Wazee, watoto na wagonjwa Mkoani Geita na mikoa jirani washauriwa kufuatilia kuagwa kwa Rais Magufuli kupitia Vyombo vya Habari

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,505
9,286
Wazee, Watoto na wagonjwa wa Wilaya ya Chato Mkoa wa Geita na mikoa jirani wameshauriwa kuaga mwili wa hayati Rais John Magufuli kwa kufuatilia kwenye vyombo mbalimbali vya habari vinavyorusha mubashara badala ya kwenda uwanjani.

Uamuzi huo unatokana na eneo la uwanja wa Magufuli ulipo wilayani humo uliotengwa kwa ajili ya shughuli za kuaga kuwa mdogo na hautaweza kuhudumia wananchi wote.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Machi 23, 2021 mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel amesema eneo la uwanja litatumiwa na familia, viongozi wa Serikali, dini na wawakilishi wa wananchi.

Amewataka wananchi wa Mkoa wa Geita hususan wa wilaya ya Geita kujitokeza barabarani Machi 24, 2021 ili waweze kutoa heshima za mwisho, akiwataka kufanya hivyo tena Machi 25.

“Chato hapatoshi ni padogo mno niwaombe wenye changamoto, wazee, watoto na wagonjwa naomba wakae nyumbani yapo maeneo yenye luninga mnaweza kuaga kwa kuangalia mubashara na eneo la maziko litahudhuriwa na watu wachache sana ambao ni familia na viongozi wakuu.

Niwaombe sana Machi 26 ni kwa ajili ya watu wachache mno naomba mkae nyumbani mtazame luninga,” amesema Gabriel.

Chanzo: Mwananchi
 
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel, amepiga 'Stop' wananchi kufika uwanjani kumuaga Hayati,Dk. John Magufuli Machi 25 mwaka huu pamoja na siku ya maziko ambayo ni Ijumaa Machi 26,2021 badala yake wabaki nyumbabi wangalie kupigia Luninga.

My Take
Serikali isione aibu kuahirisha mwili kwenda Mwanza.
 
Ni jambo jema na hata jana pia Mkuu wa Mkoa Mwanza Mongela ameshauri watu kubaki nyumbani na kufuatilia kwenye Tv hasa wazee na wenye watoto wadogo, Tahadhali ni muhimu sana
 
Inakuaje sasa wenyeji kimsingi ndo waliga kura wake tangu 1995 wakose fursa huyo ilihali watu wa dar waage
Yaani wewe inaonekana huu uzi umeusoma zaidi ya mara moja kutafuta kasoro , mwisho ukaibuka na hii
 
Ni jambo jema na hata jana pia Mkuu wa Mkoa Mwanza Mongela ameshauri watu kubaki nyumbani na kufuatilia kwenye Tv hasa wazee na wenye watoto wadogo,, Tahadhali ni muhimu sana
Sasa kama ni hivyo kuna haja gani ya kuzungusha mwili kwa siku 5 wakimtesa Mama JPM na familia yake kwa uchungu walionao wakati watu wanaweza kufuatilia kwenye TV .... Kwa nini wasiende moja kwa noja Chattle .......!!
 
Jamani Eti siku ya mapumziko ya kitaifa ni lini?
kati ya Alhamis na Ijumaa?

Awali kama Zanzibar ya kuingizwa kwenye ratiba ya kuaga ilitangazwa siku ya mazishi kuwa tarehe 25/03/2021 kuwa mapumziko ya Kitaifa.

Sasa kwa kuwa siku ya mazishi imepekwa mbele kuwa tarehe 26/03/2021 Ijumaa baada ya kuingiza Zanzibar kwenye ratiba ya kuaga ,

Je, siku ya mapumziko itabaki ile ile Alhamis au itakuwa Ijumaa?
 
Sasa kama ni hivyo kuna haja gani ya kuzungusha mwili kwa siku 5 wakimtesa Mama JPM na familia yake kwa uchungu walionao wakati watu wanaweza kufuatilia kwenye TV .... Kwa nini wasiende moja kwa noja Chattle .......!!
Imetajwa sababu ni kuwa uwanja husika ni mdogo hautoshi kuhudumia watu wengi, ni kipi huelewi mkuu.
 
Back
Top Bottom