Wazamiaji wa Ukara, Ukerewe wapewe zawadi ya ajira Serikalini

Nelson Masaduki

JF-Expert Member
Oct 27, 2017
346
380
Wanabodi,
Poleni kwa msiba wa MV Nyerere.

Nimetafakari sana kazi iliyofanywa na wenzetu, wazamiaji waliopo katika eneo la Ukara, kabla ya serikali kuanza kuifanya kazi ya kuokoa na kutoa miili ya waliofariji katika ajali ya MV Nyerere. Ninadhani, ingekuwa busara sana endapo serikali ingepata majina na taarifa za watu wote walioshiriki kazi ya kuzamia majini na kuwapa ajira serikalini. Ajira zao zisaidie katika maeneo waliyopo. Katika maeneo yote yenye maziwa, mito na bahari, waanzishe
"Rapid Rescue Team" ambayo itajumuisha watalaam wa asili na watumishi wa taasisi nyingine serikalini.

Ni wazo tu, wanaweza kulifanyia kazi
Nelson
 
Hata mm huwa nawazaga hivo, wangewapatia hata kifuta jasho cha laki 3 kwa kila mtu. Yaani wasiosoma wanafanya kazi kubwa sana kuliko waliosoma hasa katika maswala ya kijamii ya kawaida hahaha!.Wavaa tai wanazingua sana, ujuaji mwingi. Wangewafikiria hasa mkuu wa mkoa angewatambua hao watu na kuwaita ofisini kwake awatie moyo
 
Kilichoniumiza ni mada ya "giza" katika mchakato wa uokoaji.
Ni heri wazamiaji wa ukara wangesimamia show wamalize wao...........
 
Wanabodi,
Poleni kwa msiba wa MV Nyerere.

Nimetafakari sana kazi iliyofanywa na wenzetu, wazamiaji waliopo katika eneo la Ukara, kabla ya serikali kuanza kuifanya kazi ya kuokoa na kutoa miili ya waliofariji katika ajali ya MV Nyerere. Ninadhani, ingekuwa busara sana endapo serikali ingepata majina na taarifa za watu wote walioshiriki kazi ya kuzamia majini na kuwapa ajira serikalini. Ajira zao zisaidie katika maeneo waliyopo. Katika maeneo yote yenye maziwa, mito na bahari, waanzishe
"Rapid Rescue Team" ambayo itajumuisha watalaam wa asili na watumishi wa taasisi nyingine serikalini.

Ni wazo tu, wanaweza kulifanyia kazi
Nelson
nice advise mkuu!
 
Back
Top Bottom