Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,753
- 699,418
Ni red alert Kwa wadangaji wote waliofanikiwa kupora waume za watu wenye familia na ndoa za muda mrefu waliotengana, kuachana ama kutalikiana na wake zao halali za ndoa
Kabla sijaendelea niombe radhi kwa kutumia neno wadangaji naomba nisitafsiriwe vibaya na kuonekana siwaheshimu akina dada wapambanaji walioumizwa, kuchoshwa na kusalitiwa na wapenzi wao.. Akina dada ambao wako serious na maisha wenye kuhitaji mapenzi ya kweli na utulivu ili kuweza kufikia ndoto zao. Wale ambao wamegundua watu wazima wameshakomaa kiakili sasa wanaweza kutulia japo sio wote
Kitu kimoja kibaya ni kwamba hao watu wazima karibia wote ni watu wenye familia hata kama ndoa zao ziliingia mushkeli na kutengana, kuachana ama kutalikiana kisheria na wake zao.. Wana mali na vitega uchumi vinavyotokana na hiyo familia
Mapenzi ni hisia za ndani kati ya wawili na kuna wakati inafika kwasababu zozote zile hisia zikafikia ukomo na wanandoa kuachana.. Lakini mapenzi kwa watoto wao huwa hayafi.. Yatabaki milele
Wanaume na ujinga wao wote na udhaifu wao wote linapokuja suala la watoto huwezi kuwaambia kitu.. Chochote kilichopatikana wakati wao kitabaki kuwa chao kwa siri ama kwa uwazi..
Mapenzi na mahusiano ni kitu kinachochosha mno kwenye ndoa hasa zinapokuja kujitokeza tabia halisi za mwenza wako mkiwa tayari mmeshaishi muda mrefu tu na kufanya mengi pamoja ikiwemo kupata watoto na mali mbalimbali
Ukiachana na sababu nyinginezo kutokuwa mwaminifu kwenye ndoa (usaliti) ndio sababu kubwa inayovunja ndoa nyingi.. Mmoja anapokuwa anagawa hisia zake nje ya ndoa yake na mwenza wake kujua lakini akashindwa kuvumilia.. Kuvunjika hiyo ndoa ni haraka sana
Sasa binti mwenye matamanio makubwa na ndoa na ambaye amekwisha kuchezewa na kuumizwa sana, anakutana na mbaba mwenye ndoa iliyojaa changamoto anayehitaji faraja na kupendwa tena.. Hii couple huitwa perfect match
Hapo hakuna mwanafunzi bali kuna wahitimu tofauti ni madaraja tuu.. Mmoja ni mhitimu wa ndoa, sasa ana uzoefu wa kutosha anajua afanye nini lini, wapi na katika mazingira gani.. Mwingine ni mhitimu wa kupenda na kuumizwa anayehitaji kutulia sasa.. Ni fundi sasa anyezijua vema ABC za mapenzi(sio ndoa)
Hawa wanabebana kwenye hiki kipindi cha mpito na fungate la mahaba.. Kila mmoja anamuona mwenzake amepata mtu sahihi hatimaye.. Ni furaha ni vicheko ni mipango ya maisha biashara na kazi.. Maisha hatimaye yametulia na majeraha yamepona ni kufuta makovu sasa
Yakishapita yote haya ukweli wa asili unaanza kujidhihiri, kila mmoja anakumbuka alikotoka alikopitia na alipo
Baba licha ya kuachana na mama lakini ana watoto.. Mama anaweza kupata mume mwingine na kubadili kabisa ubin lakini sio watoto.. Hawa watabaki kuwa wake milele.. Fikra za kujipanga huanzia hapa!
Bidada naye anaanza kukumbuka alikopotia, alikoumizwa muda aliopoteza kugawa hisia kisha akatoswa! Sasa amejifunza hataki ujinga tena.. Anataka uhakika wa huba.. Anataka ndoa.. Huanza kwa pressure ya taratibu lakini baadae hukaza kamba!
Ukweli wa kutisha unajitokeza, baba hakuwahi kutoa talaka kwa sababu zozote zile ama hataki ndoa ya pili.. Kuna kitu huwa kimewafunga rohoni.. Kuanza mchakato wa talaka ni kitu kigumu chenye gharama maumivu na kuchukua muda na linaweza kufunua mengi.. Hayuko tayari.. Lakini afanyeje sasa?
Hapa ndio linajitokeza swala la kughushi nyaraka.. Mwali mpya bila kujua.. Kwakuwa anafosi sana analetewa nyaraka bandia za talaka, analetewa washenga bandia na hatimaye anafunga ndoa bandia
Zamani mabinti hawakupenda sana ndoa bali walipenda sana magari! Wengi walipigwa sana kwenye hili.. Walipewa magari yenye nyaraka bandia.. Na walipozingua ndio walikuja kujua kwamba kumbe walikua hawajui
Siku hizi wamejifunza ukimpa gari anataka na nyaraka halisi kwa majina yake kamili.. Tena wanafuatilia mpaka TRA wenyewe
Upigaji mpya uko kwenye ndoa feki na nyaraka bandia za ndoa! Tangu juzi masjala za mahakama, vizazi na vifo na kwenye ofisi za nyumba za ibada wageni ni wengi wakifuatilia uhalisia ama uhakiki wa vyeti vya ndoa na hati za talaka!
Mji mzito huu...! Wanawake na maendeleo.. Wakiwezeshwa wanaweza!
Sent using Jamii Forums mobile app
Kabla sijaendelea niombe radhi kwa kutumia neno wadangaji naomba nisitafsiriwe vibaya na kuonekana siwaheshimu akina dada wapambanaji walioumizwa, kuchoshwa na kusalitiwa na wapenzi wao.. Akina dada ambao wako serious na maisha wenye kuhitaji mapenzi ya kweli na utulivu ili kuweza kufikia ndoto zao. Wale ambao wamegundua watu wazima wameshakomaa kiakili sasa wanaweza kutulia japo sio wote
Kitu kimoja kibaya ni kwamba hao watu wazima karibia wote ni watu wenye familia hata kama ndoa zao ziliingia mushkeli na kutengana, kuachana ama kutalikiana kisheria na wake zao.. Wana mali na vitega uchumi vinavyotokana na hiyo familia
Mapenzi ni hisia za ndani kati ya wawili na kuna wakati inafika kwasababu zozote zile hisia zikafikia ukomo na wanandoa kuachana.. Lakini mapenzi kwa watoto wao huwa hayafi.. Yatabaki milele
Wanaume na ujinga wao wote na udhaifu wao wote linapokuja suala la watoto huwezi kuwaambia kitu.. Chochote kilichopatikana wakati wao kitabaki kuwa chao kwa siri ama kwa uwazi..
Mapenzi na mahusiano ni kitu kinachochosha mno kwenye ndoa hasa zinapokuja kujitokeza tabia halisi za mwenza wako mkiwa tayari mmeshaishi muda mrefu tu na kufanya mengi pamoja ikiwemo kupata watoto na mali mbalimbali
Ukiachana na sababu nyinginezo kutokuwa mwaminifu kwenye ndoa (usaliti) ndio sababu kubwa inayovunja ndoa nyingi.. Mmoja anapokuwa anagawa hisia zake nje ya ndoa yake na mwenza wake kujua lakini akashindwa kuvumilia.. Kuvunjika hiyo ndoa ni haraka sana
Sasa binti mwenye matamanio makubwa na ndoa na ambaye amekwisha kuchezewa na kuumizwa sana, anakutana na mbaba mwenye ndoa iliyojaa changamoto anayehitaji faraja na kupendwa tena.. Hii couple huitwa perfect match
Hapo hakuna mwanafunzi bali kuna wahitimu tofauti ni madaraja tuu.. Mmoja ni mhitimu wa ndoa, sasa ana uzoefu wa kutosha anajua afanye nini lini, wapi na katika mazingira gani.. Mwingine ni mhitimu wa kupenda na kuumizwa anayehitaji kutulia sasa.. Ni fundi sasa anyezijua vema ABC za mapenzi(sio ndoa)
Hawa wanabebana kwenye hiki kipindi cha mpito na fungate la mahaba.. Kila mmoja anamuona mwenzake amepata mtu sahihi hatimaye.. Ni furaha ni vicheko ni mipango ya maisha biashara na kazi.. Maisha hatimaye yametulia na majeraha yamepona ni kufuta makovu sasa
Yakishapita yote haya ukweli wa asili unaanza kujidhihiri, kila mmoja anakumbuka alikotoka alikopitia na alipo
Baba licha ya kuachana na mama lakini ana watoto.. Mama anaweza kupata mume mwingine na kubadili kabisa ubin lakini sio watoto.. Hawa watabaki kuwa wake milele.. Fikra za kujipanga huanzia hapa!
Bidada naye anaanza kukumbuka alikopotia, alikoumizwa muda aliopoteza kugawa hisia kisha akatoswa! Sasa amejifunza hataki ujinga tena.. Anataka uhakika wa huba.. Anataka ndoa.. Huanza kwa pressure ya taratibu lakini baadae hukaza kamba!
Ukweli wa kutisha unajitokeza, baba hakuwahi kutoa talaka kwa sababu zozote zile ama hataki ndoa ya pili.. Kuna kitu huwa kimewafunga rohoni.. Kuanza mchakato wa talaka ni kitu kigumu chenye gharama maumivu na kuchukua muda na linaweza kufunua mengi.. Hayuko tayari.. Lakini afanyeje sasa?
Hapa ndio linajitokeza swala la kughushi nyaraka.. Mwali mpya bila kujua.. Kwakuwa anafosi sana analetewa nyaraka bandia za talaka, analetewa washenga bandia na hatimaye anafunga ndoa bandia
Zamani mabinti hawakupenda sana ndoa bali walipenda sana magari! Wengi walipigwa sana kwenye hili.. Walipewa magari yenye nyaraka bandia.. Na walipozingua ndio walikuja kujua kwamba kumbe walikua hawajui
Siku hizi wamejifunza ukimpa gari anataka na nyaraka halisi kwa majina yake kamili.. Tena wanafuatilia mpaka TRA wenyewe
Upigaji mpya uko kwenye ndoa feki na nyaraka bandia za ndoa! Tangu juzi masjala za mahakama, vizazi na vifo na kwenye ofisi za nyumba za ibada wageni ni wengi wakifuatilia uhalisia ama uhakiki wa vyeti vya ndoa na hati za talaka!
Mji mzito huu...! Wanawake na maendeleo.. Wakiwezeshwa wanaweza!
Sent using Jamii Forums mobile app