EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Kumbe matapeli walishamshtukia huyu waziri long time, na kuanza kutumia jina lake kutapeli?
NOTE: Suala la matapeli kutumia jina lake kutapeli lilitokea kabla ya kulikoroga kule Afrika ya Kusini.
Ziara za kushtukiza zinazofanywa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bw. Philipo Mulugo, hivi karibuni zimeanza kumtokea puani baada ya watu wasiofahamika kutumia jina lake kujipatia fedha kwa njia ya utapeli.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam mwanzoni mwa mwezi huu, Bw. Mulugo alisema matapeli wameanza kutumia jina lake vibaya tangu aanze ziara za kushtukiza katika taasisi mbalimbali za elimu nchini. Alisema tabia ya watu kutumia jina lake kutapeli ilianza taratibu, lakini hivi sasa imezidi kushika kasi ambapo tapeli mmoja alimpigia simu Mhasibu wa Mamlaka ya Elimu nchini (TEA) na kumweleza Bw. Mulugo amemtuma sh. milioni 1.5.
"Ndugu zangu waandishi, naomba mnisaidie katika hili, kuna namba imepiga leo (jana), kwa Mhasibu wa TEA, kutaka sh. milioni 1.5 akitumia jina langu, tukio la aina hii pia limetokea katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaa?m na mikoani," alisema na kuongeza kuwa chanzo cha tatizo hilo ni ziara zake za kushtukiza.
Alisema wengine wamekuwa wakipiga simu na kuomba kiasi cha fedha wakidai Bw. Mulugo anataka kukitumia kwa ajili ya mafuta ya gari lake ili aweze kufanya kazi za Serikali kwa ufanisi. "Mimi nikitaka kufanya ziara huwa simfahamishi mtu labda bosi wangu Waziri (Dkt. Shukuru Kawambwa), nawaonya Wakurugenzi, Maofisa Elimu wa mikoa, Wilaya na wadau wa elimu waache kutumia jina langu vibaya kwani wakibainika sheria itachukua mkondo wake," alisema Bw. Mulugo. Alitoa mfano kama Mhasibu wa TEA asingepita ofisi kwake kujiridhisha kama kweli anahitaji fedha hizo, fedha hizo zingeangukia mikononi mwa matapeli.
Majira.
NOTE: Suala la matapeli kutumia jina lake kutapeli lilitokea kabla ya kulikoroga kule Afrika ya Kusini.
Ziara za kushtukiza zinazofanywa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bw. Philipo Mulugo, hivi karibuni zimeanza kumtokea puani baada ya watu wasiofahamika kutumia jina lake kujipatia fedha kwa njia ya utapeli.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam mwanzoni mwa mwezi huu, Bw. Mulugo alisema matapeli wameanza kutumia jina lake vibaya tangu aanze ziara za kushtukiza katika taasisi mbalimbali za elimu nchini. Alisema tabia ya watu kutumia jina lake kutapeli ilianza taratibu, lakini hivi sasa imezidi kushika kasi ambapo tapeli mmoja alimpigia simu Mhasibu wa Mamlaka ya Elimu nchini (TEA) na kumweleza Bw. Mulugo amemtuma sh. milioni 1.5.
"Ndugu zangu waandishi, naomba mnisaidie katika hili, kuna namba imepiga leo (jana), kwa Mhasibu wa TEA, kutaka sh. milioni 1.5 akitumia jina langu, tukio la aina hii pia limetokea katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaa?m na mikoani," alisema na kuongeza kuwa chanzo cha tatizo hilo ni ziara zake za kushtukiza.
Alisema wengine wamekuwa wakipiga simu na kuomba kiasi cha fedha wakidai Bw. Mulugo anataka kukitumia kwa ajili ya mafuta ya gari lake ili aweze kufanya kazi za Serikali kwa ufanisi. "Mimi nikitaka kufanya ziara huwa simfahamishi mtu labda bosi wangu Waziri (Dkt. Shukuru Kawambwa), nawaonya Wakurugenzi, Maofisa Elimu wa mikoa, Wilaya na wadau wa elimu waache kutumia jina langu vibaya kwani wakibainika sheria itachukua mkondo wake," alisema Bw. Mulugo. Alitoa mfano kama Mhasibu wa TEA asingepita ofisi kwake kujiridhisha kama kweli anahitaji fedha hizo, fedha hizo zingeangukia mikononi mwa matapeli.
Majira.