wa Ikwiriri, Juma Said Kitambulilo(30) na Salum Goma Makonde (50), Ustaadhi Kalilambwe(34) na Shafil Kip (30), Wasabi Sabil(45), Ramadhani Ally (23)wote wakazi wa Mbagala.
Shabani Bakari(30) Kondakta wa Hiace, mkazi wa Kibiti, Masud Abulal (27), mkazi wa Mkuranga, Ammi Mpemba (30)na Madadi Hassan Mangasongo (45) wakazi wa Jaribu na Japhet Ponsian (24), mkazi wa Dar es Salaam.
Pia yupo Said Ally China (21) mkazi wa Kimanzichana, mkazi wa Jaribu, Abdalahaman Yusuph Kihemke(45), mkazi wa Kongowe na Fikiri Said Sauze, mkazi wa Vikindu.

Wengine ni Nywari Mshigani mkazi wa Dar es Salaam, Hassan Wasabi (18), mkazi wa Kibiti na Seleman Mcharazi (47) mwingine aliyejulikana kwa jina moja la Mustafa, wote wakazi wa Mbagala na maiti ya mwanamke haijafahamika jina lake.
Waliojeruhiwa katika ajali hiyo ni Frank Sixmundi (31), dereva wa gari la Maliasili Kibiti ambaye alifika eneo ili kutoa msaada kwa majeruhi ambaye ameumia kichwani, Mohamed Salehe (49) na Charles Rogasani (23), wote wakazi wa Kibiti na Mohamed Mengine (42), mkazi wa Dar es Salaam.
Wengine ni Mniko Magige Mango (54) na Abdalah Issa (25) wakazi wa Mkuranga, Khalid Salum (32), mkazi wa Dar es Salaam, Ahmad Yusuph (23), mkazi wa Kigamboni na Shomari Yusuph (42), mkazi wa Mburahati. Majeruhi wamelazwa katika hospitali za Ikwiriri, Misheni ya Mchukwi na wengine hospitali ya Taifa Muhimbili.
 

Attachments

  • ajali (1).jpg
    ajali (1).jpg
    66.4 KB · Views: 519
Haipiti siku 2 tunaelezwa AJALI na AJALI na AJALI.

Inaonesha hakuna anaejali kwa AJALI hizi kutokea kila siku.
 
Back
Top Bottom