Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
- Thread starter
- #21
Hii VIR (Vehicle Inspection Report) Inaandikwa pale gari ikitoka melini na Chief officer au Captain wa meli huisaini kukubali ya kuwa hilo gari hivyo vitu vilivyoandikwa vipo au vimemiss.
Mteja wakati wa kuchukua gari lake kabla ya kuanza kuitupia lawama mamlaka ya bandari, inampasa kwanza kuangalia VIR kama wakati gari linashuka walirekodi kama redio, au power window n.k je vilikuwepo wakati wa upakuzi kutoka melini au la! VIR ndio itakupa majibu.
Kama havikuandikwa wakati gari linashuka, maana yake vimekwapuliwa huko huko melini. naomba udeal na transport wako.
Na kama VIR inaonyesha gari imeshuka na vifaa vyote wakati wa kulichukua gari lako unaona kuna vitu hamna basi wewe lia na Bandari.
Kabla gari haijafika hapa nchini kuna Bandari kadha wa kadha meli inapita, sasa basi mfano imepita Cape town, au Mombasa kabla ya kuja huku nchini, na wakati wa upakuzi wakakwapua kule wakati wakitoa magari ya kwao na wale ma Crew wa meli hawakuwa makini....! huwezi jua
Ection zinachukuliwa sana tu na Usiwe mnyonge fuatilia haki yako ukweli utajulikana tu, na hatua zinachukuliwa juu ya wote wanaosababishia Bandari kila siku inatupiwa lawama
Wateja huchukua magari yao kutoka bandari kavu. Wanaoshusha magari toka melini ni wafanyakazi wa bandari. Hao ndio wenye dhamana ya kuhakikisha kwamba gari imeteremka ikiwa salama au baadhi ya vifaa vimekosekana. Cha kushangaza mtu anapopokea gari hakuna vielelezo vyo vyote kuhusu upotevu au usalama wa gari isipokuwa tu makabidhiano ya gari toka bandari kavu waka limeshapitia mikono ya wengi. Hapo kuna walakini katika utendaji katika bandari yetu. Vigumu Japan kuipa vifaa kama inavyofanyika Dar, hali kadhalika bandari za uarabuni au ulaya, mtindo huu ni bandari za hapa Afrika.