Insurgent
JF-Expert Member
- Jun 26, 2007
- 469
- 18
Hivi hawa ndugu zetu zimo kichwani?! Kuumiza watu wengi ili kupata njia ya kutawala?!
Ama kweli, kuongoza chama kama disco ni hatari...sasa hivi wanatumia "muziki" unaopendwa kwenye masikio ya wengi kuleta chuki? Labda kuna wenye mawazo zaidi...lawakilisha kwenu.
CHADEMA YADAIWA KUTAKA TANZANIA INYIMWE MISAADA
CHAMA cha upinzani cha CHADEMA kinadaiwa kuwa kimeanzisha kampeni ya siri na ya chini chini kuyashauri mataifa ya Magharibi kusitisha misaada yake kwa Tanzania. Habari zinadai CHADEMA kupitia Mwenyekiti wake, Bw Freeman Mbowe, kimeanzisha kampeni kuzishawishi nchi zinazotoa misaada kwa wingi Tanzania, kusitisha misaada.
Habari hizo zinadai katika hatua ya kwanza ya kampeni hiyo, Bw Mbowe tayari amezungumza na maofisa wa balozi mbili Dar-es-salaam akiziomba kusitisha misaada hiyo.
Hoja yake ni kuwa misaada inayotolewa Tanzania inatumika vibaya, bila kuwafikia walengwa, Watanzania wa kawaida.
Habari hizo hata hivyo zinathibitisha kuwa hata hizo nchi mbili ambazo Bw. Mbowe amezungumza nazo, zimekataa mpaka sasa kumpa msimamo kamili kama kweli zinaona zinao ulazima wa kusimamisha misaada kwa Tanzania.
Kwa mujibu wa habari hizo kampeni hiyo ya Bw. Mbowe na CHADEMA inalenga kuzuia Tanzania kupata fedha ambazo zingesaidia kuimarisha sekta ya kijamii ya maeneo muhimu sana kwa wananchi ya elimu, maji, kilimo, afya, miundombinu.
Serikali mbili za CCM, katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, zimeelekeza nguvu zao katika maeneo hayo matano muhimu ambayo yanagusa moja kwa moja maisha ya wananchi wote.
Katika bajeti ya mwaka huu, zimeweka kiasi cha asilimia 52 katika maeneo hayo matano tu kwa sababu ya umuhimu wake kwa wananchi, na sehemu kubwa ya fedha hizo itatokana na misaada kutoka nchi za Magharibi.
Mkakati wa CHADEMA ni kwamba kama itafanikiwa kusitisha misaada kwa Tanzania, basi itakuwa haiwezekani tena kwa CCM kutekeleza Ilani yake hiyo na hivyo chama hicho kufanikiwa kujenga chuki kati ya wananchi na serikali yao.
Bajeti ya Serikali kwa mwaka huu wa fedha ambao umeanza miezi miwili iliyopita, inategemea misaada ya wafadhili kwa asilimia 39, ambayo ni kubwa kiasi cha kuathiri mno maisha ya Watanzania kama fedha hizo zinasitishwa na wafadhili.
Habari zinadai mkakati huo wa CHADEMA...baadhi ya wachunguzi wa masuala ya kisiasa waliozungumza na gazeti hili wanaulezea kama tahayari ya kiwango cha chini kabisa.
"Hizi siyo tu mbinu za vyama kuharibiana kisiasa, bali ni kuwatesa moja kwa moja wananchi", alisema mhadhiri mmoja mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam.
Wachunguzi pia wanasema huo ni mkakati ambao hauwezi kufanikiwa kwa sababu nchi za Magharibi haziwezi kukubali kuvuruga uhusiano wake na Tanzania kumfurahisha mtu au kutimiza ajenda na matakwa ya kisiasa ya CHADEMA.
Kama historia inavyoonyesha kusimamisha misada kwa Tanzania ni mkakati ambao unafanikiwa tu kuwaumiza zaidi Watanzania wa kawaida kuliko hao viongozi ambao CHADEMA inadai wanatumia vibaya misaada hiyo.
Uzoefu wa Tanzania wakati wa utawala wa Rais Ali Hassani Mwinyi, unadhibitisha kusimamishwa kwa misaada ni sera itakayowaumiza zaidi wananchi CHADEMA inayodai kuwatetea.
Wakati huo, nchi kadhaa za Magharibi zilisimamisha misaada kwa visingizio mbali mbali, hatua ambayo iliwaumiza sana wananchi wa kawaida wa Tanzania na kuvuruga sera za misaada za nchi za Magharibi.
Usitishaji wa misaada, hata hivyo, ni moja tu ya mikakati mipya ya CHADEMA inayolenga kuharibiana kisiasa baada ya chama hicho kukiri sera na mikakati yake imeshindwa kufanya kazi kwa kupunguza nguvu na kasi ya CCM.
Mkakati mwingine wa CHADEMA ni kujaribu kuwapaka matope watu wote ambao wanaonekana ama kudaiwa kuwa karibu na Rais Jakaya Kikwete, kama njia ya kujaribu kumlazimisha Rais kujitenga na watu hao.
Habari kuhusu mkakati huo zinadai CHADEMA kwa kushirikiana na baadhi ya watu wakiwamo wafanyabiashara wanaoficha sana msimamo wao wa kisiasa, sasa itawalenga na kuwapaka tope baadhi ya watu hao wanaodaiwa kuwa karibu na Rais Kikwete.
Miongoni mwa watu hao ambao wanalengwa na kampeni za sasa za CHADEMA ni pamoja na Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa; Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi na Mweka Hazina wa Taifa wa CCM, Bw. Rostam Aziz.
Habari hizo zinadai orodha hiyo ni ndefu zaidi kuliko viongozi viongozi hao watatu, ambao karibuni wamekuwa wakilengwa sana na kampeni za CHADEMA pamoja na washirika wake.
Shabaha ya mkakati huo wa CHADEMA ni kujaribu kumgombanisha Rais na watu ambao kw miaka mingi wamekuwa na msimamo wa kamoja kisiasa.
Viongozi hao watatu walipoulizwa kuhusu mkakati huo wa CHADEMA walikataa kusema lolote na walionyesha kutohangaishwa na jitihada hizo mpya za CHADEMA.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mwandishi wa Habari wa Waziri Mkuu, Bw. Said Nguba alisema wamepata taarifa za hatua hiyo ya CHADEMA na vyombo vya dola vinafuatilia.
Hata hivyo, alisema wao kama watekelezaji wakuu wa sera za chamba tawala, CCM hawasumbuliwi na propaganda hzio bali wataendelea kutekeleza kwa vitendo mambo ya msingi ya kuondoa kero za wananchi kwani uwezo huo Serikali inao.
Alipoulizwa jana kwa simu alikanusha kwenda ofisi za ubalozi kwa ajili ya hiyo akidai kukatiwa misada sio ajenda ya CHADEMA lakini akasema hana uhakika kama watendaji wengine walienda "kwani huenda huko kwa mambo yao"
Naye Said Mwishehe anaripoti kuwa, Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Slaa ametaja majina ya orodha ya kundi la viongozi, maofisa wa umma na mawakala anaodai ni miongoni mwa watu ambao wanaihujumu nchi kutokana na kula fedha za umma na kutoa maamuzi yanayolisababishia taifa madeni.
Katika orodha ya mafisadi aliowataja Dkt. Slaa jana katika mkutano wake na wananchi wa Temeke Mwembe Yanga, Dar-es-salaam wakiwemo wenyeviti na viongozi wa kambi ya upinzani alisema orodha yake ina mafisadi 11 ambapo kabla ya kutaja hadharani alitoa vigezo vya kisheria alivyotumia kuwabainisha mafisadi hao kwa wananchi.
"Katika kundi la orodha ya mafisadi wamo viongozi wa umma ambao kwa kutumia nyadhifa na vyeo vya katika utumishi wa umma wamefanya maamuzi ambayo taifa limepoteza mapato, utajiri na rasilimali zake na kuneemesha raia au taasisi za kigeni.
Kwa mfano wapo viongozi ambao wameshiriki kusaini mikataba mibovu katika sekta za madini pamoja na maeneo mengine", alisema Dkt. Slaa katika mkutano huo aliohutubia yeye, mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu, Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustine Mrema. Viongozi hao walitua hapo kwa helikopta.
Pia alisema viongozi ambao wamo katika orodha hiyo wamekiuka na kuvunja masharti ya katiba ya Jamhuri ya Muungano na seria ya maadili ya viongozi. Aliwataja baadhi ya mafisadi kwa kutumia ushahidi aliotaka kuutoa Bungeni alipowasilisha hoja binafsi.
Alidai viongozi hao walihusika katika mambo mbalimbali yaliyochangia kuwatia umaskini Watanzania kutokana na fedha za wananchi kutumiwa vibaya na viongozi hao.
"Ushahidi wa viongozi wote hao ambao nimewataja katika orodha ya mafisadi ambao wanaihujumu nchi ninao na nipo tayari kwenda kokote kutoa ushahidi huo kama utahitajika kwani ninao wa kutosha na wala kambi ya upinzani hatuogopi kitu katika vita hiyo ya kupambana na mafisadi wa nchi yetu", alisema Dkt. Slaa.
Bw. Mrema akihutubia wananchi hao alisema umefika wakati kwa Watanzania kuwaunga mkono wapinzani 2010 CCM isirudi madarakani upinzani uongoze nchi. "Wananchi nawaomba mbadilike. Hakuna sababu ya kuendelea kuing'ang'ania CCM wakati inashindwa kutimiza ahadi zake kwa wananchi. Nawaomba wananchi mtupigie kura upinzani ili tuongoze nchi na kuleta maendeleo kw wananchi wote", alisema.
Mwenyekiti wa CHADEMA Bw. Freeman Mbowe alisema kambi ya upinzani itaendelea kushughulikia maovu yote yanayofanywa na viongozi na kamwe hawarudi nyuma kwa kuwa mapambano yameanza na yataendelea hadi kieleweke. Alisema yeye yupo kutetea maslahi ya wananchi na ataendelea kuwa mstari wa mbele kukemea maovu na yupo tayari kukamatwa na Polisi kwani yote yale ambayo anawaeleza wananchi ana uhakika nayo.
"Nimepata taarifa Polisi wanachunguza kauli zangu na Bw. Zitto Kabwe ambazo tunazitoa kwa wananchi eti kwa madai kwamba kunachochea kuvunjika kwa amani lakini tunasema Tanzania haina amani na ndio maana wananchi wamechoka na kusikiliza maneno ya Serikali", alisema.
Baadaye alizungumza kwa simu, Bw Mbowe alisema wana ushahidi na tuhuma zote zilizotolewa na Dkt Slaa kuhusu mafisadi wa nchi hii.
Source: Majira, Sunday 16th Sept 2007
Ama kweli, kuongoza chama kama disco ni hatari...sasa hivi wanatumia "muziki" unaopendwa kwenye masikio ya wengi kuleta chuki? Labda kuna wenye mawazo zaidi...lawakilisha kwenu.
CHADEMA YADAIWA KUTAKA TANZANIA INYIMWE MISAADA
Serikali yafuatilia,
Dk. Slaa alipua mabomu
Na Mwandishi WetuDk. Slaa alipua mabomu
CHAMA cha upinzani cha CHADEMA kinadaiwa kuwa kimeanzisha kampeni ya siri na ya chini chini kuyashauri mataifa ya Magharibi kusitisha misaada yake kwa Tanzania. Habari zinadai CHADEMA kupitia Mwenyekiti wake, Bw Freeman Mbowe, kimeanzisha kampeni kuzishawishi nchi zinazotoa misaada kwa wingi Tanzania, kusitisha misaada.
Habari hizo zinadai katika hatua ya kwanza ya kampeni hiyo, Bw Mbowe tayari amezungumza na maofisa wa balozi mbili Dar-es-salaam akiziomba kusitisha misaada hiyo.
Hoja yake ni kuwa misaada inayotolewa Tanzania inatumika vibaya, bila kuwafikia walengwa, Watanzania wa kawaida.
Habari hizo hata hivyo zinathibitisha kuwa hata hizo nchi mbili ambazo Bw. Mbowe amezungumza nazo, zimekataa mpaka sasa kumpa msimamo kamili kama kweli zinaona zinao ulazima wa kusimamisha misaada kwa Tanzania.
Kwa mujibu wa habari hizo kampeni hiyo ya Bw. Mbowe na CHADEMA inalenga kuzuia Tanzania kupata fedha ambazo zingesaidia kuimarisha sekta ya kijamii ya maeneo muhimu sana kwa wananchi ya elimu, maji, kilimo, afya, miundombinu.
Serikali mbili za CCM, katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, zimeelekeza nguvu zao katika maeneo hayo matano muhimu ambayo yanagusa moja kwa moja maisha ya wananchi wote.
Katika bajeti ya mwaka huu, zimeweka kiasi cha asilimia 52 katika maeneo hayo matano tu kwa sababu ya umuhimu wake kwa wananchi, na sehemu kubwa ya fedha hizo itatokana na misaada kutoka nchi za Magharibi.
Mkakati wa CHADEMA ni kwamba kama itafanikiwa kusitisha misaada kwa Tanzania, basi itakuwa haiwezekani tena kwa CCM kutekeleza Ilani yake hiyo na hivyo chama hicho kufanikiwa kujenga chuki kati ya wananchi na serikali yao.
Bajeti ya Serikali kwa mwaka huu wa fedha ambao umeanza miezi miwili iliyopita, inategemea misaada ya wafadhili kwa asilimia 39, ambayo ni kubwa kiasi cha kuathiri mno maisha ya Watanzania kama fedha hizo zinasitishwa na wafadhili.
Habari zinadai mkakati huo wa CHADEMA...baadhi ya wachunguzi wa masuala ya kisiasa waliozungumza na gazeti hili wanaulezea kama tahayari ya kiwango cha chini kabisa.
"Hizi siyo tu mbinu za vyama kuharibiana kisiasa, bali ni kuwatesa moja kwa moja wananchi", alisema mhadhiri mmoja mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam.
Wachunguzi pia wanasema huo ni mkakati ambao hauwezi kufanikiwa kwa sababu nchi za Magharibi haziwezi kukubali kuvuruga uhusiano wake na Tanzania kumfurahisha mtu au kutimiza ajenda na matakwa ya kisiasa ya CHADEMA.
Kama historia inavyoonyesha kusimamisha misada kwa Tanzania ni mkakati ambao unafanikiwa tu kuwaumiza zaidi Watanzania wa kawaida kuliko hao viongozi ambao CHADEMA inadai wanatumia vibaya misaada hiyo.
Uzoefu wa Tanzania wakati wa utawala wa Rais Ali Hassani Mwinyi, unadhibitisha kusimamishwa kwa misaada ni sera itakayowaumiza zaidi wananchi CHADEMA inayodai kuwatetea.
Wakati huo, nchi kadhaa za Magharibi zilisimamisha misaada kwa visingizio mbali mbali, hatua ambayo iliwaumiza sana wananchi wa kawaida wa Tanzania na kuvuruga sera za misaada za nchi za Magharibi.
Usitishaji wa misaada, hata hivyo, ni moja tu ya mikakati mipya ya CHADEMA inayolenga kuharibiana kisiasa baada ya chama hicho kukiri sera na mikakati yake imeshindwa kufanya kazi kwa kupunguza nguvu na kasi ya CCM.
Mkakati mwingine wa CHADEMA ni kujaribu kuwapaka matope watu wote ambao wanaonekana ama kudaiwa kuwa karibu na Rais Jakaya Kikwete, kama njia ya kujaribu kumlazimisha Rais kujitenga na watu hao.
Habari kuhusu mkakati huo zinadai CHADEMA kwa kushirikiana na baadhi ya watu wakiwamo wafanyabiashara wanaoficha sana msimamo wao wa kisiasa, sasa itawalenga na kuwapaka tope baadhi ya watu hao wanaodaiwa kuwa karibu na Rais Kikwete.
Miongoni mwa watu hao ambao wanalengwa na kampeni za sasa za CHADEMA ni pamoja na Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa; Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi na Mweka Hazina wa Taifa wa CCM, Bw. Rostam Aziz.
Habari hizo zinadai orodha hiyo ni ndefu zaidi kuliko viongozi viongozi hao watatu, ambao karibuni wamekuwa wakilengwa sana na kampeni za CHADEMA pamoja na washirika wake.
Shabaha ya mkakati huo wa CHADEMA ni kujaribu kumgombanisha Rais na watu ambao kw miaka mingi wamekuwa na msimamo wa kamoja kisiasa.
Viongozi hao watatu walipoulizwa kuhusu mkakati huo wa CHADEMA walikataa kusema lolote na walionyesha kutohangaishwa na jitihada hizo mpya za CHADEMA.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mwandishi wa Habari wa Waziri Mkuu, Bw. Said Nguba alisema wamepata taarifa za hatua hiyo ya CHADEMA na vyombo vya dola vinafuatilia.
Hata hivyo, alisema wao kama watekelezaji wakuu wa sera za chamba tawala, CCM hawasumbuliwi na propaganda hzio bali wataendelea kutekeleza kwa vitendo mambo ya msingi ya kuondoa kero za wananchi kwani uwezo huo Serikali inao.
Alipoulizwa jana kwa simu alikanusha kwenda ofisi za ubalozi kwa ajili ya hiyo akidai kukatiwa misada sio ajenda ya CHADEMA lakini akasema hana uhakika kama watendaji wengine walienda "kwani huenda huko kwa mambo yao"
Naye Said Mwishehe anaripoti kuwa, Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Slaa ametaja majina ya orodha ya kundi la viongozi, maofisa wa umma na mawakala anaodai ni miongoni mwa watu ambao wanaihujumu nchi kutokana na kula fedha za umma na kutoa maamuzi yanayolisababishia taifa madeni.
Katika orodha ya mafisadi aliowataja Dkt. Slaa jana katika mkutano wake na wananchi wa Temeke Mwembe Yanga, Dar-es-salaam wakiwemo wenyeviti na viongozi wa kambi ya upinzani alisema orodha yake ina mafisadi 11 ambapo kabla ya kutaja hadharani alitoa vigezo vya kisheria alivyotumia kuwabainisha mafisadi hao kwa wananchi.
"Katika kundi la orodha ya mafisadi wamo viongozi wa umma ambao kwa kutumia nyadhifa na vyeo vya katika utumishi wa umma wamefanya maamuzi ambayo taifa limepoteza mapato, utajiri na rasilimali zake na kuneemesha raia au taasisi za kigeni.
Kwa mfano wapo viongozi ambao wameshiriki kusaini mikataba mibovu katika sekta za madini pamoja na maeneo mengine", alisema Dkt. Slaa katika mkutano huo aliohutubia yeye, mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu, Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustine Mrema. Viongozi hao walitua hapo kwa helikopta.
Pia alisema viongozi ambao wamo katika orodha hiyo wamekiuka na kuvunja masharti ya katiba ya Jamhuri ya Muungano na seria ya maadili ya viongozi. Aliwataja baadhi ya mafisadi kwa kutumia ushahidi aliotaka kuutoa Bungeni alipowasilisha hoja binafsi.
Alidai viongozi hao walihusika katika mambo mbalimbali yaliyochangia kuwatia umaskini Watanzania kutokana na fedha za wananchi kutumiwa vibaya na viongozi hao.
"Ushahidi wa viongozi wote hao ambao nimewataja katika orodha ya mafisadi ambao wanaihujumu nchi ninao na nipo tayari kwenda kokote kutoa ushahidi huo kama utahitajika kwani ninao wa kutosha na wala kambi ya upinzani hatuogopi kitu katika vita hiyo ya kupambana na mafisadi wa nchi yetu", alisema Dkt. Slaa.
Bw. Mrema akihutubia wananchi hao alisema umefika wakati kwa Watanzania kuwaunga mkono wapinzani 2010 CCM isirudi madarakani upinzani uongoze nchi. "Wananchi nawaomba mbadilike. Hakuna sababu ya kuendelea kuing'ang'ania CCM wakati inashindwa kutimiza ahadi zake kwa wananchi. Nawaomba wananchi mtupigie kura upinzani ili tuongoze nchi na kuleta maendeleo kw wananchi wote", alisema.
Mwenyekiti wa CHADEMA Bw. Freeman Mbowe alisema kambi ya upinzani itaendelea kushughulikia maovu yote yanayofanywa na viongozi na kamwe hawarudi nyuma kwa kuwa mapambano yameanza na yataendelea hadi kieleweke. Alisema yeye yupo kutetea maslahi ya wananchi na ataendelea kuwa mstari wa mbele kukemea maovu na yupo tayari kukamatwa na Polisi kwani yote yale ambayo anawaeleza wananchi ana uhakika nayo.
"Nimepata taarifa Polisi wanachunguza kauli zangu na Bw. Zitto Kabwe ambazo tunazitoa kwa wananchi eti kwa madai kwamba kunachochea kuvunjika kwa amani lakini tunasema Tanzania haina amani na ndio maana wananchi wamechoka na kusikiliza maneno ya Serikali", alisema.
Baadaye alizungumza kwa simu, Bw Mbowe alisema wana ushahidi na tuhuma zote zilizotolewa na Dkt Slaa kuhusu mafisadi wa nchi hii.
Source: Majira, Sunday 16th Sept 2007