pwilo
JF-Expert Member
- May 27, 2015
- 10,098
- 12,474
Kibwana shomari ana kipaji gani mzee zaidi ya kutumia nguvu tu kama kibu denis soka la kisasa linahitaji watu talented beki asist anazitafuta kwa shida hawezi hata kupiga cross nguvu nyingi akili kisoda shabash.Ukinipa Joyce lomalosa na kibwana Shomari Basi NALIA NGWENA nitakwenda na kibwana Shomari bila wasiwasi.
KIbwana Shomari ni moja kati ya kitasa kilichochongwa na Prof wa mpira na si mwingine Prof Nabbi, hakika bwana mdogo ni kitasa haswa/anajua kukaba na kusikiliza maelekezo ya kocha.
Joyce Lomalosa ni mtu wa kupanda na kumwaga maji(kupiga klos) katika lango la maadui ni mzuri kwa Hilo na ana kontrol nzuri mguuni, kontrol ambayo hufanya mpira umtii lakini si mzuri kukaba akikutana na winga machachali huwa anateseka.
KIbwana shomari anacheza beki namba 2&3 ni kilaka mzuri aliyetengenezwa na kocha Nabbi, Kuna muda wachambuzi walisema "Kama kibwana akiendelea na ubora huu Basi anaweza kuwa mrithi wa Shomari kapombe taifa stars"
Toka kocha Gamondi aingie Yanga Sc sikumbuki kibwana Shomari Mara ya mwisho kucheza ilikua ni lini naona Kibabage anapata namba na endapo Yao akiwa majeruhi kocha anachagua kumchezesha Dikson job Kama beki namba 2.
Maoni Yangu: Kama kocha anaona haingii kwenye mfumo wake ni vyema dirisha dogo atolewe hata kwa mkopo kuliko kukaa benchi wakati mashabiki tunapenda kumuona uwanjani kijana huyu kitasa aliyebarikiwa kipaji.