Waziri ataja sababu 3 za vurugu za Nyamongo

Lilombe

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
242
39
Wana JF jana usiku katika kipindi cha DAKIKA 45 kinachorushwa na ITV ambacho mgeni alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; S. Nahodha alipoulizwa juu ya kiini cha vurugu za Nyamongo alitoa sababu zifuatazo:-

  1. Kuwepo kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ambapo wengine wanafaidika na kuwepo kwa mgodi na wengine hawaifidiki. Wasiofadika na shughuli za uchimbaji madini wanashawishi vijana kuvamia mgodi kwa nia ya kuiba dhahabu.
  2. Kuwepo kwa uwingi wa vijana wasio na ajira wanaozunguka mgodi. Wengi wa vijana wanaona shughuli za mgodi haziwapi kipato cha ina yoyote hivyo wana mtazamo hasi dhidi ya wawekezaji pamoja na shughuli zao.
  3. Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi.
Pia amesema amewasiliana na Waziri Ngereja kwa nia ya kuhakikisha wawekezaji wa sekta ya madini wanatimiza masharti ya uwekezaji.
Hivyo kwa mujibu wa mahojiano ya jana usiku, Waziri hakugusia sehemu yeyote kuwa CDM ilitia MKONO katika vurugu hizo.
 
Wana JF jana usiku katika kipindi cha DAKIKA 45 kinachorushwa na ITV ambacho mgeni alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; S. Nahodha alipoulizwa juu ya kiini cha vurugu za Nyamongo alitoa sababu zifuatazo:-

  1. Kuwepo kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ambapo wengine wanafaidika na kuwepo kwa mgodi na wengine hawaifidiki. Wasiofadika na shughuli za uchimbaji madini wanashawishi vijana kuvamia mgodi kwa nia ya kuiba dhahabu.
  2. Kuwepo kwa uwingi wa vijana wasio na ajira wanaozunguka mgodi. Wengi wa vijana wanaona shughuli za mgodi haziwapi kipato cha ina yoyote hivyo wana mtazamo hasi dhidi ya wawekezaji pamoja na shughuli zao.
  3. Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi.
Pia amesema amewasiliana na Waziri Ngereja kwa nia ya kuhakikisha wawekezaji wa sekta ya madini wanatimiza masharti ya uwekezaji.
Hivyo kwa mujibu wa mahojiano ya jana usiku, Waziri hakugusia sehemu yeyote kuwa CDM ilitia MKONO katika vurugu hizo.

Ilikuwa ni taarifa ya RPC na naibu wa waziri
 
sasa huyo naibu wake alitoa wapi hayo maneno ya kuhusisha vurugu na chama 'flani' cha siasa,.
 
Amejitaidi kuzungumzia mambo ya muhimu lakini kwa kiasi kikubu hizo vurugu zinasabishwa na serikari kutowajibika kwa wananchi kuhusu wawekezaji kama umesoma kitabu kilichoandikwa na ChaChage kinaitwa "MAKUADI WA SOKO HURIA" utajua uhalisia wa suala linalotokea sehemu kama Nyamongo na sehemu nyingine zenye uwekezaji.
 
Amejitaidi kuzungumzia mambo ya muhimu lakini kwa kiasi kikubu hizo vurugu zinasabishwa na serikari kutowajibika kwa wananchi kuhusu wawekezaji kama umesoma kitabu kilichoandikwa na ChaChage kinaitwa "MAKUADI WA SOKO HURIA" utajua uhalisia wa suala linalotokea sehemu kama Nyamongo na sehemu nyingine zenye uwekezaji.

Na sababu zote alizotoa zinajulikana
Wawekezaji hawana nia ya kumuinua mtu wa chini pale walipo na hawana hata nia ya kutekeleza kile walichoambiw awafanye au kilichomo kweney mkataba la sivyo wasingewakejeli wananchi kwa kuwajengea shule ambazo mbuzi akijikuna kwenye ukuta unaanguka au barabara za kokote eti hiyo ni miundombinu
 
Nimependa hii sababu ya tatu

Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi
 
Nimependa hii sababu ya tatu

Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi

Ndio sababu kuu kwa nini wananchi wamechoka
Sio migodi tuu hadi kweney vitalu vya uwindaji na mbuga za wanyama
Misitu ya serikali
Mashamba makubwa ya wawekezaji
Wanacnhi wamechoka
Angalia wawekezaji kwenye mashamba ya miwa kule babati wanavyochoma mashamba ya wawekezaji baada ya kujikuta hawaoni tofauti yoyote ya kuwepo kw amashamba hayo bora ardhi hiyo wangepewa wao walime mazao ya chakula
 
Kama kweli hawa ni watendaji wa JK basi yeye ni kilaza, wameweza kutoa sababu wakashindwa kutoa solutions, ni viongozi au viongozwa? Hayo mawili ya kwanza hayana majibu tujuzeni.
 
Wana JF jana usiku katika kipindi cha DAKIKA 45 kinachorushwa na ITV ambacho mgeni alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; S. Nahodha alipoulizwa juu ya kiini cha vurugu za Nyamongo alitoa sababu zifuatazo:-

  1. Kuwepo kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ambapo wengine wanafaidika na kuwepo kwa mgodi na wengine hawaifidiki. Wasiofadika na shughuli za uchimbaji madini wanashawishi vijana kuvamia mgodi kwa nia ya kuiba dhahabu.
  2. Kuwepo kwa uwingi wa vijana wasio na ajira wanaozunguka mgodi. Wengi wa vijana wanaona shughuli za mgodi haziwapi kipato cha ina yoyote hivyo wana mtazamo hasi dhidi ya wawekezaji pamoja na shughuli zao.
  3. Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi.
Pia amesema amewasiliana na Waziri Ngereja kwa nia ya kuhakikisha wawekezaji wa sekta ya madini wanatimiza masharti ya uwekezaji.
Hivyo kwa mujibu wa mahojiano ya jana usiku, Waziri hakugusia sehemu yeyote kuwa CDM ilitia MKONO katika vurugu hizo.

Watanzania tumeshajua ukweli; CDM hawachomoki na machafuko ya Nyamongo, KIASHIRIA kiko wazi Viongozi wa CDM walikuwa wanaijua move yote. Walikuwa wa kwanza kukimbilia Nyamongo baada ya tukio.
 
Weee! Kusema "watanzania tumeshaujua ukweli" ni kuwasemea watanzania, ambayo literally ni KUWADHALILISHA kuwa wana akili kama yako. Mbaya sana!

Watanzania tumeshajua ukweli; CDM hawachomoki na machafuko ya Nyamongo, KIASHIRIA kiko wazi Viongozi wa CDM walikuwa wanaijua move yote. Walikuwa wa kwanza kukimbilia Nyamongo baada ya tukio.
 
inakera sana pale wanaposema wawekezaje wanatoa huduma muhimu kama kujenga shule, dispensari
kitu ambacho sio sahihi haviendani na mali wanazochuma
 

Watanzania tumeshajua ukweli; CDM hawachomoki na machafuko ya Nyamongo, KIASHIRIA kiko wazi Viongozi wa CDM walikuwa wanaijua move yote. Walikuwa wa kwanza kukimbilia Nyamongo baada ya tukio.

Watanzania wengi tuna akili timamu hatuna makengeza ya akili kama wewe.Na hata wewe ukweli unaujua ila tu ndiyo ile MTUMIKIE KAFIRI......... Ni njaa tu inakusumbua.
 
inakera sana pale wanaposema wawekezaje wanatoa huduma muhimu kama kujenga shule, dispensari
kitu ambacho sio sahihi haviendani na mali wanazochuma

Ukipiga mahesabu ya hizo shule na dispensary ni kama tone kwenye bahari maana kama ni shule ni just majengo hayana vitabu hayana walimu wa kutosha wala maabara za maana na hospital wanatoa majengo na vitanda may be ila dawa hakuna wala madakrati ni issue sasa hapo sijui ndo wamefanya nini
 
Nimependa hii sababu ya tatu

Wawekezaji kushindwa kutimiza masharti ya uwekezaji juu ya kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka migodi
Huu ni uongo mkuu, mwenye makosa ni serikali yetu, Kwenye mkutano alioufanya juzi Godbless Lema alisema baada ya mauwaji ya nyamongo alienda kwenge migodi hiyo akaomba kuongea na wakubwa...walicho kisema ni kwamba wanaishangaa sana serikali kwani wao waliandaa mpango wa kuwasaidia wananchi wa nyamongo kwa kuwapa mchanga katika mpango huu walihitaji bilion tatu kama sikosei, wakaiomba bank ya dunia ikakubali kuwapa kiasi hicho cha pesa, Barick wakampelekea waziri wa madini "Gereja", cha ajabu haja wajibu chochote mpaka mauji yametokea, wakasema hata wao kibiashara inawaharibia sana kwani biashara yao imeshuka kwa asilimia 7.5 watu hawataki kununua madini yanayo nuka damu...sasa tujiulize viongozi wetu wako kwa maslahi ya nani, je wanafaindiaka na damu ya watanzania ndiyo maana hawataki kutatua matatizo......
 
Ukipiga mahesabu ya hizo shule na dispensary ni kama tone kwenye bahari maana kama ni shule ni just majengo hayana vitabu hayana walimu wa kutosha wala maabara za maana na hospital wanatoa majengo na vitanda may be ila dawa hakuna wala madakrati ni issue sasa hapo sijui ndo wamefanya nini
Mkuu hatuna haja ya kuwalamu wawekezaji tuwalau viongozi wetu...yaani ni kama kumfumania mkeo na jamaa halafu unaanza kumlau jamaa ni ujinga wewe ulie na mkataba nae ni mkeo...hivyo na ni sisi tunatakiwa tuwakomalie hawa viongozi wetu na kwa kuwa wameshindwa kutekeleza/wametusaliti tuwaondoe....
 
Mkuu hatuna haja ya kuwalamu wawekezaji tuwalau viongozi wetu...yaani ni kama kumfumania mkeo na jamaa halafu unaanza kumlau jamaa ni ujinga wewe ulie na mkataba nae ni mkeo...hivyo na ni sisi tunatakiwa tuwakomalie hawa viongozi wetu na kwa kuwa wameshindwa kutekeleza/wametusaliti tuwaondoe....


Mkuu maoni yangu hapa yalikuw asio kuwalaume wawekezaji bali ni kuilaumu mikataba ambayo serikali imeingia na wawekezaji husika maana wawekezaji wanatekelez akile ambhacho kimeandika kwenye mkataba
Kama kwenye mkataba wako kumeandikwa utatoa huduma za kijamii kama ujenzi wa shule na dispensary mwekezaji anatekeleza hata kama shule haina madawati hiyo sio kazi yake ila yeye ni kujenga shule
Ubovu unakuja na wa kulaumiwa ni serikali ambayo wakati wanasaini mkataba haikujiuliza ni huduma zipi za kijamii na kwa kiwango gani maana walitakiwa waambiwe ni shule ya aina gani na iwe na nini so wakikabidhi shule huwezi tena kujikuta wanafunzi wa ile shule wanalalamika madawati hakuna au vitabu hakuna au hakuna huduma za maji
 
Mkuu hatuna haja ya kuwalamu wawekezaji tuwalau viongozi wetu...yaani ni kama kumfumania mkeo na jamaa halafu unaanza kumlau jamaa ni ujinga wewe ulie na mkataba nae ni mkeo...hivyo na ni sisi tunatakiwa tuwakomalie hawa viongozi wetu na kwa kuwa wameshindwa kutekeleza/wametusaliti tuwaondoe....

naungana na wewe mkuu
wakuwalaumu ni viongozi wetu wasiosimamia vyema mali asili yetu,wao wanachojali ni 10% yao wakipata hiyo kila kitu kwisha
watawala wa nchi hii wamekuwa wakiwakumbatia sana wawekezaji na kusahahu wananchi,wameweka sheria ambazo zinawanufaisha sana wawekezaji kuliko hata nchi husika,
tunalamba sana miguu ya wawekezaji sasa wanaingia hadi chumbani na hatuna la kusema

Angalia botswana kabla hujaanza project ni lazima utimize kile ambacho serikali imepanga juu ya wananchi wanaozunguka mgodi huo,lakini hapa kwetu imekuwa ni tofauti sana tena sana

tumebaki kuwalaumu wananchi na kuwazingizia kuwa ni wezi na kuwapiga lisasi kama vile ni wakimbizi

yatubidi kubadilika ktk sera na mipango yetu juu ya hii mali asili la sivyo ipo siku sehemu za machimbo zitakuwa hazishikiki
 
Back
Top Bottom