Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
Dakika chache zilizopita wajumbe wa bunge la katiba wametoka ukumbini kupewa maelekezo juu ya upigaji kura za rasimu ya katiba. Wameambiwa yafuatayo:
1. Waziri mkuu Pinda kesho saa tatu asubuhi atawahutubia wabunge kabla ya rasimu iliyorekebishwa kuwasilishwa tena. Agenda anayo mfukoni lakini inadaiwa agenda kuu ni mahakama ya kadhi ambapo Chenge amegoma kuiweka katika rasimu. Pinda atatumia hotuba yakr kuwapoza waislamu na kuwasihi wasigomee kupiga kura pamoja na kwamba mahakama ya kadhi haimo katika katiba.
2. Upigaji kura utaanza saa tisa jioni kesho na kumalizika keshokutwa jumanne. Kila mtu atatajwa na kupigia kura sura kumi kesho na zile zinazobaki zitapigiwa kura jnne.
3. Jumatano ni siku ya kufanya maridhiano kwa ibara zote zitakazokosa theluthi mbili. Maridhiano yatafanyika kwa waliopinga kupewa nafasi kutoa hoja zao na kamati ya uandishi na uongozi kutoa ufafanuzi na kisha kura kupigwa tena. Zitapigwa mara tatu na kama theluthi mbili ikikosekana itahesabika kuwa ibara hiyo imekataliwa.
4. Hii ni mengineyo: upo ugumu wa kupata theluthi mbili toka zanzibar kutokana na mgawanyiko mkubwa uliopo. Hotiba ya PM huenda ikasaidia ku-address hili pia. Kuhusu mahakama ya kadhi hali ni tete zaidi ya kawaida. Ndio sababu PM amepewa muda kesho asubuhi kujaribu kuweka ushawishi wa mwisho.
5: Kuna taarifa kuwa hatimae swala la migomo ya wafanyakazi limeingizwa katika katiba baada ya wafanyakazi nao kupanga kususa kupigia kura rasimu nzima kesho.
Nikipata mapya toka hapa dodoma usiku huu nitawawekeeni hapahapa. Kuna vikao kadhaa vya kuweka misimamo vinaendelea usiku huu sehemu kadhaa.
1. Waziri mkuu Pinda kesho saa tatu asubuhi atawahutubia wabunge kabla ya rasimu iliyorekebishwa kuwasilishwa tena. Agenda anayo mfukoni lakini inadaiwa agenda kuu ni mahakama ya kadhi ambapo Chenge amegoma kuiweka katika rasimu. Pinda atatumia hotuba yakr kuwapoza waislamu na kuwasihi wasigomee kupiga kura pamoja na kwamba mahakama ya kadhi haimo katika katiba.
2. Upigaji kura utaanza saa tisa jioni kesho na kumalizika keshokutwa jumanne. Kila mtu atatajwa na kupigia kura sura kumi kesho na zile zinazobaki zitapigiwa kura jnne.
3. Jumatano ni siku ya kufanya maridhiano kwa ibara zote zitakazokosa theluthi mbili. Maridhiano yatafanyika kwa waliopinga kupewa nafasi kutoa hoja zao na kamati ya uandishi na uongozi kutoa ufafanuzi na kisha kura kupigwa tena. Zitapigwa mara tatu na kama theluthi mbili ikikosekana itahesabika kuwa ibara hiyo imekataliwa.
4. Hii ni mengineyo: upo ugumu wa kupata theluthi mbili toka zanzibar kutokana na mgawanyiko mkubwa uliopo. Hotiba ya PM huenda ikasaidia ku-address hili pia. Kuhusu mahakama ya kadhi hali ni tete zaidi ya kawaida. Ndio sababu PM amepewa muda kesho asubuhi kujaribu kuweka ushawishi wa mwisho.
5: Kuna taarifa kuwa hatimae swala la migomo ya wafanyakazi limeingizwa katika katiba baada ya wafanyakazi nao kupanga kususa kupigia kura rasimu nzima kesho.
Nikipata mapya toka hapa dodoma usiku huu nitawawekeeni hapahapa. Kuna vikao kadhaa vya kuweka misimamo vinaendelea usiku huu sehemu kadhaa.