Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Na Joseph Mwendapole
18th July 2010
Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Mauzo ya Nje (EPZA), imesema wawekezaji wanaowekeza katika maeneo maalum watasahemewa kodi ya mapato kwa miaka kumi.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Meneja Uwezeshaji wa mamlaka hiyo, Lamau Mpolo, wakati akizungumza na Nipashe mara baada ya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji 15 kutoka nchini Thailand, ambao wamekuja kuangalia fursa za kuwekeza.
Alisema kivutio hicho cha msamaha wa kodi kimewekwa kwa makusudi ili kuvutia wawekezaji kuja kwa wingi nchini.
Alisema wawekezaji hutumia muda mrefu kujiandaa kwa ajili ya kujenga viwanda na kuanza kuzalisha hivyo kuwatoza kodi mapema kutawafanya wakimbilie nchi nyiingine.
Lamau alisema makampuni mengi yamekuwa yakianza kupata faida baada ya miaka mitano hivyo wameona kuna haja ya kuwapa unafuu wa kodi.
Mtu anaweza kuona miaka kumi ni mingi lakini mwekezaji anapokuja sio kwamba anaanza moja kwa moja kuzalisha na kuuza, anatumia muda mwingi kufanya maandalizi ya uzalishaji hivyo kumpa unafuu huo kwa miaka kumi ni mwafaka kabisa, alisema.
Sisi tunaangalia na wenzetu duniani wanafanya nini kuhusu suala la kodi kwa wawekezaji maana hawa watu wanagombaniwa kote duniani, kila nchi inajitahidi kuwavutia kwa njia mbalimbali sasa mkiweka mazingira ambayo hayawavutii wanakwenda nchi zenye mazingira mazuri kuwekeza, alisema Lamau.
Aidha, alisema baada ya miaka hiyo kumi mwekezaji analazimika kuanza kulipa kodi serikalini ila akishindwa anatakiwa kutoa sababu za msingi.
Lamau alisema mwekezaji akijieleza kwanini bado hana uwezo wa kulipa kodi serikali itaangalia sababu alizotoa na kama ikiona haikuridhika na sababu zilizotolewa basi atalazimika kulipa.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
-------------------------------------------------------------------------
Wajinga ndio waliwao
18th July 2010
Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Mauzo ya Nje (EPZA), imesema wawekezaji wanaowekeza katika maeneo maalum watasahemewa kodi ya mapato kwa miaka kumi.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Meneja Uwezeshaji wa mamlaka hiyo, Lamau Mpolo, wakati akizungumza na Nipashe mara baada ya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji 15 kutoka nchini Thailand, ambao wamekuja kuangalia fursa za kuwekeza.
Alisema kivutio hicho cha msamaha wa kodi kimewekwa kwa makusudi ili kuvutia wawekezaji kuja kwa wingi nchini.
Alisema wawekezaji hutumia muda mrefu kujiandaa kwa ajili ya kujenga viwanda na kuanza kuzalisha hivyo kuwatoza kodi mapema kutawafanya wakimbilie nchi nyiingine.
Lamau alisema makampuni mengi yamekuwa yakianza kupata faida baada ya miaka mitano hivyo wameona kuna haja ya kuwapa unafuu wa kodi.
Mtu anaweza kuona miaka kumi ni mingi lakini mwekezaji anapokuja sio kwamba anaanza moja kwa moja kuzalisha na kuuza, anatumia muda mwingi kufanya maandalizi ya uzalishaji hivyo kumpa unafuu huo kwa miaka kumi ni mwafaka kabisa, alisema.
Sisi tunaangalia na wenzetu duniani wanafanya nini kuhusu suala la kodi kwa wawekezaji maana hawa watu wanagombaniwa kote duniani, kila nchi inajitahidi kuwavutia kwa njia mbalimbali sasa mkiweka mazingira ambayo hayawavutii wanakwenda nchi zenye mazingira mazuri kuwekeza, alisema Lamau.
Aidha, alisema baada ya miaka hiyo kumi mwekezaji analazimika kuanza kulipa kodi serikalini ila akishindwa anatakiwa kutoa sababu za msingi.
Lamau alisema mwekezaji akijieleza kwanini bado hana uwezo wa kulipa kodi serikali itaangalia sababu alizotoa na kama ikiona haikuridhika na sababu zilizotolewa basi atalazimika kulipa.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
-------------------------------------------------------------------------
Wajinga ndio waliwao