Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,360
Ya wapi maisha bora, Yale tuloahidiwa,
Visiwani nako bara, hakika tuliambiwa,
Mambo kuwa barabara, chama tukikichagua
Wanaoona waseme, ya wapi Maisha Bora?
Kauli mbiu ilikuwa, ikawekwa kwenye Chama,
Hili na lile ikawa, na vinywani wakasema
Watanzania tutakuwa, na maisha bora na mema
Waliosikia waseme, ya wapi maisha bora?
Siku zazidi kimbia, kama vile langalanga,
Ulingoni kufikia, tunakiona kilanga,
Maisha yamefifia, kwa wajanja na wajinga
Waliosema waseme, ya wapi maisha bora?
Mfano mmoja natoa, usidhani ni utani,
Mjasiriamali Tanzania, anapita mitaani,
Plastiki kugombea, mkono uende kinywani
Hivi hayo utasema, kweli maisha bora?
Umeme hapa nyumbani, bei juu si utani
Imeshapita angani, inakaribia juani
Mlalahoi kabaini, umeme hauwezekani,
Ni yepi Maisha bora, Yale waliyoyasema?
Misosi acha kusema, haiingii kinywani
Tanzania sio pema, kusema utatamani,
Sukari kitu lazima, buku mbili karibuni,
Maisha bora ni ndoto, walizoziota wenzetu.
Nishati usijaribu, kuingia kituoni,
Mkweche wako jaribu, dizeli waitamani,
Hapo watakapojibu, haitakaa akilini,
Lita elfu mia saba, je haya maisha bora?
Ni mengi ningeyataja, nawaachia wenzangu,
Anyisile hebu chuja, bila kujali undugu,
Kama wengine mwaja, kujibu tatizo langu,
Maisha yaliyo bora, Ni kweli tumeyapata?
Ningeweza endelea, vidole vyatetemeka,
Huruma namuonea, wale waliojikweka
Kuni, jembe na shoka, mpaka jua latoweka
Hawajui walani, kujaza matumbo yao.
Lakini bado waambiwa, maisha bora yaaja
Visiwani nako bara, hakika tuliambiwa,
Mambo kuwa barabara, chama tukikichagua
Wanaoona waseme, ya wapi Maisha Bora?
Kauli mbiu ilikuwa, ikawekwa kwenye Chama,
Hili na lile ikawa, na vinywani wakasema
Watanzania tutakuwa, na maisha bora na mema
Waliosikia waseme, ya wapi maisha bora?
Siku zazidi kimbia, kama vile langalanga,
Ulingoni kufikia, tunakiona kilanga,
Maisha yamefifia, kwa wajanja na wajinga
Waliosema waseme, ya wapi maisha bora?
Mfano mmoja natoa, usidhani ni utani,
Mjasiriamali Tanzania, anapita mitaani,
Plastiki kugombea, mkono uende kinywani
Hivi hayo utasema, kweli maisha bora?
Umeme hapa nyumbani, bei juu si utani
Imeshapita angani, inakaribia juani
Mlalahoi kabaini, umeme hauwezekani,
Ni yepi Maisha bora, Yale waliyoyasema?
Misosi acha kusema, haiingii kinywani
Tanzania sio pema, kusema utatamani,
Sukari kitu lazima, buku mbili karibuni,
Maisha bora ni ndoto, walizoziota wenzetu.
Nishati usijaribu, kuingia kituoni,
Mkweche wako jaribu, dizeli waitamani,
Hapo watakapojibu, haitakaa akilini,
Lita elfu mia saba, je haya maisha bora?
Ni mengi ningeyataja, nawaachia wenzangu,
Anyisile hebu chuja, bila kujali undugu,
Kama wengine mwaja, kujibu tatizo langu,
Maisha yaliyo bora, Ni kweli tumeyapata?
Ningeweza endelea, vidole vyatetemeka,
Huruma namuonea, wale waliojikweka
Kuni, jembe na shoka, mpaka jua latoweka
Hawajui walani, kujaza matumbo yao.
Lakini bado waambiwa, maisha bora yaaja