Elections 2010 Ya wapi maisha bora?

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,360
Ya wapi maisha bora, Yale tuloahidiwa,
Visiwani nako bara, hakika tuliambiwa,
Mambo kuwa barabara, chama tukikichagua
Wanaoona waseme, ya wapi Maisha Bora?

Kauli mbiu ilikuwa, ikawekwa kwenye Chama,
Hili na lile ikawa, na vinywani wakasema
Watanzania tutakuwa, na maisha bora na mema
Waliosikia waseme, ya wapi maisha bora?

Siku zazidi kimbia, kama vile langalanga,
Ulingoni kufikia, tunakiona kilanga,
Maisha yamefifia, kwa wajanja na wajinga
Waliosema waseme, ya wapi maisha bora?

Mfano mmoja natoa, usidhani ni utani,
Mjasiriamali Tanzania, anapita mitaani,
Plastiki kugombea, mkono uende kinywani
Hivi hayo utasema, kweli maisha bora?

Umeme hapa nyumbani, bei juu si utani
Imeshapita angani, inakaribia juani
Mlalahoi kabaini, umeme hauwezekani,
Ni yepi Maisha bora, Yale waliyoyasema?

Misosi acha kusema, haiingii kinywani
Tanzania sio pema, kusema utatamani,
Sukari kitu lazima, buku mbili karibuni,
Maisha bora ni ndoto, walizoziota wenzetu.

Nishati usijaribu, kuingia kituoni,
Mkweche wako jaribu, dizeli waitamani,
Hapo watakapojibu, haitakaa akilini,
Lita elfu mia saba, je haya maisha bora?


Ni mengi ningeyataja, nawaachia wenzangu,
Anyisile hebu chuja, bila kujali undugu,
Kama wengine mwaja, kujibu tatizo langu,
Maisha yaliyo bora, Ni kweli tumeyapata?

Ningeweza endelea, vidole vyatetemeka,
Huruma namuonea, wale waliojikweka
Kuni, jembe na shoka, mpaka jua latoweka
Hawajui walani, kujaza matumbo yao.
Lakini bado waambiwa, maisha bora yaaja
 
Ya wapi maisha bora, Yale tuloahidiwa,
Visiwani nako bara, hakika tuliambiwa,
Mambo kuwa barabara, chama tukikichagua
Wanaoona waseme, ya wapi Maisha Bora?

Kauli mbiu ilikuwa, ikawekwa kwenye Chama,
Hili na lile ikawa, na vinywani wakasema
Watanzania tutakuwa, na maisha bora na mema
Waliosikia waseme, ya wapi maisha bora?

Siku zazidi kimbia, kama vile langalanga,
Ulingoni kufikia, tunakiona kilanga,
Maisha yamefifia, kwa wajanja na wajinga
Waliosema waseme, ya wapi maisha bora?

Mfano mmoja natoa, usidhani ni utani,
Mjasiriamali Tanzania, anapita mitaani,
Plastiki kugombea, mkono uende kinywani
Hivi hayo utasema, kweli maisha bora?

Umeme hapa nyumbani, bei juu si utani
Imeshapita angani, inakaribia juani
Mlalahoi kabaini, umeme hauwezekani,
Ni yepi Maisha bora, Yale waliyoyasema?

Misosi acha kusema, haiingii kinywani
Tanzania sio pema, kusema utatamani,
Sukari kitu lazima, buku mbili karibuni,
Maisha bora ni ndoto, walizoziota wenzetu.

Nishati usijaribu, kuingia kituoni,
Mkweche wako jaribu, dizeli waitamani,
Hapo watakapojibu, haitakaa akilini,
Lita elfu mia saba, je haya maisha bora?


Ni mengi ningeyataja, nawaachia wenzangu,
Anyisile hebu chuja, bila kujali undugu,
Kama wengine mwaja, kujibu tatizo langu,
Maisha yaliyo bora, Ni kweli tumeyapata?

Ningeweza endelea, vidole vyatetemeka,
Huruma namuonea, wale waliojikweka
Kuni, jembe na shoka, mpaka jua latoweka
Hawajui walani, kujaza matumbo yao.
Lakini bado waambiwa, maisha bora yaaja

Bahati mbaya mimi sio fundi wa mashairi ningeongeza beti kadhaa. Ubarikiwe mkuu kwa shairi safi
 

Walitufanya majuha,
Kutukosesha furaha,
Na za uongo nasaha,
Tena huku wakihaha,

Asante Ngambo Ngali,
Kwa lako zuri swali,
Tabidi kuwa wakali,
Na wayajibu maswali,

Kweli mbuzi yake kamba,
Ipo siku twawabamba,
Kama mvuvi na kamba,
Baharini akitamba.

Wametulisha upepo,
Bila hiari kuwepo,
Na wamejifanya popo,
Na bila miti kuwapo.

Maisha bora ya wapi,
Hatutaki jibu fupi,
Ukweli wao u wapi,
Tusidanganywe kwa pipi.

Watanzania tungane,
Pamoja tushikamane,
Tena tusikunje nne,
Sote tushirikiane.
 

Walitufanya majuha,
Kutukosesha furaha,
Na za uongo nasaha,
Tena huku wakihaha,

Asante Ngambo Ngali,
Kwa lako zuri swali,
Tabidi kuwa wakali,
Na wayajibu maswali,

Kweli mbuzi yake kamba,
Ipo siku twawabamba,
Kama mvuvi na kamba,
Baharini akitamba.

Wametulisha upepo,
Bila hiari kuwepo,
Na wamejifanya popo,
Na bila miti kuwapo.

Maisha bora ya wapi,
Hatutaki jibu fupi,
Ukweli wao u wapi,
Tusidanganywe kwa pipi.

Watanzania tungane,
Pamoja tushikamane,
Tena tusikunje nne,
Sote tushirikiane.

Jamaa tumeg'amua, shere walotuchezea
Na sasa wameamua, kutuletea hadaa
Kwani wameelewa, maisha bora yapaa
Jamaa wameshituka, uongo tumebaini.

Baada ya muda kupita, ahadi haijawa kweli
Mikakati kutafuta, kuwapata wafadhili
Na jibu wakalipata, wakatangaza na dili
Ni afadhali kununua, kulikoni kudanganya

Mojawapo kasimama, bajeti kakatua
Na jibu akanguruma, ili kiti kuchukua
Mafedha ya wakulima,lazima kuyachukua
Ili waweze shinda, lazima kuwe na pesa

Keti chini usikie, ni hamsini bilioni
Hizi ndio wapatiwe, kuwaingiza kitini,
Usukani wachukue, kuturudisha shidani
Fedha zote ni za nini, wakati maisha ni bora

Wahenga waliyasema, pale palipo udhia
Na wewe umekwama, kweli penyeza rupia
Ili uweze simama, ndicho wachokusudia
Hawa watu wenye chama, na sasa wameamua
Kura sasa ni bidhaa, wa wala si ridhaa.

Anyisile nakubali, Watanzania tuungane,
Pamoja tushikamane, tena tusikunje nne,
Sote tushirikiane, kuyakataa mapene

Bilioni hizo zao, tuzione kama sumu
 
Ngambo Ngali umenena, tena kwa hisia kali,
Ukweli siyo fitina, yapasa kuwa wakali,
Tuwaumbue firuna, kwa kutumia akili,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Nyingi ahadi kupewa, tena pasi na aibu,
Tumekuwa waonewa, tena tumekuwa bubu,
Hawataki kosolewa, eti na tusijaribu,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Tusiogope vichaka, kuanzisha njia mpya,
Wenye panga na mashoka, hata wale na pataya,
Tusimame bila choka, sisikilize riwaya,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Hawafai tena hawa, tena wote wameoza,
Wafanana na haluwa, isofanana na chaza,
Na wamelegea hawa, na hawawezi jikaza,
Yabidi kuwa makini na yao fedha haramu.

Yabidi kuwa makini na yao fedha haramu,
Watufanya masikini, wa akili na fahamu,
Tena hazimo kichwani, sote ni wenda wazimu,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Sote tena kwa umoja, twelimishane pamoja,
Ni sisi wenye haja, kuutengeneza umoja,
Kabla ya mwingine kuja, kutuletea viroja,
Yabidi kuwa makini na yao fedha haramu
 
Ngambo Ngali umenena, tena kwa hisia kali,
Ukweli siyo fitina, yapasa kuwa wakali,
Tuwaumbue firuna, kwa kutumia akili,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Nyingi ahadi kupewa, tena pasi na aibu,
Tumekuwa waonewa, tena tumekuwa bubu,
Hawataki kosolewa, eti na tusijaribu,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Tusiogope vichaka, kuanzisha njia mpya,
Wenye panga na mashoka, hata wale na pataya,
Tusimame bila choka, sisikilize riwaya,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Hawafai tena hawa, tena wote wameoza,
Wafanana na haluwa, isofanana na chaza,
Na wamelegea hawa, na hawawezi jikaza,
Yabidi kuwa makini na yao fedha haramu.

Yabidi kuwa makini na yao fedha haramu,
Watufanya masikini, wa akili na fahamu,
Tena hazimo kichwani, sote ni wenda wazimu,
Yabidi kuwa makini, na yao fedha haramu.

Sote tena kwa umoja, twelimishane pamoja,
Ni sisi wenye haja, kuutengeneza umoja,
Kabla ya mwingine kuja, kutuletea viroja,
Yabidi kuwa makini na yao fedha haramu

Sote tena kwa pamoja, twelimishane pamoja,
Ni sisi wenye haja, kuutengeneza umoja
Kabla ya wengine kuja, kutuletea viroja
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora.

Kudai kilicho bora, kazi rahisi hakika
Siku ya kupiga kura, alfajiri waamka
Haitakuwa hasara, kwani haki waitaka
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Kama fedha wamekupa, tuliza zako akili
Wala usilete pupa, icheze vizuri dili
Chagua aliye supa, muache wa pilipili
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Miaka mitano sasa, hakuna walichofanya
Mwanajipiga misasa, vihela kutudanganya
Kwa kutumia mapesa, haki zetu kunyang'anya
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Njia mpya nabaini, kwa mbali yajongelea
Tusafiri vijijini, mambo haya kueleza
Hela chafu si utani, demokrasi inaua
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Tuhubiri kila kona, sokoni na mashuleni
Kwa marefu na mapana, sebuleni na vyumbani
Uwezo hawana tena, sasa hatuwatamani
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Twataka kilicho bora,kuliko hiki cha enzi
Mwanza Mbeya na Tabora, uacheni usingizi
Tuwe makini na kura, tusije leta ajizi
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Hela zao tuzitupe, kama vile ni uchafu
Kwenye giza na kweupe, panapo anga na sakafu
Lazima tuwe mapepe, pasi kuwepo na hofu
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Anyisile namaliza, Bujibuji muambie
Tunaweza kutimiza, vijana tuwaimbie
Wazee kuwahimiza, wamama wasaidie
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

 
Sote tena kwa pamoja, twelimishane pamoja,
Ni sisi wenye haja, kuutengeneza umoja
Kabla ya wengine kuja, kutuletea viroja
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora.

Kudai kilicho bora, kazi rahisi hakika
Siku ya kupiga kura, alfajiri waamka
Haitakuwa hasara, kwani haki waitaka
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Kama fedha wamekupa, tuliza zako akili
Wala usilete pupa, icheze vizuri dili
Chagua aliye supa, muache wa pilipili
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Miaka mitano sasa, hakuna walichofanya
Mwanajipiga misasa, vihela kutudanganya
Kwa kutumia mapesa, haki zetu kunyang'anya
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Njia mpya nabaini, kwa mbali yajongelea
Tusafiri vijijini, mambo haya kueleza
Hela chafu si utani, demokrasi inaua
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Tuhubiri kila kona, sokoni na mashuleni
Kwa marefu na mapana, sebuleni na vyumbani
Uwezo hawana tena, sasa hatuwatamani
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Twataka kilicho bora,kuliko hiki cha enzi
Mwanza Mbeya na Tabora, uacheni usingizi
Tuwe makini na kura, tusije leta ajizi
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Hela zao tuzitupe, kama vile ni uchafu
Kwenye giza na kweupe, panapo anga na sakafu
Lazima tuwe mapepe, pasi kuwepo na hofu
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora

Anyisile namaliza, Bujibuji muambie
Tunaweza kutimiza, vijana tuwaimbie
Wazee kuwahimiza, wamama wasaidie
Waungwana amkeni, kudai kilicho bora


Kudai kilicho bora, ni kweli si kazi ngumu,
Tusitumie bakora, kusababisha ugumu,
Tusiruke kama chura, na mbeleni kutodumu
Hekima yahitajika, kulijenga taifa bora.

Kweli haki twaitaka, waungwana amkeni,
Kuziondoa hizi taka, zisishike usukani,
Hatuyaki mashaka, kupoteza umakini,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Miaka mitano sasa, hakuna walichofanya,
Wamezidi kwa anasa, na zao tabia mbaya,
Wamezidisha mikasa, tena hawana haya,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Njia moja ilobaki, hata mimi naiona,
Tung'oe vyote visiki, maendeleo kuona,
Tuache zetu hamaki, jema tukishaliona,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Kalamu siraha kubwa, Bujibuji tamweleza,
Naye Mundu bwna mkubwa, tazidi kumhimiza,
Tusiogope wakubwa, mabaya kuyachomoza,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Wakikupa we pokea, akili mwako kichwani,
Tena sije wafokea, upoteze tumaini,
Malengo kujiwekea, ili uwe wa thamani,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Ili kuweza fikia, kwenye yale yalo bora,
Lazima kuwafukia, woote wasiyo bora,
Vijijini kuwafikia, kuwapa elimu bora,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.
 
Maisha bora kwa kila mtanzania yapo katika kijitabu cha ilani ya uchaguzi CCM 2005... ukiyataka jipatie nakala.
 
Maisha bora kwa kila mtanzania yapo katika kijitabu cha ilani ya uchaguzi CCM 2005... ukiyataka jipatie nakala.

Walisimama jukwaani, kauli walizitoa
Ofisini mikutanoni, bayana kuelezea
Maisha bora nyumbani, wao wangetupatia
Hakika hawakusema, kitu juu ya kitabu.

Ilani ya uchaguzi, haiongezi ugali
Kuupata ufumbuzi, tunalisemea hili
Sisi si wanafunzi, kuvipekua vitabu
Tukitaka maisha bora, tuwaondoe wakongwe

Ilani hiyo kitabu, lakima kutekeleza
Kama inaleta taabu, shurti kutelekeza
Hii ndio sababu, nataka kuwaeleza
Hatuna maisha bora, wakongwe wapumzike

Sasa miongo mitano, hakuna tulichonacho
Inatuuma mikono, tunaitoa mimacho
Sana sana ni kibano, hakuna tulichonacho
Chama kikongwe bai, pumzikeni salama

Wakati umewadia, ni Oktoba hakika
Sehemu ya historia, oktoba ikilazimika,
Lazima kusaidia, kura kuziandika,
Ukipewa karatasi, usichague wakongwe.
Wameshindwa siku zote, kamwe sasa hawawezi
 

Kudai kilicho bora, ni kweli si kazi ngumu,
Tusitumie bakora, kusababisha ugumu,
Tusiruke kama chura, na mbeleni kutodumu
Hekima yahitajika, kulijenga taifa bora.

Kweli haki twaitaka, waungwana amkeni,
Kuziondoa hizi taka, zisishike usukani,
Hatuyaki mashaka, kupoteza umakini,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Miaka mitano sasa, hakuna walichofanya,
Wamezidi kwa anasa, na zao tabia mbaya,
Wamezidisha mikasa, tena hawana haya,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Njia moja ilobaki, hata mimi naiona,
Tung'oe vyote visiki, maendeleo kuona,
Tuache zetu hamaki, jema tukishaliona,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Kalamu siraha kubwa, Bujibuji tamweleza,
Naye Mundu bwna mkubwa, tazidi kumhimiza,
Tusiogope wakubwa, mabaya kuyachomoza,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Wakikupa we pokea, akili mwako kichwani,
Tena sije wafokea, upoteze tumaini,
Malengo kujiwekea, ili uwe wa thamani,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Ili kuweza fikia, kwenye yale yalo bora,
Lazima kuwafukia, woote wasiyo bora,
Vijijini kuwafikia, kuwapa elimu bora,
Hekima yahitajika, kujenga taifa bora.

Hekima yahitajika, kujenga taifa bora
Kilicho bora twataka, tutakipata kwa kura
Akili zahitajika, mambo yawe barabara
Jamani tuhimizane, Oktoba i karibu

Uchaguzi ndio njia, kuondoa wasofaa
Madaraka washikilia, haki kweli wamechoka
Na sasa wasubiria, Oktoba itapofika
Jamani tuangalie, tena tusidanganyike

Tuwape elimu bora, ndugu zetu vijijini
Siku ya kupiga kura, wasiingizwe mjini
Wasizifanye papara, waongo kuwabaini
Kama hicho watafanya, maisha bora si haba
 
Kazi ipo yaani ukiwa na nakala ya ilani ya uchaguzi utapata maisha bora? Tunataka utekelezaji bwana sio maandishi, ona waziri mkuu wa Japani kashindwa ahadi moja tuu kaachia ngazi

Lazima Oktoba tujiulize ya wapi maisha bora waliyotuahidi? Hivi sasa tunayo bora maisha... kesho na kesho kutwa hatujui... langu wazo ni kejeli kwao... Je maisha bora yatakuwapo kwenye ilani ya 2010 tena?
 
Back
Top Bottom