Waziri wa Mambo ya Ndani: Jeshi la Polisi litalinda Demokrasia wakati wa Uchaguzi Mkuu 2024 na 2025

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,884
12,134
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema katika uchaguzi ujao ukiwemo wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu Jeshi la Polisi litalinda Demokrasia ili kuhakikisha unakuwa uchaguzi wa Huru na Haki huku Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Camillus Wambura akisema wako tayari kuhakikisha uchaguzi unapita salama.
 
Huu ni uchaguzi wa Raia sio jeshi la polisi ,polisi unakaa ndani ya chumba cha uchaguzi ili kufanya nini???
 
Demokrasia haihitaji polisi kabisa, ni watu wapige kura kwa uhuru, na zihesabiwe kwa uwazi na Uhuru, matokeo ya kweli na halali yatangazwe. Ulinzi wa nini? Ulinzi ndio wizi!
 
Kifo cha Aquilina mlipiga danadana ndio mjali uchaguzi?
Tangu lini wameacha kutopokea maagizo toka juu.
 
Katiba ya nchi iliyopo pamoja na Sheria za nchi zilizopo zina-promote uimla (dictatorship).

Kazi Kuu kabisa ya Jeshi la Polisi ni Kusimamia Sheria pamoja na kulinda Katiba ya nchi.

Je, Jeshi la Polisi linatarajia kulinda demokrasia gani wakati Katiba na Sheria zilizopo hazitambui uwepo wa hicho kitu kinachoitwa demokrasia?? Je, ni demokrasia gani basi ambayo Jeshi la Polisi linaahidi kwamba watailinda??
 
Back
Top Bottom