Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,115
Habari Wakuu,
Leo 09/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki:Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 9, 2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
Wakili Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili Kuendelea Kusikilizwa na tupo tayari Kuendelea
Peter Kibatala: Nasi pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea
Shahidi anapanda kisha anasimama Kizimbani Jaji anaandika Kidogo
Jaji: Shahidi nakukumbusha Ulikuwa chini ya Kiapo na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo
Shahidi: Sawa Mheshimiwa, Ila kuanzia Jana Jioni hali yangu haikuwa Nzuri lakini nitaendelea Kutoa Ushahidi
Kibatala: Good Morning Inspector
Shahidi: Morning
Kibatala: Nafikiri Unakumbuka Jana tulikuwa kwenye Swala la Mbowe Kuanzisha Ugaidi
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Tulijadili Mpaka Pale ambapo Washitakiwa Walikutana pale Morogoro na Luteni Denis Urio
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Upelelezi wako Uligundua hivyo
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Na aliye Waita pale alikuwa ni Luteni Denis Urio
Kibatala: Na Utakubaliana na Mimi Kuwa Mpaka Mshitakiwa Wa Kwanza, Wapili na watatu anakutana na Denis Urio Mbowe alikuwa hawajui na hajawahi Kukutana nao
Shahidi: sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba kabla ya Kukutana Walikuwa wanafanya Shughuli zao halali
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Luteni Denis Urio aliwaita Morogoro Kwa sababu Yeye Makazi yake yalikuwa Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa namna yoyote Ile Freeman Mbowe Hakuwahi kuwa Morogoro kabla na baada ya hizo Tarehe walizokutana Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Uliwahi Kugundua Kwa wewe Kuwa Pro Active au Kuhalifiwa na Luten Denis Urio Kwamba kabla ya Mohammed Ling'wenya Kuondoka Mtwara Kuja Morogoro, ilibidi awasiliane na Mzee Ling'wenya Kupata Ruhusa
Shahidi: Sikuwahi Kufahamu
Kibatala: Pia hufahamu Luteni Denis Urio alitoa Ushahidi Mahakamani akithibitisha
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo hata nikikwambia Kwamba Mzee Ling'wenya ilibidi aitishe Kikao cha Ukoo/Familia Kujadili suala la Mtoto wao Kwenda Kwa Luteni Denis Urio
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Pia ufahamu Kwamba Wakati Wanamtoa Walimtoa Kwa Uangalizi Kwamba Wanamkabidhi Kwa Luten Denis Urio na Kwa Freeman Mbowe, Kwa sababu ni watu wanao aminika
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale
Shahidi: Fafanua tena
Kibatala: Ulikuwa unafahamu Kwamba Luteni Denis Urio, alikutana na Makundi Mawali Kwa wakati tofauti
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: aliyewaambia Bwire na Moses Lijenje na aliyewaambia Adamoo na Ling'wenya alikuwa ni Luteni Denis Urio, Je ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unaposema Kwamba alipo wasiliana na Mbowe aliwasiliana Meseji, Telegram au Simu
Shahidi: Kwa Njia ya Mdomo na Pia kwa Njia ya Mawasiliano ya Jumbe za Telegram
Kibatala: Walipoongea Denis Urio na Freeman Mbowe wewe Ulikuwepo
Shahidi: Sikuwepo
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Ulishawahi Kusikia Neno Maarufu la Kiupelelezi la "Your Word against Mine"
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kwa kuwa Wewe, Kingai, DCI hamkuwepo Wakati Mbowe anaongea na Urio
Shahidi: Hatukwepo lakini tulifanya Upelelezi
Kibatala: Watu Wawili wamezungumza, Na DCI hakuwepo, Kingai hakuwepo, na wewe hukuwepo Je si lazima sasa Tupime Maneno ya Denis Urio na Freeman Mbowe
Shahidi: Siyo lazima, Unaweza Kufanyia Kazi Maneno ya Denis Urio
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Wakati Denis Urio anakutajia Kuwa Kuna Cassa Motel, Je Uliwahi Kwenda hata Kuthibitisha
Shahidi: Sijawahi Kwenda
Kibatala: Mgahawa ambao Denis Urio alitaja Wamekutana na Mbowe Wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Urio aliwahi Kukwambia Kwamba alipanda Tax Mgulani
Shahidi: sikwenda
Kibatala: Je aliwahi Kukwambia Kwamba alikuwa Mjini alipanda bodaboda
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Uliwahi Kufika Kuona Kama Kuna Kituo cha Bodaboda
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Uliwahi Kwenda Cassa Motel Kuthibitisha Kama Gari ya Denis Urio lilifika pale
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Uliwahi Kwenda Mgulani Kuthibitisha Kwamba Denis Urio aliwahi Kufika na Kuishi Pale
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Nyie Kama Polisi mkipata Taarifa Mnairekodi au Kufanyia kazi
Shahidi: Tunafanya kazi
Kibatala: Je wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda 14 July 2020 Kule Ngerengere 92 KJ Ka kweli alikuwa kazini
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Baada tu ya Kurejea Kutoka Darfur alikamatwa Kikosini baada ya Kutajwa na Adam Kasekwa
Shahidi: Sifahamu nilifanya Uchunguzi
Kibatala: Kwakuwa umechunguza Kule 92 KJ uliongea na nani
Shahidi: Nisha sema Sikwenda
Kibatala: Kwa hiyo wewe hata 92KJ hufahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Makampuni ya Simu yanatunza Kumbukumbu za Mawasiliano
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Yanatunza Kwa Muda gani
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Je Wewe Kama Mpelelezi Uliomba Taarifa za Call Recordings katika Makampuni ya Simu Kati ya Freeman Mbowe na Denis Urio
Shahidi: Ndiyo Niliomba
Kibatala: Kwa Barua ya Tarehe Ngapi
Shahidi: Kwa Barua ya 13 August 2020
Kibatala: kwenda Kampuni gani
Shahidi: Kwenda Kwenye Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao
Kibatala: Kwa Inspector Ndowo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo wewe Uliomba Taarifa Kwa Inspector Ndowo, Je yeye ndiye Mwenye Kuhifadhi
Shahidi: Yeye Ndiye aandike Barua kwenda Tigo na Airtel
Kibatala: kwa hiyo wewe Pamoja na Mambo yote Uli Mwomba Na Rekodi za Mawasiliano ya simu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je wewe Uliona Katika Barua yake kutoka Kwenu Terms of reference suala la Call Recordings lipo
Shahidi: Halipo
Kibatala: kwa hiyo Mliomba au Hamkuomba
Shahidi: Hatukuomba
Kibatala: Uwe sasa inasililiza kwa Makini.. Haya Unafahamu Kuhusu Sheria ya EPOCA
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo ufahamu Kwamba Sheria hiyo nakupa Mamlaka Ya Kuomba Voice Recordings
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Wakati DCI na Kingai Wanakuteua waliluteua Kwa sababu ya Uwezo au Sababu ya Kitengo X
Shahidi: Sababu ya Uwezo
Kibatala: Hivi una Elimu gani
Shahidi: Kidato cha 6
Kibatala: Sekondari gani
Shahidi: Moshi
Kibatala: Ulipata Division ngapi
Shahidi: Division 3 Point 13
Kibatala: ulifaulu Kwenda Chuo
Shahidi: Hapana, CCP Moshi
Kibatala: Ok! Ndiyo Walikuchagua sababu ya uwezo huko
Kibatala: Je unafahamu Mojawapo Ya Majukumu ya Upelelezi wako ilikuwa Ku Trace kila single Cents
Shahidi: Hilo siyo Muhimu cha Muhimu Kama alitoa pesa kufadhili Ugaidi
Kibatala: Swali langu nasema kwamba Kama Mpelelezi unajukumu la Ku Account for na Ku Trace Kila single Cent
Shahidi: Nisha Jibu Kuwa siyo Muhimu
Kibatala: Je nani alikuwa na Jukumu la Kuona na Kuthibitisha zile pesa
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Na hilo Jukumu Uliteleleza Kikamilifu la Ku Trace hizo pesa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Tayari Kwamba Denis Urio alituambia kuwa Watuhumiwa Walisafiri Kutoka Walipo kuwa Kuja Morogoro, Je Unafahamu Kwamba Walikuwa Refunded
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji nani alitoa Pesa Kuwa Refund (rejeshea)
Shahidi: Luteni Denis Urio
Kibatala: Na Kwamba Unafahamu Kwamba Hawa walikuwa wanajua Kuwa walikuwa wanapewa Pesa Kurejeshewa Nauli zao
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu Kwamba ni TSh ngapi Moses Lijenje alirejeshewa
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Lini wewe Ulifahamu Kuwa Unakuja Kutoa Ushahidi
Shahidi: Alhamisi
Kibatala: Hiyo Taarifa Ulipewa na Watu serious au Uliwa chukuliwa poa
Shahidi: Nilichukua Serious
Kibatala: Hii Kesi ni Kubwa au Nyepesi
Shahidi: Kubwa
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi ni nani atakuja kutueleza Kuhusu mabadilishano ya Pesa kati ya Moses Lijenje na Khalfani Bwire kutoka kwa Denis Urio
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Shahidi anaitwa Gladys Fimbari kutoka Airtel alileta Taarifa Ya Mihamala, Je Ulisoma na Kuelewa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Pesa ambayo Wali badirishana Mikono kati Adam Kasekwa na Denis Urio ilikuwa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Pesa ambayo ilibadilishana Mikono katika ya Mohammed Ling'wenya na Denis Urio ni TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Ni wewe ulimuhoji Denis Urio
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: alikueleza?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ilikuwa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Pesa Iliyo badirishana Mikono kati ya Moses Lijenje na Khalfani Bwire ilikuwa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Unafahamu Pesa kiasi gani ambacho alipewa Mohammed Ling'wenya Nauli ya Kwemda Moshi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Wakati Washitakiwa wa Kwanza, Wapili na Watatu wanaenda Moshi Kama wanavyo Sema Watuhumiwa, Je Walikuwa Wanafahamu Wanaenda Kufanya Nini huko
Shahidi: Walikuwa hawafahamu
Kibatala: Nikumbushe Kozi Uliyosoma Kwamba Ulisomea Masuala ya Ugaidi Botswana
Shahidi: Post Blast Scene Investigation
Kibatala: Ni sahihi Kuwa Kozi hiyo inahusu Juu ya Uchunguzi Baada ya Milipuko
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Umesoma Sheria yetu ya Ugaidi hapa Tanzania
Shahidi: Nimesoma Kidogo
Kibatala: Umesoma Kuhusu Vifungu Vinavyo husika na Ufadhili wa Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Vipengele Vinavyo husika Katika Ufadhili wa Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Taja
Shahidi: 1. anayetuma lazima awe anafahamu Malengo ya fedha 2. siyo lazima awepo eneo la Tukio 3. Siyo lazima Matumizi ya pesa yajuliikane
Kibatala: Kwa hiyo hata Uchunguzi Wako Ulifuata hicho Ulicho elewa wewe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Conclusion Yako ilijilita Katika Tafsiri hiyo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Uwepo wa Pesa yenyewe ni sehemu ya Shitaka
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je nilitaka kutuma pesa Kufadhili Kitengo Cha Ugaidi Mtwara, Je Ikiwa pesa ile imeenda Kutumika Kwenye Kilimo cha Mpunga Ifakara, Je Nitakuwa nimefadhili Ugaidi
Shahidi: Inategemea
Kibatala: Inategemea na nini
Shahidi: pesa kama Imekwenda
Kibatala: Narudi swali, Je nilitaka kutuma pesa Kufadhili Kitengo Cha Ugaidi Mtwara, Je Ikiwa pesa ile imeenda Kutumika Kwenye Kilimo cha Mpunga Ifakara, Je Nitakuwa nimefadhili Ugaidi
Shahidi: Ndiyo unakuwa umefadhili Ugaidi
Kibatala: Je una Ushahidi Wowote Kwamba Ile 199,000 ilitumika Kule Moshi Walipokuwa Wamefika
Shahidi: Hilo sifahamu, najua tu kuwa walifadhili
Kibatala: Maelezo Ya Luteni Denis Urio anasema alitumiwa Kiasi cha TSh 500,000 katika Simu yake ya 0787 555200, Je alikwambia
Shahidi: aliniambia
Kibatala: 500,000 Kwa Mujibu wa Denis Urio, Mbowe alituma Kwa sababu gani
Shahidi: Kwa sababu ya Kufadhili Vitendo Vya Kigaidi
Kibatala: ambavyo ni Vitendo Vipi
Shahidi: Kulipua Vituo Vya Mafuta kukata Miti Barabarani Kudhuru Viongozi Wa Serikali
Kibatala: Unafahamu Kwamba Luteni Denis Urio anasema Katika Maelezo Yake kwamba aliwapa Khalfani Bwire na Moses Lijenje aliwapa Kuwa Refund Kama nauli
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba afafanue Je ana refer katika Maelezo au Ushahidi
Kibatala: Katika Statement yake Denis Urio anasema alitoa TSh 300,000 akawapa Moses Lijenje na Khalfani Bwire Na Katika Ushahidi Wake Denis Urio anasema Kuwa aliwapa 150,000 kila Mmoja Kuwarejeshea nauli huko alipotaka, Je unafahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kati yako wewe na Denis Urio nani yupo katika nafasi Nzuri ya Kufahamu Jinsi pesa Ilivyo gawiwa na kutumika
Shahidi: Ni Luten Denis Urio
Kibatala: Je Shahidi Ulisoma Maelezo Ya Onyo ya Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya
Shahidi: Nilisoma ila Sikumbuki Kiwango
Kibatala: Ungependa Kujikumbusha au Usinge penda
Shahidi: Ningependa Kujikumbusha
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Kielelezo Namba 1 na Kielelezo namba 13
Kibatala: Tuanze na Maelezo ya Adam Kasekwa
Kibatala: Tafuta sehemu ambapo anasema Tarehe 24 July 2020 Nilikutana na Mohammed Ling'wenya
Shahidi: "Tarehe 24 July 2020 Nilikutana na Mohammed Ling'wenya kasisitiza tuende Morogoro tukakutane na Luteni Urio tuliondoka Siku hiyo hiyo na Kukutana na Luteni Denis Urio, akasema Maelezo tutayakuta huko huko, Akatupa TSh 87,000 kila Mtu nauli ya Kwenda Moshi
Kibatala: TSh ngapi Umesoma
Shahidi: Ni TSh 87,000 kila Mmoja
Kibatala: Ulilinganisha Maelezo ya Mohammed Ling'wenya ni TSh kapewa dhidi ya Maelezo Ya Luten Denis Urio
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kama Mpelelezi Makini kabisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Luteni Denis Urio, alikwambia aliwapa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Ungependa ujikumbushe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba D4
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hicho Kielelezo alikitoa Shahidi namba 12 akitoa Ushahidi Wake, Kwa hiyo Kilikuwa katika Matumizi ya Shahidi D4 tu, Siyo Sahihi kukitumia Wakati huu
Kibatala: Mh Jaji Kaka Yangu hafahamu, Mimi nimejemga foundation kwa sababu Shahidi Ndiye aliye Muhoji Luteni Denis Urio, na Nyaraka hii ipo Mahakamani Kama Kumbukumbu za Mahakama Hiki ni Kielelezo cha Utetezi.. Naomba ni Ruhusiwe Kuendelea bila Kuwapa nafasi ya Kuficha Ushahidi
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula Mheshimiwa Jaji nimesikia Kibatala amba Wenzetu waliomba Kielelezo hiki kwa Matumizi yao, na Waliomba kwa Kutumia Kifungu cha 154 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya 6.. Dhumuni ni Kum Contradict Shahidi ambaye alikuwa ni Denis Urio, Leo hii anaposimama
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji anachokifanya wakili Abdallah Chavula Kuhusu Kutaja Vifungu,
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Samahani
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa huyu anasimama kama Nani Mwenye Hoja Kakaa Chini, Mheshimiwa Jaji Wakili Pius Hilla anafanya Vurugu
Jaji: Wakili Peter Kibatala Kaa Kwanza, Tumsililize
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Anachokifanya Wakili Peter Kibatala siyo Sahihi, Harusiwi Kutumia hayo Maelezo Kwa sababu yalikuwa kwa kazi ile tuh
Jaji: Ulisimama Wakili Kibatala
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Nimesimama na Mwenye Hoja akakaa Chini kwa sababu ni Educated, Kumbukumbu zitaonyesha nani alifanya Vurugu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mheshimiwa Jaji Hoja yangu ni kwamba Sijaleta Neno Jipya, Kuhusu Rejoinder ni Kujibu yale aliyo yajibu yeye, Hilo siyo Lengo letu
Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa kuwa Mwenzangu ametaja Vifungu na Mambo Mapya, Naomba Sasa Nipewe nafasi ya Ku' respond Kuhusu Vifungu
Jaji: Nimuache Kuhusu Kujibu Vifungu
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Muache aseme Kuhusu Vifungu, Kwa sababu Sheria haina Kificho
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Wakati Wakili Robert Kidando anataja Hoja yake hakutaja Kuhusu Vifungu Vya Sheria
JAJI: lakini Sasa Wakili Chavula alikuwa hajamaliza
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji nilikuwa naeleza Kwamba Kifungu walicho Kutumia Wenzetu Kilikuwa ni Kifungu cha 164 na Kuhusu Kupokelewe Mahakamani Mahakama ilitumia Kifungu cha 154, Kwa Sheria ambayo niliyokuwa nayo Mimi inaonekana
Katika Mstari Wa tatu wa 154 ambayo haina Subsections ANASOMA Sisi tuna tulia Mkazo katika "intended to Contradict" na "for the purpose of Contradict" Kama shahidi ni Maker wa Ile Nyaraka, Then sawa,
Hata Ile Dhana ya fairness Haipo, Ndiyo Maana Wanasheria Waka Limit itike kwa ile tuh, Kwa Dhana hiyo, Mwenzetu hana Uwezo wa kuitumia
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwanza Maneno "Maker " ni Maneno Binafsi wala Siyo Kwenye Sheria, Sheria inasema Kwamba Kama ameshiriki, Ku reduce into Writing, Hata katika hiyo 164 haikuweka Ukuta/zuio, Kifungu cha 164 ni Kufungu Kinacho zungumzia Kuingizia
164(c) unasema By Proof of former Statement, Hakuna Ukuta au Zuio, Huyu tunamuuliza kwa sababu nidiyo Mpelelezi, Kwamba atanyimwa Haki Ya Kuzungumza wakati Kuna Re examination, Shahidi ame Own suala la hayo Maelezo
Na Ikumbukwe Mheshimiwa Jaji Shahidi amesha Jibu tayari Kuhusu hiyo Statement, Vipi Ukimikataza sasa hivi na Yale Majibu ya awali, Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.
Jaji: Hoja Iliyo jitokeza ni Hoja ilianza kwa Mr Kidando Kwamba Upande wa Utetezi hawana Haki ya Kutumia Kielelezo husika, Ambapo akasimama Wakili Abdallah Chavula Kwa Kutaja Vifungu Vya Sheria, Kwamba Statement hiyo Inatumika Kwa Kum Contradict Shahidi namba 12 na siyo Vinginevyo.
Hoja hiyo ilipingwa na Upande wa Utetezi Kwamba Vifungu haviweki katazo, Mahakama kwa kuzingatia Hoja zote Kwa Kina, Inafahamu kwamba Upande wa Utetezi kwa shahidi aliyepo Mahakamani lao yao ni Kutengeneza Misingi, Shahidi aliyepo Mahakamani ni Mpelelezi Wa Shauri hili.
Wakati anaulizwa na Mawakili Wengine alisema Kwamba alitumia Nyaraka Zote Katika Upelelezi Kufikia katika hitimisho, Kwa Maana hiyo anaulizwa kuhusu Kitu alicho fanya nacho kazi, Ndiye aliye Muandika Maelezo ya Luten Denis, Kama hawezi Kujibu atatuambia kuwa hawezi.
Jaji: Kwa sababu hiyo Hatuoni sehemu ambayo ina udhibiti wa Kuendelea Kujibu. Kwa Maana hiyo Mahakama Inaruhusu Kutumika Kwa Kielelezo hicho.
Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Uamuzi Jaji kwa Kusimama na Kumuinamia Kidogo (kimasta zaidi) ile dizaini ya shivooo
Kibatala: Shahidi Tulikubaliana kuwa Moja ya Investigative tool au Workonh tool ni hii statement ya Pesa na Maelezo haya
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Soma pale Baada ya Kupokea Pesa hizo nilizitoa
Shahidi: Tarehe 22 July 2020 Baada ya Kupokea Pesa hizo nilizitoa, na Kuwapatia Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa Kama nauli
Kibatala: Sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Ile Tsh 87,000 anayosema Adam Kasekwa kila Mmoja, Je wewe Kama Mpelelezi unaona TSh 87,000 ya Adamoo na Ling'wenya inaendana na Taarifa ya Mtoa Taarifa Wenu
Shahidi: Hilo linahitaji Maelezo, Wote wanaelezea Swala la pesa, Luteni Denis Urio anasema aliwapa 190,000
Kibatala: TSh 190,000 Ipo wapi
Shahidi: Vyote Vinaendana Maelezo ya Denis Urio na akina Adam Kasekwa
Kibatala: sawasawa wacha Jibu lako liingie
Kibatala: Kama Walipewa Kila Mmoja TSh 87,000, Jumla ni TSh ngapi
Wakili wa Serikali: Samahani Ukisoma Statement ya Mshtakiwa Wa Pili (Kielelezo namba 1) kwamba alitupa nauli TSh 87,000 kila Mtu, Huku alipo Mrejesha katika TSh 199,000 aliyo wapa Adamoo na Ling'wenya
Kibatala: HAKUNA HOJA HAPO.
Jaji: Kabla ya hapo, Hoja yao ni kwamba kila Utakapo taja TSh 199,000 usiseme nauli
Kibatala: Kwenye hiyo Mheshimiwa Jaji, haina shida Nitarudi Nyuma na Kujenga Upya Misingi kurahisisha
Wakili wa Serikali Robert Kidando anamfuata Shahidi na Kutetea naye Kidogo
Shahidi: SAMAHANI MHESHIMIWA JAJI SIJISIKII VIZURI KWA KWELI.......
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Nimeongea na shahidi anasema hajisikii Vizuri kabisaaaaaa, na kapatwa na tatizo ghafla.. Mheshimiwa Jaji naomba tuweze Kupatiwa na airisho
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sisi tunaamini kuwa airisho linaombwa kwa sababu nyingine siyo sababu ya ugonjwa...
Wakili wa Serikali: Lakini Mwenzetu Kusema Shahidi aendelee tu sababu fulani fulani nafikiri Mheshimiwa Jaji si Vyema Kusema hivyo.. Baada ya Kusema hayo naomba airisho
Jaji: Je airisho la saa Moja, mpaka saa 7 au airisho la Siku Nzima au nini
Wakili wa Serikali Robert Kidando: anamfuata tena shahidi wa Jamhuri
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji anaomba airisho Mpaka Kesho pamoja hatuwezi Kujua itakuwaje..
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sisi tuna wasiwasi sana na Sababu zilizotolewa na Shahidi Kama ni sababu Njema, Sisi tunapinga airisho Mpaka Kesho, Ikupendeze Uairishe Mpaka Saa 9 Alasiri.. Tuje tuone progress Kwa sababu airisho linalo ombwa lina athiri Haki za Wateja wetu..
Na tutakaporejea tunaomba Shahidi aje na Uthibitisho Kwamba alikwenda Hospitali na alitibiwa, Ishawahi Kutokea Mara Kadhaa, Inspector Jumanne Malangahe hapa alisema hivyo hatukuona Uthibitisho, Inspector Ndowo alifanya hivyo hakuleta Uthibitisho na Sasa ni huyu
Hii ni Mahakama, Wateja Wangu Wanayo Haki ya Kufahamu au Kuona Japo Kuna Haki na kweli Inatendeka..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji anasema ana Wasiwasi, na Mheshimiwa Jaji hatuwezi kucheza na Haki za Watu, Ninachokumbuka Shahidi aliongea Asubuhi kuwa Leo hajisikii Vizuri.. Hizi Proceedings serious hatuwezi Kuleta Mzaha..
Wakili wa Serikali: Naomba airisho Mpaka Kesho ijulikane itakuwaje baada ya Shahidi Kupata Matibabu
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kurudisha Vielelezo
Jaji amekuwa kimya hapa akiandika
Jaji: Kufuatia Maombi yaliyoletwa na Shahidi, Kwamba Shahidi hajisikii Vizuri na Maombi hayo yaliungwa Mkono na Mawakili wa Serikali, Shahidi ameomba nafasi ya kwenda Kupata Matibabu, Maombi haya yamepingwa na Mawakili wa pande wa Utetezi kupitia Wakili Peter Kibatala
Kwamba Shahidi anakwepa Maswali ya Dodoso, Na Kwamba Kuna Mifano Kadhaa ya Mashahidi Waliopita, Na Kwamba Mahakama Itoe airisho Mpaka Saa 9 Alasiri.. Kwa Kuzingatia Maombi ya pande zote mbili na Shahidi Mwenyewe, Ukizingatia Shahidi alisema Kwamba Asubuhi hajisikii Vizuri
Katika Utoaji Haki wa Mahakama Zetu Shahidi lazima awe na Uwezo na Kusimama au Kukaa, Shahidi ameshasema hajisikii Vizuri, Kwa hiyo Mahakama Haiwezi Kwenda tofauti na Utaratibu juo, Mahakama Inaona Swala la Shahidi Kusema hajisikii Vizuri ni swala la Kutoa Hairisho
Na Suala linalobakia ni airisho Mpaka Muda gani, Mahakama Inaona kwamba suala la Ugonjwa siyo Suala la Kununua Spea na Kurudisha ni Suala la Afya, Mahakama Haiwezi Kumpangia Muda wa Kupata Matibabu, Kwa sababu hiyo Mahakama Inatoa airisho Mpaka Kesho
Suala la Hoja ya Utetezi wa kwamba Shahidi alikuwa anaumwa ni suala Muhimu hata Kama Uthibitisho huo utakuwa into details, Lengo ni Kulinda Privacy yake Shahidi.. Shahidi nakuonya Utatakiwa kuwa Kizimbani Kesho Saa 3 Asubuhi, Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 3 Kamili
Jaji anatoka Mahakamani
Leo 09/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki:Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 9, 2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
- Wakili Pius Hilla
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Ignasi Mwinuka
- Mawakili Wa Serikali Waandamizi
- Wakili Tulimanywa Majige
- Wakili Michael Mwangasa
- Gaston Garubindi
- Evaresta Kisanga
- Maria Mushi
- John Masoud kwa Niaba ya Nashon Nkungu
- Clinton Kipengele Kwa niaba ya John Mallya
- Fredrick Kihwelo
- Dickson Matata
Wakili Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili Kuendelea Kusikilizwa na tupo tayari Kuendelea
Peter Kibatala: Nasi pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea
Shahidi anapanda kisha anasimama Kizimbani Jaji anaandika Kidogo
Jaji: Shahidi nakukumbusha Ulikuwa chini ya Kiapo na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo
Shahidi: Sawa Mheshimiwa, Ila kuanzia Jana Jioni hali yangu haikuwa Nzuri lakini nitaendelea Kutoa Ushahidi
Kibatala: Good Morning Inspector
Shahidi: Morning
Kibatala: Nafikiri Unakumbuka Jana tulikuwa kwenye Swala la Mbowe Kuanzisha Ugaidi
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Tulijadili Mpaka Pale ambapo Washitakiwa Walikutana pale Morogoro na Luteni Denis Urio
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Upelelezi wako Uligundua hivyo
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Na aliye Waita pale alikuwa ni Luteni Denis Urio
Kibatala: Na Utakubaliana na Mimi Kuwa Mpaka Mshitakiwa Wa Kwanza, Wapili na watatu anakutana na Denis Urio Mbowe alikuwa hawajui na hajawahi Kukutana nao
Shahidi: sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba kabla ya Kukutana Walikuwa wanafanya Shughuli zao halali
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Luteni Denis Urio aliwaita Morogoro Kwa sababu Yeye Makazi yake yalikuwa Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa namna yoyote Ile Freeman Mbowe Hakuwahi kuwa Morogoro kabla na baada ya hizo Tarehe walizokutana Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Uliwahi Kugundua Kwa wewe Kuwa Pro Active au Kuhalifiwa na Luten Denis Urio Kwamba kabla ya Mohammed Ling'wenya Kuondoka Mtwara Kuja Morogoro, ilibidi awasiliane na Mzee Ling'wenya Kupata Ruhusa
Shahidi: Sikuwahi Kufahamu
Kibatala: Pia hufahamu Luteni Denis Urio alitoa Ushahidi Mahakamani akithibitisha
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo hata nikikwambia Kwamba Mzee Ling'wenya ilibidi aitishe Kikao cha Ukoo/Familia Kujadili suala la Mtoto wao Kwenda Kwa Luteni Denis Urio
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Pia ufahamu Kwamba Wakati Wanamtoa Walimtoa Kwa Uangalizi Kwamba Wanamkabidhi Kwa Luten Denis Urio na Kwa Freeman Mbowe, Kwa sababu ni watu wanao aminika
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale
Shahidi: Fafanua tena
Kibatala: Ulikuwa unafahamu Kwamba Luteni Denis Urio, alikutana na Makundi Mawali Kwa wakati tofauti
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: aliyewaambia Bwire na Moses Lijenje na aliyewaambia Adamoo na Ling'wenya alikuwa ni Luteni Denis Urio, Je ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unaposema Kwamba alipo wasiliana na Mbowe aliwasiliana Meseji, Telegram au Simu
Shahidi: Kwa Njia ya Mdomo na Pia kwa Njia ya Mawasiliano ya Jumbe za Telegram
Kibatala: Walipoongea Denis Urio na Freeman Mbowe wewe Ulikuwepo
Shahidi: Sikuwepo
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Ulishawahi Kusikia Neno Maarufu la Kiupelelezi la "Your Word against Mine"
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kwa kuwa Wewe, Kingai, DCI hamkuwepo Wakati Mbowe anaongea na Urio
Shahidi: Hatukwepo lakini tulifanya Upelelezi
Kibatala: Watu Wawili wamezungumza, Na DCI hakuwepo, Kingai hakuwepo, na wewe hukuwepo Je si lazima sasa Tupime Maneno ya Denis Urio na Freeman Mbowe
Shahidi: Siyo lazima, Unaweza Kufanyia Kazi Maneno ya Denis Urio
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Wakati Denis Urio anakutajia Kuwa Kuna Cassa Motel, Je Uliwahi Kwenda hata Kuthibitisha
Shahidi: Sijawahi Kwenda
Kibatala: Mgahawa ambao Denis Urio alitaja Wamekutana na Mbowe Wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Urio aliwahi Kukwambia Kwamba alipanda Tax Mgulani
Shahidi: sikwenda
Kibatala: Je aliwahi Kukwambia Kwamba alikuwa Mjini alipanda bodaboda
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Uliwahi Kufika Kuona Kama Kuna Kituo cha Bodaboda
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Uliwahi Kwenda Cassa Motel Kuthibitisha Kama Gari ya Denis Urio lilifika pale
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Uliwahi Kwenda Mgulani Kuthibitisha Kwamba Denis Urio aliwahi Kufika na Kuishi Pale
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Nyie Kama Polisi mkipata Taarifa Mnairekodi au Kufanyia kazi
Shahidi: Tunafanya kazi
Kibatala: Je wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda 14 July 2020 Kule Ngerengere 92 KJ Ka kweli alikuwa kazini
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Baada tu ya Kurejea Kutoka Darfur alikamatwa Kikosini baada ya Kutajwa na Adam Kasekwa
Shahidi: Sifahamu nilifanya Uchunguzi
Kibatala: Kwakuwa umechunguza Kule 92 KJ uliongea na nani
Shahidi: Nisha sema Sikwenda
Kibatala: Kwa hiyo wewe hata 92KJ hufahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Makampuni ya Simu yanatunza Kumbukumbu za Mawasiliano
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Yanatunza Kwa Muda gani
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Je Wewe Kama Mpelelezi Uliomba Taarifa za Call Recordings katika Makampuni ya Simu Kati ya Freeman Mbowe na Denis Urio
Shahidi: Ndiyo Niliomba
Kibatala: Kwa Barua ya Tarehe Ngapi
Shahidi: Kwa Barua ya 13 August 2020
Kibatala: kwenda Kampuni gani
Shahidi: Kwenda Kwenye Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao
Kibatala: Kwa Inspector Ndowo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo wewe Uliomba Taarifa Kwa Inspector Ndowo, Je yeye ndiye Mwenye Kuhifadhi
Shahidi: Yeye Ndiye aandike Barua kwenda Tigo na Airtel
Kibatala: kwa hiyo wewe Pamoja na Mambo yote Uli Mwomba Na Rekodi za Mawasiliano ya simu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je wewe Uliona Katika Barua yake kutoka Kwenu Terms of reference suala la Call Recordings lipo
Shahidi: Halipo
Kibatala: kwa hiyo Mliomba au Hamkuomba
Shahidi: Hatukuomba
Kibatala: Uwe sasa inasililiza kwa Makini.. Haya Unafahamu Kuhusu Sheria ya EPOCA
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo ufahamu Kwamba Sheria hiyo nakupa Mamlaka Ya Kuomba Voice Recordings
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Wakati DCI na Kingai Wanakuteua waliluteua Kwa sababu ya Uwezo au Sababu ya Kitengo X
Shahidi: Sababu ya Uwezo
Kibatala: Hivi una Elimu gani
Shahidi: Kidato cha 6
Kibatala: Sekondari gani
Shahidi: Moshi
Kibatala: Ulipata Division ngapi
Shahidi: Division 3 Point 13
Kibatala: ulifaulu Kwenda Chuo
Shahidi: Hapana, CCP Moshi
Kibatala: Ok! Ndiyo Walikuchagua sababu ya uwezo huko
Kibatala: Je unafahamu Mojawapo Ya Majukumu ya Upelelezi wako ilikuwa Ku Trace kila single Cents
Shahidi: Hilo siyo Muhimu cha Muhimu Kama alitoa pesa kufadhili Ugaidi
Kibatala: Swali langu nasema kwamba Kama Mpelelezi unajukumu la Ku Account for na Ku Trace Kila single Cent
Shahidi: Nisha Jibu Kuwa siyo Muhimu
Kibatala: Je nani alikuwa na Jukumu la Kuona na Kuthibitisha zile pesa
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Na hilo Jukumu Uliteleleza Kikamilifu la Ku Trace hizo pesa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Tayari Kwamba Denis Urio alituambia kuwa Watuhumiwa Walisafiri Kutoka Walipo kuwa Kuja Morogoro, Je Unafahamu Kwamba Walikuwa Refunded
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji nani alitoa Pesa Kuwa Refund (rejeshea)
Shahidi: Luteni Denis Urio
Kibatala: Na Kwamba Unafahamu Kwamba Hawa walikuwa wanajua Kuwa walikuwa wanapewa Pesa Kurejeshewa Nauli zao
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu Kwamba ni TSh ngapi Moses Lijenje alirejeshewa
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Lini wewe Ulifahamu Kuwa Unakuja Kutoa Ushahidi
Shahidi: Alhamisi
Kibatala: Hiyo Taarifa Ulipewa na Watu serious au Uliwa chukuliwa poa
Shahidi: Nilichukua Serious
Kibatala: Hii Kesi ni Kubwa au Nyepesi
Shahidi: Kubwa
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi ni nani atakuja kutueleza Kuhusu mabadilishano ya Pesa kati ya Moses Lijenje na Khalfani Bwire kutoka kwa Denis Urio
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Shahidi anaitwa Gladys Fimbari kutoka Airtel alileta Taarifa Ya Mihamala, Je Ulisoma na Kuelewa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Pesa ambayo Wali badirishana Mikono kati Adam Kasekwa na Denis Urio ilikuwa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Pesa ambayo ilibadilishana Mikono katika ya Mohammed Ling'wenya na Denis Urio ni TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Ni wewe ulimuhoji Denis Urio
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: alikueleza?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ilikuwa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Pesa Iliyo badirishana Mikono kati ya Moses Lijenje na Khalfani Bwire ilikuwa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Unafahamu Pesa kiasi gani ambacho alipewa Mohammed Ling'wenya Nauli ya Kwemda Moshi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Wakati Washitakiwa wa Kwanza, Wapili na Watatu wanaenda Moshi Kama wanavyo Sema Watuhumiwa, Je Walikuwa Wanafahamu Wanaenda Kufanya Nini huko
Shahidi: Walikuwa hawafahamu
Kibatala: Nikumbushe Kozi Uliyosoma Kwamba Ulisomea Masuala ya Ugaidi Botswana
Shahidi: Post Blast Scene Investigation
Kibatala: Ni sahihi Kuwa Kozi hiyo inahusu Juu ya Uchunguzi Baada ya Milipuko
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Umesoma Sheria yetu ya Ugaidi hapa Tanzania
Shahidi: Nimesoma Kidogo
Kibatala: Umesoma Kuhusu Vifungu Vinavyo husika na Ufadhili wa Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Vipengele Vinavyo husika Katika Ufadhili wa Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Taja
Shahidi: 1. anayetuma lazima awe anafahamu Malengo ya fedha 2. siyo lazima awepo eneo la Tukio 3. Siyo lazima Matumizi ya pesa yajuliikane
Kibatala: Kwa hiyo hata Uchunguzi Wako Ulifuata hicho Ulicho elewa wewe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Conclusion Yako ilijilita Katika Tafsiri hiyo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Uwepo wa Pesa yenyewe ni sehemu ya Shitaka
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je nilitaka kutuma pesa Kufadhili Kitengo Cha Ugaidi Mtwara, Je Ikiwa pesa ile imeenda Kutumika Kwenye Kilimo cha Mpunga Ifakara, Je Nitakuwa nimefadhili Ugaidi
Shahidi: Inategemea
Kibatala: Inategemea na nini
Shahidi: pesa kama Imekwenda
Kibatala: Narudi swali, Je nilitaka kutuma pesa Kufadhili Kitengo Cha Ugaidi Mtwara, Je Ikiwa pesa ile imeenda Kutumika Kwenye Kilimo cha Mpunga Ifakara, Je Nitakuwa nimefadhili Ugaidi
Shahidi: Ndiyo unakuwa umefadhili Ugaidi
Kibatala: Je una Ushahidi Wowote Kwamba Ile 199,000 ilitumika Kule Moshi Walipokuwa Wamefika
Shahidi: Hilo sifahamu, najua tu kuwa walifadhili
Kibatala: Maelezo Ya Luteni Denis Urio anasema alitumiwa Kiasi cha TSh 500,000 katika Simu yake ya 0787 555200, Je alikwambia
Shahidi: aliniambia
Kibatala: 500,000 Kwa Mujibu wa Denis Urio, Mbowe alituma Kwa sababu gani
Shahidi: Kwa sababu ya Kufadhili Vitendo Vya Kigaidi
Kibatala: ambavyo ni Vitendo Vipi
Shahidi: Kulipua Vituo Vya Mafuta kukata Miti Barabarani Kudhuru Viongozi Wa Serikali
Kibatala: Unafahamu Kwamba Luteni Denis Urio anasema Katika Maelezo Yake kwamba aliwapa Khalfani Bwire na Moses Lijenje aliwapa Kuwa Refund Kama nauli
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba afafanue Je ana refer katika Maelezo au Ushahidi
Kibatala: Katika Statement yake Denis Urio anasema alitoa TSh 300,000 akawapa Moses Lijenje na Khalfani Bwire Na Katika Ushahidi Wake Denis Urio anasema Kuwa aliwapa 150,000 kila Mmoja Kuwarejeshea nauli huko alipotaka, Je unafahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kati yako wewe na Denis Urio nani yupo katika nafasi Nzuri ya Kufahamu Jinsi pesa Ilivyo gawiwa na kutumika
Shahidi: Ni Luten Denis Urio
Kibatala: Je Shahidi Ulisoma Maelezo Ya Onyo ya Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya
Shahidi: Nilisoma ila Sikumbuki Kiwango
Kibatala: Ungependa Kujikumbusha au Usinge penda
Shahidi: Ningependa Kujikumbusha
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Kielelezo Namba 1 na Kielelezo namba 13
Kibatala: Tuanze na Maelezo ya Adam Kasekwa
Kibatala: Tafuta sehemu ambapo anasema Tarehe 24 July 2020 Nilikutana na Mohammed Ling'wenya
Shahidi: "Tarehe 24 July 2020 Nilikutana na Mohammed Ling'wenya kasisitiza tuende Morogoro tukakutane na Luteni Urio tuliondoka Siku hiyo hiyo na Kukutana na Luteni Denis Urio, akasema Maelezo tutayakuta huko huko, Akatupa TSh 87,000 kila Mtu nauli ya Kwenda Moshi
Kibatala: TSh ngapi Umesoma
Shahidi: Ni TSh 87,000 kila Mmoja
Kibatala: Ulilinganisha Maelezo ya Mohammed Ling'wenya ni TSh kapewa dhidi ya Maelezo Ya Luten Denis Urio
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kama Mpelelezi Makini kabisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Luteni Denis Urio, alikwambia aliwapa TSh ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Ungependa ujikumbushe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba D4
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hicho Kielelezo alikitoa Shahidi namba 12 akitoa Ushahidi Wake, Kwa hiyo Kilikuwa katika Matumizi ya Shahidi D4 tu, Siyo Sahihi kukitumia Wakati huu
Kibatala: Mh Jaji Kaka Yangu hafahamu, Mimi nimejemga foundation kwa sababu Shahidi Ndiye aliye Muhoji Luteni Denis Urio, na Nyaraka hii ipo Mahakamani Kama Kumbukumbu za Mahakama Hiki ni Kielelezo cha Utetezi.. Naomba ni Ruhusiwe Kuendelea bila Kuwapa nafasi ya Kuficha Ushahidi
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula Mheshimiwa Jaji nimesikia Kibatala amba Wenzetu waliomba Kielelezo hiki kwa Matumizi yao, na Waliomba kwa Kutumia Kifungu cha 154 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya 6.. Dhumuni ni Kum Contradict Shahidi ambaye alikuwa ni Denis Urio, Leo hii anaposimama
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji anachokifanya wakili Abdallah Chavula Kuhusu Kutaja Vifungu,
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Samahani
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa huyu anasimama kama Nani Mwenye Hoja Kakaa Chini, Mheshimiwa Jaji Wakili Pius Hilla anafanya Vurugu
Jaji: Wakili Peter Kibatala Kaa Kwanza, Tumsililize
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji Anachokifanya Wakili Peter Kibatala siyo Sahihi, Harusiwi Kutumia hayo Maelezo Kwa sababu yalikuwa kwa kazi ile tuh
Jaji: Ulisimama Wakili Kibatala
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Nimesimama na Mwenye Hoja akakaa Chini kwa sababu ni Educated, Kumbukumbu zitaonyesha nani alifanya Vurugu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mheshimiwa Jaji Hoja yangu ni kwamba Sijaleta Neno Jipya, Kuhusu Rejoinder ni Kujibu yale aliyo yajibu yeye, Hilo siyo Lengo letu
Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa kuwa Mwenzangu ametaja Vifungu na Mambo Mapya, Naomba Sasa Nipewe nafasi ya Ku' respond Kuhusu Vifungu
Jaji: Nimuache Kuhusu Kujibu Vifungu
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Muache aseme Kuhusu Vifungu, Kwa sababu Sheria haina Kificho
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Wakati Wakili Robert Kidando anataja Hoja yake hakutaja Kuhusu Vifungu Vya Sheria
JAJI: lakini Sasa Wakili Chavula alikuwa hajamaliza
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji nilikuwa naeleza Kwamba Kifungu walicho Kutumia Wenzetu Kilikuwa ni Kifungu cha 164 na Kuhusu Kupokelewe Mahakamani Mahakama ilitumia Kifungu cha 154, Kwa Sheria ambayo niliyokuwa nayo Mimi inaonekana
Katika Mstari Wa tatu wa 154 ambayo haina Subsections ANASOMA Sisi tuna tulia Mkazo katika "intended to Contradict" na "for the purpose of Contradict" Kama shahidi ni Maker wa Ile Nyaraka, Then sawa,
Hata Ile Dhana ya fairness Haipo, Ndiyo Maana Wanasheria Waka Limit itike kwa ile tuh, Kwa Dhana hiyo, Mwenzetu hana Uwezo wa kuitumia
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwanza Maneno "Maker " ni Maneno Binafsi wala Siyo Kwenye Sheria, Sheria inasema Kwamba Kama ameshiriki, Ku reduce into Writing, Hata katika hiyo 164 haikuweka Ukuta/zuio, Kifungu cha 164 ni Kufungu Kinacho zungumzia Kuingizia
164(c) unasema By Proof of former Statement, Hakuna Ukuta au Zuio, Huyu tunamuuliza kwa sababu nidiyo Mpelelezi, Kwamba atanyimwa Haki Ya Kuzungumza wakati Kuna Re examination, Shahidi ame Own suala la hayo Maelezo
Na Ikumbukwe Mheshimiwa Jaji Shahidi amesha Jibu tayari Kuhusu hiyo Statement, Vipi Ukimikataza sasa hivi na Yale Majibu ya awali, Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.
Jaji: Hoja Iliyo jitokeza ni Hoja ilianza kwa Mr Kidando Kwamba Upande wa Utetezi hawana Haki ya Kutumia Kielelezo husika, Ambapo akasimama Wakili Abdallah Chavula Kwa Kutaja Vifungu Vya Sheria, Kwamba Statement hiyo Inatumika Kwa Kum Contradict Shahidi namba 12 na siyo Vinginevyo.
Hoja hiyo ilipingwa na Upande wa Utetezi Kwamba Vifungu haviweki katazo, Mahakama kwa kuzingatia Hoja zote Kwa Kina, Inafahamu kwamba Upande wa Utetezi kwa shahidi aliyepo Mahakamani lao yao ni Kutengeneza Misingi, Shahidi aliyepo Mahakamani ni Mpelelezi Wa Shauri hili.
Wakati anaulizwa na Mawakili Wengine alisema Kwamba alitumia Nyaraka Zote Katika Upelelezi Kufikia katika hitimisho, Kwa Maana hiyo anaulizwa kuhusu Kitu alicho fanya nacho kazi, Ndiye aliye Muandika Maelezo ya Luten Denis, Kama hawezi Kujibu atatuambia kuwa hawezi.
Jaji: Kwa sababu hiyo Hatuoni sehemu ambayo ina udhibiti wa Kuendelea Kujibu. Kwa Maana hiyo Mahakama Inaruhusu Kutumika Kwa Kielelezo hicho.
Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Uamuzi Jaji kwa Kusimama na Kumuinamia Kidogo (kimasta zaidi) ile dizaini ya shivooo
Kibatala: Shahidi Tulikubaliana kuwa Moja ya Investigative tool au Workonh tool ni hii statement ya Pesa na Maelezo haya
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Soma pale Baada ya Kupokea Pesa hizo nilizitoa
Shahidi: Tarehe 22 July 2020 Baada ya Kupokea Pesa hizo nilizitoa, na Kuwapatia Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa Kama nauli
Kibatala: Sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Ile Tsh 87,000 anayosema Adam Kasekwa kila Mmoja, Je wewe Kama Mpelelezi unaona TSh 87,000 ya Adamoo na Ling'wenya inaendana na Taarifa ya Mtoa Taarifa Wenu
Shahidi: Hilo linahitaji Maelezo, Wote wanaelezea Swala la pesa, Luteni Denis Urio anasema aliwapa 190,000
Kibatala: TSh 190,000 Ipo wapi
Shahidi: Vyote Vinaendana Maelezo ya Denis Urio na akina Adam Kasekwa
Kibatala: sawasawa wacha Jibu lako liingie
Kibatala: Kama Walipewa Kila Mmoja TSh 87,000, Jumla ni TSh ngapi
Wakili wa Serikali: Samahani Ukisoma Statement ya Mshtakiwa Wa Pili (Kielelezo namba 1) kwamba alitupa nauli TSh 87,000 kila Mtu, Huku alipo Mrejesha katika TSh 199,000 aliyo wapa Adamoo na Ling'wenya
Kibatala: HAKUNA HOJA HAPO.
Jaji: Kabla ya hapo, Hoja yao ni kwamba kila Utakapo taja TSh 199,000 usiseme nauli
Kibatala: Kwenye hiyo Mheshimiwa Jaji, haina shida Nitarudi Nyuma na Kujenga Upya Misingi kurahisisha
Wakili wa Serikali Robert Kidando anamfuata Shahidi na Kutetea naye Kidogo
Shahidi: SAMAHANI MHESHIMIWA JAJI SIJISIKII VIZURI KWA KWELI.......
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Nimeongea na shahidi anasema hajisikii Vizuri kabisaaaaaa, na kapatwa na tatizo ghafla.. Mheshimiwa Jaji naomba tuweze Kupatiwa na airisho
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sisi tunaamini kuwa airisho linaombwa kwa sababu nyingine siyo sababu ya ugonjwa...
Wakili wa Serikali: Lakini Mwenzetu Kusema Shahidi aendelee tu sababu fulani fulani nafikiri Mheshimiwa Jaji si Vyema Kusema hivyo.. Baada ya Kusema hayo naomba airisho
Jaji: Je airisho la saa Moja, mpaka saa 7 au airisho la Siku Nzima au nini
Wakili wa Serikali Robert Kidando: anamfuata tena shahidi wa Jamhuri
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji anaomba airisho Mpaka Kesho pamoja hatuwezi Kujua itakuwaje..
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sisi tuna wasiwasi sana na Sababu zilizotolewa na Shahidi Kama ni sababu Njema, Sisi tunapinga airisho Mpaka Kesho, Ikupendeze Uairishe Mpaka Saa 9 Alasiri.. Tuje tuone progress Kwa sababu airisho linalo ombwa lina athiri Haki za Wateja wetu..
Na tutakaporejea tunaomba Shahidi aje na Uthibitisho Kwamba alikwenda Hospitali na alitibiwa, Ishawahi Kutokea Mara Kadhaa, Inspector Jumanne Malangahe hapa alisema hivyo hatukuona Uthibitisho, Inspector Ndowo alifanya hivyo hakuleta Uthibitisho na Sasa ni huyu
Hii ni Mahakama, Wateja Wangu Wanayo Haki ya Kufahamu au Kuona Japo Kuna Haki na kweli Inatendeka..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji anasema ana Wasiwasi, na Mheshimiwa Jaji hatuwezi kucheza na Haki za Watu, Ninachokumbuka Shahidi aliongea Asubuhi kuwa Leo hajisikii Vizuri.. Hizi Proceedings serious hatuwezi Kuleta Mzaha..
Wakili wa Serikali: Naomba airisho Mpaka Kesho ijulikane itakuwaje baada ya Shahidi Kupata Matibabu
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kurudisha Vielelezo
Jaji amekuwa kimya hapa akiandika
Jaji: Kufuatia Maombi yaliyoletwa na Shahidi, Kwamba Shahidi hajisikii Vizuri na Maombi hayo yaliungwa Mkono na Mawakili wa Serikali, Shahidi ameomba nafasi ya kwenda Kupata Matibabu, Maombi haya yamepingwa na Mawakili wa pande wa Utetezi kupitia Wakili Peter Kibatala
Kwamba Shahidi anakwepa Maswali ya Dodoso, Na Kwamba Kuna Mifano Kadhaa ya Mashahidi Waliopita, Na Kwamba Mahakama Itoe airisho Mpaka Saa 9 Alasiri.. Kwa Kuzingatia Maombi ya pande zote mbili na Shahidi Mwenyewe, Ukizingatia Shahidi alisema Kwamba Asubuhi hajisikii Vizuri
Katika Utoaji Haki wa Mahakama Zetu Shahidi lazima awe na Uwezo na Kusimama au Kukaa, Shahidi ameshasema hajisikii Vizuri, Kwa hiyo Mahakama Haiwezi Kwenda tofauti na Utaratibu juo, Mahakama Inaona Swala la Shahidi Kusema hajisikii Vizuri ni swala la Kutoa Hairisho
Na Suala linalobakia ni airisho Mpaka Muda gani, Mahakama Inaona kwamba suala la Ugonjwa siyo Suala la Kununua Spea na Kurudisha ni Suala la Afya, Mahakama Haiwezi Kumpangia Muda wa Kupata Matibabu, Kwa sababu hiyo Mahakama Inatoa airisho Mpaka Kesho
Suala la Hoja ya Utetezi wa kwamba Shahidi alikuwa anaumwa ni suala Muhimu hata Kama Uthibitisho huo utakuwa into details, Lengo ni Kulinda Privacy yake Shahidi.. Shahidi nakuonya Utatakiwa kuwa Kizimbani Kesho Saa 3 Asubuhi, Washtakiwa wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Kesho Asubuhi Saa 3 Kamili
Jaji anatoka Mahakamani