Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 3,804
- 8,797
Miaka ya nyuma nchi ikiwa chini ya utawala wa Ali Hassan Mwinyi ilikumbwa na mgogoro mkubwa wa Wauguzi na Waganga kugoma kutibu watu katika hospital kubwa ya Muhimbili. Mgomo ulikuwa mkubwa sana, sasa ikapangwa Mkuu wa nchi aende kuweka sawa mambo. Lakini akakimbia kikao na akaenda kucheza kwasakwasa ya kanda Bongoman. Takriban miaka 30 na ushee imepita, nchi imekubwa na mgomo wa wafanyabiashara wa kariakoo nao wakawa na kauli ya kutaka kuongea na Rais, matokeo yake Rais akamtuma Waziri Mkuu mara mbili. Kitendo cha kushangaza siku iliyofuata Mkuu wa nchi anaenda kuzindua minara ya urushaji matangazo ya kituo cha Azam huku alikimbia kuongea na wafanyabiashara. Je kuna umuhimu upi kwa Taifa kukimbia Kariakoo na kwenda Azam?