Waziri simbachawene ulichokiona ilala na temeke kuhusu tanesco ndiyo hali ilivyo nchi nzima

kuch-kuch

Member
Jan 14, 2014
40
17
Habari wana JF,
Leo kumesikika habari kwamba waziri wa nishati na madini mh. Simbachawene ametoa agizo la kuchukuliwa hatua kali kwa wakuu wa idara ya ufundi wa Ilala na Temeke DSM. Mheshimiwa waziri, hali uliyokumbana nayo huko ndivyo ilivyo kwa nchi nzima. Kuhusu kitengo cha dharura nadhani TANESCO hawaelewi maana ya neno 'emergency' ukitaka kuamini hili wewe mwenyewe mh. jaribu kuchukua simu yako uwapigie uone kama utajibiwa. Unapiga simu ya 'emergency' mara tano bila kupokelewa! Hata kama watapokea ukiwajulisha tatizo wanachukua wiki nzima kufika (si kushughulikia tatizo leneyewe). Baada ya hapo hesabu wiki nyingine kulishughulikia. Yaani TANESCO inakera kupita kiasi. Wafanyakazi wake wamegeuka Miungu watu ukiingia ofisini kwao hawana hata muda wa kukusikiliza. Ni mengi sana tunayashuhudia sisi wananchi wa kawaida.
 
Tanesco wezi na hawajali malalamiko ya wateja luku za vijijini wanalipisha wateja gharama za Tariff4. ingawa wanaona kabisa hao wateja wanatumia Unit 20 kwa mwezi. tumeandika barua, tumetuma email, tumepiga simu na kwenda kimwili mkoani, wilayani na makao makuu hawabadilishi. Sasa tunatamani tukuone Waziri labda utabadilisha tariff zetu. TANESCO wameshindwa
 
Habari wana JF,
Leo kumesikika habari kwamba waziri wa nishati na madini mh. Simbachawene ametoa agizo la kuchukuliwa hatua kali kwa wakuu wa idara ya ufundi wa Ilala na Temeke DSM. Mheshimiwa waziri, hali uliyokumbana nayo huko ndivyo ilivyo kwa nchi nzima. Kuhusu kitengo cha dharura nadhani TANESCO hawaelewi maana ya neno 'emergency' ukitaka kuamini hili wewe mwenyewe mh. jaribu kuchukua simu yako uwapigie uone kama utajibiwa. Unapiga simu ya 'emergency' mara tano bila kupokelewa! Hata kama watapokea ukiwajulisha tatizo wanachukua wiki nzima kufika (si kushughulikia tatizo leneyewe). Baada ya hapo hesabu wiki nyingine kulishughulikia. Yaani TANESCO inakera kupita kiasi. Wafanyakazi wake wamegeuka Miungu watu ukiingia ofisini kwao hawana hata muda wa kukusikiliza. Ni mengi sana tunayashuhudia sisi wananchi wa kawaida.

Kabla hamjawalaumu hao jamaa hebu jiulizeni kwanza. Rais Kikwete na viongozi wote wa nchi hii wanajua maana ya ''dharura''? Kwasababu naona tunataka ku-deal na dalili za ugonjwa badala ya ku-deal na ugonjwa.
 
Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Watoto hujifunza kutoka kwa Wazazina ndugu waliokaribu yao.
Lawama kwa wazazi ambayo ni Serikali.
 
Kabla hamjawalaumu hao jamaa hebu jiulizeni kwanza. Rais Kikwete na viongozi wote wa nchi hii wanajua maana ya ''dharura''? Kwasababu naona tunataka ku-deal na dalili za ugonjwa badala ya ku-deal na ugonjwa.

Mkuu naona unavyojitetea mwenyewe
 
Si tanesco peke yake. Kila idara ya wizara yoyote katika nchi hii imeoza. Kwa kifupi tu ni kwamba serikali iliyoko madarakani imechoka na ni wajibu wetu kuifundisha adabu oktoba 2015. Huu ni mwaka wetu tuutumie na tumshukuru mungu!
 
Mkuu naona unavyojitetea mwenyewe

Hata kama ningekuwa mhusika lakini hapa sio mahali pa kujitetea. Mimi naelezea hali halisi kwani viongozi wakuu hawawezi kuwa wezi na wazembe halafu utegemee wa chini yao wawe wachapakazi na waadilifu!
 
Kabla hamjawalaumu hao jamaa hebu jiulizeni kwanza. Rais Kikwete na viongozi wote wa nchi hii wanajua maana ya ''dharura''? Kwasababu naona tunataka ku-deal na dalili za ugonjwa badala ya ku-deal na ugonjwa.

Inaonekana hauko sawa yani unataka kikwete aje kutatuwa tatizo la dharura
 
Kabla hamjawalaumu hao jamaa hebu jiulizeni kwanza. Rais Kikwete na viongozi wote wa nchi hii wanajua maana ya ''dharura''? Kwasababu naona tunataka ku-deal na dalili za ugonjwa badala ya ku-deal na ugonjwa.

Sasa hapo sijui Rais kaingiaje?
 
Tatizo @ mfanyakazi mpya unaemuona hawa vijana ke/me wana ndugu zao ndani ya tanesco kama co ktk kituo hichohicho basi makao makuu au mkoa mwingine wa ki tanesco hivyo hakuwezi kukawa na ufanisi sababu hawawezi kuwajibisha watoto,wajomba,wajukuu nk zao
 
Habari wana JF,
Leo kumesikika habari kwamba waziri wa nishati na madini mh. Simbachawene ametoa agizo la kuchukuliwa hatua kali kwa wakuu wa idara ya ufundi wa Ilala na Temeke DSM. Mheshimiwa waziri, hali uliyokumbana nayo huko ndivyo ilivyo kwa nchi nzima. Kuhusu kitengo cha dharura nadhani TANESCO hawaelewi maana ya neno 'emergency' ukitaka kuamini hili wewe mwenyewe mh. jaribu kuchukua simu yako uwapigie uone kama utajibiwa. Unapiga simu ya 'emergency' mara tano bila kupokelewa! Hata kama watapokea ukiwajulisha tatizo wanachukua wiki nzima kufika (si kushughulikia tatizo leneyewe). Baada ya hapo hesabu wiki nyingine kulishughulikia. Yaani TANESCO inakera kupita kiasi. Wafanyakazi wake wamegeuka Miungu watu ukiingia ofisini kwao hawana hata muda wa kukusikiliza. Ni mengi sana tunayashuhudia sisi wananchi wa kawaida.

Jawabu ni kuvunja ukiritimba WA Tanesco, Tanesco ivunjwe vipande vitatu, Generation, Distribution na Supply, makampuni matatu yanayojitegemea Kisha tualike wawekezaji binafsi kushiriki katika biashara hiyo hiyo, bila Tanesco kushindanishwa; Wzr Chawene atapata ugonjwa wa moyo buree kijana wa watu, Hilo shirika kama taasisi zetu nyingine za umma zilivyo; Polisi, TRA, TAKUKURU, Mahakama, Halmashauri zetu, Wizara zote, ni sheeeeda! Limeoza.
 
mhe:Simbachawene njoo na mbeya sisi tumelipia service line miezi 3 nyuma lakini kuna watu wakilipia hats Leo wanaunganishiwa umeme sababu rushwa imekithiri vinginevyo tunakuomba mrudishe Bandie aliikomesha hii tabia mbeya.
 
Pole hon. S/Chawene. Kuanzia mfagizi hadi mkurugenzi wa tanesco ni ndugu wa damu. Sijawahi kuona kampuni hovyo kama tanesco. Ukipiga number za dharura hazipokelewi.
 
Jawabu ni kuvunja ukiritimba WA Tanesco, Tanesco ivunjwe vipande vitatu, Generation, Distribution na Supply, makampuni matatu yanayojitegemea Kisha tualike wawekezaji binafsi kushiriki katika biashara hiyo hiyo, bila Tanesco kushindanishwa; Wzr Chawene atapata ugonjwa wa moyo buree kijana wa watu, Hilo shirika kama taasisi zetu nyingine za umma zilivyo; Polisi, TRA, TAKUKURU, Mahakama, Halmashauri zetu, Wizara zote, ni sheeeeda! Limeoza.

Kamata like. Eg TTCL zamani kupata line ni issue faili lako litageuzwa geuzwa miaka 3. Hata tanesco ibinafishwe management ya tanesco ibaki kama regulatory authority uone kama umeme haujasambaa mpaka hapa kwetu ruangwa vijijini
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Back
Top Bottom