Wewe jamaa inaonekana kijijini kwenu hakuna maendeleo... Nenda Moshi na Kagera ujionee maendeleo ya vijijini...Vijijini Kuna centers...Muhimu kuwa na taa... Kwani taa kitu gani??View attachment 2117287
Ni dhahili serikali hii haijui mahitaji ya wananchi na haina vipaumbele. WM amewaagiza Tarura waweke taa mpaka vijijini. Hivi ni kweli sisi watu wa vijijini tunahitaji taa za barabarani? Hii ni kejeli kubwa sana.
Sisi vijijini tunahitaji madawa na vifaa tiba, tunahitaji maji na umeme wa uhakika. Tunahitaji pembejeo za bei nafuu, Tunataka mabwawa tulime kwa kumwagilia. Tunataka maghala na masoko ya mazao. Leo tunaambiwa tuletewe taa za barabarani.