Sr. Magdalena
JF-Expert Member
- Aug 10, 2011
- 803
- 472
Vijana waliokuwa na umri wa miaka chini ya 18 (<18) mwaka 2010 hawakujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa kuwa umri wao ulikuwa chini ya miaka 18 kikatiba na taratibu. Vija hao ambao SASA ni wa miaka 18, 19,20 na hata 21 hawakupiga kura siku ya uchaguzi jana kwa kuwa hawakuwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, kwa kifupi damu changa na inayochemka jana haikupata haki ya kikatiba kuchagua muwakilishi wao bungeni.
Wachenguzi wa maswala ya kisiasa wanadai kazi ya vijana hawa ilikuwa ni kutoa somo la uraia kwa wazazi wao na wazee wao na katika uchaguzi wa jana, wazee na kinamama walikuwa wengi kwenye vituo vya kupigia kura kuliko vijana.
Hii ni dhahiri kuwa wazee sasa wanaweza kubadilika na kuchagua kwa hoja na sera na si kwa mazoea kama hapo nyuma, hii ni hatua kubwa katika democrasia ya nchi yetu.
Kumbe hata wazee wakiwezeshwa na vijana wao, wanaweza, sasa wazee waichagua CDM Arumeru Mashariki je tutarajie nini kwenye chaguzi nyingine au hii ya Arumeru ilikuwa exceptional .?
Wachenguzi wa maswala ya kisiasa wanadai kazi ya vijana hawa ilikuwa ni kutoa somo la uraia kwa wazazi wao na wazee wao na katika uchaguzi wa jana, wazee na kinamama walikuwa wengi kwenye vituo vya kupigia kura kuliko vijana.
Hii ni dhahiri kuwa wazee sasa wanaweza kubadilika na kuchagua kwa hoja na sera na si kwa mazoea kama hapo nyuma, hii ni hatua kubwa katika democrasia ya nchi yetu.
Kumbe hata wazee wakiwezeshwa na vijana wao, wanaweza, sasa wazee waichagua CDM Arumeru Mashariki je tutarajie nini kwenye chaguzi nyingine au hii ya Arumeru ilikuwa exceptional .?