Wazee Mwang'onda na Hassy Kitine waasisi wa TISS imara Tanzania

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Nikiwa ni mmoja wa washiriki kupiga kura, nimebaini kwamba nchi yetu ina majasusi imara kabisa katika ukanda huu wa Afrika.

Kuna mambo ya msingi kabisa kuhusu usalama na mstakabali wa nchi ambayo yanahitaji kuweka itikadi ya vyama pembeni.

Kama mheshimiwa Edward Lowasa "angetoka" katika uchaguzi huu, basi Tanzania ingekuwa katika hali ingine kabisa.

Kama kweli Edward Lowasa ambae hapo mwanzo niliweza kumpinga na baadae kuyumbishwa kidogo na kuhama kwake kwenda Chadema, amesaidiwa kwa hali na mali na baadhi ya watu kutoka nje, kuhakikisha anaingia Ikulu.

Kama kweli UKAWA waliajiri baadhi ya raia wa kigeni kuja Tanzania na kuvuruga matokeo pale kwenye maficho yao kwa kujaribu kurekebisha kuongeza idadi ya kura.

Kuna madai mengi mengi tu yanasemwa kuhusiana na matukio mbalimbali yalotokea nchi ilipokuwa ikielekea kwenye uchaguzi mkuu.

Lakini kazi ya kunusa, kufuatilia, kubaini na hatimae kufanya shambulizi pale ofisi ya ukusanyaji kura, ilikuwa ni kazi maalum na iliopangwa kwa ustadi mkubwa.

Sasa hatua ya kwanza imefanikiwa na ilobakia ni kumalizia kesi.

Ila yote tisa, kumi ni jinsi matunda ya vijana wa wazee Apson Mwango'onda na Hassy Kitine wanavyofanya kazi yao kwa uadilifu mkubwa. Wengi wa maofisa ni matokeo ya kazi ya wazee hawa wawili katika kuuhakikisha tunakuwa na maofisa mahiri kwenye kazi hii ngumu, ingawa mara kwa mara kumekuwepo na vijana wachanga ambao bado hawajamfikia Jason Bourne.

Idaya hii ya usalama au TISS ni idara imara, makini na inazidi kufanya kazi zake ikiwa kwa mwendo wa taratibu lakini makini.

Bila shaka yoyote raisi mteule Dr John Pombe Magufuli atazidi kuimarisha idara hii kwa mtindo mwingine kabisa, nikimaanisha kuwaondoka vijana ambao hawana dhamira ya dhati kufanya kazi hio, wenye kupoteza muda kwenye mabaa na kumbi za starehe na kuchezea magari ya serikali kiasi cha kupoteza fedha za kugharamia mafuta.

Je vipi mchango wako kwa wazee hawa wawili Apson Mwang'onda na Hassy Kitine?
 
Naamini idara imeua kundi la wanamtandao lililokuwa limejiimarisha kwa utaalamu mkubwa ambapo ingekuwa nchi nyingine kingenuka ....bado tuna idara imara sana ...
 
Je, na OR hana alichochangia such kwamba naye hastahili pongezi?

- Kwa pongezi zako hizi, je kuna haja ya kufanya uchaguzi tena kipindi kijacho na kupoteza mabilioni ya shilingi na muda wa wananchi? Maana System ina mtu wake via chama tawala, na inahakikisha anapita, afe kipa afe beki......sasa uchaguzi unafanyika ili kuwafurahisha nchi wahisani AU kuwahadaa wananchi AU ni muda wa kupiga hela?
 
Je, na OR hana alichochangia such kwamba naye hastahili pongezi?

- Kwa pongezi zako hizi, je kuna haja ya kufanya uchaguzi tena kipindi kijacho na kupoteza mabilioni ya shilingi na muda wa wananchi? Maana System ina mtu wake via chama tawala, na inahakikisha anapita, afe kipa afe beki......sasa uchaguzi unafanyika ili kuwafurahisha nchi wahisani AU kuwahadaa wananchi AU ni muda wa kupiga hela?

Upo sawa kabisa lakini OR kaja baada ya hawa wawili, ndio maana TISS ya sasa chini ya OR ni matokeo ya kazi ya wazee hawa.
 
kwangu siwezi kuipongeza kwa sasa kwa kuwa kuna matukio mengi wameshindwa au wameacha yaendelee kwa makusudi

umwagiwaji wa tindikali
mauaji ya viongozi na watu wa kawaida
wizi wa
twiga
escrow
richmond
epa
madawa ya kulevya
pembe za ndovu

kutaja hayo machache

Haya ni matatizo ambayo Polisi (wakiwezeshwa) wanaweza kuyashughukia, ingawa kwa kiasi fulani TISS inaweza kuwa inatoa "tip offs".
 
Haya ni matatizo ambayo Polisi (wakiwezeshwa) wanaweza kuyashughukia, ingawa kwa kiasi fulani TISS inaweza kuwa inatoa "tip offs".

Mkuu kwani tofauti ya TISS na mapolisi wengine ni ipi? Mie nilidhani TISS ni kitengo tu kama walivyo FFU, magereza, traffic ambapo kimsingi ni walewale tu. Nawasilisha nisahihishwe.
 
Upo sawa kabisa lakini OR kaja baada ya hawa wawili, ndio maana TISS ya sasa chini ya OR ni matokeo ya kazi ya wazee hawa.

Ila hii ajenda yako siyo yenye afya sana ikisemwa mbele ya wananchi tukajua kwa dhahiri mbeleko ya tiss kwa ccm maana itazidi kukijengea chuki hichi chombo! Wakati wote, inabidi itenganishwe CCM na hiyo idara masikioni mwa wananchi! BTW, Bila mchunga kondoo ni upuuzi hata kama hao kondoo wameshiba vipi......ndio maana naamini bado OR kama yeye anastahili kujumuishwa kwenye sifa zako!

Kwa kuongezea, mimi naona mission isn't over yet, maana Watanzania sio wamoja tena baada ya huu uchaguzi hivyo inabidi kuwa unganisha haraka!
Kila mahala wakti wa kampeni, Mh Magufuli hakuwa tatizo, ila ni CCM ndio haitakiwi! Lazima waisafishe CCM kwa kuondoa dead woods, na wananchi waone ikitendeka hivyo ili Imani irudi kwa CCM na serikali pengine na kwa hiyo idara pia!

Magazeti ya chama na serikali na vyombo vingine, viache mipasho na kejeli dhidi ya wapinzani, muda wa kampeni umeisha sasa, kumbe inafaa umsifie hata adui yako maana mlichokuwa mkikigombea umeshakipata tayari, hii ni kwa mustakabari wa Taifa letu sote!
 
Ila hii ajenda yako siyo yenye afya sana ikisemwa mbele ya wananchi tukajua kwa dhahiri mbeleko ya tiss kwa ccm maana itazidi kukijengea chuki hichi chombo! Wakati wote, inabidi itenganishwe CCM na hiyo idara masikioni mwa wananchi! BTW, Bila mchunga kondoo ni upuuzi hata kama hao kondoo wameshiba vipi......ndio maana naamini bado OR kama yeye anastahili kujumuishwa kwenye sifa zako!

Kwa kuongezea, mimi naona mission isn't over yet, maana Watanzania sio wamoja tena baada ya huu uchaguzi hivyo inabidi kuwa unganisha haraka!
Kila mahala wakti wa kampeni, Mh Magufuli hakuwa tatizo, ila ni CCM ndio haitakiwi! Lazima waisafishe CCM kwa kuondoa dead woods, na wananchi waone ikitendeka hivyo ili Imani irudi kwa CCM na serikali pengine na kwa hiyo idara pia!

Magazeti ya chama na serikali na vyombo vingine, viache mipasho na kejeli dhidi ya wapinzani, muda wa kampeni umeisha sasa, kumbe inafaa umsifie hata adui yako maana mlichokuwa mkikigombea umeshakipata tayari, hii ni kwa mustakabari wa Taifa letu sote!



Well said, Msese
 
Apson Mwang'ond ndie alikuwa Mkuu wa Usalama wa Taifa na baadae Kampen meneja wa Mamvi hahahah Maji hata uyachemshe vipi hayasahau kurudi kwny asili yake ya ubaridi Mzee Ngoyai alisahau kuwa usalama wa Taifa hawastaafu bali wanastaafu kuamka asubuhi na kwenda ofisini daily
 
Ila hii ajenda yako siyo yenye afya sana ikisemwa mbele ya wananchi tukajua kwa dhahiri mbeleko ya tiss kwa ccm maana itazidi kukijengea chuki hichi chombo! Wakati wote, inabidi itenganishwe CCM na hiyo idara masikioni mwa wananchi! BTW, Bila mchunga kondoo ni upuuzi hata kama hao kondoo wameshiba vipi......ndio maana naamini bado OR kama yeye anastahili kujumuishwa kwenye sifa zako!

Kwa kuongezea, mimi naona mission isn't over yet, maana Watanzania sio wamoja tena baada ya huu uchaguzi hivyo inabidi kuwa unganisha haraka!
Kila mahala wakti wa kampeni, Mh Magufuli hakuwa tatizo, ila ni CCM ndio haitakiwi! Lazima waisafishe CCM kwa kuondoa dead woods, na wananchi waone ikitendeka hivyo ili Imani irudi kwa CCM na serikali pengine na kwa hiyo idara pia!

Magazeti ya chama na serikali na vyombo vingine, viache mipasho na kejeli dhidi ya wapinzani, muda wa kampeni umeisha sasa, kumbe inafaa umsifie hata adui yako maana mlichokuwa mkikigombea umeshakipata tayari, hii ni kwa mustakabari wa Taifa letu sote!
Uchambuzi mzuri
 
Muacheni mzee Apson apumzike sasa....tujenge nchi tuache kulia wakati mamlaka yapo "kwenu" sasa ...tujenge taifa kwa moyo wote ...
 
Huyu Apson Mwang'onda ndiye wa kulaumiwa katika uchaguzi huu. Kitendo chake cha kusideline kwa Lowasa tangu akiwa CCM na hata alipohama kwenda CHADEMA huwezi kumpongeza. Mikakati yote ovu ya upinzani kama kudivert data za tume na kujiandalia matokeo yao ni matokeo ya kazi ya Apson Mwang'onda na timu yake. Hapaswi kupongezwa hata kwa chembe labda Hanssy Kitime
 
kwangu siwezi kuipongeza kwa sasa kwa kuwa kuna matukio mengi wameshindwa au wameacha yaendelee kwa makusudi

umwagiwaji wa tindikali
mauaji ya viongozi na watu wa kawaida
wizi wa
twiga
escrow
richmond
epa
madawa ya kulevya
pembe za ndovu

kutaja hayo machache

Kamanda laiti ungejua majukumu ya hawa watu usingewalaumu kwa hayo uliyoorodhesha. Lakin Mara zote mi naamin watu hawa WaPo kwa ajili ya Taifa na watu wake hivyo hawawezi kuwa sehemu ya kuliangamiza taifa kiuchumi, kisiasa n. k Shukuru Mungu Tanzania tupo hivi t ulivyo kwa sababu ya kitengo hicho kuwa imara. wanatukanwa na wananchi, wanadharauliwa lakini hawakati Tamaa juu ya nchi yao. Hongereni TISS msikate Tamaa katika kuhakikisha nchi yetu inabaki katika amani na utulivu daima.
 
Mnaisifia idara inayoikumbatia CCM huku mambo kadhaa yameikumba nchi na kutikisa uchumi wetu...

Mitandao miovu ya wauza na waleta unga, wauzaji wa meno ya ndovu imekuwa ikiitesa nchi...

Yaani hayo ni machache kati ya mengi...
 
Huyu Apson Mwang'onda ndiye wa kulaumiwa katika uchaguzi huu. Kitendo chake cha kusideline kwa Lowasa tangu akiwa CCM na hata alipohama kwenda CHADEMA huwezi kumpongeza. Mikakati yote ovu ya upinzani kama kudivert data za tume na kujiandalia matokeo yao ni matokeo ya kazi ya Apson Mwang'onda na timu yake. Hapaswi kupongezwa hata kwa chembe labda Hanssy Kitime

kumbe hata kile kituo kinachosimamia haki za binadamu kilikuwa kinajiandalia matokeo yao ati
 
Huyu Apson Mwang'onda ndiye wa kulaumiwa katika uchaguzi huu. Kitendo chake cha kusideline kwa Lowasa tangu akiwa CCM na hata alipohama kwenda CHADEMA huwezi kumpongeza. Mikakati yote ovu ya upinzani kama kudivert data za tume na kujiandalia matokeo yao ni matokeo ya kazi ya Apson Mwang'onda na timu yake. Hapaswi kupongezwa hata kwa chembe labda Hanssy Kitime

...na wale waliopo sasa ambao kwa masikio yangu na mbele yangu waliapa kuirudisha ccm madarakani na walidiriki kuvaa sare za ccm unawazungumziaje...? hii ni sawa...?
 
Kamanda laiti ungejua majukumu ya hawa watu usingewalaumu kwa hayo uliyoorodhesha. Lakin Mara zote mi naamin watu hawa WaPo kwa ajili ya Taifa na watu wake hivyo hawawezi kuwa sehemu ya kuliangamiza taifa kiuchumi, kisiasa n. k Shukuru Mungu Tanzania tupo hivi t ulivyo kwa sababu ya kitengo hicho kuwa imara. wanatukanwa na wananchi, wanadharauliwa lakini hawakati Tamaa juu ya nchi yao. Hongereni TISS msikate Tamaa katika kuhakikisha nchi yetu inabaki katika amani na utulivu daima.

Hawajalaumiwa kuhusika, ila wamelaumiwa kufumbiwa macho pale mkosaji anapokuwa amefungamana na serikali au CCM au labda kwa kuwa na uwezo mdogo wa kufanya kazi. Maana haiwezekani hadi leo hakuna hatua iliyopigwa katika kupambana na visababishi vya hayo yaliyotajwa.
 
Ila hii ajenda yako siyo yenye afya sana ikisemwa mbele ya wananchi tukajua kwa dhahiri mbeleko ya tiss kwa ccm maana itazidi kukijengea chuki hichi chombo! Wakati wote, inabidi itenganishwe CCM na hiyo idara masikioni mwa wananchi! BTW, Bila mchunga kondoo ni upuuzi hata kama hao kondoo wameshiba vipi......ndio maana naamini bado OR kama yeye anastahili kujumuishwa kwenye sifa zako!

Kwa kuongezea, mimi naona mission isn't over yet, maana Watanzania sio wamoja tena baada ya huu uchaguzi hivyo inabidi kuwa unganisha haraka!
Kila mahala wakti wa kampeni, Mh Magufuli hakuwa tatizo, ila ni CCM ndio haitakiwi! Lazima waisafishe CCM kwa kuondoa dead woods, na wananchi waone ikitendeka hivyo ili Imani irudi kwa CCM na serikali pengine na kwa hiyo idara pia!

Magazeti ya chama na serikali na vyombo vingine, viache mipasho na kejeli dhidi ya wapinzani, muda wa kampeni umeisha sasa, kumbe inafaa umsifie hata adui yako maana mlichokuwa mkikigombea umeshakipata tayari, hii ni kwa mustakabari wa Taifa letu sote!

Umenena vyema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom