Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Baada ya kutoka Kolomije na kufika Dar es salaam Makonda alifikia Lumumba kwa utambulisho wa uCCM. Alilala katika moja ya ofisi za chama hicho siku kadhaa kabla ya Mzee Samwel Sitta kumchukua nyumbani kwake kama rafiki na Msaidizi wake.
Ni Sitta alifanikisha Makonda awe Katibu wa Chipukizi na Hamasa akisaidiwa na Jokate aka kidoti. Ni katika kipindi hicho Jaji Joseph Sinde Warioba akimaliza kukusanya maoni ya Watanzania kuhusu Katiba Mpya.
Jaji Warioba alikabidhi ripoti hiyo Ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete kwa mbwembwe zote. Hata hivyo ripoti hiyo haikumpendeza kabisa JK baada ya kuonekana asilimia 75 walitaka mfumo wa Serikali tatu na Warioba alilisisitiza kila alilopata nafasi ya kuzungumza iwe ni kwenye tv, redio, magazeti na midahalo. Katika korido za Ikulu JK alisikika akisema kwa ghadhabu, "huyu Mzee ni mchawi, Serikali tatu ilikuwa kwenye hadidu za rejea?" Alikasirika sana.
Hukumu ya hasira yake iliyoratibiwa na wavaa mawani ilikuwa ni kumdhalilisha Warioba hadharani Kwa gharama zote. Hapa ndipo yule kachero wa operesheni aliyefia ajalini Bagamoyo alipojipa kandarasi ya kumdhalilisha Jaji Warioba ili mfalme aliyenuna afurahi. Ni hapa ndipo alipoulizwa Makonda kama anaweza kufanya kazi hiyo? Naye akasema, "Naam". Kwa kazi hii Makonda aliahidiwa kupewa 10m lakini alipewa 7m tu.
Kazi Gani? Naam, Makonda alipewa jukumu la kumtia dole Mzee Warioba na wengine wa UVCCM hao hao kuhakikisha wanapiga picha vizuri akifanyiwa udhalilishaji huo mbele ya wajukuu zake. Lakini Mungu ni Mwema Makonda aliishia kumvuta Mzee Warioba bila mafanikio. Ni jambo analijutia Hadi Leo Kwa nini hakumdhalilisha Warioba kama Mpango kazi ulivyosukwa. Huu ni ujasiri usio kifani. Kwa mfuatiliaji nenda Ubungo Blue Pearl ukaulize ni nani alilipia ukumbi wa mkutano kwa ajili ya mdahalo ule wa Katiba? Wale vijana wa UVCCM walitokea wapi ghafla na mabango? Utapata jawabu la hiki nilichoamua leo kuweka wazi.
Next time nitawaambia ujasiri wa Makonda ulivyowagharimu Charles Kitwanga na Charles Mwijage. Jumapili njema na maombolezo mema ya mpendwa wetu Edward Lowassa.
Ni Sitta alifanikisha Makonda awe Katibu wa Chipukizi na Hamasa akisaidiwa na Jokate aka kidoti. Ni katika kipindi hicho Jaji Joseph Sinde Warioba akimaliza kukusanya maoni ya Watanzania kuhusu Katiba Mpya.
Jaji Warioba alikabidhi ripoti hiyo Ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete kwa mbwembwe zote. Hata hivyo ripoti hiyo haikumpendeza kabisa JK baada ya kuonekana asilimia 75 walitaka mfumo wa Serikali tatu na Warioba alilisisitiza kila alilopata nafasi ya kuzungumza iwe ni kwenye tv, redio, magazeti na midahalo. Katika korido za Ikulu JK alisikika akisema kwa ghadhabu, "huyu Mzee ni mchawi, Serikali tatu ilikuwa kwenye hadidu za rejea?" Alikasirika sana.
Hukumu ya hasira yake iliyoratibiwa na wavaa mawani ilikuwa ni kumdhalilisha Warioba hadharani Kwa gharama zote. Hapa ndipo yule kachero wa operesheni aliyefia ajalini Bagamoyo alipojipa kandarasi ya kumdhalilisha Jaji Warioba ili mfalme aliyenuna afurahi. Ni hapa ndipo alipoulizwa Makonda kama anaweza kufanya kazi hiyo? Naye akasema, "Naam". Kwa kazi hii Makonda aliahidiwa kupewa 10m lakini alipewa 7m tu.
Kazi Gani? Naam, Makonda alipewa jukumu la kumtia dole Mzee Warioba na wengine wa UVCCM hao hao kuhakikisha wanapiga picha vizuri akifanyiwa udhalilishaji huo mbele ya wajukuu zake. Lakini Mungu ni Mwema Makonda aliishia kumvuta Mzee Warioba bila mafanikio. Ni jambo analijutia Hadi Leo Kwa nini hakumdhalilisha Warioba kama Mpango kazi ulivyosukwa. Huu ni ujasiri usio kifani. Kwa mfuatiliaji nenda Ubungo Blue Pearl ukaulize ni nani alilipia ukumbi wa mkutano kwa ajili ya mdahalo ule wa Katiba? Wale vijana wa UVCCM walitokea wapi ghafla na mabango? Utapata jawabu la hiki nilichoamua leo kuweka wazi.
Next time nitawaambia ujasiri wa Makonda ulivyowagharimu Charles Kitwanga na Charles Mwijage. Jumapili njema na maombolezo mema ya mpendwa wetu Edward Lowassa.