figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,493
- 54,900
Watu zaidi ya 400 waathirika wa mafuriko Mateteni Kilosa hawatashiriki zoezi la kupiga kura.
Zaid ya kaya 100 zenye watu zaidi ya watu 400 walioathirika na mafuriko wanaoishi katika Mahema ya mateteni wilayani kilosa mkoani morogoro wamesema haWawatashiiriki zoezi la kupiga kura kutokana na serikali kushindwa kuwapa makazi ya kudumu huku wakiendelea kuishi maisha magumu kwenye mahema yaliochakaa na wengine kulazimika kulala nje kwa kukosa makazi.
Wakizungumza kwa uchungu waathirika wa mafuriko huku wakionyesha mahema yalivyo chakaa wananchi hao wametupia lawama serikali kushindwa kutimiza ahadi ya kuwapa viwanja vya kujenga makazi mapya baada ya nyumba zao kubomoka kabisa na nyingine kusombwa na maji hali inyosababisha wananchi hao kuishi kwa mateso hasa wanawake na watoto kutokana na upepo mkali huku wakieleza zaidi ya vifo saba vya watoto wachanga vimetoea katika kambi hiyo kutokana na kuugua ugonjwa wa nimonea uliosabaishwa na baridi kali kutokana na watoto kulala nje na mama zao.
Nao viongozi kijiji cha Mateteni wamesema baadhi ya wananchi wamelazimika kurudi katika makazi yao ya awali ingawa si salama kutokana na kuchoshwa na maisha magumu katika kambi hiyo ambapo wamesema waathirika hao wa mafuriko walilazimika kulima vibarua ili kupata fedha za kuwapa viongozi wa kambi kufuatilia ahadi ya viwanja katika ofisi mbalimbali kuanzia ngazi ya wilaya mkoa hadi wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi lakini hadi sasa hakuna majibu ya kupata viwanja ingawa wanazungukwana mashamba pori makubwa ambayo hayajawahi kuendelezwa kwa madai ni ya wawekezaji.
Chanzo: ITV
Zaid ya kaya 100 zenye watu zaidi ya watu 400 walioathirika na mafuriko wanaoishi katika Mahema ya mateteni wilayani kilosa mkoani morogoro wamesema haWawatashiiriki zoezi la kupiga kura kutokana na serikali kushindwa kuwapa makazi ya kudumu huku wakiendelea kuishi maisha magumu kwenye mahema yaliochakaa na wengine kulazimika kulala nje kwa kukosa makazi.
Wakizungumza kwa uchungu waathirika wa mafuriko huku wakionyesha mahema yalivyo chakaa wananchi hao wametupia lawama serikali kushindwa kutimiza ahadi ya kuwapa viwanja vya kujenga makazi mapya baada ya nyumba zao kubomoka kabisa na nyingine kusombwa na maji hali inyosababisha wananchi hao kuishi kwa mateso hasa wanawake na watoto kutokana na upepo mkali huku wakieleza zaidi ya vifo saba vya watoto wachanga vimetoea katika kambi hiyo kutokana na kuugua ugonjwa wa nimonea uliosabaishwa na baridi kali kutokana na watoto kulala nje na mama zao.
Nao viongozi kijiji cha Mateteni wamesema baadhi ya wananchi wamelazimika kurudi katika makazi yao ya awali ingawa si salama kutokana na kuchoshwa na maisha magumu katika kambi hiyo ambapo wamesema waathirika hao wa mafuriko walilazimika kulima vibarua ili kupata fedha za kuwapa viongozi wa kambi kufuatilia ahadi ya viwanja katika ofisi mbalimbali kuanzia ngazi ya wilaya mkoa hadi wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi lakini hadi sasa hakuna majibu ya kupata viwanja ingawa wanazungukwana mashamba pori makubwa ambayo hayajawahi kuendelezwa kwa madai ni ya wawekezaji.
Chanzo: ITV