Yu wapi Dkt. Masumbuko Lamwai?

Yupo mjini anaendelea na kazi yake ya uwakili kama kawaida, ile Land Cruser mkonge ameipaki siku hizi anatumia Suzuki Grand Vitara ya Blue na anaishi maeneo ya Sinza kwa Remmy.
acha uong wewe anishi kunduchu beach bonge la nyumba!
 
hana lolote, akilini kwake alijua mchaga mwenzie Mrema atashinda ili yeye apae kisiasa, bahati yake mbaya hakujua kama sisiemu ni jiwe la kifisadi, akajikwaa na kudondokea pua....kama kipindi kile alikuwa na akili, kwani siku hizi akili zimeenda wapi? walimkata kichwa? ni kwamba hana lolote, choka mbaya, na watoto mitaanni kibao kila mtaa ana watoto....pesa hamna anasubiria kamshahara ka kichuo cha tumaini kile cha kurasini.....ukijiona uko juu, usifikiri umefika, uwe tayari kwa lolote, kama una akili fanya mambo sio kwa kujilipua/kujitoa mhanga bila akili, fanya kwa kujenga future yako..


sasa mrema aliyekuwa anamkimbilia, tena kikabila kwasababu ni mchaga mwenzie yuko wapi? mbona ni kichekesho kabisa katika siasa, walifuata kivuli cha mtu, mrema ni kichekesho, kweli akili za mbayuwayu changanya na za kwako...nyie mliobaki jifunzeni kwa mwenzenu.
 
Yupo mjini Dar, anafundisha Tumaini University, unajua siasa ilimponza hasa baada ya kutokuelewa sera ya ndugu Lyatonga, Jingine alipoingia siasa hakuzingatia maadili ya uwakili ndio maana akasimamishwa kufanya kazi ya uwakili kwa uzembe.Ila kwa sasa amerudishiwa lesini yake na anafanya kazi fresh tu down town.
 
Huwa namuona pale tumaini dar campus naona hataki kusikia kuhusu siasa tena!!bado ana land cruiser yake ile mkonga aliopata akiwa mbunge!!!inamtoaa manaa imechoka hasa lakini bado anakomaa nayo tu
 
mwanzoi mwa miaka ya 2000 wakati nakua, nilikua nikisikia saaana jina la masumbuko lamwai, hasa enzi zile za utawala wa kaka benja, lakini toka kipindi hicho hadi leo sijawahi kusikia kabisa hilo jina kokote, labda ningependa kujua tu alikua ni nani na labda yuko wapi kwa kipindi hiki, msaada mwenye details!!
 
Alikuwa mbunge kupitia NCCR baadaye akajiunga na CCM,pia ni wakili, hata huvyo,Itabidi tuwaulize CCM walikompeleka
Msumbuko ni mwanasheria huyu.
Mara ya mwisho nimemkuta mahakama ya Kariakoo akitetea wezi wa kuku.
Kavaa koti linalomtosha mwanawe na miguuni makubadhi.
Wallah dunia tambara bovu!
 
Msumbuko ni mwanasheria huyu.Mara ya mwisho nimemkuta mahakama ya Kariakoo akitetea wezi wa kuku.Kavaa koti linalomtosha mwanawe na miguuni makubadhi.Wallah dunia tambara bovu!
watu! peopleeeeeee jamaniii nilkuwa nimenuna sasa nimecheka mpaka meno yote 32 nje hahahaaa
 
Dr. Masumbuko Lamwai sasa hivi ni lecturer na vilevile ni 'Dean- faculty of Law' pale Tumaini university Dar-Es-Salaam College campus ya Kurasini. At the same time bado ni wakili wa kujitegemea. Huo ni mwanzo tu, nitarudi baadaye!
 
Hahaaaaa, ila kweli jamaa kapotea. nakumbuka aliwai kulitetemesha Bunge enzi za Mkapa kabla hajahamia CCM kwa kishindo mwaka 2000. mara yangu ya mwisho kumsikia ilikuwa mwanzoni mwa mwaka 2005 kama sio 2004 wakati wa kesi ya ujambazi mtuhumiwa mkuu akiwa Nyari mfanyabiashara wa Arusha aliyekuwa anatuhumiwa kuiba madini. Mmoja wa watuhumiwa aliyekuwa anadai alitumwa na Nyari kufanya ujambazi huo alionesha mahakamani picha ya Nyari aliyopiga akiwa na Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa wakati huo Mh. Kikwete. Mtuhumiwa huyo alidai Nyari alimwambia asiwe na wasiwasi kwamba atakamatwa kwani yeye (Nyari) ni rafiki wa raisi mtarajiwa wa nchi hii kwahiyo mambo ya kukamatwa, kushtakiwa na kuhukumiwa asiyafikirie kabisa kwani hayapo.

Hapo Dr. Masumbuko Lamwai akajitokeza kumtetea Mh. Kikwete. sifaham kwamba alimtetea mahakamani au kwenye vyombo vya habari. Lamwai alisema mteja wake (Kikwete) hausiki kwa chochote na hiyo kesi na huyo mtuhumiwa. alisema inawezekana hiyo picha imetengenezwa (imekuwa doktad). Jamaa (Nyari na wenzake) walitiwa hatiani na kufungwa. Ila Nyari alikata rufaa akashinda na kuachiwa huru.

Niliwai kusikia alikuwa anafundisha Mzumbe University. Please mwenye uhakika atujuze.
 
Mwacheni Baba Mkwe wangu...
Wizi mtupuuuuu!! Kila siku wanachakachua mil2.5 za watoto wa wakulima pale Tumaini tena bila huruma na huyo kaka yao Malasusa (Askofu) hawaoni hata aibu. Wanafunzi wakikoroma tu kidogo wanafukuzwa sasa angalia na wewe siku ukimkoromea tu mwanae unapigwa kando.
 
Back
Top Bottom