Wana JF jana usiku katika kipindi cha DAKIKA 45 kinachorushwa na ITV ambacho mgeni alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; S. Nahodha alipoulizwa juu ya kiini cha vurugu za Nyamongo alitoa sababu zifuatazo:-
Hivyo kwa mujibu wa mahojiano ya jana usiku, Waziri hakugusia sehemu yeyote kuwa CDM ilitia MKONO katika vurugu hizo.
- Kuwepo kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ambapo wengine wanafaidika na kuwepo kwa mgodi na wengine hawaifidiki. Wasiofadika na shughuli za uchimbaji madini wanashawishi vijana kuvamia mgodi kwa nia ya kuiba dhahabu.
- Kuwepo kwa uwingi wa vijana wasio na ajira wanaozunguka mgodi. Wengi wa vijana wanaona shughuli za mgodi haziwapi kipato cha ina yoyote hivyo wana mtazamo hasi dhidi ya wawekezaji pamoja na shughuli zao.
- Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi.
Hivyo kwa mujibu wa mahojiano ya jana usiku, Waziri hakugusia sehemu yeyote kuwa CDM ilitia MKONO katika vurugu hizo.