AY 5225
JF-Expert Member
- Jul 16, 2023
- 484
- 1,135
Heshima yenu wakuu.
Niko Zanzibar kwa siku kadhaa sasa na nimekuja kwaajili ya kutafuta ridhiki. Naomba tips/muongozo kwa yeyote anayejua wapi naweza kupata kazi/kibarua na itapendeza zaidi malipo yakiwa ni kwa siku maana sina makazi.
Lengo langu ni kuwa na kazi mbili; moja ya kuifanya asubuhi mpaka jioni na nyingine iwe ya usiku mpaka asubuhi (ikiwa ya ulinzi itafaa pia maana nina cheti cha mafunzo ya JKT).
• Taaluma yangu ni degree ya management of social development.
• I have an excellent command of English na Kiswahili.
• Sina tatizo lolote la kiafya ninalolijua.
• Jinsia yangu ni (ME) na umri ni miaka 24.
Nina kitambulisho cha taifa na nimekuja na barua ya utambulisho wa makazi kutoka kwa mtendaji back home. Siombi mtu anisaidie makazi wala chakula, ninachoomba ni maelekezo ya wapi naweza kupata nafasi za kazi/vibarua kwa mchanganuo niliyotoa hapo nyuma na niko tayari kurudisha fadhila (pesa kidogo ya asante) kwa atakaenisaidia kufanikisha suala hili.
Nimejitambulisha kwa sheha na bag langu nimeomba anitunzie kwa muda nikiwa natafuta mahali pa kujishikiza. Kwa sasa napatikana maeneo ya Airport karibu na Golden Tulip hapa.
Naombeni muongozo wakuu.
Niko Zanzibar kwa siku kadhaa sasa na nimekuja kwaajili ya kutafuta ridhiki. Naomba tips/muongozo kwa yeyote anayejua wapi naweza kupata kazi/kibarua na itapendeza zaidi malipo yakiwa ni kwa siku maana sina makazi.
Lengo langu ni kuwa na kazi mbili; moja ya kuifanya asubuhi mpaka jioni na nyingine iwe ya usiku mpaka asubuhi (ikiwa ya ulinzi itafaa pia maana nina cheti cha mafunzo ya JKT).
• Taaluma yangu ni degree ya management of social development.
• I have an excellent command of English na Kiswahili.
• Sina tatizo lolote la kiafya ninalolijua.
• Jinsia yangu ni (ME) na umri ni miaka 24.
Nina kitambulisho cha taifa na nimekuja na barua ya utambulisho wa makazi kutoka kwa mtendaji back home. Siombi mtu anisaidie makazi wala chakula, ninachoomba ni maelekezo ya wapi naweza kupata nafasi za kazi/vibarua kwa mchanganuo niliyotoa hapo nyuma na niko tayari kurudisha fadhila (pesa kidogo ya asante) kwa atakaenisaidia kufanikisha suala hili.
Nimejitambulisha kwa sheha na bag langu nimeomba anitunzie kwa muda nikiwa natafuta mahali pa kujishikiza. Kwa sasa napatikana maeneo ya Airport karibu na Golden Tulip hapa.
Naombeni muongozo wakuu.