Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 231
- 558
Manispaa ya Morogoro (Morogoro mjini) ni mji wa zamani kidogo hivyo hata baadhi ya miundombinu iliyowekwa zamani imeshachoka ikiwemo miundombinu ya maji hasa hasa hizi meter (dira za kusoma matumizi ya maji)
Meter nyingi ni chakavu kiasi kwamba kuona unit za matumizi ni vigumu sana jambo linalopelekea hisia ya ukadiriaji wa unit kuwa kubwa
Pili mbali na ukadiriaji wa matumizi ni kwamba kawaidi uchakavu au uzèe wa kitu hupunguza ufanisi wa meter hizo
Pamoja na uchakavu na uzee wa meter hizo ikitokea ikaharibika wao moja kwa moja wanadai fidia ambayo ni Tsh.100,000/= kwa dhana kwamba watumiaji ndio walioharibu
Pamoja na uonevu huo kituko ni kwamba hata baada ya kulipa fidia haufungiwi meter mpya badala yake wanakuletea iliyokwishatumika ambayo imeng'olewa kwa mtu mwingine kwasababu mbalimbali
Sasa hapa unajiuliza, hizi faini ambazo almost ni sawa na gharama ya meter mpya zinaenda wapi? Na kwanini tulipe fidia kwa kitu kilichoharibika sababu ya kutumika kwa muda mrefu? Meter nyingi zilifungwa miaka ya mwishoni mwa 1990's
Je, gharama tunazolipa kila mwezi moja ya kazi yake si pamoja na kufanya matengenezo ikiwemo kuondoa miundombinu iliyochoka? Kwao hili hawana
Haya yote wanafanya kwasababu wanajua hakuna mbadala wa shirika lingine la maji
Nadhani mamlaka za maji wangepewa watu binafsi ufanisi ungeongezeka. Serikali wabaki kuwa moderators kwasababu wafanyakazi wengi wa mamlaka hizi ambazo ni monopoly hawajali wateja na kwa MORUWASA imekithiri
Bill za maji ziko juu kwasababu meter nyingi ni mbovu hivyo wasoma meter wanakadiria tu
Kitengo cha huduma kwa wateja kipo kwa ajili ya ku print bill tu badala ya kusaidia wateja wao wenye shida mbalimbali na wanafanya hivyo kwasababu wanajua kinachofanyika
Meter nyingi ni chakavu kiasi kwamba kuona unit za matumizi ni vigumu sana jambo linalopelekea hisia ya ukadiriaji wa unit kuwa kubwa
Pili mbali na ukadiriaji wa matumizi ni kwamba kawaidi uchakavu au uzèe wa kitu hupunguza ufanisi wa meter hizo
Pamoja na uchakavu na uzee wa meter hizo ikitokea ikaharibika wao moja kwa moja wanadai fidia ambayo ni Tsh.100,000/= kwa dhana kwamba watumiaji ndio walioharibu
Pamoja na uonevu huo kituko ni kwamba hata baada ya kulipa fidia haufungiwi meter mpya badala yake wanakuletea iliyokwishatumika ambayo imeng'olewa kwa mtu mwingine kwasababu mbalimbali
Sasa hapa unajiuliza, hizi faini ambazo almost ni sawa na gharama ya meter mpya zinaenda wapi? Na kwanini tulipe fidia kwa kitu kilichoharibika sababu ya kutumika kwa muda mrefu? Meter nyingi zilifungwa miaka ya mwishoni mwa 1990's
Je, gharama tunazolipa kila mwezi moja ya kazi yake si pamoja na kufanya matengenezo ikiwemo kuondoa miundombinu iliyochoka? Kwao hili hawana
Haya yote wanafanya kwasababu wanajua hakuna mbadala wa shirika lingine la maji
Nadhani mamlaka za maji wangepewa watu binafsi ufanisi ungeongezeka. Serikali wabaki kuwa moderators kwasababu wafanyakazi wengi wa mamlaka hizi ambazo ni monopoly hawajali wateja na kwa MORUWASA imekithiri
Bill za maji ziko juu kwasababu meter nyingi ni mbovu hivyo wasoma meter wanakadiria tu
Kitengo cha huduma kwa wateja kipo kwa ajili ya ku print bill tu badala ya kusaidia wateja wao wenye shida mbalimbali na wanafanya hivyo kwasababu wanajua kinachofanyika