The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,800
Leo tarehe 23/11/2021 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea baada ya kuahirishwa siku siku ya Jumatatu, tarehe 22 Novemba, 2021.
Kujua kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 22, 2021. Mahakama yatupilia mbali hoja tatu za utetezi. Kesi imeahirishwa hadi Novemba 23, 2021
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=========
UPDATES:
JAJI AMEINGIA MAHAKAMANI
Jaji ameshaingia Mahakamani
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa
Wakili wa Serikali Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Esther Martin
Nassoro Katuga
Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi
Jeremiah Mtobesya
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Seleman Matauka
Idd Msawanga
KHadija Aron
Maria Mushi
Jaji anaita Majina ya Washtakiwa wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: tuna shahidi Mmoja na tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Na sisi pia tupo tayari
Jaji: Enhe
Wakili wa Serikali: Shahidi ameenda Kuitwa
Shahidi anaingia
Jaji: Jina
Shahidi: 4347 Detective Afande Goodluck
Jaji: Miaka 32
Jaji: kabila
Shahidi: Mchagga
Jaji: Dini
Shahidi: Mkristo
Shahidi: Naapa kwamba Mimi H4347 Detective Sargent Goodluck Naapa kwamba Ushahidi Nitakao toa ni kweli, kweli tupu Eeh Mungu Nisaidie
Wakili wa Serikali: Pius Hilla Shahidi Unaitwa nani
Shahidi: Naitwa H4347 sergeant Goodluck
Wakili wa Serikali: Kazi yako
Shahidi: Askari Polisi
Wakili wa Serikali: Umeajiliwa tangu lini
Shahidi: 2013 Wakili wa Serikali Kituo chako cha Kazi ni wapi
Shahidi: Central Arusha
Wakili wa Serikali: Shahidi ieleze Mahakama Mnamo tarehe 04 August 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Kazi I Maeneo ya Central Police, Arusha
WS: Majira ya Jioni Siku hiyo Kitu gani Kilitokea
Shahidi: Afande Wangu Inspector Mahita alinipigia Simu na Kuniita Ofisini kwake
Wakili wa Serikali: Afande Mahita ni nani sasa hivi
Shahidi: Msaidizi Wa Mkuu wa Upelelezi
Wakili wa Serikali: Wa Wilaya gani
Shahidi: Arusha Mjini
Wakili wa Serikali: alikueleza Jambo gani
Shahidi: Aliniambia kuwa Mimi na Afande Francis tunahitajika kwa Afande RCO
WS: Wakati huo nani alikuwa RCO wa Arusha
Shahidi: alikuwa Afande Ramadhan Kingai
WS: Kwa Kingai Kitu gani kilitokea
Shahidi: Tulipofika kwa Kingai alituambia Kwamba tujiandae Kwa Safari Kuna kazi ya kwenda Kufanya
WS: Safari ya Kuelekea wapi
Shahidi: Wakati ule hakutuambia zaidi ya Tujiandae kwa Safari
WS: Ulijiandaaje Shahidi Baada ya Kutupa Maelekezo akatuambia tukachukue Silaha
WS: Baada ya hapo Nini Kilifanyika na Mkaelekea Wapi
Shahidi: Tulikuwa Afande RCO, Inspector Mahita, Mimi na Dereva wa RCO na Coplo Francis
WS: Taratibu Shahidi Jaji aweze Kuandika
Shahidi: Baada ya hapo tukaambiwa twende Arumeru Tukampitie Afande Jumanne ambaye ni OC CID wa Wilaya ya Arumeru
WS: Huko USA River Kwa Afande Jumanne Kitu gani Kilifanyika
Shahidi: Tulifika pale, tuka ingia ndani wote na Afande Kingai Akatupa Briefing Ya kazi tunayo kwenda Kufanya
WS: alisema Kitu gani
Shahidi: Akisema Kwamba amepata Taarifa Kwamba Kuna Kikundi KinajiPanga Kufanya Matendo ya Kigaidi hapa Nchini, na Kwamba ni Maeneo ya Arusha Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya.
WS: akiwataka Kwenda Kufanya kazi gani
Shahidi: Katika Briefing Alisema Kuwa Kikundi hicho Kina watu ambao wapo Mkoa wa Kilimanjaro, Moshi kwa hiyo Tunatakiwa kwenda Kuwakamata Kuzuia wasiendelee na Matendo yao
WS: Kwa hiyo Mlikuwa mnakwemda wapi
Shahidi: Tulikuwa tunakwenda Moshi
WS: Ukamataji Ukifanyika lini
Shahidi: Ukamataji Ulifanyika Tarehe 05 August 2020
WS: Ulifanyikia Eneo gani na Majira gani
Shahidi: Eneo la Rau Madukani na Majira Ya Saa Saba Mchana
WS: Rau Madukani Ipo Mji gani
Shahidi: Rau Madukani Ipo Moshi
WS: Kwa Mujibu wa Taarifa za Kingai Mlikuwa mnakwemda Kuwakamata watu wangapi Waliokwepo Moshi
Shahidi: Kwa Mujibu wa Taarifa Za Afande Kingai Alisema Watu waliofika Moshi ambao tunakwenda Kuwakamata ni watano
WS: Mliofanikiwa Kuwakamata hiyo Tarehe 05 August 2020 ni akina nani
Shahidi: NI Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa
WS: Ieleze Mahakama Iwapo Watu Mliwakamata hiyo Tarehe 05 August 2020 Kama wapo Mahakamani na Kama unawakumbuka
Shahidi: Wapo Mahakamani Wamekaa Upande wa Kulia
Wakili wa Serikali: Upande wa Kulia Wamekaa watu wengi
Shahidi: Ni Mtu wa Pili
Shahidi: anawafuata Walipo na Kuanza na Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi ameweza Kuwatambua Washitakiwa wa Pili na watatu
Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Naona hii inajirudia Mara ya tatu Sasa, Mwenye Uwezo wa Kujua Kama Shahidi ametambua Washtakiwa ni kazi ya Mahakama
Jaji: ni Sahihi Na Mimi napokea Ushahidi tu
Wakili wa Serikali: Baada ya Ukamataji, Mlielekea Wapi
Shahidi: Central Moshi
WS: Baada ya Kuwa Mmefika Kituoni Mambo gani Yalifanyika Shahidi Afande Jumanne na Afande Mahita Waliekezwa Kushuka Kwenye gari, Mimi Afande Kingai na Dereva Tulikaa Kwenye gari
WS: Kwanini Mlibaki Kwenye Gari
Shahidi: Tulikuwa na Lengo la Kwenda Kumtafuta Mtuhumiwa Wa Tatu
Wakili wa Serikali: Kwenda Kumtafuta Mtuhumiwa Wa Tatu wapi Shahidi
Shahidi: Maeneo Mbalimbali ambayo watuhumiwa Walikuwa wanatupitisha
Wakili wa Serikali: Huyu Mtuhumiwa Watatu ulipata Kujua ni Yupi
Shahidi: Nilipata Kumfahamu kwa Majina ya Kakobe au Moses Lijenje
WS: Ufutailiaji Wa huyu Kakobe au Moses Lijenje Ulianza Muda gani
Shahidi: Baada ya Kutoka Central Polis Moshi Tulienda Kumtafuta Moses Lijenje
WS: Mlipotoka Central Mlienda Maeneo gani
Shahidi: Tulipofika Central Tulienda Maeneo ya RAU Madukani
WS: Tofauti na Rau Mlikwenda Maeneo yapi Mengine
Shahidi: tulienda Majengo, Pasua, Aishi Na Boma
WS: Aishi Ipo wapi
Shahidi: Machame
WS: Boma Ipo wapi
Shahidi: Wilaya ya Hai
WS: Utafutaji wa Mtuhumiwa Uliendelea Mpaka Saa ngapi
Shahidi: Tulienda Mpaka Majira ya Saa Tano Usiku
WS: Matokeo ya Utafutaji wenu Ukoje
Shahidi: Hatukufanikiwa Kumkamata
WS: Baada ya Hapo
Shahidi: Tulitoka Boma Ng'ombe Tukarudi Moshi na Kwa Maelekezo Ya Afande Kingai Kwamba Watuhumiwa Wawekwe Lockup
WS: Baada ya Kufika Moshi Nini Kilifuata
Shahidi: Afande Kingai alisema amepokea Maelekezo Kwamba Tuwapeleke Watuhumiwa Dar es Salaam
WS: Ni Saa ngapi Mlianza Safari ya Kuelekea Dar es Salaam
Shahidi: Tulitoka Majira ya Saa Moja Jioni Kuanza Kuelekea Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Mnakumbuka Sasa Dar es Salaam Mlifika Lini na Majira ya Saa ngapi
Shahidi: Tulifika Alfajiri ya Tarehe 07 August 2020
Wakili wa Serikali: Dar es Salaam Mlifika wapi
Shahidi: Tulifikia Kituo Cha Polisi Central Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Mlipofika Central Mlielekea Maneno gani haswa
Shahidi: Tukielekea Sehemu ya Mapokezi, Charge Room (CRO)
Wakili wa Serikali: Kwa Madhumuni gani?
Shahidi: Ya Kuwakabidhi Watuhumiwa Wawekwe Lockup
WS: Kwa hiyo ni Kitu gani Kilifanyika hapo CRO
Shahidi: Afande Kingai na Afande Jumanne Waliwakabidhi Watuhumiwa
WS: baada Kuwakabidhi hawa Watuhumiwa Mlielekea wapi na Kitu gani kilifanyika
Shahidi: Afande Kingai alitoa Maelezo, to take Break, Tukanawe uso alafu turudi
WS: Mnakumbuka ni Majira ya Saa ngapi mlirejea Kituoni Shahidi Tulirejea kituoni Majira ya Saa 1 Asubuhi
WS: baada ya Kurudi Kituoni nini Kilifuata
Shahidi: Nilimkabidhi Vielelezo nilivyokuwa navyo, na Afande Kingai akasema kuna Taarifa amepata Juu ya Watuhumiwa wengine Walikuwa DSM Wamepatikana, akataka tukaendelee na Upelelezi wakati akiwaandika Maelezo.
WS: Wakati wote Kuanzia Tarehe 05 Mpaka Tarehe 06, Mpaka Mnaanza Safari, Watuhumiwa walikuwa Chini ya Uangalizi wa nani
Shahidi: Walikuwa Chini ya Uangalizi Wa Afande Mahita pamoja na Mim
WS: Ikumbushe Mahakama Watu Mnazunguka Kuanzia, Moshi, Arusha Mpka Dar es Salaam Watuhumiwa walikuwa na Hali gani
Shahidi: Watuhumiwa Walikuwa na Hali Nzuri Wakati wote
WS: Ieleze Mahakama Kwamba Tarehe 5 kwakuwa Mlikuwa Mnazunguka Na Watuhumiwa wakati wote, Je Mlikuwa wapi
Mallya: OBJECTION, Leading Question Hakuna Sehemu Yoyote katika Testimony Yake Shahidi alisema Walikula
Jaji: badilisha hilo swali
WS: Baada ya Tarehe 07 Wewe Ulielekea Wapi
Shahidi: Nilikwenda Kutafuta Taarifa Kama tukivyoelekezwa na Afande Kingai Kukamata Watuhumiwa Wengine
WS: Shahidi Sasa Washitakiwa Wapo Central na hiyo Tarehe Saba Unasema Mlienda Kutafuta Taarifa zingine, Je ni lini tena ulipata Kushughulika na Watuhumiwa tena
Shahidi: Tarehe 08 August 2020 baada ya Afande Kingai Kusema amepata na Maelekezo tuwapeleke Watuhumiwa Kutoka Central Kwenda Mbweni, Na tuliwahamisha
WS: Wakati Mnawahamisha kutoka Central kwenda Mbweni, Je washitakiwa Walikuwa na Hali gani
Shahidi: Washtakiwa wote walikuwa na Hali nzuri
WS: Unakumbuka ilikuwa saa ngapi
Shahidi: Majira ya saa mne asubuhi
Shahidi: Tukiwakabidhi, Wakaimgizwa Lockup na Baada ya hapo tuliondoka
WS: Na Kurudishashwa Nyuma, Elezea Mazingira ya Ukamataji yalikuwaje
Shahidi: Yalikuwa ni Salama Hapakuwa na Purukushani, Mazingira yalikuwa ni Salama
WS: Eneo la Rau ni Eneo la namna gani
Shahidi: Eneo la wazi ambalo lina watu wanafanya Biashara zao Shahidi Tulipofika eneo la Boma, Gari ilisimama, Afande Kingai alishuka na akarudi na Chakula akiwa na Mtu amebeba, Ndizi na Nyama tukala na Watuhumiwa na Vinywaji tukawapa
Shahidi: Tulipofika Njia panda Himo Gari Ilipata hitilafu ya Umeme, Afande Kingai akaomba Gari kwa RPC wa Kilimanjaro, Wakati tunasubiria Gari tukala Chakula na baada ya muda Gari Iiifika na Kuanza Safari
Wakili wa Serikali: Pale Njia panda Himo Mlikula Chakula watu gani
Shahidi: Tulikula watu wote Pamoja na Watuhumiwa
WS: yapo Malalamiko Hapa Mahakamani, Kwamba Baada ya kuwakamata Watuhumiwa Pale Moshi Siku ya Tarehe 05, Mliwapeleka kituoni na Kuanza kuwatesa na wewe Ulishiriki Shahidi anahamaki hapa anasema SIYO KWELI
Shahidi: Tulipofika Kituoni Pale Moshi Sisi Hatukushuka kwenye gari
WS: TARATIBU SHAHIDI
JAJI ANAANDIKA
Shahidi: Baada Ya Kufika Kituoni Watuhumiwa Hawakushuka kwenye gari na baada ya Mizunguko yote ile tulirudi Saa 5 Usiku kuwarudisha na baada ya hapo tuliwafuata kesho yake
WS: Yapo Malalamiko Pia kwamba washtakiwa Hakuwafikisha Central Police Dar es Salaam na Kwamba Tarehe 09 wewe ukiwa na Bastola ulimlazimisha Kwa kumshikia Bastola, na Kwamba Asipo Saini yake Mateso ya Moshi yatajirudia rudia
Shahidi: Siyo Kweli Kwamba hatukuwa fikisha Central Polisi Dar es Salaam, hiyo Tarehe 09 Sisi Tulipofika Pale Central Tuliambiwa kwamba tuendelee Kuwatafuta watuhumiwa wengine na Siku hiyo zoezi lilizaaa Matunda Baada ya kumkamata Khalfani Bwire.
Shahidi: na hata kule Moshi hatukuwatesa kabisa
WS: TARATIBU SHAHIDI TWENDE KWA VITUO JAJI AWEZE KUANDIKA
Shahidi: Baada ya Kumkosa Moses Lijenje tulielekea Dar es Salaam, Hakuna Mahali Watuhumiwa Waliteswa
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo kwa Hapa Dar es Salaam Watuhumiwa Mliowakamata Moshi Mliwapeleka Vituo vipi
Shahidi: Siku ya Tarehe 08 Mimi na Inspector Mahita Ndiyo tuliwapeleka Watuhumiwa Mbweni na baada ya Kukabidhi tuliondoka.
WS: Shahidi Umeeleza Vyema Washtakiwa kutokuteswa, Vipi hili la Kumtishia Mohammed Ling'wenya Kusaini na Kwamba Asiposaini Mateso yatajirudia
Shahidi: Si kweli Kwa sababu Baada ya Kuwakabidhi Kituo cha Polisi Mbweni Hatukurudi Tena.. Na Moshi....
WS: SUBIRI KWANZA
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kwa Leo Niishie Hapo
Mtobesya anamfuata Shahidi Mahala alipo
Mtobesya: Unafahamu Kitu kinaitwa Occurance Book
Shahidi: Ndiyo nakifahamu
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji ni Kitu gani
Shahidi: Ni Kitabu cha Mahudhurio ya Askari akiwa kazini
Mtobesya: Wakati Unaongozwa na WS, Ulitoa Occurance Book?
Shahidi: Sikutoa
Mtobesya: Hebu tuambie Kituo cha Polisi Central Moshi Ni kituo kilichokamilika Kumuwezesha Askari Kufanya kazi yake..?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Mtobesya: Kuna Karatasi, pen, Viti na Meza
Mtobesya: Je, Unamfahamu kwamba Kuna Mashahidi Kwenye kesi hii Walichukuliwa Maelezo Yao wakiwa Moshi
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mtobesya: Kuna Askari ambao Mlikuwa nao Kwenye Timu ambao hawakutoka Moshi
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Nimesikia Mtu anaitwa Swila Je Mlikuwa naye
Shahidi: Ndiyo
Shahidi: Tulikuwa naye, Ni Inspector Wa Polisi Hapa Dar es Salaam
Mtobesya: Tarehe 08 August Swila alikuwa anafanya kazi Kituo gani Cha Polisi
Shahidi: Sifahamu
Mtobesya: hamkumkuta Central Police Dar es Salaam
Shahidi: Hatukumkuta
Mtobesya: Nilisikia Ulimtajia, We ulijuaje anaitwa Swila
Shahidi: Ni Baada ya Afande Kingai Kusema tutaungana Na Inspector Swila huko Dar es Salaam
Mtobesya: Kwa hiyo nikisema Swila anatokea Central Dar es Salaam Utakuwa hufahamu
Shahidi: Mimi sifahamu
Mtobesya: Isaidie Mahakama, Je Unakumbuka Kuwa Uliandika Maelezo Kitu Unachokitolea Ushahidi leo
Shahidi: Nafahamu
Mtobesya: Uliandika lini
Shahidi: Tarehe 10 December 2020
Mtobesya: Uliandika Mwenyewe?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Ukiyaona Utayafahamu
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba nipewe Maelezo yake halisi
WS Robert Kidando: Hatuna Pingamizi
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kumsogelea Shahidi
Jaji: anaandika, Bado Kimya na Mtobesya bado hajamsogelea
Jaji: Kumu' approach kwa namna gani Mahakama:
Mtobesya: Kwa Maana ya Literal Meaning
Mtobesya: Shahidi Unaweza Kuikumbuka
Shahidi: Ndiyo nafahamu ni ya Kwangu
Mtobesya: Naomba Sasa Usome kwa Sauti
WS ABDALLAH CHAVULA: OBJECTION. Mheshimiwa Jaji Hatuelewi, naona Ghafla Shahidi anapewa Statement asome
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji hawa ndiyo walisema Kwamba Shahidi asome kwanza Kisha ndiyo ahojiwe
Jaji: Miye Nakumbuka walisema Kwanza tuwaongoze Mashahidi
Mtobesya: Haya shahidi Ulisema ulikuwa Unazunguka na Watuhumiwa haya tuonyeshe Kwenye Statement Yako ni Wapi Uliandika
Shahidi: Hakuna nilipoandika
Mtobesya: Nilisikia Kwamba Mlipofika Central Polis Moshi Kwamba Mlibaki Kwenye gari, Je ipo Kwenye Statement yako
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Nilisikia Kwamba Mlipozunguka Mlirudi Kituoni Saa Tano Usiku Mkawakabidhi CRO. Je hiyo nayo Ipo wapi Katika Statement yako
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Baada ya Hapo Naweza Kumkabidhi asome hii Statement yake sasa
Jaji: Mr Kibatala tusaidie kidogo
Kibatala: Mwanzo nakubalina na Mr. Mtobesya Kwamba tulikubaliana asome kwanza lakini Kwa Mood ya Leo tunakubali, Hata hivyo naona sasa ni wakati Muafaka kwa sababu Shahidi ameshaji' contradict
WS Robert Kidando: Hatuna Kipingamizi
Mtobesya: Basi naomba Shahidi Usome Kwa Sauti
Shahidi ASOMA STATEMENT YAKE YOTE, KWA SAUTI
Amemaliza Kusoma Sasa
Mtobesya: Kwakuwa umeyatambua na Kuyasoma Maelezo Yako Je Ungependa yaiingie Kama Sehemu Ya Ushahidi Wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji basi tunaomba Yaingie Kwa Uleule Utaratibu, Exhibit D1
Jaji: Basi tunayapokea Maelezo haya kama Kielelezo namba 1 cha Upande wa Utetezi Mawakili Wote wa Pande zote mbili wanakubaliana na Jaji.
Mtobesya: Tangu Mwaka Jana Mwezi wa 12 Wakati Unatoa Maelezo Yako, Ni Muda gani Umepita
Shahidi: Takribani Mwaka Mmoja
Mtobesya: Kwa hiyo Kwa maelezo Yako uliyoandika Takribani Mwaka Mmoja, Hakuna Sehemu Uliyoandika Kwamba Mlizunguka na Watuhumiwa ni sahihi
Shahidi: NI SAHIHI
Mallya: Nitakuwa Na Maswali Machache Kwa Shahidi, Naomba nipatiwe Exhibit D1
Mallya: Nakuuliza Maswali Machache ila nitataka Ujibu kwa Sauti ileile Uliyo kuwa Unamjibu Kaka Yangu Hilla
Mallya: naomba Uniseomee kwa Sauti, Sehemu hii Mheshimiwa Jaji asikie
Shahidi: "Tuliwa +chukua watuhumiwa hawa na Kuwapeleka Kituo cha Polisi Moshi"
Mallya: Hapo hapo.. Je hayo uliyasema hayo
Shahidi: Nilisema Leo Kwamba tuliopowakosa tukawarudisha Kituoni
Mallya: Kwenye Maelezo Yako Umeandika hayo Maneno
Shahidi: Hapana
Mallya: Ni sahihi Umesema Pale Moshi Kwenye Gari hukushuka
Shahidi: Sahihi
Mallya: Sasa Anza Kusoma Ulipoishia Mwanzo
Shahidi: "aliendelea kuandika Maelezo ya Mashahidi, Mimi Nilikabidhiwa Silaha pamoja na Simu"
Jaji: Mnaniacha hapo
Mallya: Naona Kuna Utofauti na Maelezo na yale yaliyochapwa ambayo tunayo
Jaji: Kwa hiyo tunafanyeje
Mallya: Unaweza Kuondoa hilo Swali
Mallya: Ulihusika Kumtoa Mtuhumiwa Yupi pale Central
Shahidi: Mimi sikuwa toa aliyewatoa ni Afande Jumanne
Mallya: na wewe uliyashuhudia
Shahidi: Hapana Sikushuhudia
Mallya: Kwa hiyo huna uhakika
Shahidi: Mimi nilikuwa naimarisha Ulinzi, lakini aliyewatoa Mahabusu siwajui
Mallya: Maelekezo ya Kuwatoa uliyapokea wewe
Shahidi: Hapana
Mallya: Kwa hiyo Sababu Ya Kuwahisha watuhumiwa kwenda Mbweni hukusikia kwa Masikio yako
Shahidi: Sikusikia
Mallya: Kwa hiyo hujui
Shahidi: Sijui
Mallya: Wakati unasema Mmeitwa na Inspector Mahita kwenda Kwa RCO Ulichukua Silaha, Je ulisema ni silaha gani
Shahidi: Sikusema
Mallya: Kuna Mahali umesema Kwamba Kuna wakati Ulihifadhi Silaha yako sehemu
Shahidi: Hapana Sikusema
Mallya: Unafahamu Gari ya RPC Kilimanjaro lina siti ngapi
Shahidi: Lina Siti 4
Mallya: Wakati Mmeharibikiwa na Gari Njia panda Himo Mlikuwa wangapi
Shahidi: Jumla Watu Saba
Mallya: Gari ya Watu 4 mmepanda Watu 7, nani alimkalia Kingai?
Shahidi: Alikaa Mwenyewe
Mallya: Siti inayofuata
Shahidi: Siti ya Pili ni Kubwa Walikuwa Wamekaa Siti Moja watu 3
Mallya: Ni Gari aina gani hiyo ambayo ina siti 1 ya Kukaa watu 3
Shahidi: FOTON
Mallya: Wakati mnawakamata Muda wa Saa Saba, uliwauliza watuhumiwa Kama Walikula?
Shahidi: Kazi yangu ilikuwa ni Kuimarisha Ulinzi, Sikuuliza
Mallya: Ulipata Kueleza Kama Walienda Msalani Wakati Wakili wa Serikali anakuongoza
Shahidi: Sikueleza, ila ni Huduma za Kibadamu
Mallya: Jibu Swali Langu
Mallya: Wakati Siku ya Tarehe 06 Mpaka Mnapata Breakdown Njia panda Himo, Ulielezea Kwamba walipata Huduma ya Chakula
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Ulishawahi Kuajiriwa Kazi ya Polisi Dar es Salaam
Shahidi: Hapana
Mallya: Umezaliwa Wapi
Shahidi: Kilimanjaro, Himo
Mallya: Ni sahihi nikisema Wewe ni Mwenyeji wa Kilimanjaro
Shahidi: huenda ni sahihi
Mallya: Nimeona Ujavaa Saa, Je Kilichokufanya Ujue Uliwakamata Saa Saba ni Kitu gani
Shahidi: Kwenye Gari Kwenye Dashboard Kuna Saa
Mallya: Kwani wale Uliwakamata Ndani ya Gari
Shahidi: Hapana, Kabla ya Kushuka niliona kwenye gari
Shahidi: Ilikuwa Ni Saa Saba Kasoro kabla Sijashuka
Mallya: Kilichokufanya Uangalie Muda ni Kitu gani
Shahidi: nilijikuta tuh nimengalia
Mallya: Kwa hiyo wewe Kwako Muda ni Kitu cha Muhimu au Siyo
Shahidi: Kitu cha Muhimu
Mallya: Kwa hiyo Kutoka Rau Mpaka Central Moshi unachukua Muda gani
Shahidi: Siwezi Kukadiria
Mallya: Ingawa sehemu zote mbili unazifahamu
Shahidi: Ndiyo
WS Robert Kidando: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hili swali la Kwamba ameandika Saa Saba, Sijui ameandika wapi
WS: Inaweza Kupotosha, tunaona Jinsi lilivyo Halipo Sawa
Mallya: huo Muda nimeutoa Kwemye statement yake Shahidi ambayo amesoma
Jaji: anachosema Wakili Wa Serikali ni pale Unaposema Kwamba "Umeandika hapa Saa Saba"
Mallya: Shahidi Soma hapa
Shahidi: "Tuliwa kamata Saa Saba
Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hapo
Jaji: Sawa sasa Endelea
Mallya: Ulipata wapi Kujua kuwa ni Saa Saba
Shahidi: Kwenye gari
Mallya: aliyeandika Maelezo ya Ushahidi wa Upekuzi, Maelezo aliyapeleka wapi
Shahidi: Sijui aliyapeleka wapi
Mallya: Kwa Kawaida mkiandika mnayapeleka wapi
Shahidi: Kwenye Jalada
Mallya: Kuna uwezekano alienda nayo Nyumbani kwake
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Kuna uwezekano aliyapeleka kwenye Jalada
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Kwa hiyo aliyeandika Maelezo hamkuonana naye tena
Shahidi: Hatukuonana naye tena
Mallya: Kuna Uwezekano Aliyepelela Dar es Salaam Maelezo Hayo
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Kwenye Maelezo Yako umesema Kwamba Mlikuwa na Askari Wengine wa Moshi ni sahihi
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kuna Sehemu Yoyote Umepata Kueleza Kwamba Mliachana Nao wapi hao Askari Wa Moshi
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Idadi ya Askari Mliokutana nao Moshi Unakumbuka?
Shahidi: Sikumbuki Idadi yao
Mallya: Shahidi Washtakiwa Wanasema Mlikuwa watu zaidi ya 10 mliwavamia, na Kuwawekea Madawa na Bastola
Shahidi: Si kweli, Tulikuwa watano
Mallya: Jaji ataona wapi Kwamba Mlikuwa watano
Shahidi: Kwenye Statement Hakuna
Mallya: Kwenye Maelezo Yako Uliandika Idadi ya Watuhumiwa Wangapi Wakati Mnatoka Arusha
Shahidi: Hapana Siku andika Watuhumiwa Wangapi
Mallya: ilituamini kwamba Watuhumiwa Walikuwa Idadi ya watatu, Je ni sehemu gani gani
Shahidi: Hakuna
Shahidi: Wakati wa kwenda Tulikuwa na Moja na wakati wa Kurudi tulikuwa na Gari mbili Fredrick Kama Mlikuwa na Ulazima kwa nini hamkushuka
Shahidi: Kimya
Kihwelo: Nitakuwa Sahihi au sitokuwa Sahihi Nikisema Kwamba Mlipofika Central Police Moshi mlipaswa Kuwakabidhi kwanza Kisha Muwachukue kwa Hatua zingine za Upelelezi
Shahidi: Unaweza Kuwa Sahihi au siyo sahihi
FREDRICK: Jibu Moja tuh
Shahidi: Hautokuwa Sahihi
Fredrick: Je Unafahamu Kwamba Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya Ni Wageni pale Moshi
Shahidi: Sifahamu
Fredrick: Wakati Mnawatafuta Adamoo na Mohammed Ling'wenya Mliwakamata bila Mtu kuwaongoza
Shahidi: Sifahamu, Afande Kingai
Fredrick: Palikuwa na Ulazima wa Kuzunguka na Watuhumiwa
Shahidi: Kwa sababu walionyesha nia ya Kusaidia Kumtafuta Mtu wa tatu
Fredrick: Nyie Mnafanya kazi Masaa 24 Siku Saba za wiki?
Shahidi: Ndiyo
FREDRICK: kwanini Mliporudi Saa 5 Usiku hamkuwahoji Watuhumiwa
Shahidi: Tulikuwa bado tunamtafuta Mtuhumiwa wa tatu
Fredrick: Ni sahihi nikisema Kwamba Kuna Kiongozi Aliwaaagiza Msiwahoji watuhumiwa
Shahidi: Hapana Siyo Sahihi
Fredrick: Ni sahihi uliwafikisha Watuhumiwa Mbweni
Shahidi: Ndiyo
Fredrick: na Kwamba Mlipowafikisha Mbweni Mkawapa Majina bandia
Shahidi: Siyo sahihi
Fredrick: Johnson John ni nani
Shahidi: Simfahamu
Fredrick: Ni sahihi upo hapa Kutoa Ushahidi Wa kweli
Shahidi: Sahihi
Fredrick: Je Msiri wa Afande Kingai ni nani
Shahidi: Sifahamu
Fredrick: Ulisema Kwamba Ulimkabidhi wa Silaha A5340 na Simu
Shahidi: Ndiyo
Fredrick: Ni sahihi pia Kwamba pale Moshi hukushuka kwenye gari
Shahidi: Sahihi
Fredrick: Nitakuwa Sahihi Nikisema Ulikuwa unatembea na Vielelezo Muda wote Ukiwa Moshi
Shahidi: Ni sahihi Nilikuwa navyo Kwenye Begi Muda wote
Fredrick: Wakati watuhumiwa Wanakabidhiwa pale Central Police Moshi ulikwepo
Shahidi: Ndiyo nikwepo lakini Nje
Fredrick: Afande Jumanne Shahidi namba Moja wa Kesi Ndogo hii, Wakati anatoa Ushahidi Hapa alisema Yeye ndiye alielekezwa kabidhi watuhumiwa pale Central, Swali kati ya wewe na Yeye nani Mkweli
Shahidi: Miye sijui lakini najua Afande Jumanne na Afande Kingai Ndiyo wakikabidhi watuhumiwa Kituoni na Mimi nilikwepo
Fredrick: Kwa Mujibu wa Maelezo yako Umesema Afande Kingai aliwapa Ruhusa Mkanawe Uso au Kupata Break
Shahidi: Ni sahihi
Fredrick: Na baada ya Kuna wa Uso na Kupata Break, Vielelezo Vilikuwa wapi
Shahidi: Vilikuwa Kwenye Begi
Fredrick: Wakati Unatoa Maelezo Yako hapa na Wakili wa Serikali, Je kuna Mahakama Popote alikuongoza ilikusema ni wapi ulivitoa Vielelezo hivyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Shahidi Habari
Shahidi: Salama
Kibatala: Wakati wa Ushahidi Wako Ulionyeshwa Kitabu (naomba nipate Detention Register)
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Wako wote ukiongozwa Je Ulionyeshwa hiki kitabu.?
Shahidi: Si Kuonyeshwa
Kibatala: wakati wa Ushahidi Wako Kuna Mahala Uliongozwa kumwambia Jaji Pale CRO ulimkuta Mtu fulani au Mwenye Haiba fulani
Shahidi: Sikusema
Kibatala: We Unamfahamu Mtu aliyekuwa CRO Duty?
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: je akiwa Mahakamami Askari huyo unaweza Kumtambua
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Pale Mapokezi Central Police Dar es Salaam palikuwa na Askari Wangapi na jinsia zao
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je katika Ushahidi Wako Kuna Mahala Popote Umemwambia Jaji Kwamba Ulishuhudia Kwamba Washtakiwa Wakifanyiwa Upekuzi
Shahidi: Sikusema Lakini...
Kibatala: sitaki lakini hapa.
Shahidi: Nataka Kufafanua, najua hatokasirika
WS Pius Hilla: Sijakasirika ila namkumbusha siyo Hilla ni Wakili Mwandamizi wa Serikali Pius Hilla.
Jaji: Kibatala Umesikia
Kibatala: Sitotilia Maanani
Kibatala: Shahidi Mwanzo nimesikia umetambua mshtakiwa kama ADAM KASEKWA
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Statement D1
Kibatala: Soma Hapo Kwenye Statement Umeandika kama nani
Shahidi: ADAM HASSAN.. Lakiniiiiiiii...
Kibatala: Sitaki lakini hapa
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Kuna sehemu Umesema Kwamba Adam Hassan ndiye Adam Kasekwa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nimesikia Sasa hivi Unacheo tofauti na Wakati ukiwakamata
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umepanda Umeshuka
Shahidi: Nimepanda
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Kuna sehemu Umesema Kwamba Adam Hassan ndiye Adam Kasekwa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nimesikia Sasa hivi Unacheo tofauti na Wakati ukiwakamata
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umepanda Umeshuka
Shahidi: Nimepanda
Kibatala: Nitakuwa sahihi Umepanda Cheo baada Kuwakamata Watuhumiwa
Shahidi: Nimepanda Cheo Kwa Elimu yangu
Jaji: Shahidi Wakili anauliza kwamba Umepanda Cheo Baada ya Kuwakamata au kabla
Shahidi: Nimepanda Mwaka huu 2021, Tarehe 13 August
Jaji: Kwa hiyo baada ya Kuwakamata
Shahidi: Ndiyo baada
Mahakama: Kicheko
Kibatala: Ni Muhimu Kuingia Kwenye Record hiyo
Kibatala na Je Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Kuna Mahali alikuongoza Kufafanua Ulivyo panda Cheo
Shahidi: Kimya
Kibatala: Kuna Sehemu Kwenye Statement Yako Umeandika KAKOBE Kama Jina lingine la Moses Lijenje
Shahidi: Kimya
Kibatala: Katika Kielelezo Namba D1 cha Utetezi Katika hiyo Statement Yako, kuna sehemu Ipo Kwamba Watuhumiwa Walikwambia kwamba Moses Lijenje Ndiyo Kakobe
Shahidi: Haipo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Dakika Moja na Mr. Mtobesya
Jaji anaitikia kwa kichwa
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kuandika Maelezo ni Jambo la Kisheria
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu akama Afisa Wa Polisi ni Muhimu Kuweka Kumbukumbu zote katika Maelezo yako
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ulishiriki Kuandika Maelezo Ya Nyongeza ya Shahidi Kwamba Uliwahi Kushuhudia Kuwakabidhi Wakina Mohammed Ling'wenya Central Dar es Salaam
Shahidi: Sijawahi Kushiriki
Kibatala: Jaji ataangalia wapi sehemu yoyote ambayo umeandika Kwamba Ulishuhudia Zoezi la Kuwakabidhi Watuhumiwa
Shahidi: Viongozi Ndiyo wanaandika
Kibatala: Pale Central Police Arusha Kuna CCTV camera
Shahidi: Ndiyo zipo
Kibatala: Zimewekwa Lini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Central Moshi zipo CCTV?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Central Dar es Salaam zipo CCTV?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je unajua Kwamba Video Recording ni sehemu ya Kifaa Kazi?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ulishawahi Kushiriki kwenye kesi ya Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: hii Ndiyo ya kwanza
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulifahamu kwamba Unaenda Kushughulikia Watuhumiwa wa Ugaidi Tangu tarehe 04 August 2020
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Toka Mnapata Taarifa ya Kushughulika na Watuhumiwa wa Ugaidi Tarehe 04 August 2020 Mpaka 05 August 2020, angalau ni Siku Moja
Shahidi: Siku...? Angalau Masaa 12
Kibatala: Kwa hiyo ni Masaa 12 ya Maandalizi, Lakini hamjarekodi Mahali
Shahidi: Hatuja Rekodi Mahali
Kibatala: Maoni yenu Kiupelelezi Watuhumiwa walikuwa Wako Nje walikuwa ni Hatari siyo Hatari
Shahidi: Siyo kwa Maoni, Kwa Taarifa Zilizotolewa ni Watu Hatari
Kibatala: Lakini pamoja na Uhatari huo bado Mlikuwa Mnazunguka Na Watuhumiwa Wawili wanawaambieni Twendeni huku na huku
Shahidi: Tulikuwa tupo tayari na Hatari yake
Kibatala: Kwani Si Mlikuwa mnaelekezwa Pa Kwenda na Njia ya Kupita kutoka kwa Watuhumiwa Maliowakamata
Shahidi: Ndiyo, Ndiyo tulikuwa tunawafuatisha wanachosema
Kibatala: Mlikuwa mnafahamu kwamba Huyo Lijenje anasilaha za Kivita
Shahidi: Miye sifahamu
Kibatala: Nilisikia Mlienda Arusha na wewe na Mahita ni Wakazi wa Arusha
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unaongozwa na WS uliwasiliana na Watu wa Arusha, Kwamba Kwa kuwa Nyie Mpo Moshi wao waende
Shahidi: Palikuwa hakuna Ulazima
Kibatala: Swali langu ni Je Ulimwambia Jaji, Ufafanuzi Utampa Mr. Pius Hilla Wakili Mwandamizi Wa Serikali?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Shahidi Boma Kuna Ofisi ya Polisi
Shahidi: Kipo Kibatala: Ofisi za Serikali pia zitakwepo
Shahidi: Ndiyo Kibatala na Mlisimama Boma Kula?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: unafahamu PGO ya 354(7) Chakula Mnakula Kituo chochote cha Polisi au Ofisi za Serikali
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Pamoja na Kujua Mkala Chakula na Watuhumiwa Boma
Shahidi: Ndiyo sababu PGO inasema kama Hakuna Ofisi ya Serikali na Mnauwezo Wa Kuwalinda Mtakula popote
Kibatala: Himo pia Mlisimama Kupata Chakula
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na pia Himo pana Ofisi ya Serikali na Kituo cha Polisi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi wako ukiongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mlijihifadhi Ofisi ya Serikali, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji au hukumwambia
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: Nilisikia Unasema Mlipata hitilafu ya Umeme Njia panda Himo, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba hitilafu ni sehemu gani au Ilifanya Vipi lishindwe Safari
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: Sasa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba nani alibaki ndani ya Gari au Nje
Shahidi: Nilimwambia Kwamba tulikaa ndani
Kibatala: Nani aliye mkabidhi Mtuhumiwa Ling'wenya CRO Central Dar es Salaam, Ni Jumanne au Mahita
Shahidi: aliwakabidhi watuhumiwa Pale Central Police Dar es Salaam ni Afande Kingai na Jumanne
Kibatala: Ni Ushahidi Wako Kwamba Kingai na Jumanne Walifikia hadi Counter
Shahidi: Nimewaona Wakiwa Kingai na Jumanne Counter wakikabidhi Watuhumiwa
Kibatala: Central Pako hivi Kuna Counter Ya Polisi ya Cement na Sehemu za Kukaa Ndugu (ANAONYESHA KWA VITENDO), Ulikaa wapi
Shahidi: Enheeeeee hapo Kwenye Ngazi
Kibatala: Kwa hiyo Ukiwa hapa Unaona Pale Counter Shahidi: Naona pale Counter, Wanachoandika Sioni ila watu nawaona
Kibatala: Mkiwa kwenye gari nani alimuuliza Mohammed Ling'wenya kuhusu Moses Lijenje?
Shahidi: Ni Afande Kingai
Kibatala: Unafahamu Kwamba hapo anakuwa ameanza Kukiri Kosa?
Shahidi: Hapana yalikuwa ni Maongezi tu ya Kawaida
Kibatala: ila Nyie ni Polisi na Mlienda Kwa ajili ya Kuwakamata
Shahidi: Ndiyo ila Ilikuwa Maongezi ya Kawaida
Kibatala: Wakati Mnawakabidhi Watuhumiwa Pale Central, Je Wakati Wanakabidhiwa wewe Bunduki Ulikabidhi Saa ngapi
Shahidi: Ndiyo nilisema Nilienda Kukabidhi Saa Moja
Kibatala: Nimekusikia Vyema Kwamba Tarehe 08 August 2020 mlipewa Maelekezo na Afande Kingai Kuwatoa Watuhumiwa Central Kuwapeleka Mbweni
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Kuna Mtu aliwaambia Kwamba walikuwa wameshahojiwa na wamekiri
Shahidi: Siku ya Tarehe 07 August 2020 Afande Kingai Alisema anabakia Kuwahoji
Kibatala: Kwa hiyo wewe hufahamu Chochote Kuhusu Maelezo Ya Ling'wenya?
Shahidi: Hapana Sijui
Kibatala: Mohammed Ling'wenya alifikishwa Mahakamani lini
Shahidi: 19 August 2020
Kibatala: Wewe Ulishiriki Kumpeleka Ling'wenya Mahakamami
Shahidi: Hapana sikuwepo
Kibatala: ulijuaje Wamepelekwa Mbweni
Shahidi: Nilisikia Kwa Afande Kingai
Kibatala: Wewe ulifika Mbweni?
Shahidi: Sijawahi kufika Mbweni
Kibatala: Wewe si uliwapeleka Mbweni
Shahidi: Ndiyo Nilifika Mbweni
Kibatala: Sasa watuhumiwa wanasema ulikuwepo Mbweni
Shahidi: Sijawahi kufika Mbweni
Kibatala: Sawa mimi kazi yangu Kuuliza Maswali, Ukijichanganya ni Kazi ya Jaji Sasa Kujua Ukweli.
Kibatala: ulisema Ulikuwa na Silaha, Je ukiongea lolote kuhusu Silaha yako
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ilikuwa silaha gani
Shahidi: ilikuwa AK 47
Kibatala: Ulizungumzia kuikabidhi pale Central
Shahidi: Hapana
Kibatala: Vituo Vyote Mahabusu Wanakuwa Chini ya OCS
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mlimtaatifu OCS kwamba Mnampelekea Watuhumiwa Pale Mbweni
Shahidi: Hapana, hiyo ni kazi ya Viongozi
Kibatala: Wakati Mnatoka Moshi Tarehe 06 August 2020, Je ulikuwa unafahamu Kwamba Moja Wapo ya Mambo yatayofanyika Kufika Dar ni Ling'wenya Kuandika Maelezo ya Onyo
Shahidi: Hapana Sikufahamu
Kibatala: Wakati Mnatoka Moshi Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Afande Kingai, Inspector Mahita, na ASP Jumanne Ambao wa Kubwa zako wakimwambia Ling'wenya Kwamba Tunakwenda Dar es Salaam na Tulifika Dar es Salaam Kuna Maelezo ya Onyo yataandikwa
Shahidi: Sikusikia
Kibatala: Wakati wote simu zilikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa nazo Mimi
Kibatala: Na wakati wote Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Hukusema Kwamba Ulitoa Simu kwa Ling'wenya Kwamba Unaweza Kuwapigia Ndugu zako au Mawakili wako
Shahidi: Sikusema Ndiyo
Kibatala: Kuna Mahala Popote Umemwambia Jaji Kwamba Wakati wowote tunazunguka Pale Moshi Mpaka Arusha, wakimwambia Ling'wenya Kwamba hapa tupo Kwenye Mazoezi Mazito ya Kisheria Mpaka Unamtaja Lijenje, Je Nikupe Simu Uongee na Ndugu au Mwanasheria
Shahidi: Hapana Sijamwambia
Kibatala: Kwa kuwa Ling'wenya alikuwa anatoa Ushirikiano Kwenu Mpaka Mkaenda Stendi ya Mabasi, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Lijenje alikuwa anaenda Mkoa gani
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Kuna Mashahidi hapa wanasema Kwamba, Ling'wenya alishakiri na Kutoa Maelezo Yake JUU YA ushiriki wake, Je Ulishawahi Kusikia Afisa yoyote akisema Kwamba Kwa kuwa Ling'wenya ameshakiri Ngoja nimpeleka Mahakamani?
Shahidi: Siku sikusikia
Kibatala: Ulishawahi Kufanya Kazi CRO
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna Karatasi Yoyote ambayo Mtu Alisha kabidhi Mtuhumiwa Hakuna Mahala Popote ambapo ANAPEWA katasi lolote pale CRO
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulimtajia Dereva Mlitoka naye Arumeru Mpaka Moshi
Shahidi: Sikumtaja Jina, Nilitaja Dereva
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama ulitaja Jina la Derava aliyewatoa Njia panda Himo Mpaka Mpak Dar es Salaam
Shahidi: Hapana Sikutaja jina
Kibatala: Mliwahi Kumuona Mkuu wa Kituo cha Polisi Central Dar es Salaam
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pale Rau Madukani kuna Ofisi ya Mtaa au Kituo cha Polisi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sina swali lingine
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Tumefanya Assessment Ya Maswali na Hakuna Swali la Kufanya Re examination Anakaa Chini
Jaji: Tunakushukuru kwa Ushahidi Wako, sasa unaweza Kwenda
Shahidi anatoka kizimbani
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka Kesho tarehe 24 November Ilituweze Kuja na Shahidi Mwingine
Jaji: Nyinyi ndiyo Mnaojua huyo Shahidi anayekuja anaushahidi Gani, Kama mnaona ni Mfupi Waje wawili
Kibatala: Sahihi Mheshimiwa Jaji
WS Robert Kidando: Tutaona Cha Kufanya, Lakini kwa huyu wa Kesho tayari yupo
Jaji: Upande wa Utetezi
Kibatala: Hatuna Pingamizi
Jaji: anaandika Kidogo Mahakama: bado ipo Kimya
Jaji: basi Mahakama inakubiana na maombi ya upande wa mashtaka kuhairisha kesi, mashtaka mnaelekezwa kwamba ukiona ushahidi siyo mrefu walete mashahidi wawili. Na washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza mpaka kesho Asubuhi saa 3 kamili
Jaji anatoka
Kujua kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 22, 2021. Mahakama yatupilia mbali hoja tatu za utetezi. Kesi imeahirishwa hadi Novemba 23, 2021
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=========
UPDATES:
JAJI AMEINGIA MAHAKAMANI
Jaji ameshaingia Mahakamani
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa
Wakili wa Serikali Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Esther Martin
Nassoro Katuga
Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi
Jeremiah Mtobesya
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Seleman Matauka
Idd Msawanga
KHadija Aron
Maria Mushi
Jaji anaita Majina ya Washtakiwa wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: tuna shahidi Mmoja na tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Na sisi pia tupo tayari
Jaji: Enhe
Wakili wa Serikali: Shahidi ameenda Kuitwa
Shahidi anaingia
Jaji: Jina
Shahidi: 4347 Detective Afande Goodluck
Jaji: Miaka 32
Jaji: kabila
Shahidi: Mchagga
Jaji: Dini
Shahidi: Mkristo
Shahidi: Naapa kwamba Mimi H4347 Detective Sargent Goodluck Naapa kwamba Ushahidi Nitakao toa ni kweli, kweli tupu Eeh Mungu Nisaidie
Wakili wa Serikali: Pius Hilla Shahidi Unaitwa nani
Shahidi: Naitwa H4347 sergeant Goodluck
Wakili wa Serikali: Kazi yako
Shahidi: Askari Polisi
Wakili wa Serikali: Umeajiliwa tangu lini
Shahidi: 2013 Wakili wa Serikali Kituo chako cha Kazi ni wapi
Shahidi: Central Arusha
Wakili wa Serikali: Shahidi ieleze Mahakama Mnamo tarehe 04 August 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Kazi I Maeneo ya Central Police, Arusha
WS: Majira ya Jioni Siku hiyo Kitu gani Kilitokea
Shahidi: Afande Wangu Inspector Mahita alinipigia Simu na Kuniita Ofisini kwake
Wakili wa Serikali: Afande Mahita ni nani sasa hivi
Shahidi: Msaidizi Wa Mkuu wa Upelelezi
Wakili wa Serikali: Wa Wilaya gani
Shahidi: Arusha Mjini
Wakili wa Serikali: alikueleza Jambo gani
Shahidi: Aliniambia kuwa Mimi na Afande Francis tunahitajika kwa Afande RCO
WS: Wakati huo nani alikuwa RCO wa Arusha
Shahidi: alikuwa Afande Ramadhan Kingai
WS: Kwa Kingai Kitu gani kilitokea
Shahidi: Tulipofika kwa Kingai alituambia Kwamba tujiandae Kwa Safari Kuna kazi ya kwenda Kufanya
WS: Safari ya Kuelekea wapi
Shahidi: Wakati ule hakutuambia zaidi ya Tujiandae kwa Safari
WS: Ulijiandaaje Shahidi Baada ya Kutupa Maelekezo akatuambia tukachukue Silaha
WS: Baada ya hapo Nini Kilifanyika na Mkaelekea Wapi
Shahidi: Tulikuwa Afande RCO, Inspector Mahita, Mimi na Dereva wa RCO na Coplo Francis
WS: Taratibu Shahidi Jaji aweze Kuandika
Shahidi: Baada ya hapo tukaambiwa twende Arumeru Tukampitie Afande Jumanne ambaye ni OC CID wa Wilaya ya Arumeru
WS: Huko USA River Kwa Afande Jumanne Kitu gani Kilifanyika
Shahidi: Tulifika pale, tuka ingia ndani wote na Afande Kingai Akatupa Briefing Ya kazi tunayo kwenda Kufanya
WS: alisema Kitu gani
Shahidi: Akisema Kwamba amepata Taarifa Kwamba Kuna Kikundi KinajiPanga Kufanya Matendo ya Kigaidi hapa Nchini, na Kwamba ni Maeneo ya Arusha Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya.
WS: akiwataka Kwenda Kufanya kazi gani
Shahidi: Katika Briefing Alisema Kuwa Kikundi hicho Kina watu ambao wapo Mkoa wa Kilimanjaro, Moshi kwa hiyo Tunatakiwa kwenda Kuwakamata Kuzuia wasiendelee na Matendo yao
WS: Kwa hiyo Mlikuwa mnakwemda wapi
Shahidi: Tulikuwa tunakwenda Moshi
WS: Ukamataji Ukifanyika lini
Shahidi: Ukamataji Ulifanyika Tarehe 05 August 2020
WS: Ulifanyikia Eneo gani na Majira gani
Shahidi: Eneo la Rau Madukani na Majira Ya Saa Saba Mchana
WS: Rau Madukani Ipo Mji gani
Shahidi: Rau Madukani Ipo Moshi
WS: Kwa Mujibu wa Taarifa za Kingai Mlikuwa mnakwemda Kuwakamata watu wangapi Waliokwepo Moshi
Shahidi: Kwa Mujibu wa Taarifa Za Afande Kingai Alisema Watu waliofika Moshi ambao tunakwenda Kuwakamata ni watano
WS: Mliofanikiwa Kuwakamata hiyo Tarehe 05 August 2020 ni akina nani
Shahidi: NI Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa
WS: Ieleze Mahakama Iwapo Watu Mliwakamata hiyo Tarehe 05 August 2020 Kama wapo Mahakamani na Kama unawakumbuka
Shahidi: Wapo Mahakamani Wamekaa Upande wa Kulia
Wakili wa Serikali: Upande wa Kulia Wamekaa watu wengi
Shahidi: Ni Mtu wa Pili
Shahidi: anawafuata Walipo na Kuanza na Mohammed Ling'wenya na Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi ameweza Kuwatambua Washitakiwa wa Pili na watatu
Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Naona hii inajirudia Mara ya tatu Sasa, Mwenye Uwezo wa Kujua Kama Shahidi ametambua Washtakiwa ni kazi ya Mahakama
Jaji: ni Sahihi Na Mimi napokea Ushahidi tu
Wakili wa Serikali: Baada ya Ukamataji, Mlielekea Wapi
Shahidi: Central Moshi
WS: Baada ya Kuwa Mmefika Kituoni Mambo gani Yalifanyika Shahidi Afande Jumanne na Afande Mahita Waliekezwa Kushuka Kwenye gari, Mimi Afande Kingai na Dereva Tulikaa Kwenye gari
WS: Kwanini Mlibaki Kwenye Gari
Shahidi: Tulikuwa na Lengo la Kwenda Kumtafuta Mtuhumiwa Wa Tatu
Wakili wa Serikali: Kwenda Kumtafuta Mtuhumiwa Wa Tatu wapi Shahidi
Shahidi: Maeneo Mbalimbali ambayo watuhumiwa Walikuwa wanatupitisha
Wakili wa Serikali: Huyu Mtuhumiwa Watatu ulipata Kujua ni Yupi
Shahidi: Nilipata Kumfahamu kwa Majina ya Kakobe au Moses Lijenje
WS: Ufutailiaji Wa huyu Kakobe au Moses Lijenje Ulianza Muda gani
Shahidi: Baada ya Kutoka Central Polis Moshi Tulienda Kumtafuta Moses Lijenje
WS: Mlipotoka Central Mlienda Maeneo gani
Shahidi: Tulipofika Central Tulienda Maeneo ya RAU Madukani
WS: Tofauti na Rau Mlikwenda Maeneo yapi Mengine
Shahidi: tulienda Majengo, Pasua, Aishi Na Boma
WS: Aishi Ipo wapi
Shahidi: Machame
WS: Boma Ipo wapi
Shahidi: Wilaya ya Hai
WS: Utafutaji wa Mtuhumiwa Uliendelea Mpaka Saa ngapi
Shahidi: Tulienda Mpaka Majira ya Saa Tano Usiku
WS: Matokeo ya Utafutaji wenu Ukoje
Shahidi: Hatukufanikiwa Kumkamata
WS: Baada ya Hapo
Shahidi: Tulitoka Boma Ng'ombe Tukarudi Moshi na Kwa Maelekezo Ya Afande Kingai Kwamba Watuhumiwa Wawekwe Lockup
WS: Baada ya Kufika Moshi Nini Kilifuata
Shahidi: Afande Kingai alisema amepokea Maelekezo Kwamba Tuwapeleke Watuhumiwa Dar es Salaam
WS: Ni Saa ngapi Mlianza Safari ya Kuelekea Dar es Salaam
Shahidi: Tulitoka Majira ya Saa Moja Jioni Kuanza Kuelekea Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Mnakumbuka Sasa Dar es Salaam Mlifika Lini na Majira ya Saa ngapi
Shahidi: Tulifika Alfajiri ya Tarehe 07 August 2020
Wakili wa Serikali: Dar es Salaam Mlifika wapi
Shahidi: Tulifikia Kituo Cha Polisi Central Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Mlipofika Central Mlielekea Maneno gani haswa
Shahidi: Tukielekea Sehemu ya Mapokezi, Charge Room (CRO)
Wakili wa Serikali: Kwa Madhumuni gani?
Shahidi: Ya Kuwakabidhi Watuhumiwa Wawekwe Lockup
WS: Kwa hiyo ni Kitu gani Kilifanyika hapo CRO
Shahidi: Afande Kingai na Afande Jumanne Waliwakabidhi Watuhumiwa
WS: baada Kuwakabidhi hawa Watuhumiwa Mlielekea wapi na Kitu gani kilifanyika
Shahidi: Afande Kingai alitoa Maelezo, to take Break, Tukanawe uso alafu turudi
WS: Mnakumbuka ni Majira ya Saa ngapi mlirejea Kituoni Shahidi Tulirejea kituoni Majira ya Saa 1 Asubuhi
WS: baada ya Kurudi Kituoni nini Kilifuata
Shahidi: Nilimkabidhi Vielelezo nilivyokuwa navyo, na Afande Kingai akasema kuna Taarifa amepata Juu ya Watuhumiwa wengine Walikuwa DSM Wamepatikana, akataka tukaendelee na Upelelezi wakati akiwaandika Maelezo.
WS: Wakati wote Kuanzia Tarehe 05 Mpaka Tarehe 06, Mpaka Mnaanza Safari, Watuhumiwa walikuwa Chini ya Uangalizi wa nani
Shahidi: Walikuwa Chini ya Uangalizi Wa Afande Mahita pamoja na Mim
WS: Ikumbushe Mahakama Watu Mnazunguka Kuanzia, Moshi, Arusha Mpka Dar es Salaam Watuhumiwa walikuwa na Hali gani
Shahidi: Watuhumiwa Walikuwa na Hali Nzuri Wakati wote
WS: Ieleze Mahakama Kwamba Tarehe 5 kwakuwa Mlikuwa Mnazunguka Na Watuhumiwa wakati wote, Je Mlikuwa wapi
Mallya: OBJECTION, Leading Question Hakuna Sehemu Yoyote katika Testimony Yake Shahidi alisema Walikula
Jaji: badilisha hilo swali
WS: Baada ya Tarehe 07 Wewe Ulielekea Wapi
Shahidi: Nilikwenda Kutafuta Taarifa Kama tukivyoelekezwa na Afande Kingai Kukamata Watuhumiwa Wengine
WS: Shahidi Sasa Washitakiwa Wapo Central na hiyo Tarehe Saba Unasema Mlienda Kutafuta Taarifa zingine, Je ni lini tena ulipata Kushughulika na Watuhumiwa tena
Shahidi: Tarehe 08 August 2020 baada ya Afande Kingai Kusema amepata na Maelekezo tuwapeleke Watuhumiwa Kutoka Central Kwenda Mbweni, Na tuliwahamisha
WS: Wakati Mnawahamisha kutoka Central kwenda Mbweni, Je washitakiwa Walikuwa na Hali gani
Shahidi: Washtakiwa wote walikuwa na Hali nzuri
WS: Unakumbuka ilikuwa saa ngapi
Shahidi: Majira ya saa mne asubuhi
Shahidi: Tukiwakabidhi, Wakaimgizwa Lockup na Baada ya hapo tuliondoka
WS: Na Kurudishashwa Nyuma, Elezea Mazingira ya Ukamataji yalikuwaje
Shahidi: Yalikuwa ni Salama Hapakuwa na Purukushani, Mazingira yalikuwa ni Salama
WS: Eneo la Rau ni Eneo la namna gani
Shahidi: Eneo la wazi ambalo lina watu wanafanya Biashara zao Shahidi Tulipofika eneo la Boma, Gari ilisimama, Afande Kingai alishuka na akarudi na Chakula akiwa na Mtu amebeba, Ndizi na Nyama tukala na Watuhumiwa na Vinywaji tukawapa
Shahidi: Tulipofika Njia panda Himo Gari Ilipata hitilafu ya Umeme, Afande Kingai akaomba Gari kwa RPC wa Kilimanjaro, Wakati tunasubiria Gari tukala Chakula na baada ya muda Gari Iiifika na Kuanza Safari
Wakili wa Serikali: Pale Njia panda Himo Mlikula Chakula watu gani
Shahidi: Tulikula watu wote Pamoja na Watuhumiwa
WS: yapo Malalamiko Hapa Mahakamani, Kwamba Baada ya kuwakamata Watuhumiwa Pale Moshi Siku ya Tarehe 05, Mliwapeleka kituoni na Kuanza kuwatesa na wewe Ulishiriki Shahidi anahamaki hapa anasema SIYO KWELI
Shahidi: Tulipofika Kituoni Pale Moshi Sisi Hatukushuka kwenye gari
WS: TARATIBU SHAHIDI
JAJI ANAANDIKA
Shahidi: Baada Ya Kufika Kituoni Watuhumiwa Hawakushuka kwenye gari na baada ya Mizunguko yote ile tulirudi Saa 5 Usiku kuwarudisha na baada ya hapo tuliwafuata kesho yake
WS: Yapo Malalamiko Pia kwamba washtakiwa Hakuwafikisha Central Police Dar es Salaam na Kwamba Tarehe 09 wewe ukiwa na Bastola ulimlazimisha Kwa kumshikia Bastola, na Kwamba Asipo Saini yake Mateso ya Moshi yatajirudia rudia
Shahidi: Siyo Kweli Kwamba hatukuwa fikisha Central Polisi Dar es Salaam, hiyo Tarehe 09 Sisi Tulipofika Pale Central Tuliambiwa kwamba tuendelee Kuwatafuta watuhumiwa wengine na Siku hiyo zoezi lilizaaa Matunda Baada ya kumkamata Khalfani Bwire.
Shahidi: na hata kule Moshi hatukuwatesa kabisa
WS: TARATIBU SHAHIDI TWENDE KWA VITUO JAJI AWEZE KUANDIKA
Shahidi: Baada ya Kumkosa Moses Lijenje tulielekea Dar es Salaam, Hakuna Mahali Watuhumiwa Waliteswa
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo kwa Hapa Dar es Salaam Watuhumiwa Mliowakamata Moshi Mliwapeleka Vituo vipi
Shahidi: Siku ya Tarehe 08 Mimi na Inspector Mahita Ndiyo tuliwapeleka Watuhumiwa Mbweni na baada ya Kukabidhi tuliondoka.
WS: Shahidi Umeeleza Vyema Washtakiwa kutokuteswa, Vipi hili la Kumtishia Mohammed Ling'wenya Kusaini na Kwamba Asiposaini Mateso yatajirudia
Shahidi: Si kweli Kwa sababu Baada ya Kuwakabidhi Kituo cha Polisi Mbweni Hatukurudi Tena.. Na Moshi....
WS: SUBIRI KWANZA
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kwa Leo Niishie Hapo
Mtobesya anamfuata Shahidi Mahala alipo
Mtobesya: Unafahamu Kitu kinaitwa Occurance Book
Shahidi: Ndiyo nakifahamu
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji ni Kitu gani
Shahidi: Ni Kitabu cha Mahudhurio ya Askari akiwa kazini
Mtobesya: Wakati Unaongozwa na WS, Ulitoa Occurance Book?
Shahidi: Sikutoa
Mtobesya: Hebu tuambie Kituo cha Polisi Central Moshi Ni kituo kilichokamilika Kumuwezesha Askari Kufanya kazi yake..?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Mtobesya: Kuna Karatasi, pen, Viti na Meza
Mtobesya: Je, Unamfahamu kwamba Kuna Mashahidi Kwenye kesi hii Walichukuliwa Maelezo Yao wakiwa Moshi
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mtobesya: Kuna Askari ambao Mlikuwa nao Kwenye Timu ambao hawakutoka Moshi
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Nimesikia Mtu anaitwa Swila Je Mlikuwa naye
Shahidi: Ndiyo
Shahidi: Tulikuwa naye, Ni Inspector Wa Polisi Hapa Dar es Salaam
Mtobesya: Tarehe 08 August Swila alikuwa anafanya kazi Kituo gani Cha Polisi
Shahidi: Sifahamu
Mtobesya: hamkumkuta Central Police Dar es Salaam
Shahidi: Hatukumkuta
Mtobesya: Nilisikia Ulimtajia, We ulijuaje anaitwa Swila
Shahidi: Ni Baada ya Afande Kingai Kusema tutaungana Na Inspector Swila huko Dar es Salaam
Mtobesya: Kwa hiyo nikisema Swila anatokea Central Dar es Salaam Utakuwa hufahamu
Shahidi: Mimi sifahamu
Mtobesya: Isaidie Mahakama, Je Unakumbuka Kuwa Uliandika Maelezo Kitu Unachokitolea Ushahidi leo
Shahidi: Nafahamu
Mtobesya: Uliandika lini
Shahidi: Tarehe 10 December 2020
Mtobesya: Uliandika Mwenyewe?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Ukiyaona Utayafahamu
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba nipewe Maelezo yake halisi
WS Robert Kidando: Hatuna Pingamizi
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kumsogelea Shahidi
Jaji: anaandika, Bado Kimya na Mtobesya bado hajamsogelea
Jaji: Kumu' approach kwa namna gani Mahakama:
Mtobesya: Kwa Maana ya Literal Meaning
Mtobesya: Shahidi Unaweza Kuikumbuka
Shahidi: Ndiyo nafahamu ni ya Kwangu
Mtobesya: Naomba Sasa Usome kwa Sauti
WS ABDALLAH CHAVULA: OBJECTION. Mheshimiwa Jaji Hatuelewi, naona Ghafla Shahidi anapewa Statement asome
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji hawa ndiyo walisema Kwamba Shahidi asome kwanza Kisha ndiyo ahojiwe
Jaji: Miye Nakumbuka walisema Kwanza tuwaongoze Mashahidi
Mtobesya: Haya shahidi Ulisema ulikuwa Unazunguka na Watuhumiwa haya tuonyeshe Kwenye Statement Yako ni Wapi Uliandika
Shahidi: Hakuna nilipoandika
Mtobesya: Nilisikia Kwamba Mlipofika Central Polis Moshi Kwamba Mlibaki Kwenye gari, Je ipo Kwenye Statement yako
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Nilisikia Kwamba Mlipozunguka Mlirudi Kituoni Saa Tano Usiku Mkawakabidhi CRO. Je hiyo nayo Ipo wapi Katika Statement yako
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Baada ya Hapo Naweza Kumkabidhi asome hii Statement yake sasa
Jaji: Mr Kibatala tusaidie kidogo
Kibatala: Mwanzo nakubalina na Mr. Mtobesya Kwamba tulikubaliana asome kwanza lakini Kwa Mood ya Leo tunakubali, Hata hivyo naona sasa ni wakati Muafaka kwa sababu Shahidi ameshaji' contradict
WS Robert Kidando: Hatuna Kipingamizi
Mtobesya: Basi naomba Shahidi Usome Kwa Sauti
Shahidi ASOMA STATEMENT YAKE YOTE, KWA SAUTI
Amemaliza Kusoma Sasa
Mtobesya: Kwakuwa umeyatambua na Kuyasoma Maelezo Yako Je Ungependa yaiingie Kama Sehemu Ya Ushahidi Wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji basi tunaomba Yaingie Kwa Uleule Utaratibu, Exhibit D1
Jaji: Basi tunayapokea Maelezo haya kama Kielelezo namba 1 cha Upande wa Utetezi Mawakili Wote wa Pande zote mbili wanakubaliana na Jaji.
Mtobesya: Tangu Mwaka Jana Mwezi wa 12 Wakati Unatoa Maelezo Yako, Ni Muda gani Umepita
Shahidi: Takribani Mwaka Mmoja
Mtobesya: Kwa hiyo Kwa maelezo Yako uliyoandika Takribani Mwaka Mmoja, Hakuna Sehemu Uliyoandika Kwamba Mlizunguka na Watuhumiwa ni sahihi
Shahidi: NI SAHIHI
Mallya: Nitakuwa Na Maswali Machache Kwa Shahidi, Naomba nipatiwe Exhibit D1
Mallya: Nakuuliza Maswali Machache ila nitataka Ujibu kwa Sauti ileile Uliyo kuwa Unamjibu Kaka Yangu Hilla
Mallya: naomba Uniseomee kwa Sauti, Sehemu hii Mheshimiwa Jaji asikie
Shahidi: "Tuliwa +chukua watuhumiwa hawa na Kuwapeleka Kituo cha Polisi Moshi"
Mallya: Hapo hapo.. Je hayo uliyasema hayo
Shahidi: Nilisema Leo Kwamba tuliopowakosa tukawarudisha Kituoni
Mallya: Kwenye Maelezo Yako Umeandika hayo Maneno
Shahidi: Hapana
Mallya: Ni sahihi Umesema Pale Moshi Kwenye Gari hukushuka
Shahidi: Sahihi
Mallya: Sasa Anza Kusoma Ulipoishia Mwanzo
Shahidi: "aliendelea kuandika Maelezo ya Mashahidi, Mimi Nilikabidhiwa Silaha pamoja na Simu"
Jaji: Mnaniacha hapo
Mallya: Naona Kuna Utofauti na Maelezo na yale yaliyochapwa ambayo tunayo
Jaji: Kwa hiyo tunafanyeje
Mallya: Unaweza Kuondoa hilo Swali
Mallya: Ulihusika Kumtoa Mtuhumiwa Yupi pale Central
Shahidi: Mimi sikuwa toa aliyewatoa ni Afande Jumanne
Mallya: na wewe uliyashuhudia
Shahidi: Hapana Sikushuhudia
Mallya: Kwa hiyo huna uhakika
Shahidi: Mimi nilikuwa naimarisha Ulinzi, lakini aliyewatoa Mahabusu siwajui
Mallya: Maelekezo ya Kuwatoa uliyapokea wewe
Shahidi: Hapana
Mallya: Kwa hiyo Sababu Ya Kuwahisha watuhumiwa kwenda Mbweni hukusikia kwa Masikio yako
Shahidi: Sikusikia
Mallya: Kwa hiyo hujui
Shahidi: Sijui
Mallya: Wakati unasema Mmeitwa na Inspector Mahita kwenda Kwa RCO Ulichukua Silaha, Je ulisema ni silaha gani
Shahidi: Sikusema
Mallya: Kuna Mahali umesema Kwamba Kuna wakati Ulihifadhi Silaha yako sehemu
Shahidi: Hapana Sikusema
Mallya: Unafahamu Gari ya RPC Kilimanjaro lina siti ngapi
Shahidi: Lina Siti 4
Mallya: Wakati Mmeharibikiwa na Gari Njia panda Himo Mlikuwa wangapi
Shahidi: Jumla Watu Saba
Mallya: Gari ya Watu 4 mmepanda Watu 7, nani alimkalia Kingai?
Shahidi: Alikaa Mwenyewe
Mallya: Siti inayofuata
Shahidi: Siti ya Pili ni Kubwa Walikuwa Wamekaa Siti Moja watu 3
Mallya: Ni Gari aina gani hiyo ambayo ina siti 1 ya Kukaa watu 3
Shahidi: FOTON
Mallya: Wakati mnawakamata Muda wa Saa Saba, uliwauliza watuhumiwa Kama Walikula?
Shahidi: Kazi yangu ilikuwa ni Kuimarisha Ulinzi, Sikuuliza
Mallya: Ulipata Kueleza Kama Walienda Msalani Wakati Wakili wa Serikali anakuongoza
Shahidi: Sikueleza, ila ni Huduma za Kibadamu
Mallya: Jibu Swali Langu
Mallya: Wakati Siku ya Tarehe 06 Mpaka Mnapata Breakdown Njia panda Himo, Ulielezea Kwamba walipata Huduma ya Chakula
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Ulishawahi Kuajiriwa Kazi ya Polisi Dar es Salaam
Shahidi: Hapana
Mallya: Umezaliwa Wapi
Shahidi: Kilimanjaro, Himo
Mallya: Ni sahihi nikisema Wewe ni Mwenyeji wa Kilimanjaro
Shahidi: huenda ni sahihi
Mallya: Nimeona Ujavaa Saa, Je Kilichokufanya Ujue Uliwakamata Saa Saba ni Kitu gani
Shahidi: Kwenye Gari Kwenye Dashboard Kuna Saa
Mallya: Kwani wale Uliwakamata Ndani ya Gari
Shahidi: Hapana, Kabla ya Kushuka niliona kwenye gari
Shahidi: Ilikuwa Ni Saa Saba Kasoro kabla Sijashuka
Mallya: Kilichokufanya Uangalie Muda ni Kitu gani
Shahidi: nilijikuta tuh nimengalia
Mallya: Kwa hiyo wewe Kwako Muda ni Kitu cha Muhimu au Siyo
Shahidi: Kitu cha Muhimu
Mallya: Kwa hiyo Kutoka Rau Mpaka Central Moshi unachukua Muda gani
Shahidi: Siwezi Kukadiria
Mallya: Ingawa sehemu zote mbili unazifahamu
Shahidi: Ndiyo
WS Robert Kidando: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hili swali la Kwamba ameandika Saa Saba, Sijui ameandika wapi
WS: Inaweza Kupotosha, tunaona Jinsi lilivyo Halipo Sawa
Mallya: huo Muda nimeutoa Kwemye statement yake Shahidi ambayo amesoma
Jaji: anachosema Wakili Wa Serikali ni pale Unaposema Kwamba "Umeandika hapa Saa Saba"
Mallya: Shahidi Soma hapa
Shahidi: "Tuliwa kamata Saa Saba
Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hapo
Jaji: Sawa sasa Endelea
Mallya: Ulipata wapi Kujua kuwa ni Saa Saba
Shahidi: Kwenye gari
Mallya: aliyeandika Maelezo ya Ushahidi wa Upekuzi, Maelezo aliyapeleka wapi
Shahidi: Sijui aliyapeleka wapi
Mallya: Kwa Kawaida mkiandika mnayapeleka wapi
Shahidi: Kwenye Jalada
Mallya: Kuna uwezekano alienda nayo Nyumbani kwake
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Kuna uwezekano aliyapeleka kwenye Jalada
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Kwa hiyo aliyeandika Maelezo hamkuonana naye tena
Shahidi: Hatukuonana naye tena
Mallya: Kuna Uwezekano Aliyepelela Dar es Salaam Maelezo Hayo
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Kwenye Maelezo Yako umesema Kwamba Mlikuwa na Askari Wengine wa Moshi ni sahihi
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kuna Sehemu Yoyote Umepata Kueleza Kwamba Mliachana Nao wapi hao Askari Wa Moshi
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Idadi ya Askari Mliokutana nao Moshi Unakumbuka?
Shahidi: Sikumbuki Idadi yao
Mallya: Shahidi Washtakiwa Wanasema Mlikuwa watu zaidi ya 10 mliwavamia, na Kuwawekea Madawa na Bastola
Shahidi: Si kweli, Tulikuwa watano
Mallya: Jaji ataona wapi Kwamba Mlikuwa watano
Shahidi: Kwenye Statement Hakuna
Mallya: Kwenye Maelezo Yako Uliandika Idadi ya Watuhumiwa Wangapi Wakati Mnatoka Arusha
Shahidi: Hapana Siku andika Watuhumiwa Wangapi
Mallya: ilituamini kwamba Watuhumiwa Walikuwa Idadi ya watatu, Je ni sehemu gani gani
Shahidi: Hakuna
Shahidi: Wakati wa kwenda Tulikuwa na Moja na wakati wa Kurudi tulikuwa na Gari mbili Fredrick Kama Mlikuwa na Ulazima kwa nini hamkushuka
Shahidi: Kimya
Kihwelo: Nitakuwa Sahihi au sitokuwa Sahihi Nikisema Kwamba Mlipofika Central Police Moshi mlipaswa Kuwakabidhi kwanza Kisha Muwachukue kwa Hatua zingine za Upelelezi
Shahidi: Unaweza Kuwa Sahihi au siyo sahihi
FREDRICK: Jibu Moja tuh
Shahidi: Hautokuwa Sahihi
Fredrick: Je Unafahamu Kwamba Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya Ni Wageni pale Moshi
Shahidi: Sifahamu
Fredrick: Wakati Mnawatafuta Adamoo na Mohammed Ling'wenya Mliwakamata bila Mtu kuwaongoza
Shahidi: Sifahamu, Afande Kingai
Fredrick: Palikuwa na Ulazima wa Kuzunguka na Watuhumiwa
Shahidi: Kwa sababu walionyesha nia ya Kusaidia Kumtafuta Mtu wa tatu
Fredrick: Nyie Mnafanya kazi Masaa 24 Siku Saba za wiki?
Shahidi: Ndiyo
FREDRICK: kwanini Mliporudi Saa 5 Usiku hamkuwahoji Watuhumiwa
Shahidi: Tulikuwa bado tunamtafuta Mtuhumiwa wa tatu
Fredrick: Ni sahihi nikisema Kwamba Kuna Kiongozi Aliwaaagiza Msiwahoji watuhumiwa
Shahidi: Hapana Siyo Sahihi
Fredrick: Ni sahihi uliwafikisha Watuhumiwa Mbweni
Shahidi: Ndiyo
Fredrick: na Kwamba Mlipowafikisha Mbweni Mkawapa Majina bandia
Shahidi: Siyo sahihi
Fredrick: Johnson John ni nani
Shahidi: Simfahamu
Fredrick: Ni sahihi upo hapa Kutoa Ushahidi Wa kweli
Shahidi: Sahihi
Fredrick: Je Msiri wa Afande Kingai ni nani
Shahidi: Sifahamu
Fredrick: Ulisema Kwamba Ulimkabidhi wa Silaha A5340 na Simu
Shahidi: Ndiyo
Fredrick: Ni sahihi pia Kwamba pale Moshi hukushuka kwenye gari
Shahidi: Sahihi
Fredrick: Nitakuwa Sahihi Nikisema Ulikuwa unatembea na Vielelezo Muda wote Ukiwa Moshi
Shahidi: Ni sahihi Nilikuwa navyo Kwenye Begi Muda wote
Fredrick: Wakati watuhumiwa Wanakabidhiwa pale Central Police Moshi ulikwepo
Shahidi: Ndiyo nikwepo lakini Nje
Fredrick: Afande Jumanne Shahidi namba Moja wa Kesi Ndogo hii, Wakati anatoa Ushahidi Hapa alisema Yeye ndiye alielekezwa kabidhi watuhumiwa pale Central, Swali kati ya wewe na Yeye nani Mkweli
Shahidi: Miye sijui lakini najua Afande Jumanne na Afande Kingai Ndiyo wakikabidhi watuhumiwa Kituoni na Mimi nilikwepo
Fredrick: Kwa Mujibu wa Maelezo yako Umesema Afande Kingai aliwapa Ruhusa Mkanawe Uso au Kupata Break
Shahidi: Ni sahihi
Fredrick: Na baada ya Kuna wa Uso na Kupata Break, Vielelezo Vilikuwa wapi
Shahidi: Vilikuwa Kwenye Begi
Fredrick: Wakati Unatoa Maelezo Yako hapa na Wakili wa Serikali, Je kuna Mahakama Popote alikuongoza ilikusema ni wapi ulivitoa Vielelezo hivyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Shahidi Habari
Shahidi: Salama
Kibatala: Wakati wa Ushahidi Wako Ulionyeshwa Kitabu (naomba nipate Detention Register)
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Wako wote ukiongozwa Je Ulionyeshwa hiki kitabu.?
Shahidi: Si Kuonyeshwa
Kibatala: wakati wa Ushahidi Wako Kuna Mahala Uliongozwa kumwambia Jaji Pale CRO ulimkuta Mtu fulani au Mwenye Haiba fulani
Shahidi: Sikusema
Kibatala: We Unamfahamu Mtu aliyekuwa CRO Duty?
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: je akiwa Mahakamami Askari huyo unaweza Kumtambua
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Pale Mapokezi Central Police Dar es Salaam palikuwa na Askari Wangapi na jinsia zao
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je katika Ushahidi Wako Kuna Mahala Popote Umemwambia Jaji Kwamba Ulishuhudia Kwamba Washtakiwa Wakifanyiwa Upekuzi
Shahidi: Sikusema Lakini...
Kibatala: sitaki lakini hapa.
Shahidi: Nataka Kufafanua, najua hatokasirika
WS Pius Hilla: Sijakasirika ila namkumbusha siyo Hilla ni Wakili Mwandamizi wa Serikali Pius Hilla.
Jaji: Kibatala Umesikia
Kibatala: Sitotilia Maanani
Kibatala: Shahidi Mwanzo nimesikia umetambua mshtakiwa kama ADAM KASEKWA
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Statement D1
Kibatala: Soma Hapo Kwenye Statement Umeandika kama nani
Shahidi: ADAM HASSAN.. Lakiniiiiiiii...
Kibatala: Sitaki lakini hapa
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Kuna sehemu Umesema Kwamba Adam Hassan ndiye Adam Kasekwa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nimesikia Sasa hivi Unacheo tofauti na Wakati ukiwakamata
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umepanda Umeshuka
Shahidi: Nimepanda
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Kuna sehemu Umesema Kwamba Adam Hassan ndiye Adam Kasekwa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nimesikia Sasa hivi Unacheo tofauti na Wakati ukiwakamata
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umepanda Umeshuka
Shahidi: Nimepanda
Kibatala: Nitakuwa sahihi Umepanda Cheo baada Kuwakamata Watuhumiwa
Shahidi: Nimepanda Cheo Kwa Elimu yangu
Jaji: Shahidi Wakili anauliza kwamba Umepanda Cheo Baada ya Kuwakamata au kabla
Shahidi: Nimepanda Mwaka huu 2021, Tarehe 13 August
Jaji: Kwa hiyo baada ya Kuwakamata
Shahidi: Ndiyo baada
Mahakama: Kicheko
Kibatala: Ni Muhimu Kuingia Kwenye Record hiyo
Kibatala na Je Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Kuna Mahali alikuongoza Kufafanua Ulivyo panda Cheo
Shahidi: Kimya
Kibatala: Kuna Sehemu Kwenye Statement Yako Umeandika KAKOBE Kama Jina lingine la Moses Lijenje
Shahidi: Kimya
Kibatala: Katika Kielelezo Namba D1 cha Utetezi Katika hiyo Statement Yako, kuna sehemu Ipo Kwamba Watuhumiwa Walikwambia kwamba Moses Lijenje Ndiyo Kakobe
Shahidi: Haipo
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Dakika Moja na Mr. Mtobesya
Jaji anaitikia kwa kichwa
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kuandika Maelezo ni Jambo la Kisheria
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu akama Afisa Wa Polisi ni Muhimu Kuweka Kumbukumbu zote katika Maelezo yako
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ulishiriki Kuandika Maelezo Ya Nyongeza ya Shahidi Kwamba Uliwahi Kushuhudia Kuwakabidhi Wakina Mohammed Ling'wenya Central Dar es Salaam
Shahidi: Sijawahi Kushiriki
Kibatala: Jaji ataangalia wapi sehemu yoyote ambayo umeandika Kwamba Ulishuhudia Zoezi la Kuwakabidhi Watuhumiwa
Shahidi: Viongozi Ndiyo wanaandika
Kibatala: Pale Central Police Arusha Kuna CCTV camera
Shahidi: Ndiyo zipo
Kibatala: Zimewekwa Lini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Central Moshi zipo CCTV?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Central Dar es Salaam zipo CCTV?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je unajua Kwamba Video Recording ni sehemu ya Kifaa Kazi?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Ulishawahi Kushiriki kwenye kesi ya Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: hii Ndiyo ya kwanza
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulifahamu kwamba Unaenda Kushughulikia Watuhumiwa wa Ugaidi Tangu tarehe 04 August 2020
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Toka Mnapata Taarifa ya Kushughulika na Watuhumiwa wa Ugaidi Tarehe 04 August 2020 Mpaka 05 August 2020, angalau ni Siku Moja
Shahidi: Siku...? Angalau Masaa 12
Kibatala: Kwa hiyo ni Masaa 12 ya Maandalizi, Lakini hamjarekodi Mahali
Shahidi: Hatuja Rekodi Mahali
Kibatala: Maoni yenu Kiupelelezi Watuhumiwa walikuwa Wako Nje walikuwa ni Hatari siyo Hatari
Shahidi: Siyo kwa Maoni, Kwa Taarifa Zilizotolewa ni Watu Hatari
Kibatala: Lakini pamoja na Uhatari huo bado Mlikuwa Mnazunguka Na Watuhumiwa Wawili wanawaambieni Twendeni huku na huku
Shahidi: Tulikuwa tupo tayari na Hatari yake
Kibatala: Kwani Si Mlikuwa mnaelekezwa Pa Kwenda na Njia ya Kupita kutoka kwa Watuhumiwa Maliowakamata
Shahidi: Ndiyo, Ndiyo tulikuwa tunawafuatisha wanachosema
Kibatala: Mlikuwa mnafahamu kwamba Huyo Lijenje anasilaha za Kivita
Shahidi: Miye sifahamu
Kibatala: Nilisikia Mlienda Arusha na wewe na Mahita ni Wakazi wa Arusha
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unaongozwa na WS uliwasiliana na Watu wa Arusha, Kwamba Kwa kuwa Nyie Mpo Moshi wao waende
Shahidi: Palikuwa hakuna Ulazima
Kibatala: Swali langu ni Je Ulimwambia Jaji, Ufafanuzi Utampa Mr. Pius Hilla Wakili Mwandamizi Wa Serikali?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Shahidi Boma Kuna Ofisi ya Polisi
Shahidi: Kipo Kibatala: Ofisi za Serikali pia zitakwepo
Shahidi: Ndiyo Kibatala na Mlisimama Boma Kula?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: unafahamu PGO ya 354(7) Chakula Mnakula Kituo chochote cha Polisi au Ofisi za Serikali
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Pamoja na Kujua Mkala Chakula na Watuhumiwa Boma
Shahidi: Ndiyo sababu PGO inasema kama Hakuna Ofisi ya Serikali na Mnauwezo Wa Kuwalinda Mtakula popote
Kibatala: Himo pia Mlisimama Kupata Chakula
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na pia Himo pana Ofisi ya Serikali na Kituo cha Polisi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi wako ukiongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mlijihifadhi Ofisi ya Serikali, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji au hukumwambia
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: Nilisikia Unasema Mlipata hitilafu ya Umeme Njia panda Himo, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba hitilafu ni sehemu gani au Ilifanya Vipi lishindwe Safari
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: Sasa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba nani alibaki ndani ya Gari au Nje
Shahidi: Nilimwambia Kwamba tulikaa ndani
Kibatala: Nani aliye mkabidhi Mtuhumiwa Ling'wenya CRO Central Dar es Salaam, Ni Jumanne au Mahita
Shahidi: aliwakabidhi watuhumiwa Pale Central Police Dar es Salaam ni Afande Kingai na Jumanne
Kibatala: Ni Ushahidi Wako Kwamba Kingai na Jumanne Walifikia hadi Counter
Shahidi: Nimewaona Wakiwa Kingai na Jumanne Counter wakikabidhi Watuhumiwa
Kibatala: Central Pako hivi Kuna Counter Ya Polisi ya Cement na Sehemu za Kukaa Ndugu (ANAONYESHA KWA VITENDO), Ulikaa wapi
Shahidi: Enheeeeee hapo Kwenye Ngazi
Kibatala: Kwa hiyo Ukiwa hapa Unaona Pale Counter Shahidi: Naona pale Counter, Wanachoandika Sioni ila watu nawaona
Kibatala: Mkiwa kwenye gari nani alimuuliza Mohammed Ling'wenya kuhusu Moses Lijenje?
Shahidi: Ni Afande Kingai
Kibatala: Unafahamu Kwamba hapo anakuwa ameanza Kukiri Kosa?
Shahidi: Hapana yalikuwa ni Maongezi tu ya Kawaida
Kibatala: ila Nyie ni Polisi na Mlienda Kwa ajili ya Kuwakamata
Shahidi: Ndiyo ila Ilikuwa Maongezi ya Kawaida
Kibatala: Wakati Mnawakabidhi Watuhumiwa Pale Central, Je Wakati Wanakabidhiwa wewe Bunduki Ulikabidhi Saa ngapi
Shahidi: Ndiyo nilisema Nilienda Kukabidhi Saa Moja
Kibatala: Nimekusikia Vyema Kwamba Tarehe 08 August 2020 mlipewa Maelekezo na Afande Kingai Kuwatoa Watuhumiwa Central Kuwapeleka Mbweni
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Kuna Mtu aliwaambia Kwamba walikuwa wameshahojiwa na wamekiri
Shahidi: Siku ya Tarehe 07 August 2020 Afande Kingai Alisema anabakia Kuwahoji
Kibatala: Kwa hiyo wewe hufahamu Chochote Kuhusu Maelezo Ya Ling'wenya?
Shahidi: Hapana Sijui
Kibatala: Mohammed Ling'wenya alifikishwa Mahakamani lini
Shahidi: 19 August 2020
Kibatala: Wewe Ulishiriki Kumpeleka Ling'wenya Mahakamami
Shahidi: Hapana sikuwepo
Kibatala: ulijuaje Wamepelekwa Mbweni
Shahidi: Nilisikia Kwa Afande Kingai
Kibatala: Wewe ulifika Mbweni?
Shahidi: Sijawahi kufika Mbweni
Kibatala: Wewe si uliwapeleka Mbweni
Shahidi: Ndiyo Nilifika Mbweni
Kibatala: Sasa watuhumiwa wanasema ulikuwepo Mbweni
Shahidi: Sijawahi kufika Mbweni
Kibatala: Sawa mimi kazi yangu Kuuliza Maswali, Ukijichanganya ni Kazi ya Jaji Sasa Kujua Ukweli.
Kibatala: ulisema Ulikuwa na Silaha, Je ukiongea lolote kuhusu Silaha yako
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ilikuwa silaha gani
Shahidi: ilikuwa AK 47
Kibatala: Ulizungumzia kuikabidhi pale Central
Shahidi: Hapana
Kibatala: Vituo Vyote Mahabusu Wanakuwa Chini ya OCS
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mlimtaatifu OCS kwamba Mnampelekea Watuhumiwa Pale Mbweni
Shahidi: Hapana, hiyo ni kazi ya Viongozi
Kibatala: Wakati Mnatoka Moshi Tarehe 06 August 2020, Je ulikuwa unafahamu Kwamba Moja Wapo ya Mambo yatayofanyika Kufika Dar ni Ling'wenya Kuandika Maelezo ya Onyo
Shahidi: Hapana Sikufahamu
Kibatala: Wakati Mnatoka Moshi Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Afande Kingai, Inspector Mahita, na ASP Jumanne Ambao wa Kubwa zako wakimwambia Ling'wenya Kwamba Tunakwenda Dar es Salaam na Tulifika Dar es Salaam Kuna Maelezo ya Onyo yataandikwa
Shahidi: Sikusikia
Kibatala: Wakati wote simu zilikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa nazo Mimi
Kibatala: Na wakati wote Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Hukusema Kwamba Ulitoa Simu kwa Ling'wenya Kwamba Unaweza Kuwapigia Ndugu zako au Mawakili wako
Shahidi: Sikusema Ndiyo
Kibatala: Kuna Mahala Popote Umemwambia Jaji Kwamba Wakati wowote tunazunguka Pale Moshi Mpaka Arusha, wakimwambia Ling'wenya Kwamba hapa tupo Kwenye Mazoezi Mazito ya Kisheria Mpaka Unamtaja Lijenje, Je Nikupe Simu Uongee na Ndugu au Mwanasheria
Shahidi: Hapana Sijamwambia
Kibatala: Kwa kuwa Ling'wenya alikuwa anatoa Ushirikiano Kwenu Mpaka Mkaenda Stendi ya Mabasi, Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Lijenje alikuwa anaenda Mkoa gani
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Kuna Mashahidi hapa wanasema Kwamba, Ling'wenya alishakiri na Kutoa Maelezo Yake JUU YA ushiriki wake, Je Ulishawahi Kusikia Afisa yoyote akisema Kwamba Kwa kuwa Ling'wenya ameshakiri Ngoja nimpeleka Mahakamani?
Shahidi: Siku sikusikia
Kibatala: Ulishawahi Kufanya Kazi CRO
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna Karatasi Yoyote ambayo Mtu Alisha kabidhi Mtuhumiwa Hakuna Mahala Popote ambapo ANAPEWA katasi lolote pale CRO
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulimtajia Dereva Mlitoka naye Arumeru Mpaka Moshi
Shahidi: Sikumtaja Jina, Nilitaja Dereva
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama ulitaja Jina la Derava aliyewatoa Njia panda Himo Mpaka Mpak Dar es Salaam
Shahidi: Hapana Sikutaja jina
Kibatala: Mliwahi Kumuona Mkuu wa Kituo cha Polisi Central Dar es Salaam
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pale Rau Madukani kuna Ofisi ya Mtaa au Kituo cha Polisi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sina swali lingine
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Tumefanya Assessment Ya Maswali na Hakuna Swali la Kufanya Re examination Anakaa Chini
Jaji: Tunakushukuru kwa Ushahidi Wako, sasa unaweza Kwenda
Shahidi anatoka kizimbani
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka Kesho tarehe 24 November Ilituweze Kuja na Shahidi Mwingine
Jaji: Nyinyi ndiyo Mnaojua huyo Shahidi anayekuja anaushahidi Gani, Kama mnaona ni Mfupi Waje wawili
Kibatala: Sahihi Mheshimiwa Jaji
WS Robert Kidando: Tutaona Cha Kufanya, Lakini kwa huyu wa Kesho tayari yupo
Jaji: Upande wa Utetezi
Kibatala: Hatuna Pingamizi
Jaji: anaandika Kidogo Mahakama: bado ipo Kimya
Jaji: basi Mahakama inakubiana na maombi ya upande wa mashtaka kuhairisha kesi, mashtaka mnaelekezwa kwamba ukiona ushahidi siyo mrefu walete mashahidi wawili. Na washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza mpaka kesho Asubuhi saa 3 kamili
Jaji anatoka