Yohana Mjinga bana..........!!!!

gambachovu

JF-Expert Member
Dec 29, 2011
1,854
292
Alipewa shilingi mbili(coins) aende kununua maziwa..
Njiani akakuta watoto wenzake wanaokota mawe na kuyarusha kwa nia ya kuapopoa shorwe(aina ya ndege). Naye (Yohana),akaamua kupopoa ndege wale.. Baadaye akaamua kuendelea na safari ya kwenda kununua maziwa. Alipofika,aliulizwa hela.Akatafuta shilingi mbili zile bila mafaniko.ndipo akakukumbuka alizitumia kupopolea ndege!

Aliporudi bila maziwa,bibi yake alimsema na kumkaripia sana! Na akampa hela nyingine huku akimsisitizia sana,kuwa anaweka kila anachotumwa mfukoni mwa kaptura yake kuepuka kupoteza.

Akapimiwa maziwa,akalipa. Wakati wa kurudi,aliyakumbuka maneno ya bibi yake alipokuwa akimkaripia.. Akaona kweli amefanikiwa kurudi na maziwa baada ya kutunza hela mfukoni. Akaona amfurahishe zaidi bibi yake,akchukua maziwa yale akaanza kuyamimina kwenye mfuko wa suruali yake! Akashangaa kuona yanapenya na kumlowesha mguuni,akamimina mpaka yakaisha! Akashangaa sana! Lakini akasema atamweleza bibi yake yote yaliyotokea.

Aliporudi alikaripiwa sana na bibi yake,na akamwita mjinga,na Yohana alisikitika sana. Hakutumwa tena maana bibi sasa alienda mwenyewe.

Siku nyingine bibi alitaka nyama ya kitoweo. Akampa hela. Akafika bucha,akauziwa nyama. Njiani akajisemea kuwa leo hatakosea tena. Sasa kwa kuwa enzi hizo hakukuwa na mifuko ya Rambo kama sasa,na yeye alitaka kufuata masharti yote ya bibi yake ,akaamua kuchukua kamba ndefu na kuifunga vizuri nyama ile,kisha nye akajifunga mkononi akawa akielekea nyumbani huku akiiburuta njiani nyama ile.. Alipokaribia kufika nyumbani,aliona aukague mzigo wake aliokuwa akiuburuta.. Cha ajabu hakuona nyama ile aliyotumwa! Akaona arudi kuitafuta..
Alirudi taratibu huku akitafuta kwa makini,ndipo aliwaona mbwa wawili wakiila nyama ile. Akaona aende kuwanyang'anya,nao wakmtishia kwa kubweka sana mpaka akakimbia kwa bibi yake...

Pata picha ya ujinga wa Yohana mjinga!
 
Una namba ya yohana ya simu?

Na ujinga wote huo,awe na simu, aringe....!!

Lazima atakuwa alifungiwaga kipande cha sabuni,na akakata tamaa tangia hapo.. We ukimwangalia personality yake,unamwonaje kwani.. Mwangalie kwa makini...
 
Alipewa shilingi mbili(coins) aende kununua maziwa..
Njiani akakuta watoto wenzake wanaokota mawe na kuyarusha kwa nia ya kuapopoa shorwe(aina ya ndege). Naye (Yohana),akaamua kupopoa ndege wale.. Baadaye akaamua kuendelea na safari ya kwenda kununua maziwa. Alipofika,aliulizwa hela.Akatafuta shilingi mbili zile bila mafaniko.ndipo akakukumbuka alizitumia kupopolea ndege!

Aliporudi bila maziwa,bibi yake alimsema na kumkaripia sana! Na akampa hela nyingine huku akimsisitizia sana,kuwa anaweka kila anachotumwa mfukoni mwa kaptura yake kuepuka kupoteza.

Akapimiwa maziwa,akalipa. Wakati wa kurudi,aliyakumbuka maneno ya bibi yake alipokuwa akimkaripia.. Akaona kweli amefanikiwa kurudi na maziwa baada ya kutunza hela mfukoni. Akaona amfurahishe zaidi bibi yake,akchukua maziwa yale akaanza kuyamimina kwenye mfuko wa suruali yake! Akashangaa kuona yanapenya na kumlowesha mguuni,akamimina mpaka yakaisha! Akashangaa sana! Lakini akasema atamweleza bibi yake yote yaliyotokea.

Aliporudi alikaripiwa sana na bibi yake,na akamwita mjinga,na Yohana alisikitika sana. Hakutumwa tena maana bibi sasa alienda mwenyewe.

Siku nyingine bibi alitaka nyama ya kitoweo. Akampa hela. Akafika bucha,akauziwa nyama. Njiani akajisemea kuwa leo hatakosea tena. Sasa kwa kuwa enzi hizo hakukuwa na mifuko ya Rambo kama sasa,na yeye alitaka kufuata masharti yote ya bibi yake ,akaamua kuchukua kamba ndefu na kuifunga vizuri nyama ile,kisha nye akajifunga mkononi akawa akielekea nyumbani huku akiiburuta njiani nyama ile.. Alipokaribia kufika nyumbani,aliona aukague mzigo wake aliokuwa akiuburuta.. Cha ajabu hakuona nyama ile aliyotumwa! Akaona arudi kuitafuta..
Alirudi taratibu huku akitafuta kwa makini,ndipo aliwaona mbwa wawili wakiila nyama ile. Akaona aende kuwanyang'anya,nao wakmtishia kwa kubweka sana mpaka akakimbia kwa bibi yake...

Pata picha ya ujinga wa Yohana mjinga!

Umenikumbusha mbali mkuu!
Nadhani kama umekumbuka hii, basi wimbo wa 'Pauli mchafu ...' bila shaka unaukumbuka.
 
Nakumbuka hii stori alinisimuliaga Maza. Leo nilikuwa natafuta kitabu chake nikajikuta huku.

Kalitabu au hii stori inaitwa Yohana mjinga na Utiivu wake. Iliandikwa mwaka 1963 na Charles Granston ambaye alikuwa ni mmishionari.
Mtandaoni kote hakuna haka kakitabu, nakatafuta sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom