jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,322
tumeshuhudia wataalam wawili wa sheria hapa nchini wakitoa ufafanuzi juu ya njia bora ya kuandika katiba, kwa kuwa wametoa ufafanuzi kila mmoja kwa wakati tofauti huku umma wa watanzania ukionekana kuukubali ufafanuzi wa kisheri wa prof. Issa Shivji, na kutia shaka utetezi wa serikali kupitia AG werema ambaye badala ya kujenga hoja, anajitahidi kujenga hofu kwa wananchi kanakwamba wanapotoshwa! vyombo vya habari tukutanishieni hawa watu wachambue na wakipenda walumbane ili sisi wananchi tubaini anaetuzuga. naomba kuwasilisha