Waziri wa Kazi, vipi kuhusu ukaguzi wa vyeti vya elimu katika kampuni binafsi?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
Ndugu zangu katika JamiiForums, bila shaka wote mu wazima wa afya,

Kwa kuzingatia ukweli kuwa sekta binafsi hapa Tanzania ndio imeajiri wafanyakazi wengi kuliko hata taasisi za serikali, hivyo kwa namna yoyote ile utendaji kazi wao una athiri (negatively or positively) kwa kiasi kubwa sana uchumi na ustawi wa taifa letu tukufu.

Baada ya Waziri wa Kazi kuamuru kufanyika kwa zoezi la ukaguzi wa vyeti kwa watumisi wote wa mashirika ya umma, atakuwa na mpango gani kwa watumishi wa sekta/makampuni binafsi walioajiriwa kwa ujanja ujanja na baadhi kwa kutoa rushwa za ngono ama kutumia vyeti visivyo halali?

Ninafahamu fika ya kuwa Waziri wa Kazi (serikali) has limited scope juu ya namna ya uendeshwaji wa mashirika na kampuni binafsi, lakini wafanyakazi wenye uwezo mdogo waliopo na kujaa huko katika kampuni binafsi wanaumiza uchumi wa nchi yetu kupitia utoaji wa huduma mbovu na zisizokidhi viwango.

Watanzania kamwe hawataweza kushindana na watu kutoka nchi zingine katika Jumuiya ya Afrika mashariki kama tatizo la ubabaishaji katika utoaji wa huduma katika sekta binafsi halitadhibitiwa mapema.

Note: Hapa tunazungumzia watu wanaotumia vyeti vya watu wengine ama bandia kupata kazi, pamoja na watu kupata kazi ambazo hawana sifa wala taaluma husika, jambo linalopelekea utoaji wa huduma mbovu zinazoathiri uchumi na ustawi wa taifa letu.
 
ndugu zangu katika jamiiforums, bila shaka wote mu wazima wa afya,

baada ya waziri wa kazi kuamuru kufanyika kwa zoezi la ukaguzi wa vyeti kwa watumisi wote wa mashirika ya umma, atakuwa na mpango gani kwa watumishi wa sekta/makampuni binafsi walioajiriwa kwa ujanja ujanja na baadhi kwa kutoa rushwa za ngono ama kutumia vyei visivyo halali. ninafahamu fika ya kuwa waziri wa kazi (serikali) has limited scope juu ya namna ya uendeshwaji wa mashirika na kampuni binafsi, lakini wafanyakazi ****** waliopo na kujaa huko katika kampuni binafsi wanaumiza uchumi wa nchi yetu kupitia utoaji wa huduma mbovu na zisizokidhi viwango. naomba kuwasilisha.
ushasema kampuni binafsi,
 
ushasema kampuni binafsi,
kaka, sawa ni kampuni binafsi lakini zinaathari sana kwa uchumi na ustawi wa taifa endapo hazitafuatiliwa kwa ukaribu sana. kumbuka huko kuna makanjanja wengi sana wamejaa believe me mkuu
 
ndugu zangu katika jamiiforums, bila shaka wote mu wazima wa afya,

baada ya waziri wa kazi kuamuru kufanyika kwa zoezi la ukaguzi wa vyeti kwa watumisi wote wa mashirika ya umma, atakuwa na mpango gani kwa watumishi wa sekta/makampuni binafsi walioajiriwa kwa ujanja ujanja na baadhi kwa kutoa rushwa za ngono ama kutumia vyei visivyo halali. ninafahamu fika ya kuwa waziri wa kazi (serikali) has limited scope juu ya namna ya uendeshwaji wa mashirika na kampuni binafsi, lakini wafanyakazi ****** waliopo na kujaa huko katika kampuni binafsi wanaumiza uchumi wa nchi yetu kupitia utoaji wa huduma mbovu na zisizokidhi viwango. naomba kuwasilisha.
Labda kampuni yako kampuni zinazowaza kutengeneza faida awafanyi makosa kwenye kuselect staff wao hata kidogo.
 
Labda kampuni yako kampuni zinazowaza kutengeneza faida awafanyi makosa kwenye kuselect staff wao hata kidogo.
mkuu, mimi nimepita huko na ninajua fika madudu yanayofanyika chini ya kapeti huko aisee, kuna watu makanjanja wa kutisha huko kaka
 
Hii style mnayoenda nayo mwisho mtataka sasa hadi wafanyabiashara nao wakaguliwe vyeti, mwisho mtasemaa hata wamiliki wa mitandao e.g. Jf wawe na vyeti vya IT, mtataka hata wasanii lazima wawe wamesomea sanaa na wana vyeti n.k .... Kagueni huko huko kwenye sekta zenu za umma
kaka umepigika ikulu nini? soon they will be there, it's just a matter of time and patience, just wait and see
 
Hii style mnayoenda nayo mwisho mtataka sasa hadi wafanyabiashara nao wakaguliwe vyeti, mwisho mtasemaa hata wamiliki wa mitandao e.g. Jf wawe na vyeti vya IT, mtataka hata wasanii lazima wawe wamesomea sanaa na wana vyeti n.k .... Kagueni huko huko kwenye sekta zenu za umma
Unaogopa nini katuni? Kwani kuna sehemu uhalifu unaruhusiwa? Au unataka ifikie sehemu wananchi wasione umuhimu wa kusoma?
 
mchane mkuu maana haelewi maana ya secta binafs huku wanaangalia uzoefu hawaangalii vyeti mkuu
nitakuwa nimewapiga ikulu na sio bure, kwa awamu hii ya JPM inayozingatia ubora kwa sekta zote zinazogusa uchumi wa nchi ni lazima waje mpaka huko
 
Hiyo sekta binafsi inayoajiri makanjanja haijitakii mema, na naamini hakuna sekta binafsi iliyopo kiushindani wa biashara ikaamua kuajiri makanjanja wakati wanajua uwepo wake unategemea na uzalishaji wa kiwango bora ili kuhimili ushindani. Mfano shule za binafsi unatarajia kuwakuta walimu mizigo huko na wale wa yes no?
 
kaka, sawa ni kampuni binafsi lakini zinaathari sana kwa uchumi na ustawi wa taifa endapo hazitafuatiliwa kwa ukaribu sana. kumbuka huko kuna makanjanja wengi sana wamejaa believe me mkuu

Sio kila kitu kina maana. Kampuni binafsi zina malengo yake. Kama wakiona hawafikii ni jukumu lao. Serikali inachukua kodi huko. Wawapangie wafanyajazi binafsi jinsi ya kuajiri?
 
mchane mkuu maana haelewi maana ya secta binafs huku wanaangalia uzoefu hawaangalii vyeti mkuu
Watanzania kwa kujitoa fahamu hatujambo. SEKTA BINAFSI, puh...acheni unafiki na wehu wa kujifanyisha. Kipindi fulani hapa nyuma, Waziri wa Kazi alitoa agizo kuwa Makampuni ya Kimataifa (binafsi hayo) yasiajiri mfanyakazi kutoka nje ikiwa anaweza kupatikana hapa mwenye elimu hiyo. Hapo hakuna aliyesema ni sekta binafsi kwa hiyo waachiwe wafanye wanavyojisikia, ila mkisikia jambo linalobana upande wetu ndio mnajua sekta binafsi.

Wahuni wasakwe hadi makanisani. Kama Padre alifoji cheti na aondolewe, nafasi yake apewe shekhe
 
Back
Top Bottom